Mtawaficha wote ila siyo GENTAMYCINE, haya Tangazeni upesi kuwa na Kipa wenu Mnata mmemuadhibu kama mlivyomuadhibu Mkude

Mtawaficha wote ila siyo GENTAMYCINE, haya Tangazeni upesi kuwa na Kipa wenu Mnata mmemuadhibu kama mlivyomuadhibu Mkude

Walipewa muda wa Udhuru wao na kutakiwa Kurejea Kambini Wao kwa Ujeuri ( Kipa Metacha Mnata na Kiungo Jonas Mkude ) wakarudi muda walioutaka Wao na Kocha Gamondi akawafukuza na kutowahitaji katika Kikosi chake na hatimaye Uongozi kuamua Kuwaadhibu ndani kwa ndani.

Na taarifa ya uhakika niliyonayo GENTAMYCINE ni kwamba Kipa Mnata na Kiungo Mkude ambao kwa pamoja walipewa Mkataba wa mwaka Mmoja Mmoja ukiisha hawatoongezewa tena na Shughuli yao itakuwa imeishia hapo kwa Kuichezea Yanga SC.

Haya Wazee wa Kukopi Taarifa zangu GENTAMYCINE hapa JamiiForums akina Ricardo Momo, Edo Kumwembe na wale Bloggers, Watangazaji wa Michezo na Wachambuzi chukueni na hii na tambeni nayo ila msisahau tu kutoa Credits Kwangu GENTAMYCINE na huu Mtandao wangu pendwa na tukuka wa JamiiForums sawa?

Mtawaficha Wote ila siyo Mimi sawa? Makipa walioko Kambini sasa ni Djigui Diarra, Abdultwalib Mshery na Yule Dogo wa Team B tu.

Mimi ndiyo GENTAMYCINE The King!!!!!
Unapenda umbea kama mwanamke wa uswahilini.
 
Mnata na mkude walisimamishwa kwa muda kwa utovu wa nidhamu lakini wamesharudi kambini wanaendelea na mazoezi
 
Mnata na mkude walisimamishwa kwa muda kwa utovu wa nidhamu lakini wamesharudi kambini wanaendelea na mazoezi
Kwanini mlifanya Siri wakati mengine huwa Mnashoboka wenyewe Kututangazia?
 
Mnaficha nini Kutangaza ili ijulikane wakati Wachezaji husika hawafanyi Mazoezi na Wenzao hivyo kuleta Sintofahamu kwa Mashabiki wenu?

Si huwa mnasema Nadanganya? Haya ipingeni / ikataeni basi na hii Taarifa yangu. Kudadadeki zenu...!!

Mimi ndiyo GENTAMYCINE The King!!!!
Kwani mambumbumbu wenzako lini walitangaza adhabu za wachezaji wao?

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom