Mtazamo kuhusu Hotuba ya JK kuzindua Bunge Maalum la Katiba

Mtazamo kuhusu Hotuba ya JK kuzindua Bunge Maalum la Katiba

Mkuu Mkandara , naona umeamua kumuunga mkono JK kwa 'upofu' kwamba kipendacho roho hula nyama mbichi. Kwanza nikueleze hakuna kero 6 alizosema Kikwete, na kwa vile unaamini ni 6 tafadhali ziorodheshe hapa.

Pili, kama zilikuwepo 6 wznz wasingekuwa na malalamiko na wala hayo yasingejitokeza katika maoni ya wananchi na wala Watanganyika wasingekuwa na malalamiko.

Ndiyo, mtalazimisha, lakini hakuna amani huko makazini, mashuleni, vyuoni n.k.
Ni bora kukawepo utaratibu utakaoheshimiwa vinginevyo madole ya macho yataenda mbali.

Mkuu kama watu walisikiliza kwa makini hotuba ya JK inawezekana wengi walikuwa wanajiuliza what was going on in his mind.

Mimi siku zote msimamo wangu ni kuwa Muungano unatakiwa kuwa wa serikali moja tu, watanzania wote tumebe majuku sawa kwa nchi yetu. Kwa hali tuliyo nayo sasa ya serikali mbili, tunaelekea kuuvunja muungano. Ukisikia mtu anasema kuendelea na serikali mbili in its current form, or in a modified form which brings us a bit back, but not to where mwalimu na Mzee Karume left us, ni kudanganyana tu.

Nashindwa kuelewa ni kwanini watu hawataki kuelewa au kusikiliza kauli ya Mzee Warioba...kwamba kwa sasa tuna nchi mbili na serikali mbili, sio serikali mbili na nchi mmoja kama tyulivyoachiwa na Mwalinu Nyerere na Mzee Karume. Hii tayari ni recipe ya kuvunja muungano, kuing'ang'ania kwa sasa ni kutangaza wazi kuwa muungano unaelekea kufa. Kwa JK kusimamia hilo kimsingi ni sawa na kusema gairi hili bovu liende kwa rais mwingine, mimi siliwezi.

Kero za Muungano si kama ziko Zanzibar tu, zilizoko Zanzibar ni za uroho, lakini zilizoko bara ni genuine, serikali mbili in whatever modified form will not address them.
 
Unajuwa wengi wamekuwa watu wa kupenda watu wengine wafikirie kwa niaba yao na sio wenyewe kufikiria. Wengi wamekuwa wanalalamika na kunung'unika bla kujua wapi pa kuyasemea na wakipewa nafasi hawasemi sababu ya woga na nafiki.

Kumbukeni Juzi Kikwete amewadanganya sana pale Bungeni uwepo wa Serikali 3 na kupendekeza Serikali 2. Bila kujua kuwa kuna mengi Kikwete ameshindwa kutoa majawabu.

Kumbukeni Sera ya CCM inasema Serikali 2 na Chama Kimoja. Hii ni khatari kubwa sana. Na CCM hao hao wanatumia nguvu kubwa sana kulinda Sera yao ya Serikali 2 na chama Kimoja
.

Tukumbuke kuwa Sasa ni wakti wa Vyama vingi. Siku yoyote katika nchi yenu inaweza itokea Serikali 2 na vyama 2. je nchi itaendeshwaje. Hapo kikwete kashindwa kujibu hilo.

Tujaalie TGK ikashinda CCM na kuunda Serikali na ZNZ ikishinda CUF na kuunda Serikali
. Tukumbuke kuwa
RAIS wa Znz ni MEMBER KATIKA BARAZA LA MAWAZIRI JMTz, hivyo anaingia katika Vikao vyote vya baraza la mawaziri wa Muungano.

Je CCM hao watakubali Maalim Seif aingie katika baraza la mawaziri wa Muungano? Je Kikwete mbona hajalisemea hilo?.

WaZnz wameliona hilo zamani sana hususan katika chaguzi za 1995 na 2000 na 2005. JMTz inatumia nguvu zake zote kuhakikisha wanalinda SERA YA NCHI ya SERIKALI MOJA hivyo kuwafitinisha wa Znz kuuwana wenyewe kwa wenyewe kwa faida ya TGK.

Nakumbuka Maneno ya Mh Ahali ya Ismail Jussa " NCHI NI KAMA NYUMBA, CHAMA NI KAMA DUKA, KWA MWENYE AKILI HAWEZI WEKA RAHANI NYUMBA YAKE KWA KILO MBILI ZA SUKARI"

ZNZ KWANZA mengine badayn.
 
HATUNA TENA MUUNGANO, KILICHOBAKIA NI USHIRIKIANO

Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere Katika kitabu chake cha "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania", ukurasa wa 15, mwalimu anasema hivi:
Nchi mbili zinapoungana na kuwa nchi moja, mifumo ya kawaida ya miundo ya katiba ni miwili: Muungano wa serikali moja au shirikisho la serikali tatu.

Mwalimu anaendelea kufafanua kwamba - kwa muungano wa aina ya kwanza hapo juu (serikali moja), kila nchi inafuta serikali yake na nchi mpya inayozaliwa baada ya hapo inakuwa ni nchi yenye serikali moja. Katika muungano wa pili (shirikiko la serikali tatu), kila nchi itajivua baadhi ya madaraka ambayo yatashikwa na serikali ya shirikisho, na serikali yake (iliyojivua baadhi ya madaraka) itakuwa na mamlaka juu ya mambo yaliyosalia (yasiyo ya shirikisho). Mwalimu anaendelea kufafanua kwamba - mambo yatakayosimamiwa na serikali ya shirikisho ni yale ambayo kama yakiendelea kubaki katika nchi zilizoungana:

Kwa kweli nchi hizo hazitakuwa zimeungana kuwa nchi moja, bali zitakuwa nchi mbili zenye ushirikiano katika baadhi ya maeneo.

Hali hii anayoijadili Nyerere ndiyo inayoendelea leo. Muungano aliouasisiwa na Karume - muungano wa nchi moja - muungano huu leo haupo tena, na hata siku Kikwete anaenda hutubia Bunge maalum la Katiba, muungano huu haukuwepo. Kilichokuwepo siku ya hotuba ya Kikwete na hata leo, ni ushirikiano wa nchi mbili huru, nchi ya zanzibar na nchi inayoitwa Tanzania Bara (iliyovaa koti la muungano). Misingi ya muungano haipo tena, kilichojitokeza ni ushirikiano na uhusiano wa udugu, ujirani na maingiliano ya kijamii na kiuchumi, huku uchumi wa Tanzania bara (Tanganyika) ukiwa ndio unabeba mzigo zaidi wa ushirikiano huu.

Kikwete juzi ameenda bungeni kupigania muungano wa serikali mbili, suala ambalo sio wananchi wengi walilipendekeza. Ushahidi wa video na sauti za watoa maoni zipo kwenye rekodi za tume. Na isitoshe, ili kuokoa muda, tume ilikuwa na utamaduni wa kuzuia wachangiaji wasirudie hoja ambazo tayari zilishazungumzwa na wachangiaji waliowatangulia, vinginevyo iwapo tume ingejua kwamba takwimu zake zingekuja chakachuliwa, ni dhahiri ingeruhusu wachangiaji kurudia hoja zile zile, hivyo matokeo yangekuwa ni makubwa zaidi (wanaotaka serikali tatu). Ushahidi wa hili upo, na ilitokea hivyo licha ya ccm kujaza watu wake kwenye mabaraza ya katiba. Pengine kwa kujua hili, ndio maana ccm inajitahidi kupotosha umma juu ya takwimu za tume kwani inajua itaumbuka kwenye kura ya maoni. Yale yaliyozuiliwa tume yatajitokeza kwenye sanduku la kura.

Katika pita pita zangu mitaani, nimegundua kuna uelewa mkubwa sana miongoni mwa wananchi kwamba nchi mbili zilizoungana 1964 kuwa nchi moja, kwahiyo nchi mmoja haiwezi kuwa na mamlaka kamili halafu bado tukasema tupo kwenye muungano ulioasisiwa na Nyerere na Karume. Kilochopo sasa na uhusiano na ushirikiano tu ambapo mshirika mmoja ndiye anayetoa zaidi. Isitoshe, hivi leo, I vigumu kutofautisha kwa asilimia mia moja yepi ni ya muungano na yepi ni ya Tanzania Bara. Hata tume ya warioba imeeleza hili kama sababu moja wapo ya kupendekeza serikali tatu.

Hatua ya zanzibar (2010) kujichukulia mamlaka ya muungano tena kimya kimya maana yake ni kwamba hakuna muungano wa nchi mbili. Tazama katiba ya znz (2010) na ya sasa ya JMT (1977) zinavyopishana.

CCM haitaki kukubali ukweli - zanzibar imejiondoa katika muungano wa serikali mbili ulioasisiwa na Nyerere na Karume, na kujitangazia mamlaka yake kamili. Kinachotakiwa kufanyika ili kulinda muungano ni kwa mshirika wa pili wa muungano (Tanganyika) kuzinduliwa ili hali iendane na katiba ya znz na pia rasimu ya katiba. Isitoshe, hili suala sio geni na wala sio la warioba bali ni la Mkataba wa muungano (1964). Vinginevyo CCM kuendelea kung'ang'ania muungano ambao mshirika mmoja amepora mamlaka ya muungano ni kutaka kuuvunja muungano uliopo. Hakuna jinsi ya kurekebisha hili zaidi ya kuizindua Tanganyika - serikali tatu, la sivyo muda sio mrefu muungano utavunjika tu kwa sababu:

Kitendo cha ccm kulazimisha muungano wa serikali mbili wakati umma tayari unajua kwamba hakuna tena nchi moja alizoacha Mwalimu bali kuna nchi mbili na serikali mbili kwa kweli ni kutaka kupandikiza chuki miongoni mwa wananchi wa "Tanzania bara". Na atakaye beba lawama iwapo vurugu na maafa yatatokea itakuwa sio mwingine bali CCM.

