Mtazamo kuhusu Hotuba ya JK kuzindua Bunge Maalum la Katiba

Mtazamo kuhusu Hotuba ya JK kuzindua Bunge Maalum la Katiba

Wazanzibari inabidi wajue wanachokitaka, hawawezi kulinda mapinduzi kwa kutumia mabavu. Waulizwe kama wao wanautaka muungano.
Watanganyika hatujali na wala sioni jinsi uamuzi utakavyoathiri maisha yetu. Ila tu, shirikisho si jambo halali kwa watanganyika.
Hatuwezi kuwa na senate ambayo uwezekano wa kubadilika kwa idadi ya maseneta upo chini ya serikali shirikishi. Hapo Warioba kachemsha vibaya sana. Na hatutaki kuwa na serikali moja itayobeba mzigo wa ulinzi na usalama bila manufaa yeyote ya kiuchumi.Serikali moja, nchi moja.
serikali moja haiwezekani. Tanganyika walikubali kwa miaka 50. Zanzibar wamekataa 2010 kwa katiba, maandishi yapo.

Serikali 2 haziwekani, Tanganyika wamechoka kubeba mzigo. Hata katika mazingira yaliyopo bado mzigo wa ulinzi na usalama tunaubeba kikamilifu. Hata siku moja hutasikia wznz wakizungumzia suala hilo. Ni mara chache tu wameongelea kwanini mkuu wa majeshi hatoka znz. Hiyo ndiyo hoja muhimu sana kwao.

Kwanini serikali 3! ni kwamba kutakuwa na mshirika atakayeongea na znz. Kwasasa hivi znz wanajificha katika koti la muungano. Si kwa ulinzi na usalama bali mambo mengi sana. Ingawa wanasema Tanganyika imejificha.

Kwa mfano, wizara ya elimu ya juu ipo znz kwa wznz, na ile ya muungano ipo kwa wote. Wizara ya afya ipo znz kwa wznz na ile ya muungano ni ya wote n.k.

Hapo Dodoma kipengele wanachokisubiri ni cha kugawana madaraka na nafasi za kazi. Kipengele cha gharama watakimbia ukumbini kwasababu hilo haliwahusu.

Upo uhalali wa wao kukimbia kwasababu katika serikali 2 wao wapo kwa mchango wa herufi za jina Tanzania.
Tatizo ni kwa Watanganyika, nani atawasemea? Mzee Mwanakijiji kaliongelea katika uzi wake vema sana.
 
Last edited by a moderator:
RAIS KIKWETE AFANYIA KAZI MANENO YA KUSIKIA

Katika kumnanga mh Warioba Rais Kikwete amesema 'nimesikia wapo wanaohoji takwimu za tume kutokana na watu waliotoa maoni.....' sisi tunasema tunayosikia.

Rais wa nchi ana vyombo vyote vya dola. Anapoongea huwa na mamlaka kwakuzingatia anazo taarifa za uhakika.
Alichokiongelea Dodoma ni maneno ya kusikia nai napofikia mahali Rais anajadili maneno ya kusikia bila kujua inatisha, inasikitisha

Ujumbe wake ni kuwa CCM watumie hoja hizo kumpinga Warioba.
Alisema ni wakati wajumbe wa bunge waangalie takwimu hizo. Hivi waangalie nini ambacho Rais hakijui na hakukijua?

Rais aliunda tume mwenyewe, akaapisha tume, akapokea rasimu ya kwanza. Kisha akahamasisha watu kushiriki katika mabaraza ya kata. CCM wakapeleka watu wengi kutoa maoni kwa kuongozwa.

Mgogoro bungeni ulihusu namna ya kupata wajumbe wa mabaraza. Rais akasaini mswada uliopitishwa kwa akidi ya wabunge 100, 220 wakiwa hawamo bungeni.

Akapigwa picha akipokea rasimu ya mwisho. Amekaa na rasimu miezi miwili akisubiri kupata idadi ya wajumbe wa kuteuliwa.Akatangaza majina na kuitisha bunge la katiba.

Katika mlolongo wote hakuna hata siku au sehemu aliyowahi kuhoji kuhusu idadi yawaliotoa maoni.
Rais ni kiongozi wa kwanza kuisoma rasimu. Hivi ina maana hakuweza kubaini hilo hadi Ijumaa alipokuja kuelezea bungeni kuwa 'amesikia'.

Well, wengi watashangaa lakini jibu ni moja, Kikwete hakuwa na majibu sahihi ya hoja za tume ya Warioba. Alichokifanya ni kuokoteza hoja na kuzikuza hata kama alipaswa kuzijua pengine kuliko mtu yoyote.

Alipoanzisha mchakato alikuwa na hadidu rejea(terms of reference) alikuwa na washauri wa kisiasa, kijamii na kiuchumi.Leo hakuwatumia katika kuandaa mchakato anakuja na kauli za mitaani 'wapo wanaosema'

Sijui kama watu wangesema tume ya Warioba amenukuu katiba ya misri Rais angekuja kueleza doubt zake! si 'amesikia'?

Taasisi ya urais inapewa kila fursa kwa gharama zote kwa maana moja, ili itimize majukumu yake kikamilifu.

Tunarudia, alichokusudia ni kuvuruga mchakato kwa kumsumanga, kumdhalilisha na kumfedhehesha Mzee Warioba, mzee Salim, Jaji Ramadhami na wenzake.

Kwa hili historia haitamwacha na itaandikwa kwa bunge hili kuvunjika.
Ni nani aliyebaki na heshima tena kama wazee wetu akina Butiku ndio hao wamevuliwa mavazi mbela ya TV?
 
Mjumbe huwa hauwawi.

Ninajaribu kuchanganya akili zangu naza kuambiwa kama Rais Kikwete anavyopenda kusema. "Akili za kuambiwa changanya naza kwako"

Nimekumbana na hili andiko la Mzee Warioba ambalo linanipa angalizo kuwa inawezekana Mzee Warioba anachokisema kilichoko ndani ya Rasimu ya pili ya Katiba hakiamini ila anawakilisha mawazo ya wengine kwa vile ndiye Mwenyekiti wa tume. Tusije tukawa tunauziwa mchezo wa kisiasa na sisi tunanunua bila kufahamu!.

Haya mahojiano yamefanyika tarehe 10/10/2011 baada ya Katiba ya Zanzibar kufanyiwa marekebisho ya kumi (10) katika kutekeleza Azimio la Baraza la Wawakilishi kuhusiana na Muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Yasije yakawa ndiyo yale yake ya Mzee Sitta na CCM!.
Jaji Warioba: Tusidanganyane, kutaka Serikali tatu ni kuvunja Muungano

Naamini Tume yetu ikiwa na wajumbe kutoka vyama vya siasa haitakuwa huru. Nadhani utaratibu wa Katiba mpya utuwezeshe kupata maoni ya wananchi.

Ninachokiona sasa ni kila kundi kwa maslahi yake linatumia hoja ya wananchi kuwa wanataka utaratibu fulani. Vivyo hivyo, Serikali nayo inataka kuweka mipaka fulani kwa maslahi ya wananchi.

Tusiweke mipaka. Wananchi watoe mawazo yao. Kuna vyama vya siasa vinasema kwa manufaa ya wananchi tuwe na Bunge la Katiba ambalo litachagua Tume na kutoa hadidu za rejea na kusimamia mchakato na baada ya kupitisha watakwenda kwa wananchi.

Sikubaliani na hilo. Wananchi waachwe wazungumze yote wanayotaka, Katiba yao iweje. Wakishakuzungumza, hiyo tume itengeneze muswada wa katiba urudi kwa wananchi. Wazungumze, kusiwe na kikundi hapa katikati kinasema kwa manufaa ya wananchi. Hapana.

Wananchi wazungumze muswada na chombo cha kupitisha kipitishe baadaye. Wasilete vikao hapa katikati huku wanajitafutia nafasi. Mchakato huu uende moja kwa moja kwa wananchi. Tusiwawekee mawazo.

Kuna wanaharakati wanataka kuleta mambo ya kuwajaza wananchi. Nina hakika wananchi wakiachiwa uhuru, watasema na wataalamu watapanga vizuri. Nasisitiza la msingi ni kuwaacha wananchi waseme wanataka nchi ya namna gani.
Suala la Muungano pia liwe katika Katiba. Tusipokuwa makini kwa maneno yanayozungumswa sasa tutavunja Muungano.
Muungano huu una misingi yake na upo kwa manufaa ya wananchi. Tufafanue manufaa hayo ni nini kwa mwananchi wa kawaida.

Wakati wote kwa mwananchi wa kawaida, kumekuwa hakuna matatizo ya Muungano. Matatizo yanatoka kwenye midomo ya viongozi.
Shughuli za wananchi wa kawaida haziangalii orodha ya mambo ya Muungano, bali haki yao kama raia. Wanajiona ni raia katika shughuli zao za kibiashara au nyingine. Mwananchi wa kawaida anaona anayo haki ya kufanya biashara mahali popote. Wananchi wamezoa hivyo. Msiwafikishe mahali wakajiona kuwa kwenda Zanzibar au kuja Bara inabidi wafuate taratibu za kwenda Kenya au Uganda.

Tunayo matatizo ya madaraka, kwamba unazo Serikali mbili kwa hiyo yale yaliyomo kwenye orodha ya Muungano ni kuonyesha Serikali hii ina madaraka gani. Wanagombania madaraka.
Kama suala ni mafuta au mengine tuzungumze. Inategemea mnavyokubaliana, tusije kuongeza au kupunguza kwenye orodha mambo ambayo yatakuja kuwatenganisha wananchi. Kama kwa mfano, kuna watu wanafikiri kuimarisha Muungano ni kuwa na serikali tatu, unaimarishaje?

Sasa hivi kiini ni ugomvi wa madaraka kati ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar. Hivi ukileta serikali tatu, ugomvi huu hautakuwapo? Ukileta Serikali ya Tanganyika yenyewe haitadai madaraka? Mwisho wataomba madaraka hadi Serikali ya Muungano isiwe na chochote.

Hivi Serikali ya Tanganyika kwa mfano ikawapo, ikataka iwe na wimbo wake wa Taifa, bendera yake, nembo yake, kisha inadai ifanye biashara ya nje, unafikiri tutakuwa tumefika wapi?
Ni kwamba tutakuwa tunaondoa Muungano na kurudisha Tanganyika na Zanzibar. Lakini kama wananchi wanataka hivyo, sawa.


Lakini tukivunja Muungano madhara yake ni makubwa sana kwa pande zote mbili. Mimi naamini wale wanaotaka serikali tatu wanajua nia yao ni kuvunja Muungano na huu ndio ukweli. Ukianzisha serikali tatu, maana yake unavunja Muungano.
Kwa Habari zaidi soma hapa,

Siasa za Tanzania siyo kama tuzijuavyo wapita njia!.
 
Mjumbe huwa hauwawi.

Ninajaribu kuchanganya akili zangu naza kuambiwa kama Rais Kikwete anavyopenda kusema. "Akili za kuambiwa changanya naza kwako"

Nimekumbana na hili andiko la Mzee Warioba ambalo linanipa angalizo kuwa inawezekana Mzee Warioba anachokisema kilichoko ndani ya Rasimu ya pili ya Katiba hakiamini ila anawakilisha mawazo ya wengine kwa vile ndiye Mwenyekiti wa tume. Tusije tukawa tunauziwa mchezo wa kisiasa na sisi tunanunua bila kufahamu!.

Haya mahojiano yamefanyika tarehe 10/10/2011 baada ya Katiba ya Zanzibar kufanyiwa marekebisho ya kumi (10) katika kutekeleza Azimio la Baraza la Wawakilishi kuhusiana na Muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Yasije yakawa ndiyo yale yake ya Mzee Sitta na CCM!.

Kwa Habari zaidi soma hapa,Siasa za Tanzania siyo kama tuzijuavyo wapita njia!.
Warioba naweza kusema hivyo,lakini haiondoi ukweli kuwa kuna tatizo la muungano. Wala haiondoi ukweli kuwa wananchi wengi walipendekeza hivyo.

Kwa maneno mengine maoni ya tume kwa namna yoyote yatakuwa yanasigishana miongoni mwa wajumbe/ Lakini je, waliongozwa na takwimyu kufika hapo walipo? jibu ni yes.

Hakuna shaka kuwa muungano waliouacha waasisi si huu tulio nao. Kwasasa tuna muungano kama alama lakini si uhalisia.
Huwezi kuwa na znz yenye kila kitu kama nchi ukasema tuna muungano.
Huwezi kuwa na waziri mkuu asiye na kazi znz ukasema tuna muungano
n.k n.k

Muhimu hapa si maneno ya kila mtu, ni hoja za wananchi. Narudia hicho ndicho walichosema katika mbaraza mengi.
Pamoja na hayo kama Warioba alikwenda kinyume na hadidu rejea, je iilikuwa sahihi kwa Rais kwenda kumsumanga kiasi hicho?
 
Hiyo Makala ya Raia mwema,iliyo muhoji mzee Warioba kipindi cha nyuma....kabla ajawa mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba!nimeamini huyu mzee ni mzalendo,sababu hii kaamua kuwathilisha maoni ya wananchi,sio yake...ukisoma makala yote unaona Warioba anapenda Serikali mbili,ila ameona wengi wataka tatu kakubali
 
Hiyo Makala ya Raia mwema,iliyo muhoji mzee Warioba kipindi cha nyuma....kabla ajawa mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba!nimeamini huyu mzee ni mzalendo,sababu hii kaamua kuwathilisha maoni ya wananchi,sio yake...ukisoma makala yote unaona Warioba anapenda Serikali mbili,ila ameona wengi wataka tatu kakubali

Niseme tena, ilikuwa kosa kubwa sana kwa ccm kuvunja Tume ya kuratibu maoni na kuwazuia wajumbe wake wasio sehemu ya bunge maalum la kuandaa katiba mpya. Hii ni kwa sababu ccm na hasa ccm wa Tanzania bara walio Dodoma are out of touch, hawana hata chembechembe ya uhalisia na ndio maana wanaongea kama 'dinosaurs'. Tume imekutana na wananchi, ime-experience hasira, kelele za wananchi. Wao ccm Dodoma wamebaki kuimba zilipendwa!

Zanzibar wamebadilisha katiba na kujiira nchi, ccm Tanzania bara wanakenua meno! Watanzania wenye asili ya bara huko Zanzibar wanapiga foleni kuomba vitambulisho ili waishi walau kwa muda Zanzibar, hawa ccm wa bara washangalia kama ma-bar medi.

Sasa hivi Mtanzania mwenye asili ya bara akitaka kuomba kitambulisho cha ukazi Zanzibar anachunguzwa kwanza tabia yake na hata akipata kitambulisho bado atakuwa anabaguliwa. Ni lini wapemba wa Kariakoo au wale wenye maduka Namanga Dar wamechunguzwa tabia ili waendeshe maduka yao? Wabunge wa ccm Tanzania bara wataendelea kufumbia macho huu udhalilishwaji wa raia wa Bara hadi lini?
 
Warioba naweza kusema hivyo,lakini haiondoi ukweli kuwa kuna tatizo la muungano. Wala haiondoi ukweli kuwa wananchi wengi walipendekeza hivyo.

Kwa maneno mengine maoni ya tume kwa namna yoyote yatakuwa yanasigishana miongoni mwa wajumbe/ Lakini je, waliongozwa na takwimyu kufika hapo walipo? jibu ni yes.

Hakuna shaka kuwa muungano waliouacha waasisi si huu tulio nao. Kwasasa tuna muungano kama alama lakini si uhalisia.
Huwezi kuwa na znz yenye kila kitu kama nchi ukasema tuna muungano.
Huwezi kuwa na waziri mkuu asiye na kazi znz ukasema tuna muungano
n.k n.k

Muhimu hapa si maneno ya kila mtu, ni hoja za wananchi. Narudia hicho ndicho walichosema katika mbaraza mengi.
Pamoja na hayo kama Warioba alikwenda kinyume na hadidu rejea, je iilikuwa sahihi kwa Rais kwenda kumsumanga kiasi hicho? Na kama ni mpabh

Wananchi wengi wala hawajapendekeza Serikali tatu, infact ni kinyume chake, katika Watu laki tatu waliohojiwa na tume katika mambo mbalimbali ya tume, Elfu thelathini na Tisa tu sawa na asilimia 10 ndiyo waliokuwa Interested na ishu ya Serikali ziwe ngapi!, HII INAONYESHA DHAHIRI ASILIMIA TISINI YA WATANZANIA KWAO MUUNDO WA SASA WA MUUNGANO SIYO ISSUE!.

Na kwa Takwimu za Tume kule zanzibar Asilimia 24 wanataka serikali mbili, asilimia 13 wanataka serikali moja na Asilimia 61 wanataka serikali ya Mkataba. KUMBE HATA KULE ZANZIBAR HAKUNA MTU HATA MMOJA ANAYETAKA SERIKALI TATU STYLE YA WARIOBA, SASA NI VIPI USEME SERIKALI TATU NI MAONI YA WANANCHI WALIO WENGI?- LABDA KWA WALE WALIOLIZUNGUMZIA SUALA LA SERIKALI NGAPI, KAMA UNAANGALIA BARA HAPO SAWA LAKINI SI ZANZIBAR!. Sasa tukiwalazimisha Wazanzibari serikali tatu "Style ya Warioba" si ni kuwaonea?.

Basi angalau Wanaotaka serikali mbili kule Zanzibar ni Asilimia 24, lakini hii ya Warioba hakuna Asilimia hata moja!
 
ALIYOYASAHAU RAIS KIKWETE

Mara ya mwisho kwa jaji warioba na rais kikwete kukutana katika suala la katiba mpya ilikuwa ni kwenye makabidhiano ya ripoti ya tume kwa rais kikwete na rais shein kwenye viwanja vya Karimjee, miezi mitatu tu iliyopita (december 30, 2013). Katika tukio hilo la kihistoria, picha mgando na video zipo zikionyesha jinsi gani viongozi hawa wawili wakiwa na furaha kwamba taifa sasa lilikuwa linaelekea kuzuri - kupata katiba itokanayo na wananchi. Katika hili, jaji warioba alitamka haya:

...Sura tano za mwanzo za rasimu ya katiba zinatokana na mchango mkubwa kutoka kwa wananchi, hasa kuhusu misingi ya taifa,tunu za taifa, maadili na miiko ya uongozi, dira ya taifa na haki za binadamu. Wananchi pia wametoa maoni mazito kuhusu uongozi na utawala wa nchi, ikiwa ni pamoja na nafasi ya wawakilishi wa bungeni.

Katika hotuba yake ya juzi, Kikwete hakuona umuhimu wa kujadili haya zaidi ya lile la wawakilishi. Katika hili, Kikwete alimsikia vizuri sana warioba siku ile pale karimjee na alielewa kwamba ni wananchi ndio waliopendekeza kwamba wabunge wapewe kikomo cha vipindi vitatu. Lakini juzi Kikwete akajadili suala hili kama vile ni wazo la warioba. Katika hili, Kikwete alitumia muda mwingi sana kuienga hoja kwamba ubunge ni grooming ground ya viongozi wa kitaifa, kwahiyo mapendekezo ya "warioba" ya ukomo wa vipindi vitatu vitazuia hilo lisitokee. Binafsi sikuwa convinced na hoja hii kwamba njia pekee ya kutengeneza viongozi wa kitaifa ni ya ubunge; hakuna scientific explanation juu ya hili zaidi ya siasa tu; isitoshe, moja ya matukio ambayo yalimfanya baba wa taifa Nyerere kuanza kung'aa kama kiongozi wa kitaifa ni pale alipokataa kuwa mbunge maslahi/mbunge wa kutumikia wanasiasa; Kama njia ya kupunguza kasi ya TANU, serikali ya kikoloni ilimteua Nyerere kwa mjumbe wa baraza la kutunga sheria (bunge) Julai 1957; aliyemteua alikuwa ni Gavana Twining; lakini baada ya miezi chini ya sita na baada ya kuhudhuria vikao viwili tu vya bunge lile, nyerere aliamua kujiuzulu kwa vile nafasi ile haikuwa na manufaa yoyote kwa wananchi ikiwa mfumo ulikuwa ni mbovu; hali hiyo tunayo leo - mfumo mbovu unaofanya wabunge wawe ni wala posho tu za walipa kodi huku wakitumika kama rubber stamp; mwalimu katika hotuba yake ya kujiuzulu alitamka haya:

I have given everything that was in my power to give and what I have given has been rejected; I came to the council expecting a little of the spirit of give and take. That spirit is not there. I would feel that I am cheating the people and cheating my own organization if I remained on the council receiving allowances and attending sundowners as an Honorouble Member, giving the impression that I was still of the service to the council when in fact I know that I am useless. I had therefore no alternative but to tender my resignation and to ask that my resignation take effect from Friday 14th December 1957, the day my last compromises were rejected by Government.

Source: Towards Ujamaa: Twenty Years of TANU Leadership, Gabriel Ruhumbika (1974).

Hapa, nyerere alikuwa amekataa kutumika kama wabunge wa ccm juzi waliokuwa wanaruka kwa shangwe na kucheza mdundiko kumshangilia Kikwete katika suala ambalo mwalimu 1957 angeenda kinyume chake - nalo ni "kukataa kutumikia status quo kwa kusaliti wananchi";

Tukiachana na mfano wa Nyerere, pia wapo viongozi kama kina Salim Ahmed Salim ambao Nguruvi3 amewajadili. Salim hajawahi kuwa mbunge wa aina ambayo kikwete anaijadili (wabunge wa jimbo) lakini bado wanabakia kuwa ni moja ya viongozi ambao historia itawaweka kama miongoni mwa viongozi bora waliopata kutokea; mifano mingine ipo mingi - mzee pius msekwa, huyu hajawahi kuwa mbunge wa aina anayojadili Kikwete; hata leo hii, watu kama asha rose migiro, umaarufu wao ni kupitia ubunge wa kulazimisha, sio kutokana na matakwa ya wananchi; kwa kifupi, hoja kwamba kuweka kikomo cha vipindi vya ubunge kutazuia taifa kupata viongozi ni hoja ya kisiasa na isiyokuwa na tija kwa taifa;

Sambamba na hoja hii, Kikwete pia alijadili madhara yatakayojitokeza iwapo mawaziri watakoma kutokana na wabunge, kwamba shughuli zitakuwa haziendi kwa vile wabunge hawatakuwa na fursa ya kuwahoji au kubadilishana mawazo na mawaziri kwa ufanisi kama ilivyo sasa ambapo mawaziri ni sehemu ya wabunge; katika hili, Rais Kikwete hakuweza kuelezea faida za mawaziri kutotokana na wabunge, ambazo ni nyingi na tume ilizijadili kwa kina; ukiangalia hasara zilizowasilishwa na Kikwete juu ya hili kisha ukafananisha na faida zilizowasilishwa na tume kisha kufanya a cost-benefit analysis ndogo tu utabaini kwamba the benefits outweighs the costs;

Hotuba ya Jaji Warioba Karimjee wakati akikabidhi ripoti ya tume kwa Rais Kikwete na Rais Shein Desemba 30, 2013 ilihudhuriwa na viongozi wakuu wa kitaifa, marais wastaafu, mawaziri wakuu wastaafu pamoja na mabalozi wa nje. Karibia wote hawa walikuwepo Dodoma pia. Katika hafla ile ya karimjee, warioba alisema haya:

Hii ni mara ya kwanza kwa nchi yetu kuwashirikisha kwa ukamilifu wananchi katika kutunga katiba ya nchi yao. Nia ya mchakato huu ni kupata katiba inayokubalika na wananchi. Ili katiba ikubalike na wananchi ni jambo la msingi maoni yao yapewe uzito unaostahili. Nayasema haya kwa sababu tangu rasimu ya kwanza itolewe maneno yaliyopewa uzito na wananchi hayakupewa uzito katika mijadala ya viongozi, wasomi na vyombo vya habari.

Katika hotuba yake juzi, Kikwete alianza vizuri kwa kurudia maneno haya kwamba mchakato huu tofauti na nyuma umehusisha wananchi moja kwa moja; Lakini kitendo cha Kikwete baadae kuja kujadili yaliyomo kwenye rasimu kama vile ni ya warioba inatoa tafsiri mbili: kwanza aidha Kikwete hajaisoma vizuri rasimu ile na badala yake amesomewa na wasaidizi wake; au warioba yupo sahihi anaposema hapo juu kwamba. "tangu rasimu ya kwanza itolewe maneno yaliyopewa uzito na wananchi hayakupewa uzito katika mijadala ya viongozi, wasomi na vyombo vya habari."

Kuna uwezekano kwamba maneno yaliyopewa uzito na wananchi hayajapewa uzito katika mijadala ya viongozi wa CCM, na hii ndio sababu kubwa kwanini ccm imekuwa na mtazamo kwamba rasimu hii ni ya warioba, na sio ya tume ya katiba iliyoteuliwa kwenda kusikiliza maoni ya waanchi;

Kikwete na CCM wamepuuza kabisa maneno ya warioba siku ile karimjee kwamba:
Utangulizi wa katiba unaeleza kuwa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania imetungwa na wananchi wa Tanzania; utangulizi unatoa taswira na picha halisi ya jamhuri ya muungano na watu wake, historia yao, matarajio yao, misingi ya taifa na masuala muhimu ambayo wananchi wanataka kuyaendeleza katika jamii, kizazi hadi kizazi.

Kwa kauli ya Kikwete juzi, tusitarajie yafuatayo kutimia baada ya mchakato wa katiba kumalizia:

"utangulizi ambao utatoa taswira na picha halisi ya jamhuri ya muungano na watu wake, historia yao, matarajio yao, misingi ya taifa na masuala muhimu ambayo wananchi wanataka kuyaendeleza katika jamii, kizazi hadi kizazi."

Katika hotuba yake juzi, Kikwete alijadili suala la serikali tatu kama vile tume ya katiba ililipendekeza bila ya kuweka maandalizi pamoja na misingi ya uendeshwaji wake; Kikwete anasahau kwamba katika hotuba ya Warioba pale Karimjee, Warioba alisema yafuatayo:

Sura ya kumi na saba inapendekeza muda wa mpito wa miaka minne, kuazia tarehe ya kuanza kutumika kwa katiba mpya hadi tarehe 31 Disemba 2018; katika kipindi hicho sheria zilizopo hivi sasa zitaendelea kutumika hadi zitakapobadilishwa. Sheria zinazotumika Tanzania bara zitakuwa za Tanganyika na sheria zinazotumika Tanzania bara na zanzibar zitakuwa sheria za jamhuri ya muungano. Yapo pia mapendekezo kuhusu masuala ya kufanyiwa kazi katika muda wa mpito. Mambo haya ni pamoja na:

1. Kutungwa kwa katiba ya Tanganyika.
2.Kurekebisha katiba ya zanzibar ya mwaka 1984 ili kuwiana na masharti ya katiba ya jamhurir ya muungano wa Tanzania ya mwana 2014.
3.Mgawanyo wa rasilimali baina ya serikali ya jamhuri ya muungano na serikali za nchi washirika.
4.Kuundwa kwa tume na taasisi za kikatiba zilizoanishwa kwenye katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania mwaka 2014 na kwa kuzingatia masharti ya katiba hiyo;
5.Kufanya maandalizi na kuendesha uchaguzi mkuu wa mwaka 2014 kwa kuzingatia masharti ya katiba ya jamhuri ya muungano ya mwaka 2014; na
6. Kufanya maandalizi ya mambo yote muhimu kwa ajili ya utekelezaji bora wa masharti ya kikatiba yaliyomo kwenye katiba ya jamhuri ya muungao wa Tanzania ya mwaka 2014.

Aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya, Kikwete hakugusia kabisa maelezo haya ya warioba aliyoyatoa miezi mitatu tu iliyopita, licha ya Kikwete kurudia mara kwa mara kwamba ameisoma sana rasimu husika.

Inaendelea bandiko linalofuata...



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Inatoka bandiko #68


Kati ya mambo muhimu yaliyowasilishwa na tume ambayo Kikwete alishindwa kuyajadili kwa hoja, na kwa kiasi fulani kuyakwepa ni haya yaliyojadiliwa na warioba pale karimjee wakati wa kumkabidhi Kikwete Rasimu:

Eneo jingine ni mgongano kati ya katiba ya muuungano na katiba ya zanzibar. Katiba ya zanzibar ya mwaka 1984 imeweka masharti kwamba sheria zinazotungwa na bunge la jamhuri ya muungano hazitatumika zanzibar hadi zipelekwe kwenye baraza la wawakilishi. Aidha kodi itakayoamuliwa na bunge kutozwa na serikali ya muungano lazima ipate ridhaa ya baraza la wawakilishi zanzibar.

Mambo haya yameleta mgongano wa kikatiba. Juhudi zilizofanywa na pande zote mbili hazikufanikiwa kuondoa mgongano huo. Zaidi ya hapo, mabadiliko ya katiba ya zanzibar yaliyofanywa mwaka 2010 yametamka wazi kwamba zanzibar ni nchi kati ya nchi mbili za muungano wakati katiba ya jamhuri inaelekeza kwamba Tanzania ni nchi moja; mabadiliko ya katiba ya zanzibar pia yamehamisha baadhi ya madaraka ya serikali ya muuungano kwenda zanzibar.

Kitendo cha Kikwete kutoligusia suala hili kinafaya hoja zake zote juu ya mfumo wa muungano, hasa kupinga serikali tatu, kuwa hoja zisizokuwa a mashiko kwani katiba ambayo aliapa kuitetea na kuilinda imevunjwa "on his watch", na katika hotuba yake juzi, umma ulikuwa unamtarajia asimame pale kama rais wa Jamhuri ya muungano kwa kujadili hilo lakini mwisho wake alikuwa anaongea (pengine bila kujijua) kama rais wa Tanzania bara kuliko wa Jamhuri kwani yapo masuala aliyogusia ambayo hakuwa na mamlaka ya kuyagusia, bali ni ya Rais Shein ingawa yalikuwa yanahusu wananchi wa Tukuyu; hili limeacha gumzo kubwa sana mtaani;

Hata kama kuna mikakati ya chini kwa chini kuishawishi zanzibar kubadili vipendele tata kwenye katiba yake ya 2010, ccm haiwezi kufanikiwa katika hilo, na haya yalisemwa vyema sana na jaji warioba pale karimjee mbele ya rais, miezi mitatu iliyopita:

Wakati wa kukusanya maoni ya wananchi, Tume ilibaini kwamba haitakuwa rahisi kubadili katiba ya zanzibar kuifanya zannzibar kuonekana kuwa sehemu ya jamhuri ya muungano badala ya kuwa na sura ya nchi kamili; mabadiliko ya aina hiyo yatahitaji kura ya maoni kama katiba ya zanzibar inavyoelekeza; kwa tathmini ya tume, baada ya kuwasikiliza wananchi wa zanzibar, ni dhahiri kwamba pendekezo la kuifanya zanzibar isionekane kama nchi halitakubaliwa kwenye kura ya maoni.

Kikwete alilisikia hili, na lazima nafasi yake kitaasisi ina taaifa hizi, lakini cha ajabu ni kwamba, juzi katika hotuba yake hajaligusia suala hili ipasavyo huku ukweli ukibakia kwamba bila ya uangalifu, ni suala hili ndio litapelekea Tanganyika kurudi kwa gharama yoyote ile;

Ni vigumu kubaini ccm na serikali yake zitatatua vipi mgogoro huu wa kikatiba kwa kung'ang'ania serikali mbili ambazo zinaendesha nchi mbili - Ya Tanzania bara na Ya Zanzibar;

Kikwete alijadili vyema sana kwamba sasa muda wa kuendelea kuweka viraka kwenye katiba ya 1977 umeisha, taifa sasa linahitaji katiba itakayotatua migogoro yote iliyopo; lakini muda sio mrefu, Kikwete akaanza kupingana a hoja yake mweyewe pale alipoanza kujenga hoja kwamba serikali mbili ndio ufumbuzi pekee wa matatizo yaliyopo; hapa alisahau kwamba anaposema serikali mbili, asipoijadili katika muktadha wa nchi mbili za sasa, hoja yake nzima inakosa mashiko;

Katika hili, Kikwete alimsikia vizuri sana jaji warioba pale karimjee miezi mitatu tu iliyopita kwamba:

Kwa kifupi tathmini yetu ni kwamba ukarabati mkubwa unahitajika ili kuendelea na muundo wa serikali mbili; maeneo mawili makubwa yanahitaji mabadiliko; jambo la kwanza ni kuwa na mambo ya kutosha kwenye orodha ya muungano, ikiwa ni pamoja na mambo ya maendeleo na kiuchumi; jambo hili likifanyika, litazidisha malalamiko kwa upande wa zanzibar kuwa hadhi na madaraka yake yanazidi kupotea; aidha, mambo ya muungano yakipunguzwa sana serikali ya muungano itakuwa inashughulika zaidi na zaidi na mambo ya Tanganyika; na zanzibar itaona Tanganyika ndio muungano; lakini kwa upande mwingine Tanganyika nayo itaona si haki nayo isiwe na uhuru wa kuendesha mambo yake kama ilivyo kwa zanzibar.

Jambo la pili ni kuondoa mgongano na mgogoro wa kikatiba; hiyo maana yake ni zanzibar kubadili katiba yake ili zanzibar na Tanganyika ziwe ni sehemu za nchi moja badala ya kuwa nchi kamili; kama zanzibar na tanganyika zikiwa nchi kamili haitawezekana nchi moja ikawa na hadhi na uhuru wake na nchi nyingine isiwe na uhuru (autonomy) wake.

Kwa tathmini ya tume, tunaona ukarabati huo ni mgumu. Hii ndiyo sababu kubwa ya kupendekeza muundo wa serikali tatu ili pande zote ziwe na hadhi sawa; kila upande utashughulikia mambo yasiyo ya muungano na serikali ya muungano itabaki na mambo machache ya msingi ambayo yanaungaisha taifa.

Hii ni hoja ya msingi sana ambayo Kikwete alijadili kwa hoja za pembejeo na vifaru; akasahau kwamba pale karimjee, warioba alisema kwamba

Kuhusu ulinzi na usalama, sura ya kumi na tano inatamka kwamba jukumu la ulinzi na usalama wa jamhuri ya muungano ni la kila raia. Kwa kuzingatia maoni ya wananchi waliyoyatoa katika mabaraza ya katiba, rasimu sasa inapendekeza kuwepo kwa jeshi la polisi moja na idara ya usalama moja kutoka katika jamhuri ya muungano wa Tanzania;

Hivyo vifaru alivyojadili kikwete ni vigumu kuelewa alikuwa anazungumzia vifaru chini ya amiri jeshi mkuu yupi kati ya amiri jeshi mkuu wa vikosi vya ulinzi na usalama zanzibar ambae tayari yupo (Shein) kufuatia katiba ya znz 2010 au amiri jeshi mkuu wa vikosi vya ulinzi na usalama wa Tanzania bara iliyovaa koti la muungano; vinginevyo kwa mapendekezo ya tume, suala hili halitakuwa na matatizo yoyote; lakini hata kama aayosema kikwete yatajiri, mlinzi wa kweli wa muungano ni wananchi, kwani iwapo ni wao watakaounda muungano, basi wataulinda kwa hali na mali, na hata hivyo vifaru na bunduki vitafikia mahali vitaachia ridhaa ya wananchi itawale;

Nimalizie kwa nukuu kutoka kwa mzee Jumbe kwenye kitabu chake "The Partnership: Muungao wa Tanganyika na zanzibar, miaka 30 ya dhoruba, 1995, UK 115:


Haikujitokeza kwenye akili ya Karume na mashahidi wake watatu kujiuliza kwanini Tanganyika ambayo Katiba yake ilikuwa na uzuri wa kutosha wa kuazimwa na kutumikia serikali ya muungano, Tanganyika ikiwa na taasisi zake imara na kada za wafanyakazi wazoefu, kama vile kwa upande wa zanzibar, isiweze kuachiwa kuendesha mambo yake yale yasio ya muungano.

Hiyo ndio ingelikuwa ni njia rahisi, ya kueleweka. Kutumia katiba ya Tanganyika kwa ajili ya serikali ya muungano na kuazisha taasisi zote zihitajikanazo kwa uendeshaji wake na kutenga kabisa taasisi na kada ya wafanyakazi wa Tanganyika ili kuitumikia Tanganyika kama ilivyo Zanzibar yenye taasisi zake kamili na kada yake ya wafanyakazi;

Labda kulikuwa kuahitajika ujanja zaidi katika kuficha udanganyifu uliokuwa umeingizwa ndani ya katiba. Baada ya kuhakikisha kuwa ameweka msingi kwa hatua yake ya kwanza, mpangaji wa njama hizo akachukua haraka hatua yake ya pili.

Hatua ya pili anayozungumzia jumbe ni ujio wa sheria za muungano siku moja tu baada ya mkataba wa muungano kusainiwa, sheria ambazo ziliundwa kinyemela ili kuvunja nguvu mkataba wa muungano kama ndio legal foundation ya muungano; sheria hii ndio ilijenga mazingira ya kuja kuifanya katiba ya TANU kuwa ni sehemu ya katiba ya muda ya JMT ya 1965; ni uchakachuaji huu ambao ulikuwa ni kinyume na mkataba wa muungano, ndio unaipa ccm kiburi leo hii kupuuza maoni ya wananchi juu ya mfumo wa muungano wanaoutaka;

Maneno ya jumbe hapo juu ni muhimu sana katika harakati za kuzindua Tanganyika;


Bila ya Tanganyika, Tanzania Haiwezekani Kwani Tanzania ni Kwanza lakini Tanganyika ni Kabla.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Hiyo Makala ya Raia mwema,iliyo muhoji mzee Warioba kipindi cha nyuma....kabla ajawa mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba!nimeamini huyu mzee ni mzalendo,sababu hii kaamua kuwathilisha maoni ya wananchi,sio yake...ukisoma makala yote unaona Warioba anapenda Serikali mbili,ila ameona wengi wataka tatu kakubali

Naunga mkono hoja; hiki kitendo kimempa heshima kubwa sana jaji warioba kwani alionyesha msimamo wake awali (serikali mbili) lakini baadae akaweka msimamo wake huo pembeni na kusikiliza wananchi wanasema nini;

CCM ilitakiwa nayo ifanye hayo hayo aliyofanya jaji warioba; Chama kitakuja kujuta muda sio mrefu kwamba warioba kama kada wake, alikijengea mazingira mazuri sana ya kurudisha imani yake kwa wananchi; chama kimepoteza fursa hii muhimu ambayo kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi, hatimaye serikali yake kwa mara ya kwanza ingepata uhalali wa kuongoza nchi kwa mujibu wa katiba itokanayo na wananchi, kitu ambacho hakijawahi kutokea; uhalali wa ccm kutawala leo unatokana na mabakibaki ya vyanzo vikuu vifuatavyo:

1. Historia ya TANU na CCM ya kabla ya 1992, ya kutetea wanyonge wa ndani na nje ya nchi; this source of legitimacy is gone by the wind, na wakulaumu ni ccm wenyewe kwani leo chama kinatetea wale wenye nguvu wa ndani (matajiri na mafisadi) na wa nje ya nchi (wawekezaji).

2. Azimio la arusha ambalo liliweka utaifa kwanza (kwa dhati, sio porojo za ilani ya uchaguzi), huku wananchi wakiwekwa at the centre/heart ya mikakati yote ya maendeleo kiuchumi na kijamii; just as the above source of legitimacy [see item (1)], this source too is gone by the wind na wakulaumu ni ccm yenyewe ambapo 1992, iliua azimioa la arusha na kuleta azimio la znz ambalo kimsingi, sasa linatumika kama kichaka cha ufisadi na kujilimbikizia mali ya umma; hata nyerere aliwahi sikika akishangaa hili kutokea tena bila hata ya kuambiwa;

3. Source ya tatu ya legitimacy wakati ule ilikuwa ni charisma & integrity ya Mwalimu; leo mwalimu hayupo, na wala hakuna dalili kwamba kuna viongozi ndani ya ccm watakaoweza kuvaa viatu vyake;isitoshe, viongozi wa aina hii leo wanachukuliwa na makada wa ccm kama wasaliti na maadui, hivyo juhudi zao za kutafuta uongozi zitapigwa vita na fitina za kila aina;hawataweza pita michakato ya uongozi ccm;

Wakati wa nyerere umma haukujali sana katiba kwa sababu hizo hapo juu, lakini katika mazingira ya sasa ya mfumo wa vyama vingi, the only source of legitimacy ambayo itapelekea taifa kuwa na amani na utulivu ni katiba mpya, na katiba hiyo ikitokana na wananchi, the ruled and rulers won't have any other options bali kuishi kwa kuizingatia; vinginevyo wananchi kamwe hawawezi kulinda kitu ambacho hawajakitengeneza; it won't happen;

Kikwete ameenda bungeni juzi huku serikali na chama chake kikiwa na legitimacy ya kutawala ambayo haitokani na katiba ya nchi bali mabakibaki ya masuala hayo hapo juu;

Kitendo cha kikwete kuridhia mchakato wa katiba kilikuwa ni muhimu na cha kishujaa kwani hatimaye ccm ingekuwa na fursa ya kujenga uhalali wa kutawala kwa njia ya katiba kama chanzo cha uhalali utawala wake;

Kikwete angeshauriwa vizuri sana na mapema kabisa - baada ya idara ya usalama, washauri wake wa masuala ya siasa, uchumi na kijamii kumueleza uhalisia wa mambo 2010, hasa baada ya katiba mpya ya znz kupitishwa, wangemueleza mapema kabisa kwamba mzee hali ni ngumu kwani hoja ya serikali tatu haikwepeki tena, kwahiyo ni sawa ccm iendelee na msimamo wake wa serikali mbili lakini chama kiseme kwamba iwapo maoni ya wananchi kupitia mabaraza ya katiba yatasema kitu tofauti, basi ccm itayazingatia maoni hayo kwa kuzingatia mazingira yaliyopo. Kitendo hiki kingeipa ccm mtaji mkubwa sana wa kisiasa na kukiwezesha chama kuaminiwa na umma hata kama kingekuja na msimamo baadae (kwa hoja) kwamba migogoro iliyopo inatatulika chini ya serikali mbili; ni kweli uamuzi huu ungaugawa umma lakini bado ccm ingebakisha a good number of votes for 2015;vinginevyo ccm imepoteza fursa hii, na hili litakigharimu sana chama kwenye uchaguzi mkuu ujao, hasa katika majimbo ya mijini (kura za urais na ubunge); maeneo ya vijijini yataendelea kuipa ccm uhalali wa kutawala kupitia mabakibaki ya three sources of legitimacy nilizojadili hapo juu, lakini kwa mijini, the major source of legitimacy ya uongozi wa ccm na serikali yake itakuwa ni katiba itokanayo na wananchi;

Kinachofanyika ndani ya ccm sio sustainable for the party na pia si stable for the country; the tred shows kwamba by 2025, karibia majority ya wananchi watakuwa wanaishi mijini - hawa watakuwa wapiga kura kwa kigezo cha katiba kama source of legitimacy kwa serikali na chama husika; kwa mwendo huu, ccm itakuwa inaendesha siasa za "mabakimabaki" in terms of legitimacy and eventually dissapear in the political grave yard ya Tanzania; the year is 2025 iwapo katiba ya kiccm itadumu, au just after 2015 iwapo katiba ijayo ya ki ccm haitadumu;

Katika hali hii "HAKITADUMU CHAMA CHA MAPINDUZI";




Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
....

Nadhani kuna sehemu kubwa sana ya katiba hii ambayo wote tunafunga macho kuitazama, na tunaweka mawiwo na machewo kwenye sehemu moja tuu ya katiba nayo ni muungano. Hii inaweza kuleta madhara makubwa sana.

Ndiyo maana watu waliotegemea madhara haya walishauri....muafaka juu ya wa Muungano upatikane kwanza kabla ya kufikiria Kutunga Katiba mpya.Ilitakiwa ipigwe kura ya maoni, wananchi waamue kama wanataka muuungano ama la, kama wangekubali kuwa wanataka muungno ilitakiwa ipigwe kura nyingine ni muundo upi wa muuungano wanautaka. baada ya hapo tufikirie Kutunga katiba mpya.
 
Wananchi wengi wala hawajapendekeza Serikali tatu, infact ni kinyume chake, katika Watu laki tatu waliohojiwa na tume katika mambo mbalimbali ya tume, Elfu thelathini na Tisa tu sawa na asilimia 10 ndiyo waliokuwa Interested na ishu ya Serikali ziwe ngapi!, HII INAONYESHA DHAHIRI ASILIMIA TISINI YA WATANZANIA KWAO MUUNDO WA SASA WA MUUNGANO SIYO ISSUE!.

Na kwa Takwimu za Tume kule zanzibar Asilimia 24 wanataka serikali mbili, asilimia 13 wanataka serikali moja na Asilimia 61 wanataka serikali ya Mkataba. KUMBE HATA KULE ZANZIBAR HAKUNA MTU HATA MMOJA ANAYETAKA SERIKALI TATU STYLE YA WARIOBA, SASA NI VIPI USEME SERIKALI TATU NI MAONI YA WANANCHI WALIO WENGI?- LABDA KWA WALE WALIOLIZUNGUMZIA SUALA LA SERIKALI NGAPI, KAMA UNAANGALIA BARA HAPO SAWA LAKINI SI ZANZIBAR!. Sasa tukiwalazimisha Wazanzibari serikali tatu "Style ya Warioba" si ni kuwaonea?.

Basi angalau Wanaotaka serikali mbili kule Zanzibar ni Asilimia 24, lakini hii ya Warioba hakuna Asilimia hata moja!
Wananchi wengi ni idadi gani?
Unajua siasa za muungano zilivyo bara. Wangapi walijua kuwa znz imevunja katiba ukiwemo wewe.

Nina uhakika hukujua, hivyo mtu wa Simiyu znz kwake si issue. Hii haina manaa anakubaliana na mfumo, hapana! Maana yake ni kuwa hajui kodi yake inakwenda kumhudumia mzanzibar, hajui anabaguliwa znz. Mwammko uliopo ndio unawasha moto.

Wengi ukiwemo hawakujua kua tunahitaji ruhusu ya BLW ili kujenga vyoo vya shule zetu.

Hao wa Mkataba kutoka znz wameulizwa waeleze mkataba ni nini na unafanyaje kazi.
Maalim Seif, Ahmed Rajab, Jusa Ismail ambao ni vongozi wa mkataba hawajaweza kusema hata neno moja.

Hao wznz wanaotaka mkataba ni wale waliotaka serikai 3 kupitia CUF. Kwa vile wengi wanamfuata maalim hata kama anakwenda chooni matokeo ndiyo yakawa mkataba.

Mkataba hauelezeki ni ujinga. Hatuwezi kusema kitu tusichojua maana yake halafu ukadhani watu watakubali.

Mkuu, wewe na JK tunaomba takwimu mkituonyesha kitu tofauti na Warioba
 
....
Hao wa Mkataba kutoka znz wameulizwa waeleze mkataba ni nini na unafanyaje kazi.
Maalim Seif, Ahmed Rajab, Jusa Ismail ambao ni vongozi wa mkataba hawajaweza kusema hata neno moja. ...
Mkuu, inasemekana walijibu hivi


........

Nilikuwa siielewi dhana ya Muungano wa Mkataba, bahati nzuri nimeipata, hiyo, hapo chini. Kwa haraka haraka nilichokigundua kama kweli haya ndiyo maoni ya watu wote wa Zanzibar, basi, wazanzibar hawataki Muungano. Tanzania Bara tujiandae kutengwa, nasisitiza, kama kweli Muungano wa Mkataba ndiyo hitaji hasa ya Wazanzibari.


"...Baada ya kuukataa muundo wa Muungano wa Katiba, wanatoa hii dhana ya mfumo ulio tofauti kabisa yaani mfumo wa Muungano wa Mkataba. Wengi Visiwani hivi sasa wanaiunga mkono dhana hii ambayo pengine ndio yenye suluhisho bora na mujarab kwa Muungano.

Mahusiano yatayojengwa kwa Mkataba yatairejeshea Tanganyika na pia Zanzibar mamlaka yao kamili ya kidola na yatawezesha kuwapo na utaratibu wa ushirikiano kati ya nchi mbili zilizo sawa na zilizo huru na zenye mamlaka kamili ya kidola.


Mkataba utaoongoza mahusiano hayo utaweka wazi ni mambo gani nchi hizo zitashirikiana na namna ushirikiano wao wa baadaye utavyokuwa.
Pale nchi iliyo na mamlaka yake kamili inapoandikiana mkataba wa kuwa na ushirikiano au muungano na nchi nyingine inakuwa haiyapotezi mamlaka yake au uhuru wake. Hali hiyo ni kinyume na Muungano wa kikatiba uliopo sasa ambao umeifanya Zanzibar iyahaulishe kwenye Serikali ya Muungano mamlaka na madaraka yake ya kimsingi.Zanzibar imezitoa mhanga nguvu zake za kidola wakati mwenzake Tanganyika haikulazimika kujitosa na kutoa mhanga kama huo kwa vile utawala wa Tanganyika unaendeshwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano.


Jambo jingine lenye kuvutia panapokuwako ushirikiano au muungano wa Mkataba ni kwamba kila nchi iliyotia saini mkataba wa muungano inakuwa na nguvu ya ‘turufu’. Hivyo hata katika mambo yaliyokubaliwa kuingizwa katika ushirikiano nchi inayohusika inaweza kuitumia nguvu yake ya turufu na ikaomba hifadhi ya watu wake endapo inahisi kwamba inahatarishwa na sera za huo muungano katika utekelezaji wa mahusiano na ushirikiano wa nchi hizo.


Muungano wa aina hiyo, yaani wa Mkataba, utairejeshea Serikali ya Umoja wa Kitaifa mamlaka na madaraka muhimu ambayo Zanzibar haikuwa nayo kwa muda wa miaka 48. Yakitumiwa vyema madaraka hayo yataiwezesha Zanzibar kutekeleza sera zitazoirejeshea Zanzibar adhama na fahari iliyokuwa nayo zamani na kuifanya ishiriki kikamilifu katika shughuli za kanda ya Afrika ya Mashariki na ya Kati na hata kupindukia mipaka ya kanda hii.


Raia Mwema - Tofauti ya Muungano wa Katiba na wa Mkataba
 
KIKWETE AMEPOTOSHWA NA WASHAURI WAKE KUHUSU TAKWIMU ZA TUME YA WARIOBA JUU YA MFUMO WA MUUNGANO

Kuna takwimu za tume ya katiba ambazo juzi Rais Kikwete aliziwasilisha ambazo kimsingi waliompatia maelezo hayo aidha hawana utaalam wa "statistics" au wameamua kuingiza siasa katika "statistics"; hii sio ajabu kwa Taifa letu kwani hata uchumi umekuwa ukitumikia siasa throughout; na hata katika formation of the union, the process was fraught with legal manipulation and political expediency bila ya kujalisha costs encountered kwa wananchi;

Kwa vile kada maarufu wa CCM humu jamvini Gamba la Nyoka amerudia tena upotoshaji huu ambao kimsingi umeidhahalisha tume ya warioba iliyo sheheni wasomi na watalaam wa masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na fani ya takwimu, nikiwa ni mmoja wa wananchi wanaounga mkono mapendekezo ya tume kwa vile yanaakisi maoni ya wananchi, nimeona niliweke hili sawa na katika mahali pake for good ili tujadili mengine ya maana. Awali hapa jamvini, Gamba la nyoka alirudia takwimu za Kikwete, nanukuu:
Gamba la Nyoka" post=9036019]Wananchi wengi wala hawajapendekeza Serikali tatu, infact ni kinyume chake, katika Watu laki tatu waliohojiwa na tume katika mambo mbalimbali ya tume, Elfu thelathini na Tisa tu sawa na asilimia 10 ndiyo waliokuwa Interested na ishu ya Serikali ziwe ngapi!, HII INAONYESHA DHAHIRI ASILIMIA TISINI YA WATANZANIA KWAO MUUNDO WA SASA WA MUUNGANO SIYO ISSUE!.

Na kwa Takwimu za Tume kule zanzibar Asilimia 24 wanataka serikali mbili, asilimia 13 wanataka serikali moja na Asilimia 61 wanataka serikali ya Mkataba. KUMBE HATA KULE ZANZIBAR HAKUNA MTU HATA MMOJA ANAYETAKA SERIKALI TATU STYLE YA WARIOBA, SASA NI VIPI USEME SERIKALI TATU NI MAONI YA WANANCHI WALIO WENGI?- LABDA KWA WALE WALIOLIZUNGUMZIA SUALA LA SERIKALI NGAPI, KAMA UNAANGALIA BARA HAPO SAWA LAKINI SI ZANZIBAR!. Sasa tukiwalazimisha Wazanzibari serikali tatu "Style ya Warioba" si ni kuwaonea?.

Basi angalau Wanaotaka serikali mbili kule Zanzibar ni Asilimia 24, lakini hii ya Warioba hakuna Asilimia hata moja!

Ni muhimu tukaacha upotoshaji, na kama ni upotoshaji usiokusudiwa basi kuna haja ya kuelewa unachozungumza kabla haujajenga hoja. Ikizingatiwa kwamba wananchi wengi ni illiterate katika suala zima la takwimu, upotoshaji huu ulioletwa humu jamvini na gamba la nyoka ni kitu cha hatari sana kwani ina maanisha kwamba pia unatumika katika kuwapa taarifa juu ya uchumi wao, rasilimali zao, kodi zao n.k; hii ni hatari kwa mustakabali wa taifa.

Nikirudi kwenye hili juu ya takwimu za tume:

Based on "probability mathematics" hata kama jumla ya idadi ya watanzania ingekuwa haijulikani kwa tume ya warioba, it still wouldn't have been a problem kwani probability maths prove kwamba population size huwa sio a relevant matter, unless labda kama sample yako exceeds a few percent ya jumla ya idadi ya watu unayo examine; kwa maana hii, sample ya watu hata 500 (mia tano!) tu kwa mfano is equally useful katika kuchunguza maoni ya watu/wakazi hata 15,000,000 (milioni kumi na tano) kama ambavyo sample ya 500 ingefanikisha katika idadi ya watu 100,000 tu. Ndio maana ni kawaida kwa Survey Systems kupuuzia population size hasa pale idadi ya watu inapokuwa kubwa sana au pale idadi ya watu katika eneo husika inapokuwa haijulikani; sample ya watu elfu thelathini na tano ingekuwa ni issue only if population husika ingekuwa inajulikana kwamba ni ya kundi fulani maalum mfano wanachama milioni sita inaosemekana ni wa ccm, vinginevyo kutafuta maoni randomly, hata hao waliofikiwa na warioba na tume yake ni wengi kupitiliza.

Nisisitize tu kwamba,based on probability mathematics, sample ya watanzania hata elfu na mia tano kwa watanzania milioni 45 inatosha kupata jibu. Isitoshe, mchakato wa katiba hauishi na tume ya warioba au bunge la katiba kwani hatua ya mwisho ni kura ya maoni ambayo itajumuisha wananchi wengi zaidi; swali muhimu kwa kina Nape Nnauye (wasemaji wa chama) - Iwapo ccm ina uhakika kwamba watanzania walio wengi wameridhika na mfumo wa serikali mbili - kwamba 90% ya watanzania wanataka serikali mbili:

*Kwanini hotuba ya Kikwete jana ilitumia zaidi ya nusu ya muda wake kujadili suala la mfumo wa muungano?

*Kama ccm ipo sahihi na takwimu zake, kwanini isingesubiria kura ya maoni to prove tume ya katiba wrong badala ya kuishambulia tume?

Mwisho, based on my thread, hasa juu ya probability of mathematics, najua wapo watakaojenga hoja kwamba mjadala hapa ni demokrasia na kwamba kwamba demokrasia haiitaji mijadala ya probability. Napenda kuwaeleza wajenga hoja hii I advance kwamba, ili kuitendea haki demokrasia, scientific approaches zina nafasi yake na zimekuwa proven kutenda haki wakati wote.

Sio watanzania wote mtawadanganya kwa kuchakachua takwimu; jamii yetu ina wasomi na waelewa mambo ambao jukumu lao ni kuelimisha jamii kwa manufaa ya taifa; katika hili la serikali tatu, kamwe hatutarudi nyuma; jaji warioba hana haja ya kurudi mbele ya umma kujibu hoja. Pumzika mzee wetu warioba, hongera kwa kazi ya tume uliyoiongoza kwa mapenzi ya dhati kwa taifa lako. Vijanna wazalendo wa taifa hili tunaothamini mchango wako na tunaoheshimu sana maoni ya wananchi kwa kuvua itikadi zetu za chama, tupo wengi. Hii ni kwasababu, mkataba wa muungao (1964), hakuna sehemu unataja vyama vya TANU wala ASP.

Tutakufanyia kazi ya kujibu mapigo "kwa hoja" bila kuchoka kwani kufanya hivyo ni kuwa upande wa wananchi. Labda vifaru vitumalize.

TANZANIA KWANZA, TANGANYIKA KABLA.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Tujitegemee
Bandiko #73 linaeleza kwa ufupi dhana ya mkataba halielezi mkataba unahusu nini na kwanini, kwa faida gani.Wanaosema mkataba waje na mambo ya mkataba, hakuna anayeeleza mkataba ni wa jambo gani.

Wazanzibar wanasema mkataba utawarudishia mamlaka kamili . Nafasi ya kurudisha mamlaka kamili haipataikani kwa mkataba bali kujitoa katika muungano. Ni mamlaka gani wanayotaka zaidi ya ya katiba ya 2010?

Tatu, mkataba maana yake ni kuitumia Tanganyika katika mambo yanayowahusu.
Kwa mfano wznz wanataka mkataba ili wapate hifadhi ya ulinzi na usalama, ardhi na ajira.
Swali mktaba huo utawanufaisha vipi Watanganyika.

Nimeeleza kuwa mkataba wanaosema hawajaweza kuweka mambo husika, kuchukulia dhana hiyo na kuifanyia kazi ni sawa na pale nitakpokwambia 'Twende' bila kujua tunakwenda wapi.

Nne, Wanasema kila mwanachama atakuwa na kura ya turufu. Kura hiyo atakuwa nayo Tanganyika kwasababu yeye ndiye anayehitajika.

Tanganyika haiwezi kuwekewa kura ya turufu ikiwa haina mafao yoyote yale na mkataba.
Hivyo itaendelea ku-dictate terms and conditions za mkataba, ndiyo yenye uwezo na inaytotegemewa na znz


Tano, kuna sababu gani za kuwa na mkataba? Kwani tofauti ya mkataba na MoU ni ipi?
Tuna MoU na Msumbiji kupitia TAMOFA kwanini tusiwe na MoU na znz kupitia 'TAZOFA'?

Sita, kama tunahitaji Mkataba kwanini tusiende EAC tukakutana huko ambako tayari kuna mikataba badala ya kufanya mambo pekee yetu tukiwa nchi tofauti.

Hoja yangu inasimama kuwa kama wznz hawataweza kuweka mambo yanayohusu mktaba wazi, hatuwezi kuwasikiliza kwasababu wanatuambia twende bila kutuambia wapi.

Kwanini wznz wadhani wana hadhi, sifa na sababu za kuamua ushirikiano na Tanganyika na wala si Tanganyika ambayo znz si robo yake kwa kila kitu .


Hakuna sababu za mkataba kwasababu WAZANZIBAR HAWAJUI nini wanataka.
Wangalijua wanataka nini leo wasingepiga makofi wakati Mzee Warioba, Mzee Salim, Mzee Butiku, Mzee Augustino Ramadhani wanadhalilishwa na ksuimangwa mbele ya uso wa dunia.

