GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
UTANGULIZI
Sijawahi hata Siku moja kuficha Hisia zangu za 'Kukukubali' sana hasa kwa aina ya 'Misimamo' yako thabiti, uwezo wa Kufikiri ( Akili ) na pia Kuchambua mambo 'Kiumakini' kabisa. Na hapa nisikufiche si Mimi tu ambaye ni mwana CCM nakiri na kulisema hili ila nina uhakika hata wana CCM wengi tu nao wapo kama Mimi juu yako sema tu hawakuonyeshi Kiuwazi japo Mioyoni mwao upo sana tu.
MTAZAMO
Sina shaka kabisa na Wewe Kutia Nia na hatimaye Chama chako cha CHADEMA Kukuamini na Kukuteua kuwa Mgombea wao kwani Kisheria na Kikatiba hii ni Haki ya Kila Mtanzania mwenye Sifa Kamili kufanya hivyo. Wasiwasi wangu Kwako upo sehemu ndogo tu kwamba umewahi kufanya 'Timing' Kipindi hiki kibaya Kwako Kisiasa na badala yake kwa mwaka 2025 ndiyo ulikuwa muda Muafaka.
USICHOKIJUA
Mtani wangu kutoka Singida Tundu Lissu najua unaweza 'usiamini' ila kwakuwa GENTAMYCINE 'nakupenda' ngoja nikuambie tu ukweli kuwa pamoja na kwamba unaona una Watu (Wafuasi) wengi wakiwa nawe kila uendako ila ukweli ni kwamba 'Kitakwimu' ni 25% tu hao unaowaona ndiyo 'Wamejiandikisha' Kupiga 'Kura' mwaka huu na 'Wamehakiki' vyema kabisa Majina yao Vituoni.
ULILOLISAHAU WEWE NA CHADEMA YAKO
Hapa sitokulaumu Wewe sana Mtani wangu Tundu Lissu kwakuwa muda mwingi ulikuwa katika 'Matibabu' yako huko 'Ughaibuni' ila lawama zangu nyingi nazipeleka kwa CHADEMA kwa 'Kujisahau' Kwao muda mwingi 'Kuwahimiza' Wanachama wao waende 'Kujiandikisha' Vituoni na badala yake wao muda Wao mwingi walitumia 'Kuwekeza' katika 'Kupambana' tu na Serikali ( Dola )
UMAKINI WA CCM UPO HAPA
Tayari CCM walishafanya 'Utafiti' wao wa ndani tena 'Kiumakini' kabisa na 'Kujiridhisha' kuwa wana uhakika wa Kura 8,000,000 ( Milioni Nane ) kutokana na 'Wanachama' wao nchi nzima hivyo wakaendelea katika Kuwatafuta wengine ili kuongeza hiyo idadi huku 'wakiwahimiza' sana Wanachama wao hao 'Kujiandikisha' na hata 'Kuhakiki' Majina yao Jambo ambalo wamefanikiwa 100%.
MKAKATI WA KISIASA ULIOIMALIZA KABISA CHADEMA
Wakati CHADEMA yako muda mwingi 'ikiwekeza' katika 'Kulaumu' na 'Kupambana' na Mamlaka ( Dola ) hasimu walisahau kuwa Siasa zote duniani pia huwa zina 'Umafia' ndani yake na mliosoma 'Political Science' mtanielewa hivyo baada ya 'Kuhisiwa' kuwa mtaendelea kuwa 'Tishio' mkatafutiwa 'Adui Rafiki' wa huko huko 'Upinzani' asaidiwe na wa Kwao ili 'Kuzigawa' Kura zenu nyingi.
FAIDA PEKEE AMBAYO TUTAIPATA KUTOKA KWAKO
Mtani wangu Tundu Lissu wala 'usidanganyike' na 'wasikudanganye' uwezo wa Wewe Kushinda na kuwa Rais wetu haupo na huna hasa kutokana na 'Mikakati' iliyoko na pia kwa 'Mpinzani' wako kufukia karibia 90% ya yale 'Mashimo' yote ya 'Kimapungufu' katika 'Utawala' wake. Kitu pekee utakachofanikiwa nacho ni 'Kuwajaza' tu Watanzania wachache Imani za Chuki na Majungu pia.
USHAURI WANGU KWAKO
Kwakuwa nina uhakika kuwa hutoweza 'Kutoboa' hata iweje ( japo utajitutumua ) ningependa tumia sasa uwezo wako huu mkubwa wa 'Ushawishi' ulionao katika 'Kuwahimiza' Watanzania wanaokuamini na Wafuasi wako 'Wawachague' Wabunge wengi wa CHADEMA ili angalau wakiwa wengi basi muweze kuwa na 'Nguvu' Bungeni ambayo inaweza 'Kukujenga' kwa 2025 Ukigombea.
UWEPO WAKO NI TIJA KUBWA KWA CCM KUENDELEA KUJIJENGA ZAIDI
Nakujua na ni matuamini yangu makubwa kuwa hata katika Mikutano yako ya Kampeni zilizoanza utakuwa unatumia muda mwing sana 'Kuinanga' ile mbaya CCM na Mwenyekiti wake ila usisahau tu kuwa kwa kadri utakavyokuwa 'unawasema' CCM na Rais wao ndiyo utakuwa 'unawafunua' na 'kuwajenga' zaidi ili wazidi 'Kujikita' na 'Kujidhatiti' kabisa Madarakani na Kiutawala.
HITIMISHO
Nakutakia tu Kampeni njema Mtani wangu Tundu Lissu Wewe pamoja na Vyama vingine vyote vya Upinzani nchini Tanzania ila niwaombeni tu tumieni 'Muhula' huu wa mwisho wa Rais Dkt. Magufuli kuwepo 'Madarakani' kwa nyie 'Wapinzani' Kwanza Kujitathmini na Kujijenga zaidi huku mkiwa 'Wamoja' na muache 'Unafiki' ili basi Chaguzi zijazo muingie mkiwa ni Wamoja kabisa.
Wako Mtani wako
GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE ( Majina yangu Kamili ni Kalemera Rwigyema Mazimpaka Kadogoo )
Sijawahi hata Siku moja kuficha Hisia zangu za 'Kukukubali' sana hasa kwa aina ya 'Misimamo' yako thabiti, uwezo wa Kufikiri ( Akili ) na pia Kuchambua mambo 'Kiumakini' kabisa. Na hapa nisikufiche si Mimi tu ambaye ni mwana CCM nakiri na kulisema hili ila nina uhakika hata wana CCM wengi tu nao wapo kama Mimi juu yako sema tu hawakuonyeshi Kiuwazi japo Mioyoni mwao upo sana tu.
MTAZAMO
Sina shaka kabisa na Wewe Kutia Nia na hatimaye Chama chako cha CHADEMA Kukuamini na Kukuteua kuwa Mgombea wao kwani Kisheria na Kikatiba hii ni Haki ya Kila Mtanzania mwenye Sifa Kamili kufanya hivyo. Wasiwasi wangu Kwako upo sehemu ndogo tu kwamba umewahi kufanya 'Timing' Kipindi hiki kibaya Kwako Kisiasa na badala yake kwa mwaka 2025 ndiyo ulikuwa muda Muafaka.
USICHOKIJUA
Mtani wangu kutoka Singida Tundu Lissu najua unaweza 'usiamini' ila kwakuwa GENTAMYCINE 'nakupenda' ngoja nikuambie tu ukweli kuwa pamoja na kwamba unaona una Watu (Wafuasi) wengi wakiwa nawe kila uendako ila ukweli ni kwamba 'Kitakwimu' ni 25% tu hao unaowaona ndiyo 'Wamejiandikisha' Kupiga 'Kura' mwaka huu na 'Wamehakiki' vyema kabisa Majina yao Vituoni.
