Mtazamo kuhusu Hotuba ya JK kuzindua Bunge Maalum la Katiba

Mtazamo kuhusu Hotuba ya JK kuzindua Bunge Maalum la Katiba

Basically unakubalina nami kuwa mzigo wa kuiendesha znz ameubeba Mtanganyika.

Lakini pia si kweli kuwa znz haiwezi kuiendesha. Leo muungano ukifa znz itabaki kuwa na vyombo vya ulinzi na usalama kama jeshi. Je, hizo gharama za kuliendesha jeshi watazitoa wapi? Kama zipo kwanini wasiweze kuchangia sasa hivi kiwango hicho walicho nacho?

Ukisoma rasimu ya Warioba katika yale mambo 7, yote ni lazima kwa kuwa na muungano au usiwepo. Lazima znz itakuwa na uhusiano wa kimataifa na kuchangia gharama zake. Lazima itakuwa na vyama vya siasa na usajili wake na lazima itakuwa na katiba na taasisi zake. Zote hizo zinahitaji gharama, kwanini useme hawawezi? Muungano ukifa leo utaweza kusema znz itafutika! jibu ni hapana, itakuwepo na kujiendesha, sasa kwanini leo waonekane hawawezi?

Kinachotokea ni kiburi cha znz kwamba Tanganyika itachangia. Wao hoja kubwa ni misaada na mikopo. Warioba kaonyesha kuwa serikali 3 zitawapa uwezo huo wa kukopa na kupata misaada. Kama ni hivyo kwanini wasiweze kuchangia muungano.

Na muhimu sana wznz wenyewe wanataka mamlaka kamili. Hivi mamlaka hayo yatapatikanaje kama wanaamini kuwa hawawezi kujiendesha. Wanataka ubia sawa katika muungano, ubia huo upo wapi kama hawana cha kuchangia.
Au ndio ubia wa nafasi za ubalozi, vyeo na ajira ambazo hawajui gharama zake.
Kwamba Mtanganyika aumie ili mznz achangie mambo yasiyo na tija kama vyeo na nafasi wanazolilia sana za ubalozi!
Kwa wenzetu hawana gharama, wanachotaka ni usawa wa vyeo, watoto wao kusoma bure, watalii kuja Dodoma kwa jina la wabunge n.k. Hali hii itaendelea hadi lini.

Dvelopment phase ni ndoto. Nyerere na Karume walianza hivyo, maendeleo tuliyofikia ni yale ya katiba ya ZNZ kujitoa katika muungano kijanja, wakivizia maeneo yenye gharama wamsukumie Mtaanganyika. Hivi kwanini hamulioni hili?

Kwasasa hivi muungano haupo, kilichopo ni znz kutumia jina kupata mafao. Wakati huo huo kutumia uzanzibar kunyanyasa Mtanganyika. Tutakuwaje na development phase wakati Mtanganyika ana kibali kuishi znz.


Nguvu unajua kuzungumza bila kutumia data ni sawa na ile rasimu ya Warioba ambayo imejaa assumption kama kujaribu kuhakiki mwezi ni sawa na juwa. Sasa kama unasema kwamba Zanzibar wanaseza kujiendesha tuangalie ni kwa vipi, GNI (Gross National Income) ni 850Million USD (2012 data) jee unadhani wanaweza kutoa asilimia zozote kufund kitu chochote hapo. Hiyo pesa inalipa salary mchezo umekwisha.

Ndio maana nasema tujadilini Muungano au No muungano tusizunguke mbuyu kwa kusema serikali 3 ndio solution.
 
Ni dhahiri kwamba wanaotaka serikali tatu hawana malengo ya kuboresha muungano, bali wanataka kuvunja Muungano, Ila kwa kuwa Mazingira ya sasa hayaruhusu kuvunja muungano wanataka waende step by step ili hatimaye muungano ujifie kifo cha mende!.

(1) Wengi wanaotetea serikali ya Tanganyika wanafanya hivyo kwa sababu wamechoka na kelele za Wazanzibari, Wamekasirishwa na kitendo cha Zanzibar kuvunja katiba kwa kujiita "Nchi" kwa hiyo kwa hasira wanataka serikali ya TAnganyika!!. Je kuwa na serikali ya Tanganyika kutaizuia vipi Watanganyika au Wazanzibari kuvunja katiba huko mbeleni, waheshimiwa hawa hawatuambii!!!. Wanaamini Serikali ya Tanganyika itatatua hayo!

(2) Wanaoitaka sana serikali ya Tanganyika kwani Hamuwezi kuipata nje ya Muungano wa magumashi wa serikali Tatu?- ANZENI KAMPENI YA KUVUNJA MUUNGANO IELEWEKE WAZI!, KUSUBIRI ZILETWE SERIKALI TATU HALAFU MUUNGANO UFE NI NJIA YA MZUNGUUKO SANA , NJIA FUPI NI KUVUNJA MUUNGANO ASAP!

