Kazi yangu ni kukuonesha uislamu utarudi pangoni kama nyoka na uta shrinksKijana utaendelea kuonekana kituko, hizo hadithi hazionyeshi ya kuwa watu hawaingii katika Uislamu au hawaukubali au hawashawishiki na Uislamu.
1. Hadithi ya kwanza inaelezea namna Uislamu ulivyo anza kuingia ulikuwa unaonekana ni kitu kipya yaani mgeni, na utarudi ukiwa katika hali hiyo hiyo ya ugeni kama ulivyoanza. Kisha Mtume akasema bishara njema kwa wale watakao onekana wageni, hii inamaanisha ya kuwa hao ndiyo watakuwa sahihi, leo hii Waislamu wako wengi lakini hawaufati ule uislamu sahihi na wale wanao ufata wanaonekana kuwa wameleta dini mpya na hii ndiyo maana ya Hadithi.
Lakini katika mapokezi mengine anasema mtume ya kuwa, hao watakao onekana wageni ni kwa sababu wanatengeneza yale ambayo wameyaharibu watu.
2. Hadithi ya pili inaonyesha zama za mwisho zinapokaribia watu watakuwa na imani haba, na imani itarudi kule ilipoanzia.
3. Hadithi ya tatu ina maana sawa na hadithi ya kwanza.
Sasa hoja yako hapo iko wapi kijana ? Mpaka najiuliza kwanini umetumia hadithi hizi ambazo ziko dhidi yako, ila nahitimisha ni kwa ujinga wako.
“Faith will shrink back to Medina as a snake shrinks back to its hole.” (Bukhari and Muslim.) Mishkat al-Masabih 160