ULILOLISAHAU WEWE NA CHADEMA YAKO
Hapa sitokulaumu Wewe sana Mtani wangu Tundu Lissu kwakuwa muda mwingi ulikuwa katika 'Matibabu' yako huko 'Ughaibuni' ila lawama zangu nyingi nazipeleka kwa CHADEMA kwa 'Kujisahau' Kwao muda mwingi 'Kuwahimiza' Wanachama wao waende 'Kujiandikisha' Vituoni na badala yake wao muda Wao mwingi walitumia 'Kuwekeza' katika 'Kupambana' tu na Serikali ( Dola )
UMAKINI WA CCM UPO HAPA
Tayari CCM walishafanya 'Utafiti' wao wa ndani tena 'Kiumakini' kabisa na 'Kujiridhisha' kuwa wana uhakika wa Kura 8,000,000 ( Milioni Nane ) kutokana na 'Wanachama' wao nchi nzima hivyo wakaendelea katika Kuwatafuta wengine ili kuongeza hiyo idadi huku 'wakiwahimiza' sana Wanachama wao hao 'Kujiandikisha' na hata 'Kuhakiki' Majina yao Jambo ambalo wamefanikiwa 100%.
MKAKATI WA KISIASA ULIOIMALIZA KABISA CHADEMA
Wakati CHADEMA yako muda mwingi 'ikiwekeza' katika 'Kulaumu' na 'Kupambana' na Mamlaka ( Dola ) hasimu walisahau kuwa Siasa zote duniani pia huwa zina 'Umafia' ndani yake na mliosoma 'Political Science' mtanielewa hivyo baada ya 'Kuhisiwa' kuwa mtaendelea kuwa 'Tishio' mkatafutiwa 'Adui Rafiki' wa huko huko 'Upinzani' asaidiwe na wa Kwao ili 'Kuzigawa' Kura zenu nyingi.
FAIDA PEKEE AMBAYO TUTAIPATA KUTOKA KWAKO
Mtani wangu Tundu Lissu wala 'usidanganyike' na 'wasikudanganye' uwezo wa Wewe Kushinda na kuwa Rais wetu haupo na huna hasa kutokana na 'Mikakati' iliyoko na pia kwa 'Mpinzani' wako kufukia karibia 90% ya yale 'Mashimo' yote ya 'Kimapungufu' katika 'Utawala' wake. Kitu pekee utakachofanikiwa nacho ni 'Kuwajaza' tu Watanzania wachache Imani za Chuki na Majungu pia.
USHAURI WANGU KWAKO
Kwakuwa nina uhakika kuwa hutoweza 'Kutoboa' hata iweje ( japo utajitutumua ) ningependa tumia sasa uwezo wako huu mkubwa wa 'Ushawishi' ulionao katika 'Kuwahimiza' Watanzania wanaokuamini na Wafuasi wako 'Wawachague' Wabunge wengi wa CHADEMA ili angalau wakiwa wengi basi muweze kuwa na 'Nguvu' Bungeni ambayo inaweza 'Kukujenga' kwa 2025 Ukigombea.
UWEPO WAKO NI TIJA KUBWA KWA CCM KUENDELEA KUJIJENGA ZAIDI
Nakujua na ni matuamini yangu makubwa kuwa hata katika Mikutano yako ya Kampeni zilizoanza utakuwa unatumia muda mwing sana 'Kuinanga' ile mbaya CCM na Mwenyekiti wake ila usisahau tu kuwa kwa kadri utakavyokuwa 'unawasema' CCM na Rais wao ndiyo utakuwa 'unawafunua' na 'kuwajenga' zaidi ili wazidi 'Kujikita' na 'Kujidhatiti' kabisa Madarakani na Kiutawala.
HITIMISHO
Nakutakia tu Kampeni njema Mtani wangu Tundu Lissu Wewe pamoja na Vyama vingine vyote vya Upinzani nchini Tanzania ila niwaombeni tu tumieni 'Muhula' huu wa mwisho wa Rais Dkt. Magufuli kuwepo 'Madarakani' kwa nyie 'Wapinzani' Kwanza Kujitathmini na Kujijenga zaidi huku mkiwa 'Wamoja' na muache 'Unafiki' ili basi Chaguzi zijazo muingie mkiwa ni Wamoja kabisa.
Wako Mtani wako
GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE ( Majina yangu Kamili ni Kalemera Rwigyema Mazimpaka Kadogoo )