Mtaji wa pamoja kwenye mradi wa kilimo- (joint capital)

Mtaji wa pamoja kwenye mradi wa kilimo- (joint capital)

Mkuu Revolution tunakuomba urudi kwenye uzi wako huku.
Kama unamaanisha ulichokiandika, basi natuanze sasa hivi. Binafsi ardhi ninayo ila ningekushauri tuanze mdogo mdogo kama wengi walivyopendekeza. Tuanze na ekari10 kwa kilimo cha umwagiliaji. Mimi shamba lililo karibu na chanzo cha maji ninalo na muda wa kujitolea kukaa shamba upo wa kutosha even over a year.
Nikomee hapa kwanza, utakapojibu post hii tutaendelea na mazungumzo hapahapa ili kila mdau apate wasaa wa kushiriki na kuchangia mawazo.

Mkuu Kisima na wadau wengine ninashukuru kwa kuonyesha support kwenye wazo hili. Mawazo ya wadau wengi naona yamejikita kwenye capital kuwa ni kikwazo...kweli hata mimi nalijua hilo lakini nilipotoa hili.wazo niliona hicho ndicho kianzio kizuri ambacho kama group tunaweza kuanza vizuri hata hivyo niliplan hiyo capital tuichange kidogo kidogo even over a year. Najua kabisa kuwa na hii hela kwa mkupuo kwa wengi wetu ni mtihani, hata kwangu pia.

Heshima yako mkuu Kisima nakukubali sana kaka.Mkuu Revolution nathibitisha uwepo wangu kwenye hili wazo japo mimi si mkazi wa Dar ila nitaomba kupewa updates kama mtapiga hatua ili nijue ushiriki wangu utakuwa wa namna gani
 
Last edited by a moderator:
faiza,

Ukiona vijana wanakuzingua, njoo uungane na mimi tupige kazi Mkuranga kwetu karibu na Mpafu, pale si karibu na kwenu Boza?

Kuungana huko kwahitaji physical appearance? Au mtu unaweza kuweka capital then ukasubiria faida tu baadae?
 
Pamoja sana mkuu xfactor.
Mdau Revolution kinachosumbua wengi ni fearness, ni vijana wachache sana walio na utayari wa kushiriki kwenye uzalishaji kupitia kilimo. Wanaona kujiengage kwenye kilimo ni udharirisha vyeti vyao na hii chimbuko lake ni jamii tulizokulia na malezi elekezi kutoka kwa wazazi kuhusu matokeo baada ya kuacquire elimu kinachofuata ni ajira na kuvaa tai-Hii imepitwa na wakati vijana tubadilike.
Binafsi nimekuwa nikiwasilia na wadau kadha wa kadha juu ya kuunganisha nguvu ili tufanye kitu kinachoonekana, lakini huwa tunaishia kujaza server ya JF pasipo utekelezaji. Inachosha na kukatisha tamaa.
Naungana na mkuu Malila na Chasha Poultry Farm najua mlianza kivyenu vyenu kama nilivyo mimi. Japo changamoto zipo nyingi, kwakua nimechagua kuwa nyani basi sina budi kuikwepa mishale.

Mkuu Revolution njoo tupige kazi, utasubiri mwitikio wa wadau wengi mpaka lini? issue ni performance kaka.
 
Last edited by a moderator:
Ni wazo zuri sana.

Linahitaji kufanyiwa kazi kwa kina.

Count me in, ikiwa hicho kigezo cha umri utakiondoa. Kwanini mtubague wazee?

Vijana wanatubagua siye wa above 45, sijui hawataki tuwekeze pesa yetu?
 