(3) Mwalimu alisema wanaodhani kuendesha serikali ya shirikisho siyo gharama kubwa nanukuu "ni watu wanaofikiri kwa ndimi zao wawaulize wazanzibari". na kiukweli kabisa kuendesha aina ya muungano wa serikali tatu unafaa zaidi kwa nchi zinazoshabihiana kwa ukubwa (idadi ya watu, uchumi au eneo), otherwise zinaweza kwa na ushirikiano wa karibu , kiukweli kabisa hakuna mtu aliyeipinga hoja hii kwa hoja mpya madhubuti

(4)kwa maoni yangu KULIKO KUWA NA SERIKALI TATU NI BORA TUGAWANE MBAO, KWA SABABU TIJA YA SERIAKLI TATU NI NINI HASWA?,

SERIKALI MBILI ZILIZOBORESHWA NDIYO MUJARRAB KWA MAZINGIRA YETU (WATU NA MAZINGIRA KAMA ANAVYOSEMA MKANDARA)
Nadhani upo mbali na historia. Suala la serikali 3 halikuanza na Warioba. Limeanza tokea wakati wa Mwalimu, Jumbe, likaja G55, zikaundwa tume 7. Katika tume zote zikiwa chini ya makada wa CCM hoja ni serikali 3.

Sauti ya serikali 3 ni CUF, Uamsho na hivi karibuni CCM. Ni hoja ya wznz , na kusema Warioba ni makosa.
Alichokifanya ni ku summarize na kufanyia analysis maaoni na muundo utakaokidhi haja ya mazingira na wakati.

Taasisi zilitozotoa maoni ya serikali 3 ni Ofisi ya makamu wa kwanza wa Rais, Ofisi ya waziri mkuu wa JMT, Baraza la wawakilishi znz , taasisi za elimu za juu pamoja na watu mashuhuri na nguli katika migogoro ya kikatiba.

Wanaotetea znz hawajakasarishwa na uvunjaji wa katiba. Wanachokifanya ni kuzuia matatizo makubwa mbele ya safari.
Znz imevunja katiba na haikukemewa.JK hakuweza kunyanyua ulimi na kukemea kitendo kiovu kuliko vyote katika historia ya nchi.

Tungalikuwa watu makini JK angeshaondoka ofisini siku nyingi.
Ameshindwa kuilinda na kuitetea katiba ya JMT hadi kufikia mahali JMT inakuwa idara ya Baraza la wawakilishi(BLW)

Leo Kikwete hawezi kusema kwasababu yeye ni Tanzania, hawezi kufungua kesi ya kikatiba dhidi ya rais wa znz ambaye znz ni mjumbe wa baraza la mawaziri la Kikwete. Watanganyika hawana mtu wa kuwasemea.

Miswada ya kujenga wodi za wazazi lazima ikaIdhinishwe na kundi la watu 50 wanaoitwa BLW.
Hata tukiataka kujenga nyumba 100 kwa walimu wa shule lazima wazanzibar 80 ndani ya bunge la JMT wakibali, halafu Mh waziri mkuu wa JMT apeleke maombi ya kukubaliwa kwa Pandu Kificho na wenzake 49(BLW)watathmini ulazima wa kufanya hayo.

Uwepo wa Tanganyika una maana kuu hizi, kuimarisha muungano kwa ''kutowaumiza wznz''
Kutenganisha mambo ya muungano na yasiyo ili Tanganyika ijue lipi ni mzigo wake na znz nayo
Kupunguza gharama kwa Mtanganyika ambaye anayebeba mzigo wa kodi ili kuibembeleza znz kwa pipi, kashata na urojo.

Na mwisho, itajenga nidhamu kwasababu leo tungekuwa Tanganyika ingeliwezekana kwenda mahakama ya juu na kusema ZNZ wamevunja katiba. Kwavile hatuna Tanganyika hatuna wa kutusimamia na hapo tunakuwa loser.

Mwalimu aliposema hivyo alikuwa anaangalia znz kama sehemu ya Tanzania.
Wznz wameamua kwa makusudi kabisa kukimbia muungano(2010).

Nyerere alisema kama hawataka muungano hatawapiga mabomu, ninyi wenzetu kwanini mnataka wapigwe mabomu huko mitaani kwa kuidai znz yao? Mbona hamsemi ya Nyerere kwa ukamilifu wake.

Kuhusu kuvunja jahazi, mbona limevunjika kwa katiba ya 2010? Sasa hivi ni kuziba nyufa kwa serikali 3, kama hutataki basi hewala, mbao zipo wapi kila mmoja achukue upande wake na misumari, kila la heri

Na mwisho, unasema serikali 2 zilizoboreshwa ndiyo njia MUJARABU.
Nakuomba usikimbie hili bandiko ili tupate elimu yake. Mwenzako Mkandara kila akiulizwa anakimbia.

1. Kuna njia zipi za kuboresha muungano ambazo kwa miaka 50 hazikuweza kutumika na sasa tunadhani zinazweza kuondoa kero.

2. Kwa vile kuna malalamiko ya Tanganyika kuwa Tanzania na kufaidika na Tanzania, tunawezaje kutenga mambo ya Znz, Tanzania na yale yasiyo ya muungano.

3. Kwa mambo yasiyo ya muungano ambalo ni lalamiko kubwa kwa wazanzibar, tutayaweka wapi, yashughulikiwe na nani na gharama kutoka wapi.

Tafadhali sana jikite katika maswali hayo matatu ili tupate elimu ya serikali mbili Mujarabu.

