Mtanzania Anarudishwa Bongo Kutoka Marekani. Ana USD 10,000 (23M Tshs) Tu. Mnampa Ushauri Aitumieje?

usd 10,000 nyingi sana Le mutuz alirudi na usd 1000.
 
Kutokujua cha kufanya anaporudi nyumbani ndio changamoto kubwa ya wanadiaspora wote wanaoamua kurudi Tz. Wapo ambao hurudi na elimu na utaalam ambao huwasaidia vyema kuanzisha biashara ama kuekeza fedha zao kwa utaratibu mzuri.

Kwake ndugu yetu inakuwa ngumu kumshauri anze vipi kwasababu hatumjui utaalam na uzoefu alionao. Sio vyema kumshauri cha kufanya kwa kuwa wengi wanaofanikiwa huwa wanafanya wanachokijua katika kujikwamua na changamoto zinazosababishwa na uchumi wa Tz.

Biashara, kuwekeza ama kufanya ujasiriamali ni baadhi tuu ya maeneo ambayo mtu mwenye mtaji ama asiyekuwa nao huwa anawaza kujiingiza. Ila kitu kibaya zaidi katika maisha ni kukosa wazo sahihi la kujiendeleza na ndio maana nyenzo kubwa katika kufanikiwa ni maarifa na uthubutu kuhusu mtaji ni kitu cha pili na cha maana sana katika kutafuta mafanikio.

Ningeshauri bwana mdogo aende benki yoyote inayotoa ushauri wa kibiashara akapata kushauriwa namna ya kuwekeza au kifungua biashara kitaalam na wajuzi wa mambo katika sekta ya fedha.
 
24m ni mtaji mkubwa kama ana akili ya kijasiriamali. Kuhusu atafanya nini inategemea na yeye mwenyewe. Aje atulie asome mchezo atajua aanzie wapi.
Kitendo cha kusoma mchezo 10m inakuwa imeshakatika. 24m ni mtaji mdogo sana wamachinga wengi wanao huo mtaji kwa sasa. Mambo yamebadilika sana Tanzania, watu wana pesa sana. Ukitoka nje na 24m ni kuja kuteseka tu ni ngumu kutoboa maana watu siku hizi wanajua kuchungulia fursa siyo kama zamani.
 
Ha ha ha.
 
Kama ni dereva anunue bajaji apige kazi boss yeye mwenyewe.atunze chombo vizuri.
Bajaji ni mkoa wowote inalipa na atajiamlia mwenyewe muda gani apumzike?
 
Hiyo mbona ni hela ya mboga mkuu, milioni 23 hajui azitimiaje? Ndo maana imeonekana hastahili kuendelea kuishi huko
 
Kama anategemea pia hiyo pesa kuanzia maisha kama kupanga nyumba na matumizi mengine haitatosha
 
Asije na cash huko huko states atafute used iphone au computer ashuke nazo bongo za kutosha

Ajichanganye k/ko makumbusho lazima zitoke
 
Ushauri wako ni WA kimotiveshno speaker zaidi aisee una mpoteza huyu
 

Yaani ulichobaki nacho [emoji1369]ni laptop + usd2500 nyingine sahau kabisaa mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…