Pamoja sana mkuu xfactor.
Mdau Revolution kinachosumbua wengi ni fearness, ni vijana wachache sana walio na utayari wa kushiriki kwenye uzalishaji kupitia kilimo. Wanaona kujiengage kwenye kilimo ni udharirisha vyeti vyao na hii chimbuko lake ni jamii tulizokulia na malezi elekezi kutoka kwa wazazi kuhusu matokeo baada ya kuacquire elimu kinachofuata ni ajira na kuvaa tai-Hii imepitwa na wakati vijana tubadilike.
Binafsi nimekuwa nikiwasilia na wadau kadha wa kadha juu ya kuunganisha nguvu ili tufanye kitu kinachoonekana, lakini huwa tunaishia kujaza server ya JF pasipo utekelezaji. Inachosha na kukatisha tamaa.
Naungana na mkuu Malila na Chasha Poultry Farm najua mlianza kivyenu vyenu kama nilivyo mimi. Japo changamoto zipo nyingi, kwakua nimechagua kuwa nyani basi sina budi kuikwepa mishale.

Mkuu Revolution njoo tupige kazi, utasubiri mwitikio wa wadau wengi mpaka lini? issue ni performance kaka.

Umesema vyema kisima ni heri kuwa wachache wenye malengo sawa kuliko kutaka idadi kubwa mje kuvurugana badae.. Na mtaji wa kuanza si lazima muwe na mahela yote hayo inawezekana kuanza kama wakulima kawaida mkikua mnasajili kampuni
 
Last edited by a moderator:
Pamoja sana mkuu xfactor.
Mdau Revolution kinachosumbua wengi ni fearness, ni vijana wachache sana walio na utayari wa kushiriki kwenye uzalishaji kupitia kilimo. Wanaona kujiengage kwenye kilimo ni udharirisha vyeti vyao na hii chimbuko lake ni jamii tulizokulia na malezi elekezi kutoka kwa wazazi kuhusu matokeo baada ya kuacquire elimu kinachofuata ni ajira na kuvaa tai-Hii imepitwa na wakati vijana tubadilike.
Binafsi nimekuwa nikiwasilia na wadau kadha wa kadha juu ya kuunganisha nguvu ili tufanye kitu kinachoonekana, lakini huwa tunaishia kujaza server ya JF pasipo utekelezaji. Inachosha na kukatisha tamaa.
Naungana na mkuu Malila na Chasha Poultry Farm najua mlianza kivyenu vyenu kama nilivyo mimi. Japo changamoto zipo nyingi, kwakua nimechagua kuwa nyani basi sina budi kuikwepa mishale.

Mkuu Revolution njoo tupige kazi, utasubiri mwitikio wa wadau wengi mpaka lini? issue ni performance kaka.

Siku moja nilikwenda dcb kufungua ac,sehemu ya kazi nikajaza peasant-mkuranga,wale mabinti waliangua kicheko,wakasema hawajawahi ona mtu aliyejaza hivyo tangu waanze kazi. Kila mtu anajaza eti ni mfanyabiashara ndogo ndogo. Umeona shida ilipo, badala ya kufuatilia nalima nini na mtaji wangu ukoje, je naweza kukopesheka, wao wanaona kituko mkulima kufungua ac.

Nina rafiki yangu Mjerumani analima mboga mboga na anafuga kuku, amewaajiri Wabongo ktk ardhi walimozaliwa. Nawasihi tubadilike ili kilimo kitukomboe sisi kwanza na wageni baadae. Tukishindwa sasa kuunganisha nguvu wakati fursa zingalipo, huko mbele hatutaweza kabisa.
 
Kuungana huko kwahitaji physical appearance? Au mtu unaweza kuweka capital then ukasubiria faida tu baadae?

Kuonana uso kwa uso sio lazima kama mtu unajiamini. Kuna mradi mmoja nilifanya na watu watatu hatujawahi onana uso kwa uso,ila mimi najua wapi wanatokea na wao wanajua wapi pa kunipata. Kikubwa ni aina ya mradi,mtaji na trust btn/among basi. Lakini project lazima iwe clear kwa wote, sio mmoja ndio anajua ilipo.
 
Maendeleo makubwa ya wananchi wa ulaya na amerika yamesukumwa kwa kiasi kikubwa na vyama vya ushirika na kampuni za ushirika kama kwenye wazo hili.
Pongezi kwa mtoa wazo.
 