Ukumbi ni wako
 
Nguvu unajua kuzungumza bila kutumia data ni sawa na ile rasimu ya Warioba ambayo imejaa assumption kama kujaribu kuhakiki mwezi ni sawa na juwa. Sasa kama unasema kwamba Zanzibar wanaseza kujiendesha tuangalie ni kwa vipi, GNI (Gross National Income) ni 850Million USD (2012 data) jee unadhani wanaweza kutoa asilimia zozote kufund kitu chochote hapo. Hiyo pesa inalipa salary mchezo umekwisha.

Ndio maana nasema tujadilini Muungano au No muungano tusizunguke mbuyu kwa kusema serikali 3 ndio solution.
Kama ni hivyo Muungano ukivunjika nani atawahudumia?
Pili, mamlaka kamili wanayotaka ni yapi?
Kwanini gharama za nchi huru (katiba 2010) zibebwe na Mtanganyika? Kwanini sisi na si Kenya au Comoro

Mbona data tumeshaweka siku nyingi? Kwani unataka zipi?
 
Mtanganyika na Bongolander,

Kwa kuongezea tu kidogo katika suala la gharama ambalo mnajadiliana na Nguruvi3, ningependa kuchangia yafuatayo:

Muundo wa serikali mbili wa sasa unaifanya serikali ya muungano kwa kiwango kikubwa sana kushughulikia zaidi mambo ya Tanzania Bara (Kimsingi Tanganyika), hasa katika eneo ambalo linawagusa zaidi znz - suala zima la economic development; kwa mujibu wa katika ya JMT (1977), serikali ya muungano (basically ya Bara), ina mamlaka ya kusimamia mambo ya muungano na yasiyo ya muungano kwa upande wa "Tanzania Bara"; kwa mantiki hii ya kikatiba, Serikali ya muungano inajishughulisha mno na masuala kama vile Maji, afya, umeme, kilomo, elimu, nishati na madini, maliasili na utalii, ujenzi na mengine mengi ambayo "siyo ya muungano"; hilo ni moja;

Pili, wakati wa vipindi vya bunge la bajeti kila mwaka, bunge la muungano huwa linatenga siku mbili hadi nne kujadilia masuala haya yasiyo ya muungano. Msisitizo: Bunge la muungano hutumia muda mwingi zaidi kujadili masuala yasiyo ya muungano, yani ya Tanzania Bara (Tanganyika). Na masuala ya muungano yani: Ulinzi, mambo ya nje, mambo ya ndani, muda unaotenga huwa hauzidi siku moja ya majadiliano; kuna nyakati hutengewa hata nusu siku;siku zikizidi huwa ni nadra na ni kwa kutokusudiwa; tuendelee:

Maswali ya wabunge wa bunge hili la muungano juu ya masuala ya maendeleo pia huwa yanahusu Tanzania bara pekee; lini umesikia kuna maswali ya wabunge kuhusu kuchelewa kukamilika kwa barabara inayoenda "raha leo"? Kumbuka, hili ni bunge la muungano - lenye kujadili na kufanya maamuzi kisera na kisheria kwa wananchi wa pande zote mbili; tuendelee:

Miradi ya maendeleo: Ziara za wabunge kukagua miradi hii huwa zinahusu Tanzania bara tu/masuala yasiyokuwa ya muungano kwa bara, lakini ziara hizi zimejaa watalii kutoka zanzibar kama anavyojadili Nguruvi3. Mambo yote haya yanasimamiwa na Waziri Mkuu eti wa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania", wakati ukweli kama unavyojadiliwa na nguruvi3, huyu hana mamlaka yoyote kuhusu Zanzibar. Tuendelee:

Muundo huu wa serikali mbili umepelekea kuwepo kwa wizara na taasisi ambazo zenye mwonekano wa:
1. Muungano tu.
2. Mambo ya Tanzania bara.
3. Mambo mchanganyiko - ya muungano na yasiyokuwa ya muungano.

Hali hii inatupa wakati mgumu sana wa ktofautisha baina ya gharama za muungano na zisizo za muungano katika wizara na taasisi husika. Hata serikali yenyewe inapata wakato mgumu sana kutofautisha gharama hizi;

Kundi la pili na la tatu hapo ndio moja ya vyanzo vikuu vya kero zilizopo sasa yani - mambo ya Tanzania bara na mambo ya mchanganyiko; nguruvi3 kayaelezea kwa undani zaidi kwa ufasaha sana.

Ni vigumu sana kuelewa kwanini hatuoni tatizo hili; na hii ndio mantiki ya serikali tatu kama anavyojadili Nguruvi3 iwapo bado tunautaka muungano;

Hatuna jinsi bali kuleta serikali tatu, na wazanzibari wanahitaji sana Tanganyika kama tulivyokwisha jadili - hivyo ndivyo watakuwa na mamlaka kamili wanayoitaka. Na kama alivyojadili nguruvi3, yapo ya msingi ambayo lazima wagharamie hata kama muungano utakufa. Vinginevyo:

Kwa sasa, serikali ya muungano haina mamlaka ya kutosha juu ya masuala ya maendeleo kwa upande wa zanzibar kama nilivyoonyesha. Hata mawaziri wengi na serikali vile vile hulazimika kupanga mipango ya maendeleo kwa ajili ya Tanzania bara kuliko zanzibar;ushahidi upo wazi katika bajeti za kila mwaka; zanzibar huwa na mipango yake, lakini kama alivyojadili nguruvi3, ili zanzibar ipate resources kama mikopo na misaada, ni lazima ipitie serikali ya muungano; mfumo huu umeleta matatizo makubwa sana, na licha ya juhudu za serikali ya muungano kulitatua, hakuna ufumbuzi umepatikana hadi leo;
Bongolander na Mtanganyika:
Njia pekee ya kufanya maendeleo ya zanzibar yawe na uzito sawa na mambo ya Tanzania bara ni kuyaweka mambo yote hayo kuwa chini ya serikali ya muungano yani - Tanzania kuwa na serikali moja kama mnavyopendekeza; lakini ukweli ni kwamba hili haliwezi tokea kwani zanzibar's grievances has always been "kumezwa na muungano"; Mtanganyika, uutakebehi sana hoja zetu za serikali tatu kama njia ya kulinda muungano, lakini facts ndio hizo hapo - serikali moja haitatokea kamwe, na watakaopinga ni Zanzibar;

Next, nitakuja na mapendekezo ya CCM ambayo yapo katika rasimu yake mbadala, mapendekezo ambayo kwa kweli yataibua vihoja bungeni;

Cc Gamba la Nyoka



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi
Mtanganyika , Mkandara na Gamba la Nyoka wanaamini kuwa serikali 2 ni jawabu.
Wasichojibu ni mambo uliyouliza hapo juu na niliyowahi kuuliza.

Kipi kifanyike ambacho hakijafanyika miaka 50 ili kuondoa kero zilizopo na si kinadharia?
Pili, katika serikali 2 tunawezaje kutenga mambo ya Muungano, na yasiyo ya muungano ili znz iridhike?
Tatu, yale yasio ya muungano yashughulikiwe na nani,kwa gharama kutoka wapi.

Ukishauliza haya masuala wanakimbia, baada ya wiki wanarudi na hoja zile zile.
Hebu tuwasikilize pengine wanajikusanya mahali, they will come back swinging lol
 
Watetezi wa serikali mbili wakiongozwa na kina Gamba la Nyoka, wanatetea maboresho ambayo kwa kweli yatazua vihoja bungeni watu wao walioandaliwa watakapopewa fursa ya kuchangia kuhusiana na suala la muungano ndani ya BLK. Yafuatayo ni baadhi ya maboresho ambayo ni sehemu ya mapendekezo ya ccm kuhusu rasimu ya katiba yaliyowasilishwa na Asha Rose Migiror kwenye NEC kwa nafasi yake ndani ya chama: Mapendekezo haya ndio kina Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba, Gamba la Nyoka, MwanaDiwani, ZeMarcopolo wanayapigania na muda sio mrefu, tutawaona baadhi yao kwenye Luninga wakisimamia hoja hizi kama chama bungeni:

1. Kwanza, ndani ya muundo wa muungano wa serikali mbili kuwepo na baraza la wawakilishi la Tanzania Bara. Kazi ya baraza hili itakuwa ni kushughulikia eti masuala ya Tanzania bara peke yake.

Pia chama kina pendekeza kwamba majimbo ya Jamhuri ya muungano yaundwe upya kukidhi haja hii, na yale ya BLW yabaki kama yalivyo kama majimbo ya uchaguzi wa bunge la JMT.

Mapendekezo ya ccm yanazidi kujaa vituko na kupendekeza kwamba - Wakati wa bunge la Muungao kujadili masuala ya muungao, wabunge wote watashiriki majadiliano. Lakini mara tu itakapoanza mijadala juu ya Tanzania bara, wale watalii wa Nguruvi3 kutoka zanzibar hawataruhusiwa kushiriki katika hii mijadala.

Vihoja ndai ya mapendekezo vinaendelea kwamba: Bunge hili la JMT litakuwa na spika na aibu wake, hawa watatokea pande tofauti za muungano. Wakati bunge linajadili mambo ya Tanzania bara, spika au naibu spika as long as anatokea bara-ndiye atakayeendesha vikao hivi vya masuala ya Tanzaia bara; yule ambae anatokea Znz, yeye hatoruhsiwa kushiriki vikao vya bunge wakati vinajadili masuala ya Tanzaia bara.

Sijui ccm imeingiwa na matatizo gani. Suala hili la kuanzisha baraza la wawakilishi la Tanzania bara litakaloshughulikia mambo ya Tanzaia bara "CHINI YA SERIKALI MBILI" litakuwa ni kituko cha mwaka kwani halitaweza kutekelezeka; awali hapo juu nilijadili jinsi gani mambo ya muugano, yasiyo ya muungao na yale mchanganyiko yalivyozaa kero nyingi. Katika hali hii, kitendo cha kuzuia wabunge wa znz kutoshiriki katika vikao juu ya mambo ya muungano kutazidi kuchochea migogoro. Sijui gamba la yoka anapojadili maboresho ya mfumo wa serikali mbili ana maana gani na wenzake kwa taifa let; hali hii itachochea migogoro kwa sababu "hakuna mambo ya Tanzaia bara peke yake chini ya mfumo wa serikali mbili", kama yapo, Gamba la Nyoka, Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba, njooni mtuelimishe; ufahamu wetu ni kwamba chini ya serikali mbili kuna mambo ya zanzibar mambo ya tanzania bara tu;njooni to prove us wrong tafadhali;

Vile vile, Gamba la Nyoka na wenzako, ndani ya serikali mbili, haiwezekani mkaleta bunge la Tanzania bara na mkatuambia kwamba linawakilisha wananchi wa Tanzania bara;haiwezekani; hii ni kwasababu:

