TANZIA Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde afariki dunia. Azikwa makaburi ya Kinondoni,Dar es Salaam

TANZIA Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde afariki dunia. Azikwa makaburi ya Kinondoni,Dar es Salaam

Ngumu kupoa slim..yan naumwa hapa ila nahis nimezidi kuumwa

QUOTE="Slim5, post: 30655174, member: 196493"]Pole sana..... Kazi ya Mungu..... [/QUOTE]
 
Dstv wataubeba huu msiba ..dah ..Magu yuko wapi atangaze..maana huyu alikua shabiki kindaki ndaki wa ccm
 
Ephraim Kibonde amefariki usiku wa kuamkia Leo tarehe 7 machi 2019

Hatujapoa bado na msiba wa Ruge Leo Kibonde hatunae

Huzuni sana Mungu awape faraja watoto wake

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli duniani tunapita....ninakumbuka mwaka 2015 tulikutana Golden Tulip kwenye get together party ya Heineken...nikakukumbusha miaka ya 1981/2 Tambaza Secondary enzi za Mzee Kalumuna...nikakutajia majina ya mamates kama William Chiume,Jonathan Haule,John Peter,Godius Kahyarara wengine wakubwa kama Yahya Tuli...nikakuuliza ulikua darasa lipi...mm nilikua U...ukanijibu hapana sikusoma Tambaza ila Azania...japo story nyingi redioni zilikua za Tambaza miaka hiyo na ulizipata kutoka kwa marafiki...hasa za kupigana na maaskari polisi watunza foleni na mainspector wa UDA pamoja na migambo wao...pia ugomvi wa Kinondoni Muslim na Tambaza uliotokea Muhimbili Pri school...nitakukumbuka sana ulikuwa unanikumbusha mbaali sana na nikawa mpezi sana wa kipindi chako cha Jahazi....tangulia mate..ni njia yetu wote...mbele yako...nyuma yetu....Mungu aiweke roho yako mahali pema peponi Ephraim....so sad....
 
Kuna watu wanajiona hapa duniani wao ndio wao.....tukumbushane jamani, tutende mema, tuwandee mema wenzetu, tuondoe vinyongo kwa wenzetu, tunayoyafanya na kujivunia ni upepo tu! Mungu akisema rudi huna cha kujitetea
 
Pumzika Kibonde, poleni familia poleni clouds.
 
Poleni sana CMG kwa misiba miwili mikubwa....

JF naona siku hizi mnachagua nani anafaa kuweka uzi na nani hafai kuweka uzi...

Nikiwa mwanza kikazi,leo asubuhi napata habari za kifo cha Kibonde toka kwa Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mwanza...

Naingia kwenye page ya clouds ya IG wameshatoa taarifa za kifo cha staff wao...

Nami naandika thread hapa juu ya kifo cha Kibonde,naweka na supporting document toka page ya Clouds ya IG...

Nashangaa uzi wangu unafutwa... nakutupwa kwenye dustbin,ila aliyekuja nyuma yangu anaachwa na uzi wake...

Maswali yangu kwenu JF...
a) Hivi naweza toa taarifa za uongo kuhusu kifo cha mtu?? Kwa manufaa ya nani hasa. Hivi mlitaka muamini nini hasa kama nilichofanya mimi,ndicho alichofanya mleta mada nyuma yangu??

b) Je mnapenda watu.wapi wa namna gani watoe thread/uzi ndiyo uamini??

c) Nimepata taarifa toka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mwanza,pia Clouds wenyewe wakawa washatoa kabisa taarifa zao kwenye IG page yao... Ila mkaona hapana mkatoa uzi wangu.

Mnakera sana tena sana....Msipende kubagua nani anafaa na nani hafai kuweka uzi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu haipendezi kupotosha, pia ulipaswa kuanzisha mada ya malalamiko inayojitegemea kwenye jukwaa husika na sio kwenye bandiko la taazia.

Mada yako umeanzisha dakika tatu baada ya mada hii kuanzishwa.

JF inatenda haki kwa wote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Eee Mungu wangu bora hata Ruge aliumwa muda mrefu jamani. Duu nilikuwa nasikiliza jahazi kwasababu yake. Nimesikitika sana.
 
Back
Top Bottom