Kwa idadi hiyo ya watu unayotaka kuanza nayo changamoto itakuja kwenye utekelezaji, maana patakosa ufanisi, commitment na kutofautiana kwa interest pia kila Mtu ataona anasauti. Anza wewe zen utapata tu shareholders baadae na sauti utakuwa nayo wewe as a founder wa hilo jambo. Kila lakher
 
Ok, japo niko nje ya huo umri ila nimeipenda hii;
Eka tatu ni kidogo sana kwa hiyo idadi ya watu 10-15.

Mil 10/= zote za nini sasa? Hapa utakimbiza wadau.

Kwa kuweka nia pengine kila mdau afungue akaunti yake maalum
akusanye walau 3m/= kwa mwaka mmoja huku mikakati ya kupata eneo
ikiendelea;

If you will not mind consider may name.
 
Mkuu Revolution njoo tupige kazi, utasubiri mwitikio wa wadau wengi mpaka lini? issue ni performance kaka.

Kwa heshima na taadhima naomba nishirikishwe kwenye huo mkutano na makubaliano
 
Last edited by a moderator:
Naiona Tanzania ikifunguka ahsante MUNGU. Vijana wanaanza kutumia akili na elimu zao kukabili na kuyashinda matatizo yao.Nimependa mno wazo la mtoa mada na wachangiaji. Umri Wangu ni zaidi ya masharti yaliyopo. Uanachama nikizuwiwa kuchangia mawazo nitaendelea kushiriki. Tuanzeni utekelezaji bila kusubiri mtaji fedha mkubwa. Cha muhimu ni wazo zuri la nini cha kuanza nacho. Mtaji ni kama mmea ukitunzwa vizuri unakua ukitunzwa vibaya unakufa. Umri usiwe kigezo cha ushiriki Bali mawazo yanayofanana. Mapema kabisa amueni mnataka kuendesha kama nini ? Kampuni, Chama cha Ushirika, Kikundi kilichosajoliwa/kisichosajiliwa, Joint venture au partnership. Tambueni mapema udhaifu na nguvu za kila mfumo kabla ya kuanza. Ushauri Wangu ni vema kukutana. Nimependa mno wazo litakalofuta Taifa la kutengeneza vijana wa kununua na kuuza tu. Tutende tusiishie kuwaza na kusema
 
Kuungana huko kwahitaji physical appearance? Au mtu unaweza kuweka capital then ukasubiria faida tu baadae?

Kuonana uso kwa uso sio lazima kama mtu unajiamini. Kuna mradi mmoja nilifanya na watu watatu hatujawahi onana uso kwa uso,ila mimi najua wapi wanatokea na wao wanajua wapi pa kunipata. Kikubwa ni aina ya mradi,mtaji na trust btn/among basi. Lakini project lazima iwe clear kwa wote, sio mmoja ndio anajua ilipo.

Kwa mtazamo wangu na experience yangu, kuweka fedha na kusubiria faida inawezekana kwa biashara au mradi ambao tayari umesimama vizuri. Kwa biashara au mradi unaoanza ni vizuri ukawepo ushiriki wa member wote moja kwa moja, ukumbuke siku zote reality ya field inakuwa tofauti sana na mipango ya mezani. Nikupe mfano wangu binafsi, wakati fulani nilinunua ardhi kubwa kiasi kama eka 50+, katika kulima nikaamua kushirikiana na rafiki yangu mmoja, katika msimu wa kwanza changamoto zikiwa nyingi sana katika kila hatua kuanzia usimamizi, ukosefu wa wafanyakazi, ugumu wa upatikanaji wa mbegu bora, utafutaji na upatikanaji wa masoko, uhifadhi wa mazao na kadhalika. Lakini katika mipango ya mezani kila kitu kilionekana perfect sana kama kusubiri tu faida ije mifukoni, kwa hiyo tuliona ni kama pale tunaweka pesa na kusubiri faida. Changamoto zilipoanza kujitokeza rafiki yangu anauliza inahitajika pesa kiasi gani??? You know what, it was not about money! It was about a complete involvement and solutions finding. Ilifika mahali kichwa kinauma hadi najiuliza "Hivi tuko wawili au niko peke yangu?" Unapoweka fedha na kusubiri faida wakati mwenzako anaparangana ni kama unakuwa mwanahisa tu katika kampuni yenu lakini mwanahisa mwenzio ndio mfanyakazi na mzalishaji wa kampuni yenu.
Weka fedha na kusubiri faida katika mradi ambao umeshaanza na kunyooka, sio mradi unaoanza coz uwezekano wa kutokuelewana ni mkubwa! Vipi wote mkiweka fedha mkasubiri faida, nani atasimamia michakato yote????
 