Bunge hili la Tanzania bara chini ya serikali mbili halitakuwa na serikali kama msimamizi;litasimamiwa na serikali ipi kati ya hizo zenu mbili????nani atawajibika serikalini iwapo yale yanayopitishwa na bunge la bara hayatekelezwi? Jibu ni hakuna kwani bunge hili litakuwa halina serikali;

Naamini kabisa kwamba mwigulu anayejitapa kwamba ni mchumi daraja la kwanza, nape na pia gamba la nyoka wote ni wasomi. Na katika elimu ya awali kabisa tena humu humu nchini tunafundishwa kwamba -duniani kote, bunge ni moja ya mihimili mitatu ya dola mingine ikiwa ni serikali na mahakama; sasa Tanzania bara itakuwepo vipi na bunge lisilo na serikali? Kweli mmefikia hatua ya kutuona wananchi wajinga kiasi hiki?
Gamba la Nyoka na wenzako wa hoja juu ya maboresho ya serikali mbili kimfumo (nape, mwigulu etc), hakuwezi kuwepo mabunge mawili ndani ya bunge la Muungano yani - bunge la muungano na bunge la Tanzania bara bila ya pia kuwa na serikali yake yenye baraza la mawaziri la Tanzania bara na bila ya rais au waziri mkuu au hata gavana wa Tanzania bara;haiwezekani;
Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba, MwanaDiwani, @zermacopolo, Gamba la Nyoka, zomba, Ritz, makamba junior ambaye nae anaponda serikali tatu huku akiwa ni sehemu ya vihoja vinavyopendekezwa na NEC, msijifiche, njooni mjibu maswali haya:

1.Je, nafasi ya mawaziri wa tanzania bara wasiokuwa wa muungano itakuwa ni ipi wakati baraza la mawaziri litakapokuwa linajadili mambo ya muungano?

2. Je, ikitokea kwamba Rais ni mmoja yani rais wa JMT tu, nani atakaa kama mwenyekiti wa mawaziri ambao watakuwa wanasimamia mambo ya Tanzania bara katika serikali ya muungano?

3.Je, iwapo Rais atatokea Zanzibar, ataweza kusimamia masuala ya Tanzania bara? Kwa mamlaka ipi? Au mmeshawafuta wazanzibari katika rais wa JMT?

4. Je, rais wa muungano kutokea bara atakuwa na mamlaka yepi ya kusimamia masuala ya bara wakat atakuwa amewekwa katika nafasi yake na pande zote mbili za muungano?

Jamani:
Kuna pande mbili za muungano bila ya kuwepo kwa serikali ya Tangayika? Kwanini tunataka kuongeza migogoro isyokuwa na tija kwa taifa?

Rais Kikwete juzi bungeni mwanzoni kabisa wa hotuba yake alisema kwamba hii iwe katiba ambayo itaweka to rest migogoro yote hii isiyokwisha; je hili litawezekana kweli kwa mapendekezo yenu ya chama (CCM)?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3 your points make a lot of sense. Lakini nikianza kuangalia ponti moja baada ya nyingine, naona kama kwa upande fulani watu wa Zanzniabr wanatuona sisi wajinga?

Kama tuna watalii wanaolipwa milioni 800 kwa mwezi, wakati dada zetu wanalazimika kujifungua sakafuni huu ni ukatili tunaojifanyia wenyewe.

Kama contribution yao kwenye bajeti ya ulinzi ni Tsh 0, i will count it as negative kwa kuwa tutakuwa tunawalipa "wanajeshi" na tutakuwa tunagharamia military instalations kule visiwani.

Mkuu Gamba la nyoka nashindwa kukuelewa unaposema kuwa kukiwa na serikali tatu, ile ya Zanzibar haiwezi kujiendesha na hata haiwezi kutoa mchango kwenye serikali ya Shirikisho, inaweza kufanya hivyo kwa miezi miwili au miaka michahce kabla ya ku-colapse, kwa hiyo una suggest tuendelee na system ya sasa. Tukiangalia gharama alizoainisha Mkuu Nguruvi3 tunaona wazi kuwa sisi watanganyika tunakuwa na upendo wa mshumaa, kuteketea kwa ajili ya kuwapa mwanga Zanzibar...hii maana yake nini? tunafanya hivi kwa faida gani, is there any intelligent reason as to why should we be financing Zanzibar. Muugano ni muungano kwa manufaa yetu watanzania wote au ni muungano tunaougharamia na kuogopa kuuvunja kwa ajili ya mizimu ya Mzee Karume na Mwalimu Nyerere??

Kama kweli tunautaka Muungano, na kama kweli unaona serikali mbili hazitatui kero genuine za bara, then let Zanzibar cease to exist as Tanganyika did, if not possible let Tanganyika resurrect na itatue matatizo yake, na imanage budget yake.
 
Lakini nikianza kuangalia ponti moja baada ya nyingine, naona kama kwa upande fulani watu wa Zanzniabr wanatuona sisi wajinga?

Kama tuna watalii wanaolipwa milioni 800 kwa mwezi, wakati dada zetu wanalazimika kujifungua sakafuni huu ni ukatili tunaojifanyia wenyewe.

Kama contribution yao kwenye bajeti ya ulinzi ni Tsh 0, i will count it as negative kwa kuwa tutakuwa tunawalipa "wanajeshi" na tutakuwa tunagharamia military instalations kule visiwani.

Mkuu Gamba la nyoka nashindwa kukuelewa unaposema kuwa kukiwa na serikali tatu, ile ya Zanzibar haiwezi kujiendesha na hata haiwezi kutoa mchango kwenye serikali ya Shirikisho, inaweza kufanya hivyo kwa miezi miwili au miaka michahce kabla ya ku-colapse, kwa hiyo una suggest tuendelee na system ya sasa. Tukiangalia gharama alizoainisha Mkuu Nguruvi3 tunaona wazi kuwa sisi watanganyika tunakuwa na upendo wa mshumaa, kuteketea kwa ajili ya kuwapa mwanga Zanzibar...hii maana yake nini? tunafanya hivi kwa faida gani, is there any intelligent reason as to why should we be financing Zanzibar. Muugano ni muungano kwa manufaa yetu watanzania wote au ni muungano tunaougharamia na kuogopa kuuvunja kwa ajili ya mizimu ya Mzee Karume na Mwalimu Nyerere??

Kama kweli tunautaka Muungano, na kama kweli unaona serikali mbili hazitatui kero genuine za bara, then let Zanzibar cease to exist as Tanganyika did, if not possible let Tanganyika resurrect na itatue matatizo yake, na imanage budget yake.
Bongolander Watu wa zanzibar wanatuona wajinga kwasababu kila wanapotikisia kiberiti hupewa watakacho.

Kila wanapotafuta manufaa fulani basi hutanguliza muungano.
Utakumbuka tulikuwa tulikwenda znz kwa passport. Tanganyika waliposema waje na zao ilichukua wiki mbili wakafuta . Karibuni wamerudi kule kule, sisi hatujitambui na hutuona wajinga.

Mifano, waziri mkuu Pinda anaposema serikali 2 mufaka wakati yeye hawezi kuongea na sheha wa shehia yoyote znz hiyo inatufanya tuonekane dhalili kwao.

Tena waziri mkuu anapeleka mswada wa kujenga wodi za akina mama kwa Pandu Kificho na wenzake 50 waliochaguliwa kwa majimbo ya watu 5,000!! inasikitisha.

Watalii 80 kutoka znz kama wabunge hulipwa pesa nyingi kuliko wafanyakazi wa wizara ya habari au madini. Tujiulize, hawa watalii wanakuja na jambo gani bora kuliko wafanyakazi wa wizara ya nishati na madini kwa ujumla wao?

Wanafunzi huchaguliwa kwa uzanzibar na si ufaulu, wanapewa pesa za kusomea.
Mwaka jana walidhaminiwa 1000 kutoka znz achilia mbali wale wanaoishi Tanganyika.

Kwa hesabu za chini kabisa,kama kila mmoja anagharamiwa kwa milioni 3 jumla ni bilioni bilioni 3.(kiwango kidogo cha makadirio). Halafu wakimaliza shule hawatakiwi kurudisha mikopo kwasababu ni wzn. HawatAfuti kazi kwasababu wanapata upendeleo kama walivyoanza kwa uzanzibar tu. Hivi kwanini wasituone wajinga.

Mtangayika analipa kodi kubwa. Mtoto wake anapigana kupata nafasi.
Kama ana Div II mkopo ni hatiani kwasababu kuna nafasi 1000 za div IV ni za znz.

Mtanganyika akimaliza kabla ya kuanza kazi mkopo arudishe ili zile pesa ziendelee kusomesha wznz wengine. Mtoto wa Tanganyika analipa mkopo, analipa kodi na baba yake analipa kodi.
Mwisho wa kodi zao ni nchi jirani ya znz.

Wazanzibar wanakusanya pesa za shirika lao la ZMO. Ada za Maritime kule IMO ni kodi za Mtanganyika. Inayojulikana IMO ni Tanzania na kwavile mchango wa znz ni nada, zero au sifuri zigo anabeba Mtanganyika.

ZMO inasajili meli na kuchukua pesa, ada za chama analipa Mtanganyika.
Kwanini wasituone wajinga.

Gharama za ulinzi na usalama ni zero, I mean nil. Hutasikia hata siku moja wakitaka ulinzi na usalama uondolewe katika muungano. Wanafahamu zigo la kubeba ulinzi na usalama ni zito, Mpagazi na mlipa kodi wa Tanganyika anawajibika.

Ukisikia wanataka mkataba, si jambo jingine ni ulinzi na usalama.
Jana walikuwa kibandamaiti hakuna hata mmoja aliyesema vunja muungano.
Wote wanataka mkataba. Mkataba maana yake Watanganyika endeleeni kubeba zigo.

Makusanyo yao ya mwezi ni bilioni 12, kuendesha serikali kikamilifu wanakuja hazina Dar kuchukua mishahara. Ni haki yao, si wznz bwana! Ukumbuke, wanapata 4.5% ya pato la taifa ambalo ni pato la Tanganyika.

Mwaka jana wakapewa bilioni 32 tu kwenda znz bila sababu zikisemwa pesa za mazingira. Kwamba mlipa kodi wa Tanganyika anapaswa kuhudumia mazingira ya nchi jirani ya znz(katiba 2010).

Wafanyakazi wao wanafanya kazi halmashauri kama wakurugenzi na wakuu wa Wilaya, nao ni sehemu ya watalii wa Dodoma.

