Kahesa Andrew
Member
- Apr 3, 2012
- 82
- 35
Oooh ok nashukuru kwa kunielewesha mkuuZembwela sio mtangazaji, ni muongeaji kwenye radio, nikama hao kina gigy money sijui na kida Idrisa na wengine wanao fanania hivyo, utangazaji ni fani lazima ukasomee. utangazaji ni fani kama udakitari na ualimu, kuna ethics zake, kufanya kazi kwenye kituo cha habari hakikufanyi kuwa mwanahabari. Kama kuna mtu ameingia kwenye field ya habari kutokana na umashuhuri wake au namna yoyote kisha akaona kuna future ndani ya habari, inabidin afanye maarifa ili aingie darasani kusomea hiyo kazi.
Clouds ndio nini? Ni basi la kwenda upcountry?Vipindi vingi vya clouds ni utoto mtupu na aibu tu nina miaka 3 sifunguagi clouds kabisa ni ujinga ujinga tu!
Dah... wangekuwa na akili ya kujitambua wangeanzisha radio yao
Huwezi mchanganya zembwela na hao waganga njaaNiliwahi kumsikia Joseph Kusaga anasema yeye kwenye Ajira zake za Utangazaji huwa haangalii suala la Elimu anachokiangalia ni kipaji chako hata kama umeishi la Saba.
Naamini ndio ukweli wenyewe na wengi wameamua kufuata mtindo huo wa kuangalia vipaji zaidi na sio Elimu, ndio maana tunawasikia Wakina Mpoki, Zembwela, Gigy money japo sijui huyu waliangalia kigezo gani n.k
Wameona kwa wenzao wakenya na wao wanaangalia Kipaji zaidi kuliko elimu ndio maana Redio zao nyingi zimejaa wachekeshaji.
Ubaya wetu tumebaki kuwaangalia wale wale tu na hivyo tunakuwa kama tunawagombania badala ya kuibua hawa ambao wana elimu lakini pia wana kipaji ambao wamekosa watu wa kuwashika mkono.
Dah mkubwa fella, babu talle wanauhusiano mkubwa na hao unaowataja na ukitaka kutoboa inabidi uwapigie magoti sio vizuri,wasanii wanakosa uthubutuIpo haja ya kuboreshwa radio nyingine pamoja na kutoa promote wanamuziki sababu wakati mwengine radio 1 tu kama clouds kumsusia mwanamuziki na kufeli moja kwa moja haijakaa sawa.
Fursa za kuanzisha redio nyingine zenye ushindani inabidi iongezeke ili ushindani usiwe upande mmoja.
Hata mimi naona hivyo, vipindi vingi havina maudhui, lakini wanasema ukiona hivyo ujuwe umri unakutupa mkono...Yawezekana ni ushamba wangu au umri, binafsi baadhi ya vipindi vingi vya Clouds FM sioni maudhui yake na faida chanya za kuijenga jamii yetu na kwa maendeleo ya taifa. Nadhani wangepewa nafasi ya kupromoti sanaa tuu, vingine waachie wengine
Yuko Choice Fm...kipindi flani hivi cha usiku...niliwai msikia ukoJamani Gigy Money anatangaza redio gani?
Hata hawa kina fella, babu tale na sallam wanatakiwa kujenga misingi kwa maendeleo ya mziki wa Tanzania hasa kimataifa. Ili isitokee siku wakifulia/ kufariki watu waanze moja kutafuta channel za kimataifa. Kuna wasanii wengi wazuri wanatakiwa kufika level za kimataifa pia kuna mameneja wengi wazuri wanaohitaji soko la mataifa kuwasaidia waTzDah mkubwa fella, babu talle wanauhusiano mkubwa na hao unaowataja na ukitaka kutoboa inabidi uwapigie magoti sio vizuri,wasanii wanakosa uthubutu