Kwa mtazamo wangu na experience yangu, kuweka fedha na kusubiria faida inawezekana kwa biashara au mradi ambao tayari umesimama vizuri. Kwa biashara au mradi unaoanza ni vizuri ukawepo ushiriki wa member wote moja kwa moja, ukumbuke siku zote reality ya field inakuwa tofauti sana na mipango ya mezani. Nikupe mfano wangu binafsi, wakati fulani nilinunua ardhi kubwa kiasi kama eka 50+, katika kulima nikaamua kushirikiana na rafiki yangu mmoja, katika msimu wa kwanza changamoto zikiwa nyingi sana katika kila hatua kuanzia usimamizi, ukosefu wa wafanyakazi, ugumu wa upatikanaji wa mbegu bora, utafutaji na upatikanaji wa masoko, uhifadhi wa mazao na kadhalika. Lakini katika mipango ya mezani kila kitu kilionekana perfect sana kama kusubiri tu faida ije mifukoni, kwa hiyo tuliona ni kama pale tunaweka pesa na kusubiri faida. Changamoto zilipoanza kujitokeza rafiki yangu anauliza inahitajika pesa kiasi gani??? You know what, it was not about money! It was about a complete involvement and solutions finding. Ilifika mahali kichwa kinauma hadi najiuliza "Hivi tuko wawili au niko peke yangu?" Unapoweka fedha na kusubiri faida wakati mwenzako anaparangana ni kama unakuwa mwanahisa tu katika kampuni yenu lakini mwanahisa mwenzio ndio mfanyakazi na mzalishaji wa kampuni yenu.
Weka fedha na kusubiri faida katika mradi ambao umeshaanza na kunyooka, sio mradi unaoanza coz uwezekano wa kutokuelewana ni mkubwa! Vipi wote mkiweka fedha mkasubiri faida, nani atasimamia michakato yote????

Kuna miradi pasua kichwa, mradi wa kilimo ukiwemo. Kuna miradi isiyo na faida ya haraka, hii kuweka hela na kusubiri faida ni hatari kwa mtu ambaye hana misuri mizuri ya kiuchumi. Kuna miradi ya faida ya chap chap, hii pia ni hatari sana kama team ina watu wasio waaminifu.

Ni nani yuko tayari kuingiza hela za mwenzake ktk mradi ulioanza kuonyesha matokeo chanya? Kwa mazingira ya Tz ya sasa, ni vizuri muanze wote tangu kuchagua mradi,kukabili changamoto. Miradi kama ufugaji wa ng`ombe wa nyama uko wazi sana, ila sio wa ng`ombe wa maziwa, ni pasua kichwa kwa small scale kama mme-share mtaji. Ranch ya mbuzi,kondoo kwa sababu ni rahisi kidogo.


Twende mbele turudi nyuma, ku-share bila kusajiri kampuni, ni pasua kichwa. Hata walokole wanagombana, itakuwa sisi wa kuokotana mitaani? Sisemi haiwezekani kabisa, ila inahitaji uzalendo wa kiwango cha juu, kama ulivyosema, ww uko chaka unahangaika na mvua/jua/vibarua,wadudu waharibifu na jamaa yako yuko Rose Garden anasoma e mail zako pembeni kaweka red wine huku anapungwa pepo kwa mbali!!!!!! Halafu siku ya mahesabu itoke 50/50!!


Dawa ni kufungua ofisi rasmi na atafutwe ceo wenu mkali wa mambo basi.
 
Ok, japo niko nje ya huo umri ila nimeipenda hii;
Eka tatu ni kidogo sana kwa hiyo idadi ya watu 10-15.