Hivi mtu anatokaje kwa mtipura kwenda Singida kuwa Mkurugenzi.
Gharama za kumtunza na mafao yake analipa Mtanganyika. Ni kwasababu tu ni wznz.
Kwanini wasituone matutusa wakubwa.

Huu muungano wa serikali 2 aliyeubeba ni mlipa kodi wa Tanganyika, mznz anasubiri fursa tu, mchango wake kwa miaka 50 si zaidi ya mara 4.

Lakini wanataka mamlaka kamili, sasa anapotokea Mkuu Mtanganyika au Gamba la Nyoka na kusema hawawezi si kweli.

Wamepewa uwezo na tume ya Warioba kukopa na kupata misaada. Kwanini wasitumie rasilimali zao ikiwemo mikopo na misaada kuchangia katika muungano.
Akina Mtanganyika wanasema,tuendelee na muungano huu kwasababu ni Mujarab Mtanganyika kubeba zigo.

Tunahitaji Tanganyika ili tushughulikie matatizo yetu makubwa si kushghulika na nchi jirani ya znz.
Leo Dodoma hakuna anayeitetea Tanganyika kwavile ni CCM.

Kwamba mtu huyo anaona sawa Watanganyika kurithisha zigo kwa watoto wao, anaona raha Waziri mkuu kwenda kuomba kibali cha kujenga wodi ua kununu kitanda wodi ya wazazi eti mpaka Pandi Kificho na wenzake 49 wa BLW watakapokubali.

Ukipanga gharama mkuu Bongolander machozi yatakutoka.
Yatazidi kumiminika utakapobaini kuwa hakuna cha ziada kutoka znz isipokuwa shukrani za matusi. Ni muda muafaka tuondoe mambo 22 tubaki na 7, kama hayakubaliki tugawane mbao.

Yes mkuu upo sawa, wametuona matutusa sana kwasababu kila wanachotaka wanapewa, si kwasababu ni wanadamu bali ni raia wazuri na bora wa znz. Swali ni je, Watanganyika wanaelewa au ndiyo akina Gamba laNyoka wasioweza kutueleza nini kifanyike isipokuwa kukariri, muungano ufanyiwe maboresho!
 
TUACHE UPOTOSHAJI KUHUSU ZANZIBAR KUTOKUWA NA UWEZO WA KUJIENDESHA NA KUGHARAMIA MUUNGANO

Hoja juu ya uwezo wa zanzibar kujitegemea ni hoja iliyojaa mantiki za kisiasa zaidi kuliko kiuchumi. Hoja hii imejaa upotoshaji kuliko ukweli, upotoshaji unaoongozwa na kina Gamba la Nyoka na wenzao kwa nia ya kuwatisha wazanzibari wasiendeleze harakati zao za kurudi katika mkataba wa muungano wa 1964 ambao uliweka wazi mazingira ya serikali tatu - machache ya kuchangia kwa pamoja kishirikisho, na yaliyobakia kila nchi shiriki kuyasimamia kivyake. Huko nyuma tulijadili suala hili, lakini kama anavyosema Nguruvi3, kina Gamba la Nyoka waa utamaduni wa kukimbia hoja, kisha baada ya majumaa au miezi kadhaa, wanarudi humu kurudia hoja zile zile dhaifu.

Kabla ya Mwaka 1964 (mwaka wa muungano), zanzibar ilikuwa ni taifa huru kiuchumi na kisiasa. Lilijiendeshea mambo yake yenyewe, and in actual sense, zanzibar huko nyuma ilikuwa ni moja ya economic power houses barani Africa, ikiwa katika ligi moja na nchi kama Ghana na Misri in terms of economic performance and activities. Hata Tanganyika haikuwa inafua dafu kiuchumi mbele ya Zanzibar, sasa kwanini leo tuseme zanzibar haitakuwa na uwezo wa kujiendesha? Huku ni kuitusi zanzibar kwani wananchi walipomwaga damu kupigania mapinduzi yao, hawakufanya hivyo ili waje baadae kuwa tegemezi kwa Tanganyika.

Ni baada ya muungano tunaona zanzibar ikianza kubadilika kiuchumi. Hii ilitokana na muungano kuwa na sura ya kisiasa zaidi ambapo uchumi ukafanywa mtumishi wa siasa za muungano. katika hali hiyo, masuala ya uchumi yakawa treated kama masuala ya muungano ambayo yakapangwa to be shared equally na pande zote mbili za muungano. Hadi hapo zanzibar ikawa na uchumi imara tu ambao ungeweza kujiendesha na pia kuchangia gharama za mambo (11) ya muungano.

Kilichofuatia baadae katika historia I kuona zanzibar ikichangia mara tatu tu katika gharama za kuendesha muungano - 1964/5, 1965/6, 1966/7, na kila mwaka kiasi kikizidi kupungua. Sasa kina Gamba la Nyoka wanakuja na viroja hapa pengine kwa kutazama suala hili lakini wanasahau kwamba muda mfupi baada ya muungano, zanzibar ikapewa kilimo cha uchumi na Tanganyika (iliyovaa koti la muungano) kupitia sheria namba (9) ya tarehe 1/5/1964. Sheria hii ilitoka kama amri na haikushirikisha viongozi wa zanzibar bali wa Tanganyika kwa kutumia mamlaka iliyopewa Tanganyika ya kipindi cha mpito. Sheria hiyo ni kama ifuatavyo:

TANGAZO LA SERIKALI Na. 246 lililochapwa 1/5/1966.