Taratibu umma unaanza kuelewa kwamba misingi mikuu ya dola ni:
1.Watu
2.Ardhi
3.Mamlaka Kamili, na
4.Uhusiano wa Kimataifa.

Zanzibar kupitia katiba yake ya 2010 ipo katika hatua za mwisho kabisa za kufanikisha masuala haya, na hakika hawawezi rudi nyuma. Ili kurudi nyuma, katiba yao inaelekeza ifanyike kura ya maoni ambayo itahitaji robo tatu ya kura kufanikisha hilo. Hilo kamwe halitatokea kwani the "union question" has always been the "zanzibar question"; Ndio maana hata tume ya warioba baada ya kujiridhisha na umma wa wazanzibari na pia viongozi wao na opinion leaders, ikawa dhahiri kwa tume kwamba kura ya maoni haitaweza badilisha safari ya zanzibar waliyoanza 2010. Lakini kama alivyojadili Nguruvi3, hotuba ya JK juzi iliacha kabisa kugusia suala hili muhimu.

Kwa vile Zanzibar haiwezi kurudi nyuma kwenye suala la muungano wa nchi moja, sasa ni wakati wao kuelewa kwamba hatua hiyo haitoshi kwani bila ya Tanganyika, Zanzibar yenye mamlaka kamili haiwezekani.

Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
KIKWETE AMEPOTOSHWA NA WASHAURI WAKE KUHUSU TAKWIMU ZA TUME YA WARIOBA JUU YA MFUMO WA MUUNGANO

Kuna takwimu za tume ya katiba ambazo juzi Rais Kikwete aliziwasilisha ambazo kimsingi waliompatia maelezo hayo aidha hawana utaalam wa "statistics" au wameamua kuingiza siasa katika "statistics"; hii sio ajabu kwa Taifa letu kwani hata uchumi umekuwa ukitumikia siasa throughout; na hata katika formation of the union, the process was fraught with legal manipulation and political expediency bila ya kujalisha costs encountered kwa wananchi;

Kwa vile kada maarufu wa CCM humu jamvini Gamba la Nyoka amerudia tena upotoshaji huu ambao kimsingi umeidhahalisha tume ya warioba iliyo sheheni wasomi na watalaam wa masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na fani ya takwimu, nikiwa ni mmoja wa wananchi wanaounga mkono mapendekezo ya tume kwa vile yanaakisi maoni ya wananchi, nimeona niliweke hili sawa na katika mahali pake for good ili tujadili mengine ya maana. Awali hapa jamvini, Gamba la nyoka alirudia takwimu za Kikwete, nanukuu:


Ni muhimu tukaacha upotoshaji, na kama ni upotoshaji usiokusudiwa basi kuna haja ya kuelewa unachozungumza kabla haujajenga hoja. Ikizingatiwa kwamba wananchi wengi ni illiterate katika suala zima la takwimu, upotoshaji huu ulioletwa humu jamvini na gamba la nyoka ni kitu cha hatari sana kwani ina maanisha kwamba pia unatumika katika kuwapa taarifa juu ya uchumi wao, rasilimali zao, kodi zao n.k; hii ni hatari kwa mustakabali wa taifa.

Nikirudi kwenye hili juu ya takwimu za tume:

Based on "probability mathematics" hata kama jumla ya idadi ya watanzania ingekuwa haijulikani kwa tume ya warioba, it still wouldn't have been a problem kwani probability maths prove kwamba population size huwa sio a relevant matter, unless labda kama sample yako exceeds a few percent ya jumla ya idadi ya watu unayo examine; kwa maana hii, sample ya watu hata 500 (mia tano!) tu kwa mfano is equally useful katika kuchunguza maoni ya watu/wakazi hata 15,000,000 (milioni kumi na tano) kama ambavyo sample ya 500 ingefanikisha katika idadi ya watu 100,000 tu. Ndio maana ni kawaida kwa Survey Systems kupuuzia population size hasa pale idadi ya watu inapokuwa kubwa sana au pale idadi ya watu katika eneo husika inapokuwa haijulikani; sample ya watu elfu thelathini na tano ingekuwa ni issue only if population husika ingekuwa inajulikana kwamba ni ya kundi fulani maalum mfano wanachama milioni sita inaosemekana ni wa ccm, vinginevyo kutafuta maoni randomly, hata hao waliofikiwa na warioba na tume yake ni wengi kupitiliza.

Nisisitize tu kwamba,based on probability mathematics, sample ya watanzania hata elfu na mia tano kwa watanzania milioni 45 inatosha kupata jibu. Isitoshe, mchakato wa katiba hauishi na tume ya warioba au bunge la katiba kwani hatua ya mwisho ni kura ya maoni ambayo itajumuisha wananchi wengi zaidi; swali muhimu kwa kina Nape Nnauye (wasemaji wa chama) - Iwapo ccm ina uhakika kwamba watanzania walio wengi wameridhika na mfumo wa serikali mbili - kwamba 90% ya watanzania wanataka serikali mbili:

*Kwanini hotuba ya Kikwete jana ilitumia zaidi ya nusu ya muda wake kujadili suala la mfumo wa muungano?

*Kama ccm ipo sahihi na takwimu zake, kwanini isingesubiria kura ya maoni to prove tume ya katiba wrong badala ya kuishambulia tume?

Mwisho, based on my thread, hasa juu ya probability of mathematics, najua wapo watakaojenga hoja kwamba mjadala hapa ni demokrasia na kwamba kwamba demokrasia haiitaji mijadala ya probability. Napenda kuwaeleza wajenga hoja hii I advance kwamba, ili kuitendea haki demokrasia, scientific approaches zina nafasi yake na zimekuwa proven kutenda haki wakati wote.

Sio watanzania wote mtawadanganya kwa kuchakachua takwimu; jamii yetu ina wasomi na waelewa mambo ambao jukumu lao ni kuelimisha jamii kwa manufaa ya taifa; katika hili la serikali tatu, kamwe hatutarudi nyuma; jaji warioba hana haja ya kurudi mbele ya umma kujibu hoja. Pumzika mzee wetu warioba, hongera kwa kazi ya tume uliyoiongoza kwa mapenzi ya dhati kwa taifa lako. Vijanna wazalendo wa taifa hili tunaothamini mchango wako na tunaoheshimu sana maoni ya wananchi kwa kuvua itikadi zetu za chama, tupo wengi. Hii ni kwasababu, mkataba wa muungao (1964), hakuna sehemu unataja vyama vya TANU wala ASP.

Tutakufanyia kazi ya kujibu mapigo "kwa hoja" bila kuchoka kwani kufanya hivyo ni kuwa upande wa wananchi. Labda vifaru vitumalize.

TANZANIA KWANZA, TANGANYIKA KABLA.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mchambuzi, nadhani umetanabaisha mambo mengi kuhusu uchukuaji wa takwimu, nakubaliana na wewe Sample Size inaweza kutoa picha kamili ya population yote. However, swala muuhimu ni jinsi gani hii sample size imechukuliwa na ni data za aina gani zinachambuliwa na hii sample size, vingenevyo matokeo yaneweza kuwa Bias (sample size error).


Nitachambua hapa kuonyesha kwamba jee ni kwa jinsi gani uchambuzi (analysis) ulifanya hapo juu haujachukulia baadhi ya vigezo.
1. Kwanza, ni Watanzania wachache sana wanaojua kuhusu faida na hasara za serikali moja, mbili au tatu. Hivyo mimi na wewe tunakubaliana kwamba Wananchi wengi hawana elimu ya kutosha kufahamu faida na hasara za muundo wowote wa serikali. Sehemu kubwa ya population imejifunza kwa juu juu tuu kuhusu serikali 1,2 au tatu kwa kupitia vyombo vya habari ambavyo vingi vinazungumzia maono na sio facts.
Kutokana na hilo nadhani tutakubaliana kwamba population ambayo sample size imechukuliwa haina ufahamu wa kutosha kuhusu swala linaloulizwa kuhusu serikali moja, mbili au tatu. Sasa kama Population in defects jee unadhani sample size itakuwa safe? Hapa ndio maana tunaweza kusema kwamba analysis ulifanya hapo juu haija jumlisha vigezo vyote.
Na ndio maana wengi wetu tunasema huwe kupata usahihi wa matokeo sababu population yako labda chini ya 10% ndio inaufahamu wa swala rejea, hivyo kuchukua sample size kama aliyochukua Jaji Warioba kuna chance ikawa haipo sawa.

2. Umegusia kwamba jee ni kwa nini CCM isingesubiri kura ya maoni ( just to disclose am not CCM and I will be the last to join that party unless kufanyike significant changes). Ndugu yangu kwanza unafahamu ya kwamba Jaji Warioba alileta rasimu ikiwa na conclusion kwamba serikali tatu ndio jawabu la Watanzania. Hivyo rasimu ilikuja ikiwa tayari imeelea upande mmoja. Na alilosema Jaji Warioba ni kwamba wengi wamasema serikali tatu. Hili sio kweli sababu Wanzanzibar wengi wamasema Muungano wa Mkataba (contractual union), na maamuzi yao ni asilimia 50% za maamuzi ya mwisho ( Zanzibar ni nusu na Tanganyika ni nusu). Hivyo kusema kwamba Watanzania wamekubali serikali tatu ni kutulaghai kwani ndugu zetu wa Visiwani wao wanataka Muungano wa Mkataba. Hivyo utaona kwamba teyari uwanja wa serikali uwe za aina gani ulikuwa unawapa nguvu wale wanao taka tatu, sababu Jaji Warioba amekuwa akizinadi tatu kama ndio conclusion. Hivyo, Jakaya alikuwa ana haki za msingi kusema kwamba sio haraka haraka (not too fast), kuna challenges kwenye hizo tatu kama ilivyo hizi mbili, na akatanabaisha kwa ufasaha. Kitu ambacho Jaji Warioba hakufanya.

3. Ndugu yangu Mchambuzi na wengine wengi wanao nanga hotuba ya Jakaya Kikwete, please don't miss the forest for the trees (mna shindwa kutazama kwa macho angavu). Jakaya amefanya lile ambalo ametakiwa kufanya kikatiba, kwamba kutoa maoni yake yeye kama Mtanzania. Hakuna sehemu hata moja kwenye ile hotuba alipowalazimisha Wabunge wapigie kura serikali mbali, bali amewaasa kwamba kila maamuzi yana madhara. Jambo ambalo Mwalimu Nyerere alikuwa anafanya, Nelson Mandela amefanya na viongozi wote wenye sifa za uwongozi wanafanya. Huwezi kukaa kimya sababu tuu wewe ni raisi basi inabidi uwe neutral, mwisho wa siku hawatakumbukwa wale ambao wamepigia debe serikali tatu, lakini wale walio kaa kimya na kutoeleza maono yao kuhusu serikali madhara ya serikali ya tatu. Hivyo mimi kama kijana nasema JK amefanya alichotakiwa kufanya. Job well done.

Lakini vilevile tusisahau ya kwamba wengi wanao taka serikali ya tatu, hasa hasa kwa upande wetu wa bara sababu wamechoshwa na Tanzania bara kuwa baba ya Mtoto wao Zanzibar ambaye haachi kunung'unika. Hivyo baba anaona kama umejiona umekuwa basi simama mwenyewe, hii ni legit approach, lakini lazima tutazama katika mlengo tofauti. Jee ni nini faida ya maamuzi haya, na nini hasara za maamuzi haya na jee uwiano wa faida na hasara ukoje, na mwisho wa siku jee maamumizi yetu ni ya maendeleo au Kisiasa zaidi?
 
Mods, naomba mfute hii post, nilikosea thread na nipo in remotes areas, siwezi access computer na kufuta bandiko hili. Natanguliza shukrani na sahamani kwa usumbufu

Cc invincible
 
Last edited by a moderator:
WaZnz wameliona hilo zamani sana hususan katika chaguzi za 1995 na 2000 na 2005. JMTz inatumia nguvu zake zote kuhakikisha wanalinda SERA YA NCHI ya SERIKALI MOJA hivyo kuwafitinisha wa Znz kuuwana wenyewe kwa wenyewe kwa faida ya TGK.
Nakumbuka Maneno ya Mh Ahali ya Ismail Jussa " NCHI NI KAMA NYUMBA, CHAMA NI KAMA DUKA, KWA MWENYE AKILI HAWEZI WEKA RAHANI NYUMBA YAKE KWA KILO MBILI ZA SUKARI" ZNZ KWANZA mengine badayn.
Hapa ndipo siwaelewi.
Juzi tumewaona Dodoma wakimshangilia sana Kikwete, leo tunaambiwa na barubaru eti Tanganyika inawafitinisha.

Pandu Kificho alikuwa katika kila FM akihubiri serikali 2. Alipoondoka znz alikuwa na waraka wa serikali 3,kaulizwa Dodoma kaukana. leo tunaambiwa Watanganyika tunawafitinisha.

Jusa ndiye kaandika kanuni za bunge, tunaambiwa Watanganyika tunawafitinisha.
Prof Sheriff, Duni Haji na kila mzanibar wapo active kusaidiana na CCM, leo tunaambiwa Tanganyika inawafitinisha.

Huko nyuma tuliwahi kumwambia barabaru, wznz wapeleke mswada kuhusu muungano bunge la JMT.Tukawaambia wanaweza kujiondoa kama walivyofanya 2010
Tukawaambia wapeleke mswada BLW
Tukashauri wasije Dodoma

Hayo yote wakasema CCM znz inawafitinisha. Leo wapo 200 na ushee pale Dodoma hakuna anayethubutu kufungua kinywa.
Kina Vuai ndio wenyekiti wakisaidiana na kina Sita. Halfu tunaambi kuna kuna kufitininishwa.

Kama znz kwanza walipaswa wawe wameondoka Dodoma, thubutu nani aseme na kwa nguvu gani.

Barubaru, Tanganyika tumeshakuambia hatuna cha kupoteza.
Tukasema katika mambo 22 yaliyoondolewa na tume ya Warioba hakuna Mtanganyika aliyeshtuka. Muungano ukifa leo Tanganyika haitababaika.

Ninyi wznz ujanja wenu ni kutafuta sababu za kuficha madhaifu yenu.
Elimu yenu ipo katika mikutano na Nyerere laanatulah baasi, watu wanaondoka kwenda kulala wameipigania znz.

Wajanja akina Jusa wanatumia washona nyavu kwenye mikutano, ukweli ukitimia hawana kauli.

Nani kawafitinisha wznz kuja Dodoma ili hali wamekuja na mabegi yao na wamekodi guest house kwa pesa zao.
Zanzibar kwanza inashia malindi na Chumbe, wakipanda meli hakuna mwenye nyodo tena, wanakuja taifa kubwa Tanganyika.

Eti fitna, kama ni fitna Uamsho na CUF wanafanya nini Dodoma.
 
Mchambuzi, nadhani umetanabaisha mambo mengi kuhusu uchukuaji wa takwimu, nakubaliana na wewe Sample Size inaweza kutoa picha kamili ya population yote. However, swala muuhimu ni jinsi gani hii sample size imechukuliwa na ni data za aina gani zinachambuliwa na hii sample size, vingenevyo matokeo yaneweza kuwa Bias (sample size error).

Nitachambua hapa kuonyesha kwamba jee ni kwa jinsi gani uchambuzi (analysis) ulifanya hapo juu haujachukulia baadhi ya vigezo.
1. Kwanza, ni Watanzania wachache sana wanaojua kuhusu faida na hasara za serikali moja, mbili au tatu. Hivyo mimi na wewe tunakubaliana kwamba Wananchi wengi hawana elimu ya kutosha kufahamu faida na hasara za muundo wowote wa serikali. Sehemu kubwa ya population imejifunza kwa juu juu tuu kuhusu serikali 1,2 au tatu kwa kupitia vyombo vya habari ambavyo vingi vinazungumzia maono na sio facts.
Kutokana na hilo nadhani tutakubaliana kwamba population ambayo sample size imechukuliwa haina ufahamu wa kutosha kuhusu swala linaloulizwa kuhusu serikali moja, mbili au tatu. Sasa kama Population in defects jee unadhani sample size itakuwa safe? Hapa ndio maana tunaweza kusema kwamba analysis ulifanya hapo juu haija jumlisha vigezo vyote.
Na ndio maana wengi wetu tunasema huwe kupata usahihi wa matokeo sababu population yako labda chini ya 10% ndio inaufahamu wa swala rejea, hivyo kuchukua sample size kama aliyochukua Jaji Warioba kuna chance ikawa haipo sawa.
Kwa uelewa wangu, tunapojadili suala la biased sample, tunamaanisha kwamba - sample husika katika study imechukuliwa kwa namna ambayo baadhi ya members of the population wannaokuwa targeted by the study are less likely to be included in the study than other members; kwa maaa nyingine, sample hii inakuwa ni "non-random sample" au kwa maneno yako, "biased sample", kwani watu wote hawakuwa "equally likely" kuwa selected; that's the only way you can discuss issue ya biased sample in statistics. Je, kwa mtazamo wako, sample iliyotumika katika kukusanya maoni ya wananchi haikuwa random?

Kuhusu suala la wananchi kutokuwa na ufahamu juu ya muungano, katika opinion polls mbalimbali, huwa kuna option ya sijui; katika mazingira ya tume, wananchi hawakulazimishwa kutoa maoni juu ya kipengele cha muungano, walifanya hivyo kutokana na ridhaa yao na kwa uelewa wao, vinginevyo ambao walikuwa hawana uelewa wa suala husika aidha walikaa kimya au walitoa maoni juu ya masuala mengine. That's how the mathematics of probability would treat hii issue ya knowledge about the phenomenon at hand;

2. Umegusia kwamba jee ni kwa nini CCM isingesubiri kura ya maoni ( just to disclose am not CCM and I will be the last to join that party unless kufanyike significant changes). Ndugu yangu kwanza unafahamu ya kwamba Jaji Warioba alileta rasimu ikiwa na conclusion kwamba serikali tatu ndio jawabu la Watanzania. Hivyo rasimu ilikuja ikiwa tayari imeelea upande mmoja. Na alilosema Jaji Warioba ni kwamba wengi wamasema serikali tatu. Hili sio kweli sababu Wanzanzibar wengi wamasema Muungano wa Mkataba (contractual union), na maamuzi yao ni asilimia 50% za maamuzi ya mwisho ( Zanzibar ni nusu na Tanganyika ni nusu). Hivyo kusema kwamba Watanzania wamekubali serikali tatu ni kutulaghai kwani ndugu zetu wa Visiwani wao wanataka Muungano wa Mkataba. Hivyo utaona kwamba teyari uwanja wa serikali uwe za aina gani ulikuwa unawapa nguvu wale wanao taka tatu, sababu Jaji Warioba amekuwa akizinadi tatu kama ndio conclusion. Hivyo, Jakaya alikuwa ana haki za msingi kusema kwamba sio haraka haraka (not too fast), kuna challenges kwenye hizo tatu kama ilivyo hizi mbili, na akatanabaisha kwa ufasaha. Kitu ambacho Jaji Warioba hakufanya.

Unasahau vitu kadhaa aidha kwa makusudi au bahati mbaya;

1. Muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba awali haikuweka suala la muungano kuwa sehemu ya mjadala wa katiba mpya; Wazanzibari walipopelekwa muswada ule huku serikali ikiwakilishwa na samuel sitta, wazanzibari waliuchana na kuuchoma moto kwa vile haukuwaruhusu kujadili muungano; hii ni kwa sababu the union question has always been the zanzibar question; nia yao has always been kuifufua Tanganyika kwani wanajua kwamba hiyo ndio njia pekee ya zanzibar kuwa na mamlaka kamili in practice;

Ni baada ya tukio hili, sitta akatumia busara kutuliza hali ya hewa, mambo yakatulia, na baadae Kikwete kurudhia kwamba suala la muungano liwekwe kwenye sheria ya mabadiliko ya katiba; kwahiyo tofauti na unavyofikiri, bila ya shinikizo la wazanzibari, suala la mfumo wa muungano lingewekewa vipingamizi na ccm kuwa sehemu ya mjadala wa wananchi kupitia tume ya katiba;

2. Suala lingine ambalo aidha kwa bahati mbaya au kwa makusudi unalisahau ni kwamba katika hadidu rejea za tume, tume ilielekezwa kudumisha na kuboresha muungano; kufuatia hali hii, na kufuatia tukio la zanzibar mbele ya sitta pamoja na migogoro ya muda mrefu ya muungano ambayo serikali mbili imepelekea hadi zanzibar kuvunja katiba ya muungano kupitia katiba yake ya 2010, jibu sahihi la kudumisha na kuboresha muungano ni serikali tatu; hata taasisi zote muhimu maoni yao ni serikali tatu; sasa unaposema hili ni wazo la warioba, unasahau sio tu historia ya sakata la Tanganyika kuanzia jumbe (1964), bali pia hadidu rejea za tume.

Kufuatia mabadiliko ya katiba ya znz (2010) ambapo sasa muungano ni wa nchi mbili, ina maana muungano wa nyerere na karume (wa nchi moja haupo tena). Na ili znz ibadili hilo leo, katiba yao inasema inahitaji kura ya maoni theluthi tatu; tume ya warioba ilishaelezwa znz kwamba hilo halitatokea;

3. Na tatu, ukizungumza tu habari ya muungano wa mkataba, maana yake ni serikali tatu; Nguruvi3 amejadili hili vyema huko juu hivyo kuokoa muda, sitalirudia.

"Ndugu yangu Mchambuzi na wengine wengi wanao nanga hotuba ya Jakaya Kikwete, please don't miss the forest for the trees (mna shindwa kutazama kwa macho angavu). Jakaya amefanya lile ambalo ametakiwa kufanya kikatiba, kwamba kutoa maoni yake yeye kama Mtanzania. Hakuna sehemu hata moja kwenye ile hotuba alipowalazimisha Wabunge wapigie kura serikali mbali, bali amewaasa kwamba kila maamuzi yana madhara. Jambo ambalo Mwalimu Nyerere alikuwa anafanya, Nelson Mandela amefanya na viongozi wote wenye sifa za uwongozi wanafanya. Huwezi kukaa kimya sababu tuu wewe ni raisi basi inabidi uwe neutral, mwisho wa siku hawatakumbukwa wale ambao wamepigia debe serikali tatu, lakini wale walio kaa kimya na kutoeleza maono yao kuhusu serikali madhara ya serikali ya tatu. Hivyo mimi kama kijana nasema JK amefanya alichotakiwa kufanya. Job well done.

Mtanganyika, hakuna anayemshambulia Kikwete bali sote tunatoa maoni na mitazamo yetu kama wadau wa suala husika; tumejadili mengi kwa hoja lakini upande wa pili wa hoja mnachagua yale tu yanayowafaa;

Kichwa cha uzi huu ni "mtazamo wa hotuba ya JK bungeni", na isitoshe, Mwenyekiti wa BMK Samuel Sitta jumatatu pia aliwaambia wabunge anawapa hadi jumatano kutafakari na kuja na mitazamo yao juu ya hotuba za JK na Warioba; sasa iwapo wabunge wanafanya hayo, tena baada ya sisi wananchi kutangulia na uamuzi huo, kosa letu lipo wapi? Jibuni hoja;

"Lakini vilevile tusisahau ya kwamba wengi wanao taka serikali ya tatu, hasa hasa kwa upande wetu wa bara sababu wamechoshwa na Tanzania bara kuwa baba ya Mtoto wao Zanzibar ambaye haachi kunung'unika. Hivyo baba anaona kama umejiona umekuwa basi simama mwenyewe, hii ni legit approach, lakini lazima tutazama katika mlengo tofauti. Jee ni nini faida ya maamuzi haya, na nini hasara za maamuzi haya na jee uwiano wa faida na hasara ukoje, na mwisho wa siku jee maamumizi yetu ni ya maendeleo au Kisiasa zaidi?"

Mtanganyika, hoja yako hii inajichanganya na hoja zako za awali hapo juu; lakini kwa vile umejadili hili, nikukumbushe tu kwamba maswali yako yote hapo juu Nguruvi3 ameyajadili kwa kina sana; sasa ni zamu yako wewe kuja na counter arguments/views kwani hapo utakuwa unatimiza dhamira ya uzi huu, hivyo kuutendea haki;



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mtanganyika
Nadhani hukuangalia hoja za sample size za Mchambuzi vema.

Kwanza kuhusu sample size, kama unadhani kulikuwa na possibility za sample error
1. Je ilikuwa muafaka kwa rais kuziongelea kabla au ndani ya bunge.
Kumbuka kauli za sample error zilianza na wanaCCM akina Nape.

Huoni Rais kuzungumzia tena akisema 'Ninasikia' ilikuwa kubeba majungu na kuyafanya maongezi ya taifa?Kulikuwa na tatizo gani Rais kuita wataalam wa takwimu ili wamthibitihishie ukweli au uongo.

2. Je, huoni kufanya hivyo kulikuwa kuchagiza wajumbe wakatae maoni ya tume aliyoiunda yeye mwenyewe.

Kwavile kulikuwa na ukiukwaji wa kanuni ili kwenda baada ya Warioba huoni kuzungumzia suala la takwimu kulikuwa kumjibu Warioba ili hali alikuwa na nafasi ya kuliongelea jambo hilo popote na pengine kabla ya uchochezi.

3.Kuhusu Watanzania wengi, Warioba alieleza katika rasimu ya kwanza kuwa wznz hawakuweza kueleza mkataba ni wa kitu gani na nini kiwe mkataba kwa faida gani na ya nani.

Hivyo liliondoka katika agenda mapema kwasababu ya kukosa mashiko.
Hata hivyo lazima uwaelewe wazanzibar ni watu wanaofuata upepo.

Ni wznz walioanzisha suala la serikali 3 takribani miaka 30 iliyopita.
Hivyo uhalali huo upo kwasababu hata chama kikuu cha CUF kina sera hizo.
Ni bahati nzuri Watanganyika wameliangalia kwa mapana na kuona lina umuhimu kwa upande wao.

Kwa wznz suala la mkataba hakuna anayeweza kueleza kuanzia viongozi hadi mvuvi. Hawa wamesikia kutoka kwa Ahmed Rajab na Seif ambaye naye pia alikuwa ni serikali 3. Hivyo ilikuwa busara Warioba kupima kama wenzetu wanaelewa wanaongelea nini.

Lakini pia hautuwezi kukana ukweli kuwa wakati wa kura ya maoni waliohojiwa walikuwa Watanzania. Kudhani wznz wanafaa kusikilizwa zaidi ya watu milioni 40 si kuwatendea haki. Hilo ni tofauti na kupiga kura wanapopewa 50 per cent

Hoja kuu ni kuwa Rais wa nchi hawezi kuongelea mambo ya mitaani ili hali ana uwezo wa kupata kila aina ya ukweli kwa kutumia kila rasimali.
Rais anapozungumza na taifa kwa kutumia maneno' Nimesikia' ni aibu.

Mkuu, JK hotuba yake haiwezi kufanana na za viongozi waliomtangulia.
Nyerere, Mwinyi na Mkapa walikuwa wanaongea kwa authoirty.

Nikupe mifano
Nyerere tunajua alivyokuwa na uwezo wa kujenga hoja hatuna cha kueleza

Mwinyi
Alikuwa mwingi wa busara . Suala la vyama vingi alisimamia vizuri sana kwa hekima

Mkapa
Akiwa songea aliwajibu Tucta (Juwata) kuhusu suala la mishahara akichukua takwimu za kicuhumi, inflation na kuonyesha ni vipi kipato kimekuwa na faida hata kama mshahara upo pale pale

Kikwete
Akiongea ni mipasho.Rais wa nchi anasema ‘nimesikia' sijui sisi mitaani tusemeje
Rais analalamika kuogeza rushwa sijui sisi tusemeje
Rais anakuwa na position mbili kwa suala moja, sijui hapo tusemeje

Haikuwa muafaka kutoa maoni yanayomsumanga Warioba, wazee na wasomi.
Kuna uwezekano angejenga hoja za kitaifa bila kuwadhalilisha wazee.
Kwamba leo Warioba ameshindwa takwimu watu 600 wajadili!!1
 
Last edited by a moderator:
hatuna tena muungano, kilichobakia ni ushirikiano

baba wa taifa mwalimu nyerere katika kitabu chake cha "uongozi wetu na hatima ya tanzania", ukurasa wa 15, mwalimu anasema hivi:


Mwalimu anaendelea kufafanua kwamba - kwa muungano wa aina ya kwanza hapo juu (serikali moja), kila nchi inafuta serikali yake na nchi mpya inayozaliwa baada ya hapo inakuwa ni nchi yenye serikali moja. Katika muungano wa pili (shirikiko la serikali tatu), kila nchi itajivua baadhi ya madaraka ambayo yatashikwa na serikali ya shirikisho, na serikali yake (iliyojivua baadhi ya madaraka) itakuwa na mamlaka juu ya mambo yaliyosalia (yasiyo ya shirikisho). Mwalimu anaendelea kufafanua kwamba - mambo yatakayosimamiwa na serikali ya shirikisho ni yale ambayo kama yakiendelea kubaki katika nchi zilizoungana:



Hali hii anayoijadili nyerere ndiyo inayoendelea leo. Muungano aliouasisiwa na karume - muungano wa nchi moja - muungano huu leo haupo tena, na hata siku kikwete anaenda hutubia bunge maalum la katiba, muungano huu haukuwepo. Kilichokuwepo siku ya hotuba ya kikwete na hata leo, ni ushirikiano wa nchi mbili huru, nchi ya zanzibar na nchi inayoitwa tanzania bara (iliyovaa koti la muungano). Misingi ya muungano haipo tena, kilichojitokeza ni ushirikiano na uhusiano wa udugu, ujirani na maingiliano ya kijamii na kiuchumi, huku uchumi wa tanzania bara (tanganyika) ukiwa ndio unabeba mzigo zaidi wa ushirikiano huu.

Kikwete juzi ameenda bungeni kupigania muungano wa serikali mbili, suala ambalo sio wananchi wengi walilipendekeza. Ushahidi wa video na sauti za watoa maoni zipo kwenye rekodi za tume. Na isitoshe, ili kuokoa muda, tume ilikuwa na utamaduni wa kuzuia wachangiaji wasirudie hoja ambazo tayari zilishazungumzwa na wachangiaji waliowatangulia, vinginevyo iwapo tume ingejua kwamba takwimu zake zingekuja chakachuliwa, ni dhahiri ingeruhusu wachangiaji kurudia hoja zile zile, hivyo matokeo yangekuwa ni makubwa zaidi (wanaotaka serikali tatu). Ushahidi wa hili upo, na ilitokea hivyo licha ya ccm kujaza watu wake kwenye mabaraza ya katiba. Pengine kwa kujua hili, ndio maana ccm inajitahidi kupotosha umma juu ya takwimu za tume kwani inajua itaumbuka kwenye kura ya maoni. Yale yaliyozuiliwa tume yatajitokeza kwenye sanduku la kura.

Katika pita pita zangu mitaani, nimegundua kuna uelewa mkubwa sana miongoni mwa wananchi kwamba nchi mbili zilizoungana 1964 kuwa nchi moja, kwahiyo nchi mmoja haiwezi kuwa na mamlaka kamili halafu bado tukasema tupo kwenye muungano ulioasisiwa na nyerere na karume. Kilochopo sasa na uhusiano na ushirikiano tu ambapo mshirika mmoja ndiye anayetoa zaidi. Isitoshe, hivi leo, i vigumu kutofautisha kwa asilimia mia moja yepi ni ya muungano na yepi ni ya tanzania bara. Hata tume ya warioba imeeleza hili kama sababu moja wapo ya kupendekeza serikali tatu.

Hatua ya zanzibar (2010) kujichukulia mamlaka ya muungano tena kimya kimya maana yake ni kwamba hakuna muungano wa nchi mbili. Tazama katiba ya znz (2010) na ya sasa ya jmt (1977) zinavyopishana.

Ccm haitaki kukubali ukweli - zanzibar imejiondoa katika muungano wa serikali mbili ulioasisiwa na nyerere na karume, na kujitangazia mamlaka yake kamili. Kinachotakiwa kufanyika ili kulinda muungano ni kwa mshirika wa pili wa muungano (tanganyika) kuzinduliwa ili hali iendane na katiba ya znz na pia rasimu ya katiba. Isitoshe, hili suala sio geni na wala sio la warioba bali ni la mkataba wa muungano (1964). Vinginevyo ccm kuendelea kung'ang'ania muungano ambao mshirika mmoja amepora mamlaka ya muungano ni kutaka kuuvunja muungano uliopo. Hakuna jinsi ya kurekebisha hili zaidi ya kuizindua tanganyika - serikali tatu, la sivyo muda sio mrefu muungano utavunjika tu kwa sababu:

Kitendo cha ccm kulazimisha muungano wa serikali mbili wakati umma tayari unajua kwamba hakuna tena nchi moja alizoacha mwalimu bali kuna nchi mbili na serikali mbili kwa kweli ni kutaka kupandikiza chuki miongoni mwa wananchi wa "tanzania bara". Na atakaye beba lawama iwapo vurugu na maafa yatatokea itakuwa sio mwingine bali ccm.

Taratibu umma unaanza kuelewa kwamba misingi mikuu ya dola ni:
1.watu
2.ardhi
3.mamlaka kamili, na
4.uhusiano wa kimataifa.

Zanzibar kupitia katiba yake ya 2010 ipo katika hatua za mwisho kabisa za kufanikisha masuala haya, na hakika hawawezi rudi nyuma. Ili kurudi nyuma, katiba yao inaelekeza ifanyike kura ya maoni ambayo itahitaji robo tatu ya kura kufanikisha hilo. Hilo kamwe halitatokea kwani the "union question" has always been the "zanzibar question"; ndio maana hata tume ya warioba baada ya kujiridhisha na umma wa wazanzibari na pia viongozi wao na opinion leaders, ikawa dhahiri kwa tume kwamba kura ya maoni haitaweza badilisha safari ya zanzibar waliyoanza 2010. Lakini kama alivyojadili nguruvi3, hotuba ya jk juzi iliacha kabisa kugusia suala hili muhimu.

Kwa vile zanzibar haiwezi kurudi nyuma kwenye suala la muungano wa nchi moja, sasa ni wakati wao kuelewa kwamba hatua hiyo haitoshi kwani bila ya tanganyika, zanzibar yenye mamlaka kamili haiwezekani.

Tanzania kwanza, tanganyika kabla.



Sent from my blackberry 8520 using jamiiforums

hivi dawa ya zanzibar kuvunja katiba mwaka 2010 ni kuongeza serikali ya tatu?

Kama hoja ni quality ya maoni na si wingi wa maoni basi nilitegemea "busara" za tume zipendekeze serikali moja kwa sababu kiukweli kabisa ndiyo muungano munaofaa, halafu pindi itakapofika kura za maoni tujue mbivu ni zipi na mbichi ni zipi kwa maana ushiriki wa wananchi utakuwa mpana zaidi kipindi hiki, na pia elimu ya jambo hili itatolewa sana na maamuzi yatakuwa kweli maamuzi halisi ya wananchi.

Kama alivyosema mwalimu kwamba muundo huu wa serikali tatu, kiukweli kabisa siyo muungano bali ni ushirikiano mkubwa baina ya nchi mbili, basi ni dhahiri kilichopendekezwa na warioba ni ushirikiano mkubwa kabisa baina ya tanganyika na zanzibar na si muungano, swali linakuja je ni kweli tume ya warioba inaamini wananchi hawataki muungano?.

Zanzibar wananchi wengi wanataka muungano wa mkataba, na si serikali tatu tu for the case of serikali tatu, je tume imewapa nini raia hawa?- namnukuu jaji warioba mwenyewe akitamka kwamba kuwa na muungano wa mkataba kiukweli maana yake ni kuvunja muungano:, sasa kama ni hivyo kwa nini basi warioba na tume yake wasitafsiri kuwa zile asilimia 60.9 ya wanaotaka mkataba maana yake ni kwamba hawataki muungano?
 
Hapa ndipo siwaelewi.
Juzi tumewaona Dodoma wakimshangilia sana Kikwete, leo tunaambiwa na barubaru eti Tanganyika inawafitinisha.

Pandu Kificho alikuwa katika kila FM akihubiri serikali 2. Alipoondoka znz alikuwa na waraka wa serikali 3,kaulizwa Dodoma kaukana. leo tunaambiwa Watanganyika tunawafitinisha.

Jusa ndiye kaandika kanuni za bunge, tunaambiwa Watanganyika tunawafitinisha.
Prof Sheriff, Duni Haji na kila mzanibar wapo active kusaidiana na CCM, leo tunaambiwa Tanganyika inawafitinisha.

Huko nyuma tuliwahi kumwambia barabaru, wznz wapeleke mswada kuhusu muungano bunge la JMT.Tukawaambia wanaweza kujiondoa kama walivyofanya 2010
Tukawaambia wapeleke mswada BLW
Tukashauri wasije Dodoma

Hayo yote wakasema CCM znz inawafitinisha. Leo wapo 200 na ushee pale Dodoma hakuna anayethubutu kufungua kinywa. Kina Vuai ndio wenyekiti wakisaidiana na kina Sita. Halfu tunaambi kuna kuna kufitininishwa.

Kama znz kwanza walipaswa wawe wameondoka Dodoma, thubutu nani aseme na kwa nguvu gani.

Barubaru, Tanganyika tumeshakuambia hatuna cha kupoteza.
Tukasema katika mambo 22 yaliyoondolewa na tume ya Warioba hakuna Mtanganyika aliyeshtuka. Muungano ukifa leo Tanganyika haitababaika.

Ninyi wznz ujanja wenu ni kutafuta sababu za kuficha madhaifu yenu.
Elimu yenu ipo katika mikutano na Nyerere laanatulah baasi, watu wanaondoka kwenda kulala wameipigania znz.

Wajanja akina Jusa wanatumia washona nyavu kwenye mikutano, ukweli ukitimia hawana kauli.

Nani kawafitinisha wznz kuja Dodoma ili hali wamekuja na mabegi yao na wamekodi guest house kwa pesa zao.
Zanzibar kwanza inashia malindi na Chumbe, wakipanda meli hakuna mwenye nyodo tena, wanakuja taifa kubwa Tanganyika.

Eti fitna, kama ni fitna Uamsho na CUF wanafanya nini Dodoma.

Nguruvi3,

Kwanini unachukua hoja nusu mstari na kuitolea maamuzi yako. HOJA YANGU HAPO KATIKA BANDIKO LANGU ILIKUWA HII KAMA UNAO UBAVU REJEA NA UIJADILI NA SIO KULETA BLA BLA ZAKO.

Kumbukeni Sera ya CCM inasema Serikali 2 na Chama Kimoja. Hii ni khatari kubwa sana. Na CCM hao hao wanatumia nguvu kubwa sana kulinda Sera yao ya Serikali 2 na chama Kimoja.

Tukumbuke kuwa Sasa ni wakti wa Vyama vingi. Siku yoyote katika nchi yenu inaweza
itokea Serikali 2 na vyama 2. je nchi itaendeshwaje. Hapo kikwete kashindwa kujibu hilo.

Tujaalie TGK ikashinda CCM na kuunda Serikali na ZNZ ikishinda CUF na kuunda Serikali
. Tukumbuke kuwa
RAIS wa Znz ni MEMBER KATIKA BARAZA LA MAWAZIRI JMTz, hivyo anaingia katika Vikao vyote vya baraza la mawaziri wa Muungano.

Je CCM hao watakubali Maalim Seif aingie katika baraza la mawaziri wa Muungano? Je Kikwete mbona hajalisemea hilo?.

sasa na wewe kama unao ubavu au hoja mbadala kwa hili basi Bismillah

Kama kweli hamuwezi kupoteza kitu kama Znz wakijitoa katika huo mvungano , MBONA RAIS WENU JK amelalamika sana kuutaka huo muungano tena AMESISITIZA WA SERIKALI MBILI NA KUKATAA KATAKATA KUANZISHWA KWA SERIKALI YA TGK. Je ujiulizi kwanini? au uoni kama mnanufaika nyie na huo mvungano? Na zidi jiuliza kwanini muendelee kuwabeba Znz?

kumbuka nyie ni WADANGANYIKA. Na siku zote CHA MGEMA ULIWA NA WALEVI. Wacha wajinafasi lakin msimamo ni ule ule ZNZ KWANZA.

POLE SANA

 
hivi dawa ya zanzibar kuvunja katiba mwaka 2010 ni kuongeza serikali ya tatu?

Kama hoja ni quality ya maoni na si wingi wa maoni basi nilitegemea "busara" za tume zipendekeze serikali moja kwa sababu kiukweli kabisa ndiyo muungano munaofaa, halafu pindi itakapofika kura za maoni tujue mbivu ni zipi na mbichi ni zipi kwa maana ushiriki wa wananchi utakuwa mpana zaidi kipindi hiki, na pia elimu ya jambo hili itatolewa sana na maamuzi yatakuwa kweli maamuzi halisi ya wananchi.

Kama alivyosema mwalimu kwamba muundo huu wa serikali tatu, kiukweli kabisa siyo muungano bali ni ushirikiano mkubwa baina ya nchi mbili, basi ni dhahiri kilichopendekezwa na warioba ni ushirikiano mkubwa kabisa baina ya tanganyika na zanzibar na si muungano, swali linakuja je ni kweli tume ya warioba inaamini wananchi hawataki muungano?.

Zanzibar wananchi wengi wanataka muungano wa mkataba, na si serikali tatu tu for the case of serikali tatu, je tume imewapa nini raia hawa?- namnukuu jaji warioba mwenyewe akitamka kwamba kuwa na muungano wa mkataba kiukweli maana yake ni kuvunja muungano:, sasa kama ni hivyo kwa nini basi warioba na tume yake wasitafsiri kuwa zile asilimia 60.9 ya wanaotaka mkataba maana yake ni kwamba hawataki muungano?

Unachojadili hapo juu hakina mantiki zaidi ya kujikanyaga tu; unazungumza kama vile Tanzania ni nchi moja wakati Tanzania tunayoijadili hapa ni nchi mbili yenye serikali mbili; sasa hauoni kwamba nchi mbili zenye serikali tatu ndio njia ya kurekebisha hali ya sasa? Au hizi kwako ni changamoto na upepo tu, vitapita;

Hoja juu ya takwimu na juu ya "muungano wa mkataba", hizi tumezijadili, na bado haujaja na counter arguments zenye mashiko na zenye hadhi ya kujibiwa;



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Unachojadili hapo juu hakina mantiki zaidi ya kujikanyaga tu; unazungumza kama vile Tanzania ni nchi moja wakati Tanzania tunayoijadili hapa ni nchi mbili yenye serikali mbili; sasa hauoni kwamba nchi mbili zenye serikali tatu ndio njia ya kurekebisha hali ya sasa? Au hizi kwako ni changamoto na upepo tu, vitapita;

Hoja juu ya takwimu na juu ya "muungano wa mkataba", hizi tumezijadili, na bado haujaja na counter arguments zenye mashiko na zenye hadhi ya kujibiwa;



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Wewe unataka mantiki gani zaidi ya Upofu wa kijinga uliojivika wa "I'm Holier than thou?"
Hasira zenu za Zanzibar kuvunja katiba, mnataka kuwaadhibu Watanzania bara kwa kuwaongezea Zigo la serikali nyingine!, Kama mmekasirika Zanzibar kuvunja katiba wapelekeni katika mahakama ya katiba!

Nyinyi mnafahamu kabisa kwamba kuwa na serikali tatu kunauweka Muungano wetu rehani, Warioba na Tume yake wamekiri hilo katika rasimu yao, na wameshindwa kupendekza kifanyike nini kuondoa changamoto hizo!

Nyinyi hamtaki kukiri kuwa maoni ya tume juu ya muungano yameakisi kwa kiwango kikubwa mawazo ya watoa maoni wa Tanzania bara, lakini kwa Kule Zanzibar wengi hawana matazamo huo, WAO WANATAKA AINA YA MUUNGANO KAMA WA EU, KWA LUGHA NYINGINE WANATAKA USHIRIKIANO WA KARIBU SANA NA TANGANYIKA LAKINI SIYO KUUNDA NCHI MOJA SERIKALI TATU!

Wewe unijibu usinijibu, haijalishi, hoja ndizo zinazosimama hapa, Ukikosa hoja hasira hazisaidii mkuu unaweza kukaa pembeni ukaacha wenye hoja wasonge mbele na mjadala!.

SERIKALI MBILI ZILIZOBORESHWA NDIZO ZINAZOTUFAA, TATU HAZIFAI ZITAUA MUUNGANO!
 
Wewe unataka mantiki gani zaidi ya Upofu wa kijinga uliojivika wa "I'm Holier than thou?"
Hasira zenu za Zanzibar kuvunja katiba, mnataka kuwaadhibu Watanzania bara kwa kuwaongezea Zigo la serikali nyingine!, Kama mmekasirika Zanzibar kuvunja katiba wapelekeni katika mahakama ya katiba!

Nyinyi mnafahamu kabisa kwamba kuwa na serikali tatu kunauweka Muungano wetu rehani, Warioba na Tume yake wamekiri hilo katika rasimu yao, na wameshindwa kupendekza kifanyike nini kuondoa changamoto hizo!

Nyinyi hamtaki kukiri kuwa maoni ya tume juu ya muungano yameakisi kwa kiwango kikubwa mawazo ya watoa maoni wa Tanzania bara, lakini kwa Kule Zanzibar wengi hawana matazamo huo, WAO WANATAKA AINA YA MUUNGANO KAMA WA EU, KWA LUGHA NYINGINE WANATAKA USHIRIKIANO WA KARIBU SANA NA TANGANYIKA LAKINI SIYO KUUNDA NCHI MOJA SERIKALI TATU!

Wewe unijibu usinijibu, haijalishi, hoja ndizo zinazosimama hapa, Ukikosa hoja hasira hazisaidii mkuu unaweza kukaa pembeni ukaacha wenye hoja wasonge mbele na mjadala!.

SERIKALI MBILI ZILIZOBORESHWA NDIZO ZINAZOTUFAA, TATU HAZIFAI ZITAUA MUUNGANO!

Sina hasira bali furaha kwamba Tanganyika ipo njiani kuzinduliwa;hoja zako zimeshajadiliwa lakini kwa vile wewe ni Kada wa chama, tena in a conservative outfit, kamwe hautaona outside the box;

Umekuja na hoja zako uchwara za kubeba takwimu za JK, nimejibu, sasa hauna la kusema zaidi ya kutafuta loophole ya kuzidi kupotosha; Ukaja na hoja za kutetea hotuba ya JK ambayo tumeichambua hoja kwa hoja, huku tukijadili mantiki ya serikali tatu na historia ya hoja hii, badala ya kukumbuka historia, unadakia tu suala la 2010 kule zanzibar na kuita hoja zetu ni hasira zetu dhidi ya wazanzibari kuvunja katiba 2010;

Nirudie tena kwamba, sina hasira bali furaha ya uzinduzi wa Tanganyika kwani ikiwa sasa tuna muungano wa nchi mbili, hauna hoja yoyote ya kugeuza ukweli kwamba muungano wa Mwalimu na Karume haupo tena, na harakati zenu za kushawishi BLW waende kubadili kifungu husika cha katiba yao hakitafanikiwa kwani the union question has always been the zanzibar question, na jibu lake ni shirikisho tu. Katika mazingira haya, Barubaru husema "Pole Sana".
Wananchi wapo tayari kubeba unaloita zigo ili mradi ni zigo worth kuligharamia kuliko kiini macho cha sasa kinacho nyonya wananchi maskini.

Vua Gamba la Nyoka wa kijani,
Vaa gwanda la utaifa wako wa Tanzania as long as:

Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Unachojadili hapo juu hakina mantiki zaidi ya kujikanyaga tu; unazungumza kama vile Tanzania ni nchi moja wakati Tanzania tunayoijadili hapa ni nchi mbili yenye serikali mbili; sasa hauoni kwamba nchi mbili zenye serikali tatu ndio njia ya kurekebisha hali ya sasa? Au hizi kwako ni changamoto na upepo tu, vitapita;

Hoja juu ya takwimu na juu ya "muungano wa mkataba", hizi tumezijadili, na bado haujaja na counter arguments zenye mashiko na zenye hadhi ya kujibiwa;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mkuu mchambuzi nguruvi3 gamba la nyoka na mtanganyika baadhi ya watu tunahitaji msaada kuhusu sula ala gharama za serikali 3. Mimi napinga serikali mbili na napinga serikali tatu, Muungano ninaoona unafaa ni ule wa serikali moja.

Lakini natatizika sana ninaposikia watu wanasema serikali tatu ni gharama, gharama gani zitakazoongezeka kama serikali ya tatu itatokana na kupunguza ukubwa na majukumu ya serikali ya JMT?

Na kwanini hatuzungumzii gharama kubwa za sasa, hasa kwa upande wa bara kwa kuwalipa mishahara mikubwa watu wa visiwani wanaofanya kazi bara kwa gamba la utanzania, na wabunge wa kutoka ZNZ wanaolipwa bungeni kwa sababu tu ya kukaa mule bungeni bila kufanya lolote la maana, au kuwapa nyadhifu kubwa zenye malipo makubwa watu amabo wanatoka visiwani ambao qualification yao kubwa ni uzanzibar, kwani hizo sio gharama kubwa?

Out of curiosity, tuna takwimu zozote zinazoonesha serikali ya shirikisho itagharimu kiasi gani?
 
Mkuu mchambuzi nguruvi3 gamba la nyoka na mtanganyika baadhi ya watu tunahitaji msaada kuhusu sula ala gharama za serikali 3. Mimi napinga serikali mbili na napinga serikali tatu, Muungano ninaoona unafaa ni ule wa serikali moja.

Lakini natatizika sana ninaposikia watu wanasema serikali tatu ni gharama, gharama gani zitakazoongezeka kama serikali ya tatu itatokana na kupunguza ukubwa na majukumu ya serikali ya JMT?

Na kwanini hatuzungumzii gharama kubwa za sasa, hasa kwa upande wa bara kwa kuwalipa mishahara mikubwa watu wa visiwani wanaofanya kazi bara kwa gamba la utanzania, na wabunge wa kutoka ZNZ wanaolipwa bungeni kwa sababu tu ya kukaa mule bungeni bila kufanya lolote la maana, au kuwapa nyadhifu kubwa zenye malipo makubwa watu amabo wanatoka visiwani ambao qualification yao kubwa ni uzanzibar, kwani hizo sio gharama kubwa?

Out of curiosity, tuna takwimu zozote zinazoonesha serikali ya shirikisho itagharimu kiasi gani?
Mkuu Bongolander hili la gharama tumeliongeaa sana, kuna watu wanawafanya Watanzania wapuuzi. Baadhi yao ni Nape na Pinda.

Tumeeleza kwa undani jinsi gharama zitalavyopungua badala ya kuongezeka.
Hadi sasa tuna wizara kamili inayoshughulikia muungano ikiwa na watu wengi.

Katika shirikisho, kuna mambo 7 ambayo kimsingi ni 5. Mambo hayo haata bila ya muungano ni lazima kila nchi itakuwa nayo. Mfano, ulinzi na usalama, mambo ya nje n.k.
Kilichopo ni kuwa hayo 7 yatachangiwa na tume imeeleza kutokana na ukubwa wa uchumi na watu.

Kwasasa hivi katika hayo 7 kwa mfano ulinzi na usalama znz inachangia sifuri. Rasimu inasema lazima ichangie hata kama ni kidogo. Ndio maana ni mwiko kwa mznz kuongelea ulinzi na usalama kwasababu katika mambo wanayopata free ride hilo ni mojawapo.

Nikupe mfano, bajeti ya ulinzi na usalama ni trilioni moja na ushee. Endapo znz itaambiwa ichangie 5% ni appron 50 bilioni. Kwa sasa ni 0 Tsh.

Kuna mambo 22 ambayo Mtanganyika ameyabeba mwenyewe.
Mfano, Znz wana wizara ya elimu ya juu. Utashangaa wanapewa mgao wa JMT kwa elimu ya juu wakati wana wizara yao ya elimu ya juu ambayo Mtanganyika hatii mguu, na wakati huo huo wana free ride ya watoto wao kusoma bila mkopo Tanganyika.

Ukiondoa mambo 22 na kubaki na 7 utakuwa umempunguzia Mtanganyika mzigo mkubwa sana.
Hayo 15 ni mzigo kwasababu znz inachangia sifuri, zero! Utakuwa umeondoa malalamiko mengi

Mzigo wa Watalii wa znz Dodoma kaubeba Mtanganyika. Mzigo wa mishahara ya znz kaubeba Mtanganyika, mzigo wa nishati ya umeme kaubeba Mtanganyika na Zigo la pesa zisizo na audit kupitia ofisi ya makamu wa Rais kaubeba Mtanganyika.

Mzigo wa wafanyakzi wa znz katika muungano ambao sifa kubwa ni uzanzibar kaubeba Mtanganyika, kuanzia mishahara hadi mafao ya uzeeni.

Dodoma peke yake tuna Watalii 80 kutoka znz ambao kila mwezi mmoja analipwa milioni 10 sawa na milioni 800 kwa mwezi. Kwa mwaka ni zaidi ya bilioni 9.6 ambazo SMZ inachangia.

Hoja kubwa ni kuwa misaada na mikopo inakuja kwa jina la Tanzania. Tume imesema wznz wapewe nafasi ya kukopa na kulipa madeni yao. Wapewe nafasi ya kutafuta misaada yao.
Tanganyika nayo iwe hivyo, hivi kuna tatizo gani hapo?

Wenye hoja ya misaada na mikopo wanasahu gharama kubwa alizobeba Mtanganyika katika muungano wa serikali 2. Gharama zote za Dodoma sasa hivi kazibeba Mtanganyika.

Haiingii akilini kusema kuwa ni nafuu kuwa na mambo 22 ya muungano kuliko mambo 7. Sijui hesabu hizo wenzetu wanazipata wapi. Halafu wapo wanaodai eti mambo ya muungano yatenganishwe tukiwa na serikali 2, tunawauliza hayo yasiyo ya muungano kwa upande wa Tanganyika yahudumiwe na nani na kwa gharama kutoka wapi, hakuna jibu.

Kwa ufupi serikali 2 zimembebesha Mtanganyika mzigo mkubwa sana wa kodi.
Tumewauliza wa serikali 2 watupe namna watakavyoendesha serikali bila upande mmoja kuumia na jinsi serikali 3 zitakavyoongeza gharama.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Bongolander hili la gharama tumeliongeaa sana, kuna watu wanawafanya Watanzania wapuuzi. Baadhi yao ni Nape na Pinda.

Tumeeleza kwa undani jinsi gharama zitalavyopungua badala ya kuongezeka.
Hadi sasa tuna wizara kamili inayoshughulikia muungano ikiwa na watu wengi.

Katika shirikisho, kuna mambo 7 ambayo kimsingi ni 5. Mambo hayo haata bila ya muungano ni lazima kila nchi itakuwa nayo. Mfano, ulinzi na usalama, mambo ya nje n.k.
Kilichopo ni kuwa hayo 7 yatachangiwa na tume imeeleza kutokana na ukubwa wa uchumi na watu.

Kwasasa hivi katika hayo 7 kwa mfano ulinzi na usalama znz inachangia sifuri. Rasimu inasema lazima ichangie hata kama ni kidogo. Ndio maana ni mwiko kwa mznz kuongelea ulinzi na usalama kwasababu katika mambo wanayopata free ride hilo ni mojawapo.

Nikupe mfano, bajeti ya ulinzi na usalama ni trilioni moja na ushee. Endapo znz itaambiwa ichangie 5% ni appron 50 bilioni. Kwa sasa ni 0 Tsh.

Kuna mambo 22 ambayo Mtanganyika ameyabeba mwenyewe.
Mfano, Znz wana wizara ya elimu ya juu. Utashangaa wanapewa mgao wa JMT kwa elimu ya juu wakati wana wizara yao ya elimu ya juu ambayo Mtanganyika hatii mguu, na wakati huo huo wana free ride ya watoto wao kusoma bila mkopo Tanganyika.

Ukiondoa mambo 22 na kubaki na 7 utakuwa umempunguzia Mtanganyika mzigo mkubwa sana.
Hayo 15 ni mzigo kwasababu znz inachangia sifuri, zero! Utakuwa umeondoa malalamiko mengi

Mzigo wa Watalii wa znz Dodoma kaubeba Mtanganyika. Mzigo wa mishahara ya znz kaubeba Mtanganyika, mzigo wa nishati ya umeme kaubeba Mtanganyika na Zigo la pesa zisizo na audit kupitia ofisi ya makamu wa Rais kaubeba Mtanganyika.

Mzigo wa wafanyakzi wa znz katika muungano ambao sifa kubwa ni uzanzibar kaubeba Mtanganyika, kuanzia mishahara hadi mafao ya uzeeni.

Dodoma peke yake tuna Watalii 80 kutoka znz ambao kila mwezi mmoja analipwa milioni 10 sawa na milioni 800 kwa mwezi. Kwa mwaka ni zaidi ya bilioni 9.6 ambazo SMZ inachangia.

Hoja kubwa ni kuwa misaada na mikopo inakuja kwa jina la Tanzania. Tume imesema wznz wapewe nafasi ya kukopa na kulipa madeni yao. Wapewe nafasi ya kutafuta misaada yao.
Tanganyika nayo iwe hivyo, hivi kuna tatizo gani hapo?

Wenye hoja ya misaada na mikopo wanasahu gharama kubwa alizobeba Mtanganyika katika muungano wa serikali 2. Gharama zote za Dodoma sasa hivi kazibeba Mtanganyika.

Haiingii akilini kusema kuwa ni nafuu kuwa na mambo 22 ya muungano kuliko mambo 7. Sijui hesabu hizo wenzetu wanazipata wapi. Halafu wapo wanaodai eti mambo ya muungano yatenganishwe tukiwa na serikali 2, tunawauliza hayo yasiyo ya muungano kwa upande wa Tanganyika yahudumiwe na nani na kwa gharama kutoka wapi, hakuna jibu.

Kwa ufupi serikali 2 zimembebesha Mtanganyika mzigo mkubwa sana wa kodi.
Tumewauliza wa serikali 2 watupe namna watakavyoendesha serikali bila upande mmoja kuumia na jinsi serikali 3 zitakavyoongeza gharama.

Nguvu asante sana kwa kuchambua, na hapo ndio maana nasema muungano wa serikali tatu ni kupotezeana muda tuu, kwani Zanzibar hawana economic strength ya kuchangia kuongoza hata hayo mambo 7. Na kama mnataka tuwe na uchangiaji proportional kwenye kuendesha serikali ya Muungano ni obvious Zanzibar itashindwa in few years. Zanzibar National Income yao haiwezi kusastain hata Zanzibar kujiendesha yenyewe, sasa ukisema wachangie at proportional level (kitu ambacho ni wishful thinking) miaka 2 au mitatu mbele wata collapse na tutarudi kwenye ubao kuanza upya.

Ndio maana mimi nasema kwamba hiii structure ya serikali tatu ambayo Jaji Warioba na wengine wana champion ni kupotezeana muda tuu, sababu miaka mitatu mminne this thing will collapse. Sasa kwa nini tuwekeze muda kwenye kitu kitachokufa. Uvivu wa kufikiri tulionao na uwoga wa kufanya maamuzi magumu ndio unatumaliza mpaka tunakuja na simple ideas kama hizi za serikali tatu.

Make no mistake, mimi sio mshabiki wa serikali mbili, na am not naive kudhani serikali mmoja inaweza kupewa nafsi. However, kama mnataka huu muungano basi lazima tutengeneze framework ya kwenda kwenye serikali moja. I know hii ni ngumu kufikirika sababu ya uvivu wetu wa kufikiri, lakini ni kitu kinachowezekana.

Kwa kutumia mfumo tulio nao, tunaweza kutengeneza development phase ambazo tutakuwa tunakubaliana ndani ya muda tutakao kubaliana. Mfano by 2030 jeshi liwe moja, hakuna sijui kokosi cha ulinzi znz bali ni Jeshi la Tanzania. Hii framework inawezekana na ina potential ya kudumu kuliko hizi kelele za serikali 3.

Kuliko tuongee serikali 3 bora tujadili economic block kati yetu na Zanzibar.
 
Ni dhahiri kwamba wanaotaka serikali tatu hawana malengo ya kuboresha muungano, bali wanataka kuvunja Muungano, Ila kwa kuwa Mazingira ya sasa hayaruhusu kuvunja muungano wanataka waende step by step ili hatimaye muungano ujifie kifo cha mende!.

(1) Wengi wanaotetea serikali ya Tanganyika wanafanya hivyo kwa sababu wamechoka na kelele za Wazanzibari, Wamekasirishwa na kitendo cha Zanzibar kuvunja katiba kwa kujiita "Nchi" kwa hiyo kwa hasira wanataka serikali ya TAnganyika!!. Je kuwa na serikali ya Tanganyika kutaizuia vipi Watanganyika au Wazanzibari kuvunja katiba huko mbeleni, waheshimiwa hawa hawatuambii!!!. Wanaamini Serikali ya Tanganyika itatatua hayo!

(2) Wanaoitaka sana serikali ya Tanganyika kwani Hamuwezi kuipata nje ya Muungano wa magumashi wa serikali Tatu?- ANZENI KAMPENI YA KUVUNJA MUUNGANO IELEWEKE WAZI!, KUSUBIRI ZILETWE SERIKALI TATU HALAFU MUUNGANO UFE NI NJIA YA MZUNGUUKO SANA , NJIA FUPI NI KUVUNJA MUUNGANO ASAP!

(3) Mwalimu alisema wanaodhani kuendesha serikali ya shirikisho siyo gharama kubwa nanukuu "ni watu wanaofikiri kwa ndimi zao wawaulize wazanzibari". na kiukweli kabisa kuendesha aina ya muungano wa serikali tatu unafaa zaidi kwa nchi zinazoshabihiana kwa ukubwa (idadi ya watu, uchumi au eneo), otherwise zinaweza kwa na ushirikiano wa karibu , kiukweli kabisa hakuna mtu aliyeipinga hoja hii kwa hoja mpya madhubuti

(4)kwa maoni yangu KULIKO KUWA NA SERIKALI TATU NI BORA TUGAWANE MBAO, KWA SABABU TIJA YA SERIAKLI TATU NI NINI HASWA?,

SERIKALI MBILI ZILIZOBORESHWA NDIYO MUJARRAB KWA MAZINGIRA YETU (WATU NA MAZINGIRA KAMA ANAVYOSEMA MKANDARA)
 
Gamba la Nyoka,

Hoja zetu juu ya Tanganyika hazikuanza na suala la katiba ya zanzibar (2010). Ukipata muda na kama utakuwa na interest, tembelea profile yangu na utazame najadili nini juu ya umuhimu wa kuiridisha Tanganyika; nje ya mijadala ya mwaka huu, mwaka 2013 kurudi nyuma, hakuna sehemu tumetaja katiba ya znz ya 2010; pamoja na hayo, mijadala ile kama kawaida mmeikimbia; nisingependa kurudia hoja zangu za kule humu kwani zipo kule archived;

Nikufahamishe tu kidogo:
Suala la katiba ya znz (2010) linaendana na hoja zetu za muda mrefu kwamba zanzibar itakuwa na mamlaka kamili iwapo tu itahakikisha kwamba inashinikiza kurudi kwa Tanganyika; kwahiyo walichofanya ni sahihi na ni kwa mujibu wa mkataba wa muungano wa 1964; tunapotaja taja uvunjaji wa katiba ya JMT kulikofanywa na znz ni katika kuonyesha mapungufu yaliyopo kwa ccm na serikali yake inayoendelea kupigania mfumo wa serikali mbili ambao kwa kweli, mwisho wake ni maafa kwa muungano wenyewe;



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Nguvu asante sana kwa kuchambua, na hapo ndio maana nasema muungano wa serikali tatu ni kupotezeana muda tuu, kwani Zanzibar hawana economic strength ya kuchangia kuongoza hata hayo mambo 7. Na kama mnataka tuwe na uchangiaji proportional kwenye kuendesha serikali ya Muungano ni obvious Zanzibar itashindwa in few years.

Zanzibar National Income yao haiwezi kusastain hata Zanzibar kujiendesha yenyewe, sasa ukisema wachangie at proportional level (kitu ambacho ni wishful thinking) miaka 2 au mitatu mbele wata collapse na tutarudi kwenye ubao kuanza upya.

Ndio maana mimi nasema kwamba hiii structure ya serikali tatu ambayo Jaji Warioba na wengine wana champion ni kupotezeana muda tuu, sababu miaka mitatu mminne this thing will collapse. Sasa kwa nini tuwekeze muda kwenye kitu kitachokufa. Uvivu wa kufikiri tulionao na uwoga wa kufanya maamuzi magumu ndio unatumaliza mpaka tunakuja na simple ideas kama hizi za serikali tatu.

Make no mistake, mimi sio mshabiki wa serikali mbili, na am not naive kudhani serikali mmoja inaweza kupewa nafsi. However, kama mnataka huu muungano basi lazima tutengeneze framework ya kwenda kwenye serikali moja. I know hii ni ngumu kufikirika sababu ya uvivu wetu wa kufikiri, lakini ni kitu kinachowezekana.

Kwa kutumia mfumo tulio nao, tunaweza kutengeneza development phase ambazo tutakuwa tunakubaliana ndani ya muda tutakao kubaliana. Mfano by 2030 jeshi liwe moja, hakuna sijui kokosi cha ulinzi znz bali ni Jeshi la Tanzania. Hii framework inawezekana na ina potential ya kudumu kuliko hizi kelele za serikali 3.

Kuliko tuongee serikali 3 bora tujadili economic block kati yetu na Zanzibar.
Basically unakubalina nami kuwa mzigo wa kuiendesha znz ameubeba Mtanganyika.

Lakini pia si kweli kuwa znz haiwezi kuiendesha. Leo muungano ukifa znz itabaki kuwa na vyombo vya ulinzi na usalama kama jeshi. Je, hizo gharama za kuliendesha jeshi watazitoa wapi? Kama zipo kwanini wasiweze kuchangia sasa hivi kiwango hicho walicho nacho?

Ukisoma rasimu ya Warioba katika yale mambo 7, yote ni lazima kwa kuwa na muungano au usiwepo. Lazima znz itakuwa na uhusiano wa kimataifa na kuchangia gharama zake. Lazima itakuwa na vyama vya siasa na usajili wake na lazima itakuwa na katiba na taasisi zake. Zote hizo zinahitaji gharama, kwanini useme hawawezi? Muungano ukifa leo utaweza kusema znz itafutika! jibu ni hapana, itakuwepo na kujiendesha, sasa kwanini leo waonekane hawawezi?

Kinachotokea ni kiburi cha znz kwamba Tanganyika itachangia. Wao hoja kubwa ni misaada na mikopo. Warioba kaonyesha kuwa serikali 3 zitawapa uwezo huo wa kukopa na kupata misaada. Kama ni hivyo kwanini wasiweze kuchangia muungano.

Na muhimu sana wznz wenyewe wanataka mamlaka kamili. Hivi mamlaka hayo yatapatikanaje kama wanaamini kuwa hawawezi kujiendesha. Wanataka ubia sawa katika muungano, ubia huo upo wapi kama hawana cha kuchangia.
Au ndio ubia wa nafasi za ubalozi, vyeo na ajira ambazo hawajui gharama zake.
Kwamba Mtanganyika aumie ili mznz achangie mambo yasiyo na tija kama vyeo na nafasi wanazolilia sana za ubalozi!
Kwa wenzetu hawana gharama, wanachotaka ni usawa wa vyeo, watoto wao kusoma bure, watalii kuja Dodoma kwa jina la wabunge n.k. Hali hii itaendelea hadi lini.

Dvelopment phase ni ndoto. Nyerere na Karume walianza hivyo, maendeleo tuliyofikia ni yale ya katiba ya ZNZ kujitoa katika muungano kijanja, wakivizia maeneo yenye gharama wamsukumie Mtaanganyika. Hivi kwanini hamulioni hili?

Kwasasa hivi muungano haupo, kilichopo ni znz kutumia jina kupata mafao. Wakati huo huo kutumia uzanzibar kunyanyasa Mtanganyika. Tutakuwaje na development phase wakati Mtanganyika ana kibali kuishi znz.

 
Back
Top Bottom