Mtangazaji wa Sibuka Radio aliyesoma Vichwa vya Habari leo arudi tena Darasani anatia 'Kichefuchefu' Kumsikiliza

Tumerikamata ri tuhumiwa

Ajari mbaya imetokea wiraya ya tarime

Sisi ndo jeshi la porisi utake usitake razima tukufunze adabu
 
Kuna wengine wanakosea kuita juventus, wengine wanatamka juventasi na wengine juventusi
 
Huwa nachukia sana kuona mtu aliyesomea mambo ya habari anaharibu lugha ya kiswahili waziwazi.

pia wazungumzaji (hasa watu wa mjini) wana makosa mengi sana mfano;- ela badala ya hela, abari badala ya habari, haidi badala ya ahidi. N.k

Inastaajabisha sana mswahili hajui kiswahili.
 

unataka kumfurahisha nani !. kiswahili sina ajira nacho kama umeelewa pita huko .kachukue kiswahili kikulishe basi
 
Umemsagia kunguni
 
Simiyu ila kwa hapa Dar es Salaam wapo Mwenge Bamaga nyuma ya Hotel Maarufu ya aliyekuwa Hawara Mwandamizi ( Mpango wa Kando ) wa Aliyelala mazima Ziwa Victoria Mkoani Geita.
Nimecheka sana hii post eti Hawara mwandamizi ha ha
 

kuna wajinga kama nyie .lugha unataka tunyooke imekusaidia nini hata masaki ijawahi kutumika.
 
Vituko ni vingi redioni na televisheni, hata kwenye redio na televisheni maarufu watangazaji wanakosea kutamka maneno au majina. Ni uzembe na uvivu wa hali ya juu kwa mtangazaji kutamka kimakosa maneno wakati kuna msaada tele upo kwenye kamusi vitabuni na kwenye kompyuta na simu. Watangazaji wanatakiwa wawe wadadisi wa lugha nyingi kujua kutamka majina yao kwa ufasaha, hasa hawa wa vipindi vya michezo. Anakuja mchezaji wa kigeni au kocha wanashindwa kutamka jina lake kwa usahihi.
 
Tupo wengi sana tunaosikiliza redio hasa vipindi muhimu kama amka na bbc dira ya dunia mchana na jioni na makala zenye kuelimisha japo media nyingi watangazaji hawana utashi wa kuleta habari sikuhizi ni kutangaza kamari tu
Umepata wapi muda huu wa Kumjibu na hadi Kumuelimisha huyo Mpumbavu?

Cc: kitalembwa
 
Miaka 10 ijayo hakutakua na lugha ya Kiswahili
Ninachoshangaa na Kukushangaa Wewe hunipendi kabisa GENTAMYCINE lakini umekuwa Mmoja wa Watu ambao uwepo hapa JamiiForums haunogi na haukamiliki mpaka Usome Mada ( Threads ) zangu.

Asante Mungu kwa Karama Uliyonipa.
 
Nilijisikia vibaya Jumapili iliyopita kanisani pale msomaji Aliposoma malahika badala ya malaika.

Kuna hawa wa a,e,i,o,u badala ya h mfano (hajafika - ajafika) na kinyume chake mf. Hapa - apa.

Na wale wanaochanganya l na r
 
Watangazaji aina hii wapo wengi, inashangaza walisoma shule zipi ambazo hazifundishi kiswahili. Au walimu wao wa kiswahili hawakufundisha jinsi ya kuandika na kutamka maneno ya kiswahili kwa ufasaha. Kiswahili wanakosea, kiingereza ndiyo vituko zaidi. Kifaransa ndiyo vioja vikubwa, majina ya kifaransa wanayatamka kiingereza kilichokosewa. Wachambuzi wa soka nao wameungana na hao watangazaji kuharibu lugha fasaha. Shule zipo wakasome ili wafanye kazi zao kwa weledi na umahiri
 
Punguza Makasiriko Mkuu
Utakufa kabla ya siku zako
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ Ndio maana unaweza kuwahandle watu humu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Angekuwa anawamudu wababe wa humu jukwaani, nikiwemo mimi hapa mbabe wake namba 1 kabisa kuwahi kutokea hapa duniani; Tate Mkuu, asingetukana watu hovyo.

Huyu Popoma wenu siku zote huwaonea watu wanyonge, akiwemo huyo mtangazaji wake wa Sibuka.

Ila siyo wababe kama mimi Tate Mkuu, na wababe wengine kama Nifah , ukikaidi utapigwa2, Matola, LIKUD, vibertz, OKW BOBAN SUNZU, na wengineo wengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…