Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
Lipo suala moja muhimu ambalo halijajadiliwa hapa kuhusiana na nini JK atagusia, nalo ni juu ya kazi ya bunge la katiba.
Tangia bunge hili maalum lianze kikao, na hata kabla kidogo, kumekuwepo mjadala mkali unaohoji mamlaka ya bunge hilo juu ya rasimu ya katiba iliyowasilishwa na tume. Katika mijadala hii, wapo waliojadili kwamba bunge hili lina mamlaka ya kubadilisha na hata kuondoa chochote itakachoridhia, huku upande mwingine wa hoja ukijadili kwamba hilo haliwezekani. Makada wengi wa ccm wamekuwa kwenye upande unaojenga hoja kwamba bunge hili lina uwezo wa kubadilisha na hata kuondoa vifungu mbalimbali vitakavyo ridhiwa; nadhani Kikwete atagusia hili, huku akiegemea kwenye hoja ya makada wa ccm;
Ukweli unabakia wazi kwamba bunge la katiba halina mamlaka ya kubadili rasimu kama ilivyowasilishwa na tume ya mabadiliko ya katiba. Kuna tatizo moja kubwa:
Kifungu cha 25(2) kikisomwa kwa kiingereza kinaweka suala hili la bunge kutokuwa na mamlaka hiyo lakini tafsiri yake kwa kiswahili ndio imetoa upenyo kwa wavurugaji kuingiza siasa zao. Pamoja na haya, ujumbe wa kifungu hiki kisheria ni kwamba- rasimu hii, kama itakavyowasilishwa na tume ya mabadiliko ya katiba ndiyo itakuwa msingi wa utekelezaji wa madaraka ya bunge katika kutengeneza/kuandika katiba mpya; kwa maana hii:
Kinachoweza kufanywa na bunge la katiba ni kuboresha au kuongeza hapa na pale lakini bila ya kuathiri msingi mkuu wa rasimu hiyo. Hivyo rasimu inabakia kuwa ndiyo mhimili mkuu wa katiba mpya inayotarajiwa;
Nimejaribu verify uelewa wangu huu na wataalam wa sheria, wanasema nachojadili ni sahihi na kuongeza kwamba vinginevyo, bunge la JMT lilitunga sheria ambayo haikulipa bunge la katiba mamlaka ya kubadili vifungu vya rasimu kwa jinsi inavyofaa; na iwapo bunge la JMT lingekuwa limetunga sheria hiyo, basi ingesemwa wazi kwani sheria huwa haipindi pindi mambo bali hunyoosha mambo, hivyo sheria ingetungwa na bunge la JMT kusema kitu kama:
Au sheria ingetumia maneno yanayofanania na haya; vinginevyo kwa jinsi sheria inavyotamka hivi leo, ukweli ambao hauepukiki ni kwamba rasimu ya katiba ilikusudiwa kuwa mhimili na msingi mkuu; tatizo lililojitokeza ni kwamba tume iliamua kutojifunga na matakwa ya chama, na huu ndio msingi wa porojo za sasa za kulitafutia bunge la katiba nguvu ambazo haizistahili;
Kuna hoja pia inayojadiliwa kwamba bunge la katiba kupitia kifungu 25(1) cha sheria husika kinalipa bunge hili mamlaka yasiyo na mipaka katika kujadili na hata kubadilisha vifungu vyote vya rasimu; kifungu hiki kinasema kwamba:
"Bunge la katiba litakuwa na mamlaka ya kutengeneza katiba mpya na kutengeneza vifungu vitakavyohusiana na ufanyaji kazi wa katiba hiyo."
Katika hili, nimepata nafasi ya kumsoma wakili peterr kibatala ambae anasema:
Kuna suala lingine muhimu kibatala anajadili kuhusiana na sintofahamu kubwa inayoweza tokea iwapo BLK litafanya kosa linalopigiwa debe na makada wa CCM:
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Tangia bunge hili maalum lianze kikao, na hata kabla kidogo, kumekuwepo mjadala mkali unaohoji mamlaka ya bunge hilo juu ya rasimu ya katiba iliyowasilishwa na tume. Katika mijadala hii, wapo waliojadili kwamba bunge hili lina mamlaka ya kubadilisha na hata kuondoa chochote itakachoridhia, huku upande mwingine wa hoja ukijadili kwamba hilo haliwezekani. Makada wengi wa ccm wamekuwa kwenye upande unaojenga hoja kwamba bunge hili lina uwezo wa kubadilisha na hata kuondoa vifungu mbalimbali vitakavyo ridhiwa; nadhani Kikwete atagusia hili, huku akiegemea kwenye hoja ya makada wa ccm;
Ukweli unabakia wazi kwamba bunge la katiba halina mamlaka ya kubadili rasimu kama ilivyowasilishwa na tume ya mabadiliko ya katiba. Kuna tatizo moja kubwa:
Kifungu cha 25(2) kikisomwa kwa kiingereza kinaweka suala hili la bunge kutokuwa na mamlaka hiyo lakini tafsiri yake kwa kiswahili ndio imetoa upenyo kwa wavurugaji kuingiza siasa zao. Pamoja na haya, ujumbe wa kifungu hiki kisheria ni kwamba- rasimu hii, kama itakavyowasilishwa na tume ya mabadiliko ya katiba ndiyo itakuwa msingi wa utekelezaji wa madaraka ya bunge katika kutengeneza/kuandika katiba mpya; kwa maana hii:
Kinachoweza kufanywa na bunge la katiba ni kuboresha au kuongeza hapa na pale lakini bila ya kuathiri msingi mkuu wa rasimu hiyo. Hivyo rasimu inabakia kuwa ndiyo mhimili mkuu wa katiba mpya inayotarajiwa;
Nimejaribu verify uelewa wangu huu na wataalam wa sheria, wanasema nachojadili ni sahihi na kuongeza kwamba vinginevyo, bunge la JMT lilitunga sheria ambayo haikulipa bunge la katiba mamlaka ya kubadili vifungu vya rasimu kwa jinsi inavyofaa; na iwapo bunge la JMT lingekuwa limetunga sheria hiyo, basi ingesemwa wazi kwani sheria huwa haipindi pindi mambo bali hunyoosha mambo, hivyo sheria ingetungwa na bunge la JMT kusema kitu kama:
Bunge la katiba halitafungwa kwa namna yoyote ile na rasimu ya katiba
Au sheria ingetumia maneno yanayofanania na haya; vinginevyo kwa jinsi sheria inavyotamka hivi leo, ukweli ambao hauepukiki ni kwamba rasimu ya katiba ilikusudiwa kuwa mhimili na msingi mkuu; tatizo lililojitokeza ni kwamba tume iliamua kutojifunga na matakwa ya chama, na huu ndio msingi wa porojo za sasa za kulitafutia bunge la katiba nguvu ambazo haizistahili;
Kuna hoja pia inayojadiliwa kwamba bunge la katiba kupitia kifungu 25(1) cha sheria husika kinalipa bunge hili mamlaka yasiyo na mipaka katika kujadili na hata kubadilisha vifungu vyote vya rasimu; kifungu hiki kinasema kwamba:
"Bunge la katiba litakuwa na mamlaka ya kutengeneza katiba mpya na kutengeneza vifungu vitakavyohusiana na ufanyaji kazi wa katiba hiyo."
Katika hili, nimepata nafasi ya kumsoma wakili peterr kibatala ambae anasema:
Namna bora ya kutafsiri vifungu vya 25(1) na (2) ni kuvipa uhai vifungu vyote viwili bila ya kuathiri kimojawapo kiasi kwamba kisiwe na maana kabisa. Hii ina maana kwamba ilikuwa lazima kifungu cha 25(1) kiwepo ili kulipa bunge mamlaka kujadili rasimu na kuliongezea nyama inapobidi - kisheria tunaita enabling provision au substantive provision.
Kifungu cha 25(2) unaweza sema ni kifungu elekezi cha namna ya bunge kutekeleza mamlaka yake (procedural provision) - maelekezo yanayojumuisha mipaka ya mamlaka hiyo.
Mipaka na mamlaka ni sehemu muhimu ya mamlaka ya chombo chochote cha kisheria kwani huelezea wapi uhalali wa mamlaka husika huishia.
Kifungu hiki cha 25(2) kitashirikiana a kanuni za bunge katika kuweka misingi ya bunge kufanya kazi zake za kujadili rasimu ya katiba.
Ukiacha tafsiri ya kifungu husika ambacho kinaweza kubishaniwa, namna nyingine ya kutafsiri sheria ni kuangalia mazingira yaliyozunguka kifungu cha sheria husika.
Mchakato wa kuandaa rasimu ulianza kwa tume kukusanya maoni ya wananchi na kisha kuandaa rasimu ya kwanza. Rasimu hiyo ikafanyiwa kazi kwa njia ya kupatiwa mabaraza ya katiba na njia nyingine na kisha tume ikachukua maoni kutoka huko na kuandaa rasimu ya pili ambayo ndiyo hii iliyopelekea bunge kujumuika tayari kuijadili. Swali kuu la msingi ni:
Je, michakato yote hii ya awali iliyojumuisha wananchi moja kwa moja ilikuwa na maana gani iwapo tena kila kitu kinaweza kufumuliwa kwa kadri ya utashi wa bunge la katiba?
Hapa siyo sahihi kusema kwamba michakato yote miwili inapumuliana na kubebana (complement each other).
Na pegine ni mchakato upi unaowapa wananchi sauti ya moja kwa moja katika katiba mpya kati ya rasimu iliyosheheni maoni yao na bunge la katiba ambalo halijachaguliwa moka kwa moja na wananchi; na wala wananchi hawana namna yoyote ile ya kulidhibiti?
Mtu anaweza kuja na hoja kwamba bunge la katiba linajumuisha wabunge waliochaguliwa moja kwa moja na wananchi, na hivyo wanawakilisha maoni yao;
Hoja hii ingekuwa na nguvu iwapo maelekezo ya mchakato mzima kwa mujibu wa sheria yangekuwa kwa tume kukusanya maoni na kuandaa rasimu na kisha kuyawasilisha katika bunge la JMT na baraza la wawakilishi ili yajadiliwe na kisha kupelekwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya maoni.
Mchakato wa namna hii ambao binafsi ningeupendelea zaidi ungebakisha umiliki wa mchakato mzima na hasa rasimu yenyewe na hatimaye katiba, moja kwa moja kwa wananchi;
Huu ungefanana na njia ambayo wenzetu wa Kenya walipitia, ambapo ile rasimu maarufu kama rasimu ya Bomas (Bomas Draft) ndio ulikuwa msingi mkuu wa majadiliano bungeni (bunge la kawaida) kabla ya kufikishwa kwa wananchi kwa kura ya maoni.
Kuna suala lingine muhimu kibatala anajadili kuhusiana na sintofahamu kubwa inayoweza tokea iwapo BLK litafanya kosa linalopigiwa debe na makada wa CCM:
Tufikirie tu kwa mfano bunge la katiba linaamua kwamba linaweza kubadilisha vitu vyote vya msingi katika rasimu na katiba inapelekwa kwenye kura ya maoni na kupitishwa na baadae mahakama inasema tafsiri sahihi ya sheria ni kwamba rasimu haikutakiwa kubadilishwa na bunge la katiba.
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums