Mtazamo kuhusu Hotuba ya JK kuzindua Bunge Maalum la Katiba

Mtazamo kuhusu Hotuba ya JK kuzindua Bunge Maalum la Katiba

Nilipo underline,

Naomba nikusahihishe kidogo.

Pesa za waliokuwa wafanyakazi wote wa EAC zilitolewa na UK baada ya tafiti na kujua stahili za wafanyakazi wote kutokana na mishahara yao na nchi wanazotoka na zikapelekwa kwa nchi zote husika. Kenya na Uganda waliwalipa kama ilivyoelezwa katika mchanganuo wao. TZ walizitumia katika Vita ya Uganda na hivyo kutowalipa wastahafu hao mpaka leo.

Mwongo mkubwa! Usiudanganye umma. Lazima ujiridhishe na maandiko kabla ya kuandika. Katika jukwaa hili ustaarabu hutamalaki na ni nadra kusoma neno kama muongo. Kwako tunalitumia kwasababu huoenkani kuliheshimu jukwaa.

Jumuiya ya Afrika mashariki ilikufa mwaka 1977.
Vita ya Kagera ilikuwa 1978 chini ya mwaka mmoja tangu EAC ivunjike.

Dr Victor Umbrich alimaliza mediation of assets and liabilities of the defunct EAC mwishoni mwa miaka ya 1988-90.
Baada ya taarifa ya Victor Umbrich mgawanyo wa mali ukamalizika na kuundwa chombo kingine cha kuangalia namna ya uhusiano wa siku za baadaye. Wakati huo waliokuwa madarakani ni Ali Hassan Mwinyi, Moi na Museveni.

Nyerere hakuwa madarakani wala Amin hakuwepo Uganda. Hiyo research iliyofanyika umehadithiwa bila kuingia maktaba kujiridhisha na ulichosikia mitaani. Haiwezekani jumuiya ife 1977 na mwaka 1978 research imekamilika. Na labda ujiulize UK ilitoa pesa katika misingi gani. Hadithi za mitaani kwa mtu wa doctorate level ni aibu.

Wafanyakazi wa nchi nyingine walilipwa miaka zaidi ya 15 baada ya kifo cha EAC.

Sijui inakusaidia nini kusema uongo. Tafadhali sana jiridhishe na unachoandika. Too low
 
Mwongo mkubwa! Usiudanganye umma. Lazima ujiridhishe na maandiko kabla ya kuandika. Katika jukwaa hili ustaarabu hutamalaki na ni nadra kusoma neno kama muongo. Kwako tunalitumia kwasababu huoenkani kuliheshimu jukwaa.

Jumuiya ya Afrika mashariki ilikufa mwaka 1977.
Vita ya Kagera ilikuwa 1978 chini ya mwaka mmoja tangu EAC ivunjike.

Dr Victor Umbrich alimaliza mediation of assets and liabilities of the defunct EAC mwishoni mwa miaka ya 1988-90.
Baada ya taarifa ya Victor Umbrich mgawanyo wa mali ukamalizika na kuundwa chombo kingine cha kuangalia namna ya uhusiano wa siku za baadaye. Wakati huo waliokuwa madarakani ni Ali Hassan Mwinyi, Moi na Museveni.

Nyerere hakuwa madarakani wala Amin hakuwepo Uganda. Hiyo research iliyofanyika umehadithiwa bila kuingia maktaba kujiridhisha na ulichosikia mitaani. Haiwezekani jumuiya ife 1977 na mwaka 1978 research imekamilika. Na labda ujiulize UK ilitoa pesa katika misingi gani. Hadithi za mitaani kwa mtu wa doctorate level ni aibu.

Wafanyakazi wa nchi nyingine walilipwa miaka zaidi ya 15 baada ya kifo cha EAC.

Sijui inakusaidia nini kusema uongo. Tafadhali sana jiridhishe na unachoandika. Too low

Nguruvi3 acha kukurupuka kwani nilichoandika mimi kwa kifupi ndicho ulichofafanua wewe LAKIN UMESHINDWA TU KUTOA JIBU KWA NINI UK WALILIPA?

Na hakuna pahala niliposema walilipwa lini. ULITAKIWA KUJIULIZA KWANINI UGANDA NA KENYA walilipwa na TZ hawalipwa kwanini?

Lakin kwa kukusaidia zaidi pesa hizo zilitumika kulipia madeni ya vita yenu na Uganda. Kama utakumbuka baada ya vita ya Uganda, NYERERE aliwaambia wananchi wake kuwa WAFUNGE MIKANDA YA KIUCHUMI KWA MIEZI 18. Jiulize je mpaka anaondoka duniani aliwahi kuwaambia MUIFUNGUE mikanda hiyo?

Kumbuka ahali yangu lugha nzuri ni silaha, lugha chafu ni kujidhalilisha. kama hujui tueleze tukudarsishe kwani ndio nia ya barza hii.

Pole sana
 
Pesa za waliokuwa wafanyakazi wote wa EAC zilitolewa na UK baada ya tafiti na kujua stahili za wafanyakazi wote kutokana na mishahara yao na nchi wanazotoka na zikapelekwa kwa nchi zote husika.

Kenya na Uganda waliwalipa kama ilivyoelezwa katika mchanganuo wao.
TZ walizitumia katika Vita ya Uganda na hivyo kutowalipa wastahafu hao mpaka leo.


?

Lakini kwa kukusaidia zaidi pesa hizo zilitumika kulipia madeni ya vita yenu na Uganda.
Pesa kutumika katika vita ni tofauti na pesa kutumika katika kulipa madeni.
Nadhani baada ya kukupa data unafanya U-turn. Jiridhishe kwanza kabla ya kuandika. Mitaani unaweza kueleweka, si kila mahali utaeleweka.
 
Pesa kutumika katika vita ni tofauti na pesa kutumika katika kulipa madeni YA VITA. ULISAHAU KUMALIZIA HAPA. NITENDEE HAKI
Nadhani baada ya kukupa data unafanya U-turn. Jiridhishe kwanza kabla ya kuandika. Mitaani unaweza kueleweka, si kila mahali utaeleweka.

Labda kwa lugha ya kwako ndio ujaelewa lakin kwangu mimi kutumika katika kulipa madeni ya vita ua uganda na kutumika katika vita ya uganga ni sawa tu kwani muradi mkuu hapo zilitumika katika vita ya uganda kwa kulipa baada ya vita.

Labda kwa faida ya wasomaji wengine wasojua hilo TUPAMBANULIE KWANINI UK WALITOA PESA HIZO.n Na je NYERERE alipowaambia wananchi wake wafunge mikanda ya kiuchumi kwa miezi 18, je ilipotimu aliwaambia wafungue? kwanini alishindwa kufanya hivyo?

Mimi nitasherehesha kukwambia zilikuwa kiasi gani na zilitumikaje kwani wakti huo nilikuwa wizara ya fedha na mipango.

Pole sana

 
Labda kwa faida ya wasomaji wengine wasojua hilo TUPAMBANULIE KWANINI UK WALITOA PESA HIZO. Na mimi nitasherehesha kukwambia zilikuwa kiasi gani na zilitumikaje kwani wakti huo nilikuwa wizara ya fedha na mipango.

Nilichosema ni kuweka sawa kauli zako mbili.
1. Pesa zilitumika katika vita
2. Pesa zilitumika kulipa madeni

Hivi ni vitu viwili tofauti. Hakuna mahali nimesema pesa zilitolewa.
 
HOTUBA YA JK YAKOSA MASHIKO
MBUINU ZA KUHARIBU MCHAKATO ZAANZA KWA KUTUMIA GHARAMA ZA IKULU
WAZEE SASA HUNYWA CHAI IKULU, VIJANA WASITA KUMUUNGA MKONO.


Katika kuonyesha kuwa hotuba ya Rais ilikosa mashiko na ushawishi kwa wananchi, siku za karibuni JK amekuwa katika harakati za kukutana na wazee Ikulu ili kutafuta kuungwa mkono.
Anachotaka ni kuungwa mkono na kundi la wazee,mkakati uliokuwa --------- miaka ya nyuma.

Kundi la wazee ambao wengine hata kuandika majina yao hawawezi ni kundi dhaifu sana katika nchi.Yanapotokea machafuko kama ilivyokuwa Kenya, wazee hawakuwa na ushawishi,walibaki kuwa victims.Kuwatumia ni kupoteza rasilimali za taifa, na hili lipo katika rekodi JK, alitambue.

Kundi lenye ushawishi ni la vijana ambao si tu wanatafuta mustakabali wao, bali pia mustakabali wa vizazi vyao.

Baada ya hotuba yake tumeona hata makundi ya vijana wa CCM yakisita kumuunga mkono.
Hii maana yake ni moja, dhamira zao zinawasuta tena linapokuja suala la Tanganyika.

Vijana na wasomi wanaona hotuba kukosa mtizamo wa kitaifa, kuingiza siasa na kibaya zaidi kujikita katika kuwatukana akina Warioba, Salim, Butiku, maprofesa na tume kwa ujumla.

Wazee akina Warioba walishika madaraka ya nchi JK akiwa hajulikani.
Wanifahamu nchi vizuri kuliko JK.

Wazee hao hawakusoma hotuba za Nyerere bali waliishi na Nyerere wakimwakilisha na kudurusu hotuba zake.

Mbinu alizotumia JK kumkariri Nyerere na Karume hakika zilishusha hadhi na heshima yake.
Hata vijana wanajiuliza, ni kwa nguvu zipi JK anaweza kumtukana Mwanadiplomasia kama Salim Ahmed Salim anayemfahamu Mwalimu tangu miaka ya 60 mwanzoni?

Wengi wanajiuliza hivi JK na Butiku nani anamfahamu Nyerere na nchi hii vizuri.
Kuna uwezekano wa kutofautiana mawazo lakini hilo halitoi fursa ya kutukana wazee hao na maprofesa kana kwamba nchi hii haina elders na watu wenye busara.

Lengo la JK kuwaita wazee linatafsiriwa kama ushawishi wake kwa wajumbe wa bunge la katiba. Ni aina ya kuwatisha kuwa hata wazee wanakubaliana naye.
Hii ni mbinu hafifu na dhaifu na inafumua udhaifu wake zaidi.

Endapo hakuweza kuwashawaishi wajumbe, huku akitumia masaa 2 kumtukana Warioba ni aghalabu kuwatumia wazee wenye njaa kunywa nao chai kutaleta matokeo tofauti.

Gharama anazotumia kuwasafirsha wazee hao ni za serikali na hivyo anapaswa kuulizwa kama alikuwa na dhamira njema na mchakato, na kama hayo si matumizi mabaya ya kodi za wananchi.

JK alipewa nafasi ya kuchagua wajumbe, inabidi ajiulize, kama tume iliona tofauti, na wajumbe wake wa kuteuliwa wanaona tofauti basi yeye atakuwa anaona tofauti sana na ukweli uliopo.

Kukosa mashiko ya hotuba ikiwa ni pamoja na mbinu za kumwalika Warioba ili wamnange ni dalili kuwa JK ni kiongozi wa nchi hii ambaye ana mvuto tu wa kuonekana hana mvuto mwingine wowote, si kisiasa, si busara wala si kiuongozi.

Tusemezane

 
HOTUBA YA KUMDHALILISHA WARIOBA ILIVYOKOSA UMAKINI
JK YUPO TAYARI KUWAPA WAZANZIBAR WANACHOOMBA KWA GHARAMA ZA MTANGANYIKA
ASHINDWA KUELEZA YALE YASIYO YA MUUNGANO NANI ASHUGHULIKIE?


Wana duru bado tunaendelea kuiangalia hotuba ya JK bungeni ambayo madhara yake yameanza kuonekana.
Ukifuatilia wachangiaji wengi, hakika utagundua wamekariri na hawana ufahamu wa wanachozungumza.
Tulisema siku za nyuma bunge la katiba litakuwa kijiwe cha kubadilishana mipasho na matusi, sasa yanatimia.

Wazungumzaji wengi hawana ufahamu,kuhoji na wala hawajui wanachozungumzia.
Haiwezekani mtu asimame na kusema serikali 2 ndio muafaka bila kueleza kwa namna gani

Hayo yanatokana na ukweli kuwa hotuba ya JK ingawa haikuwa na mashiko kwa jamii, ilikuwa na upotoshaji kwa bunge, sasa matokeo yake yapo wazi.

JK alieleza mambo 11 yaliyoongezwa katika mambo ya muungano hadi kufikia 22. Hakuna shaka kuwa mambo hayo 11 yalimsaidia mzanzibar zaidi kwa gharama za Mtanganyika.
Akazungumzia jinsi mambo mengine yalivyoondolewa ingawa yaliingizwa kwa sheria za bunge

Utaratibu ulipo ni kuwa sheria inafutwa na sheria nyingine ya bunge na wala si Rais.
Matatizo tuliyo nayo baadhi yametokana na amri za rais 'decree' za siku za nyuma kama la Tanganyika kuchukua jina la Tanzania na kuwa Tanzania. Rejea bandiko la Mchambuzi
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/635645-siri-ya-hati-ya-muungano-na-njama-za-kuuficha.html

Suala la mafuta na gesi, baraza la mitihani, bandari na anga yalikuwa miongoni mwa mambo ya muungano. Ingawa mengine hayakuwepo mwanzo ni dhahiri kuwa kuingizwa kwake kulikuwa kwa misingi ya sheria.

Zanzibar imeyaondoa bila kufahamisha JMT. Hilo tu linatosha kuifanya ZNZ iwe na mamlaka makubwa juu ya katiba ya JMT . ZNZ ina uwezo wa kuvunja katiba ya JMT bila kuulizwa.
Ndivyo wamefanya kwa miaka ya karibuni na hasa mwaka 2010.

Rais Kikwete anaposema wamezungumza na Aman ili kuondoa baadhi ya mambo ni makosa.
Lazima ima kupitia utaratibu wa kisheria na kama ni kwa decree basi iwepo taarifa.
Hivyo JK alishiriki kuivunja katiba aliyoapa kuilinda ili kuwafurahisha wznz.

Kaendele na kusema zimebaki kero 6 tu sasa hivi. JK akizitaja zote zikuhusu malalamiko ya WZNZ na kudharau ya Watanganyika ili kuwapendeza wznz kwa kuwaambia pipi na peremende zaidi zinakuja. Tumeona wajumbe wa znz walivyokomalia serikali 2 utadhani sio wzn wale wanaoshinda mikutanoni wakimtukana Nyerere na makafir wa Tanganyika.

JK akasema mambo mengine yataondolewa ili znz iwe na uwezo kama wa kukopa, misaada na taasisi zake. JK hakusema kuyatenga mambo hayo kutawezaje kutenganisha mambo ya muungano na yale ya ZNZ.

Znz ni sehemu ya Tanzania, sasa inawezaje kukawa na baraza la mitihani la znz na la JMT?
Kunawezaje kukawa na wizara ya utalii znz na ya JMT ambayo znz haitashiriki.
Kunawezaje kuwa na wizara ya elimu ya juu ya znz na JMT ikiwa znz ni sehemu ya JMT?

Huu ni upotoshaji mkubwa. Huwezi kuwa na mambo ya muungano na yasiyo ya muungano ukiwa na serikali 2. Inawezakana tu kwa ukweli kuwa Mzanzibar atapewa fursa zaidi za kuneemeka kwa mgongo wa Mtanganyika ili hali gharama za neema hizo ni za Mtanganyika.

Hatari waiyoiona wabunge wa Tanzania bara katika BMLK ni hii ya Mtanganyika kuitwa Mtanzania ili abebe mzigo wa Tanzania ambao utakuwa na zigo la znz pembeni huku znz ikiwa likizo.

Nanyi Watanganyika nje ya bunge lazima mjiulize, hivi inawezekanje ukawa na SMZ na JMT halafu ukatenga mambo katika sehemu 3. Sehemu ya 3 itahudumiwa na nani ikiwa sehemu ya pili ni JMT.

Jambo hili tumeliongelea sana katika uzi wa
https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/631833-duru-za-siasa-gharama-za-muungano-siri-isiyozungumzwa.html Tumesema kuwa unapoipa znz fisca autonomy halafu ukaipa access kwa JMT kwa maneno mengine unaipa znz access kwa fiscal autonomy ya Tanganyika. Wakati resources za Tanganyika zikiwa zimeelemewa kuongeza znz ambayo haina mchango ni kumbebesha Mtanganyika mzigo mkubwa sana bila sababu.

Lakini muhimu ni kujiuliza Tanganyika inapobeba muungano peke yake ni sawa na investment.
Je, tuantegemea return gani kwa investment hiyo kubwa kupitia kodi za Watanganyika?

Ni kwanini Mtanganyika apinde mgongo kulipa kodi kubwa ili hali inakwenda nchi jirani?
 
Mkuu Nguruvi3,

Nini mtazamo wako kuhusu Jaji Warioba kutunukiwa nishani ya muungano. Hatua hii ina maana gani, na ina athari gani kwa mchakato wa katiba unaoendelea?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3,

Nini mtazamo wako kuhusu Jaji Warioba kutunukiwa nishani ya muungano. Hatua hii ina maana gani, na ina athari gani kwa mchakato wa katiba unaoendelea?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mchambuzi , hili umenigusa sana. Tafadhali naomba subira tunaandaa nbandiko maalumu kuhusu suala hili.

Kwa ufupi tutaelezea kuhusu haya
1. Aibu ya Kikwete
2. Mbinu za kudhoofisha rasimu
3. Wagawe uwatawale
4. Kupooza hasira ndani ya chama na wananchi
5. Kupunguza kasi ya chati ya Warioba inayozidi kung'aa
5. Aibu mbele ya jumuiya ya kimataifa.

Bandiko lipo njiani.
 
Back
Top Bottom