Mil 10/= zote za nini sasa? Hapa utakimbiza wadau.

Kwa kuweka nia pengine kila mdau afungue akaunti yake maalum
akusanye walau 3m/= kwa mwaka mmoja huku mikakati ya kupata eneo
ikiendelea;

If you will not mind consider may name.

Mamdenyi,

Hivi ule msitu wa nguzo pale njiani ulishauza au bado, nipe bei niutokee august. Nikifika mara nyingi huwa nakula pale Mambo ya Tanga. Bado uko kule au umeshahama?
 
Siuzi tena,
Navuta vuta nije kupata pesa ndefu;.

......... Kile kikundi chenu cha JF cha mashamba ya mafinga kimefikia wapi?
Nasikitika sana nilichelewa..........
Mamdenyi,

Hivi ule msitu wa nguzo pale njiani ulishauza au bado, nipe bei niutokee august. Nikifika mara nyingi huwa nakula pale Mambo ya Tanga. Bado uko kule au umeshahama?
 
Malila John Kachembeho mpo sahihi,hata mimi najua kuwa inachosha sana kama mmoja ndio yupo busy na mradi halafu mwingine amekaa tu anasubiri faida,ndio maana nikaanza kwa kuuliza kama inakubalika maana wengine wapo nje ya dar na Tanzania lakini wana imani na mradi husika kuwa utalipa hivyo wangependa kashiriki lakini uwepo wao physical ni impossible
 
Last edited by a moderator:
Malila John Kachembeho mpo sahihi,hata mimi najua kuwa inachosha sana kama mmoja ndio yupo busy na mradi halafu mwingine amekaa tu anasubiri faida,ndio maana nikaanza kwa kuuliza kama inakubalika maana wengine wapo nje ya dar na Tanzania lakini wana imani na mradi husika kuwa utalipa hivyo wangependa kashiriki lakini uwepo wao physical ni impossible

Nimekujibu kuwa kuna baadhi ya miradi inawezekana kabisa. Mingine ni pasua kichwa. Na nikakwambia kuna mradi mmoja nimefanya na watu wako nje ya nchi vizuri bila kuleteana shida.

Kikubwa ni uchaguzi mzuri wa mradi na kupanga vizuri hatua za utekelezaji, ili kila hatua ipimwe kabla haijaumiza. Mimi nimekuwa nikichagua miradi ya muda mrefu, miradi ya namna hii inabidi uwe na subira sana, lakini mtaji wake naingiza kidogo kidogo.
 
Nimekujibu kuwa kuna baadhi ya miradi inawezekana kabisa. Mingine ni pasua kichwa. Na nikakwambia kuna mradi mmoja nimefanya na watu wako nje ya nchi vizuri bila kuleteana shida.

Kikubwa ni uchaguzi mzuri wa mradi na kupanga vizuri hatua za utekelezaji, ili kila hatua ipimwe kabla haijaumiza. Mimi nimekuwa nikichagua miradi ya muda mrefu, miradi ya namna hii inabidi uwe na subira sana, lakini mtaji wake naingiza kidogo kidogo.

Crystal clear mkuu,napataje details ya miradi uliyonayo kwa sasa ambayo unaruhusu kushirikisha watu?
 
Siuzi tena,
Navuta vuta nije kupata pesa ndefu;.

......... Kile kikundi chenu cha JF cha mashamba ya mafinga kimefikia wapi?
Nasikitika sana nilichelewa..........

Hujachelewa, anzia tulipo.
Kumbe unakijua kikundi chetu, dada tuko vizuri,namshukuru Mungu ametubeba sana,kwa sasa tumeshapanuka sana na tumeingia Njombe na tunaelekea Lizabon tukaoteshe Cedrela/mtiki. Juzi nilipita hapo ndio nikakumbuka tangazo lako, nilikuwa natoka Kitete wilaya ya Kilombero kupitia Mgololo.

Kama hewa ya Ukaa itatufikia na sisi, nadhani humu jf nitakuwa siji kabisa!!!!!!! Ma-don ya Mafinga yatapiga hela hadi basi.
 
Back
Top Bottom