Inashangaza sana akina Kificho, Jusa, Prof Sherrif, Seif Idd, Duni Haji n.k. ambao ndio wanaosimamia Mkataba, ni hao hao wanaokaa vikao na CCM kuhujumu jitihada za kuipata Tanganyika ambayo ingefungua milango kwa Zanzibar yenye mamlaka kamili.

Wabunge kutoka ZNZ nao wanashangaza sana. Wapo mstari wa mbele kuhujumu tume ya Warioba iliyowasikiliza na kuja na kitu kinachofanana na mkataba tena kwa takwimu na vielezo kwa kina na undani.
Tulitegemea wznz waungane na wapenda mabadiliko lakini wameamua kuwasaliti wznz wenzao na Tanzania kwa ujumla.

Huko nyuma tuliwashauri wznz kuwa, wapeleke mswada bunge la JMT kupitia wabunge wao wakidai ima kuvunjwa muungano au serikali 3 au vinginevyo. Tukawashauri wapeleke mswada BLW kuhusu malalamiko yao. Tukashauri wasusie tume ya Warioba ili kuhitimisha kazi mapema. Tukawashauri wasije Dodoma ili kazi iishe na malaka kamili yapatikane
Siku zote walisema vyombo vya dola vimewahujumu.

Nafasi imepatikana kupitia BMLK mbako wao peke yao wana uwezo wa kuzuia jambo lolote lile na hata kukataa uandikwaji wa katiba. Jambo la kushangaza ndio wapo mstari wa mbele kudai serikali mbili na kushangilia kwa nguvu tume ilipokuwa inadhalilishwa na Kikwete.

Kumbuka kuna wajumbe 15 waliokuja kwa masilahi ya Znazibar. Tanganyika haikuwa na wajumbe hivyo nafasi walikuwa nayo. Kitendo cha kushangilia kwa bidiii hotuba ya Warioba si kuwa kimeidhalilisha tume, bali kimedhalilisha wajumbe 15 kwamba nao wameshiriki katika kile CCM na JK wanakiita 'maoni binafsi ya Warioba'.
 
Mkuu Mchambuzi

Katika bandiko lako #74 umeeleza kwa hesabu maana ya sample size. Kitu cha kushangaza Rais ambaye anadai 'amesikia' na yeye kuzungumzia uvumi mbe ya TV hajaeleza ukubwa wa sample size iliyotakiwa ulikuwa uweje.
Hili swali hawezi kulijibu @Nape, Pinda, Mwigulu Nchemba na mkuu Mkandara

Wanachotaka kusema ni kuwa idadi ya waliohojiwa walitakiwa wawe watanzania wote wakiwemo vichanga kule wodi ya wazazi. Hawana ushahidi wa takwimu.

Inasikitisha sana kuona Rais wa nchi akishindwa kuwatumia wataalam wa Takwimu kumweleza nini kilipaswa kufanywa.
Inasikitisha sana maprofesa na wazee wenye busara zao katika tume wametusiwa na kudhalilishwa na Kikwete kiasi cha kwamba huenda wasifikirie tena kutokea hadharani.

Kikwete kama hakuwa na hoja, ingetosha kueleza kile anachokijua, kitendo cha kuzama na kwadhalilisha hawa wazee mbele ya vijana, akina mama, wazee n.k. ni kuwavunjia heshima sana. Anawatukana vipi ili hali yeye hana data?

Rais analitupia bunge la watu 600 jukumu la kuangalia data badala ya kuita wataalamu wampe ukweli. Tena anafanya hivyo akimtaja mzee Warioba kuhakikisha kuwa zile nguo chache alizovaa anamvua na mzee wa watu sasa hana la kusema tena. AMebaki akiumia maisha yake.
Kikwete, Nyerere alisema msipowaheshimu wazee hamtafanikiwa.
 
KIKWETE AKUBALI UVUNJWAJI WA KATIBA
ALA SAHANI MOJA NA WARIOBA, KAFUMBIA MACHO UHAINI


Ni jambo la kushangaza maongezi ya JK katika kuchangia rasimu hayakugusa suala moja nyeti sana, katiba.Tunafahamu uvunjwaji wa katiba ya JMT uliofanywa na wazanzibar, kujiundia nchi yao, majeshi yao, Amir jeshi wa majeshi, wimbo wao wa taifa na bendera.

Tunafahamu katiba ya 2010 ya znz inavyoeleza ukubwa wa katiba hiyo juu ya katiba ya JMT.
Kutokana na mambo hayo, yapo mengi yaliyotokea ambayo chanzo ni uvunjwaji wa katiba.

Hapa duru tunarudia tena, JK aliapa kuilinda katiba ya JMT. Kitendo cha kuachwa ivunje ni kosa la kikatiba. Nchi za wenzetu JK angekuwa yupo Chalinze pengine akijishughulisha na kampeni za mwanawe na si Urais.

Pamoja na uzito wa jambo hilo, JK amesikika akizungumzia kuhusu kupungua kwa kero kutoka 26 hadi 6.

Suala la katiba si kero, ni suala la kisheria ambalo Rais alipaswa kuliongelea na kulitolea ufafanuzi. Katika mambo yaliyowahi kufanyika na kuidhihaki katiba ya nchi hilo ni nambari moja.

Kwa mshangao kabisa, Rais akakaa kimya kuhusu tatizo hilo akiendelea kuaminisha watu kuwa suluhu ya kero inaendelea.

Tena katika kufanya hivyo JK akafumbia macho uvunjwaji wa katiba ili kuwafurahisha wazanzibar.
Hayo ameyafanya kwa gharama kubwa ya heshima ya tume ya Warioba.

Kama alivyosema, Warioba amefanya ABCD katika hali ya kuonyesha mzee wetu amefanya mambo kinyume na alivyoagizwa. Warioba ni waziri mkuu, alishakuwa makamu wa rais, ni mzoefu katika mambo ya sheria, alishakuwa mwanasheria mkuu n.k.

Ndivyo ilivyokuwa kwa wasaidizi wake akina Butiku, Salim Ahmed na Jaji Ramadhani
Pamoja, wapo waliobobea katika fani mbali mbali za sheria na maprofesa takribani watatu.

Kwenda na kusimama mbele ya bunge na taifa na kuwanyanyasa watu hawa kana kwamba Warioba hakujua afanye nini, au kuhoji takwimu kwa meneno ya mtaani, ni kitendo cha dhalili sana.

Kuna wakati bunge linaweza kuwahitaji wazee hawa kwa ufafanuzi.
Pamoja na Kikwete kuweka kikwazo kuwa wamemaliza kazi yao, sidhani kama wazee na wasomi hawa wanaweza kutokea mbele ya taifa kutokana na simanzi, aibu na dhalilili waliyofanyiwa na Rais.

Ikizingatiwa waliombwa kufanya kazi ya taifa, jambo la mwisho lilikuwa kudhalilishwa na aliyewatuma tena wakimpa habari kila hatua waliyofikia.

Katiba imevunjwa na wazanzibar, JK hakusema hata neno moja.
Hilo hakuliona ni muhimu au kubwa, alichokiona kikubwa taifa linachopaswa kusikia ni namna alivyomvuruga mzee Warioba kwa kumuwekea maneno kama ya majeshi, kumuonyesha mbabaishaji na kumdhalilisha bila Warioba kuwa na nafasi tena katika maisha yake ya kuweka kumbu kumbu sawa sawa.

Rais kuwashambulia wanatume na hasa kumlenga mzee Warioba akifumbia macho uvunjwaji wa katiba ifikiriwe endapo kweli ana nia njema na taifa.

Nia njema haipatikani kwa kumzomea, kumzushia na kuzogoa wazee kama akina Warioba, Butiku, Salim n.k. Nia njema si kuhoji weledi wa marofesa kama Baregu na Palamagamba Kabudi n.k.
Mardhiano ya kitaifa ni kuzingatia sheria, kama katiba inavunjwa rais akimshambulia Wariona inafikirsha.

Tusemezane
 
SAMWEL SITTA

FYI

Kuna uzi tulioongelea kwa uchache kuhusu Sitta kabla ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa BMLK.
Kutokana na mambo yalivyo tete na uwezekano wa bunge kuvunjika umeonelea ni vema wanajamvi wakapata nafasi ya kumjadili Sitta kuanzia historia yake , sasa na mtarajio ya siku zijazo.

Sitta ni mtu muhimu sana katika harakati mbali mbali za kitaifa, na hili la katiba ni mtu muhimu zaidi kwa hujuma za bunge- Dodoma.
Ni mtu anayeaminika lakini undani wake unatisha.

Tutakuwa na uzi tofauti unaomhusu kikamilifu.
Tafadhali ukisoma Duru za siasa usiache kuangalia links ikiwemo ya Sitta ili twende pamoja.
 
Back
Top Bottom