SHERIA ZA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR, 1964.

AMRI

Kwa mujibu wa vifungu 3(b) na 8 Vya Sheria Zilizotajwa

AMRI YA UTARATIBU WA KIPINDI CHA MPITO, 1964.

1. Amri hii itajulikana kama amri ya utaratibu wa kipindi cha mpito 1964, na itaanza kutumika siku ya muungano.

2. Amri hii itasomwa kama sehemu ya katiba ya muda.
....
....
....

9. Mali na Mikataba:
Mali zote na haki juu ya mali za jamhuri ya Tanganyika na mali zote na haki juu ya mali za jamhuri ya watu wa zanziba zilizokuwa zinamilikiwa au kutumiwa au zilizomilikiwa au kutumiwa kimsingi kuhusiana na mambo ya muungano, zitakuwa kuanzia siku ya muungano chini ya jamhuri ya muungano.

Kimsingi, kupitia sheria hii, assets zote za zanzibar pamoja na savings zake kubwa sana kwenye benki moja huko uingereza, zikahamishiwa kwenye himaya ya muungano. Zanzibar ikabaki kapa in a blink of an eye. Na sheria hii inasema kwamba itaanza kutumika siku ya muungano wakati mkataba ukiwa umeshasainiwa. Huu ulikuwa ni uchakachuaji mkubwa ulioipa zanziba kilema cha uchumi hadi leo. Kina Gamba la Nyoka, Nape Nnauye na wengine hawajui haya.

Zanzibar ndio ilikuwa kwanza imetoka katika mapinduzi, na haikuwa hata haija thaminisha mali zake na akiba yake kubwa kwenye benki huko London (Narodny Bank). Akiba ya Zanzibar by the time Karume anafariki 1972 ilikuwa about 25 Million Pounds Za mwingereza. Fedha hizi zilichangiwa na bei nzuri ya karafuu soko la dunia ambapo ilirurka kutoka $550 kwa tani miaka ya mwanzo ya mapinduzi na kufikia $1,500 kwa tani 1967-8; Karume alitumia fedha nyingi kujengea wananchi makazi, miundo mbinu kwa mafanikio makubwa;

Fedha na mali zote hizi zikachukuliwa na Tanganyika iliyovaa koti la muungano. Lipo suala lingine la kifedha ambapo Zanzibar Bank ambayo ilitakiwa iwe ni benki kuu ya zanzibar, nayo ikavurugwa na sheria za muungano.

Licha ya yote haya, leo zanzibar bado wana uwezo wa kusimama kiuchumi kwa mafanikio tu kwani uchumi unategemea natural resources, human capital, leadership na political will among others. Zanzibar wana rasilimali nyingi tu - wana mafuta, gesi, utalii, uvuvi, a free port, kutaja vichache tu. Lakini yote haya yamevurugwa na muungano wa kisiasa. Kwa mfano, Katiba ya muungano (1977) haisemi hadi leo zanzibar watanufaika vipi na rasilimali zake, na wala haizungumzi economic justice za wazanzibari. Uchumi na rasilimali zinatajwa kijuu juu tu na kisiasa.

Iwapo zanzibar watapewa fiscal and economic autonomy, hakuna shaka kwamba wataweza kuamka kiuchumi pengine kuliko hata Tanganyika. Sisi Tanganyika hatuna nia ya kujenga uchumi wa wananchi, je Zanzibar wakiamua to build a strong domestic economy kwa manufaa ya wananchi, kwanini wasifanikiwe? Haitachukua zaidi ya miaka 15, tutabaki midomo wazi. Lakini ni iwapo wataamua leo na wataendelea na juhudi zao zilizoanza na katiba yao ya 2010.

Kuna many wealthy small islands in the world ambazo zilikuwa na chanhamoto kama tu zanzibar kwa maana ya idadi ndogo ya watu na eneo dogo la ardhi, lakini kwa vile they had political will, leo sio tu wapo huru kiuchumi, bali pia wapo mbele sana ya nchi kubwa na zenye rasilimali zaidi yao.

Zanzibar ina urefu wa kilometa 1,500 na upana wa kilometa 30, huku idadi yake ya watu ikiwa ni karibia 1.4 million. Tufananishe na nchi jirani yake ya Mauritius:

Mauritius ukubwa wake haufikii zanzibar, ni kama robo mbili tu ya zanzibar - ina urefu wa Kilometa 45 na upana wa kilometa 65. Lakini bado it performs better sio tu zaidi ya Zanzibar bali Tanzania kwa ujumla. Most major economic and commercial indicators zinadhihirisha ukweli huu. Kwa mfao, kwa mujibu wa World Economic Forum's Travel and Tourism Competitiveness Index ya hivi karibuni juu ya Middle East and Africa, Mauritius wapo ranked top FIVE, wakati Tanzania ipo ranked 19th. Tanzania hii hii yenye wanasiasa wanaobeza potentials za nchi ndogo wakati chini ya utawala wao, "ukubwa wa pua haujawahi kuwa wingi wa makamasi". Vile vile, kwenye Global Index, Mauritius is 40th, Bwana mkubwa Tanzania is 98th.

Tukumbuke kwamba tofauti na Tanzania yenye kila aina ya vivutio vya kitalii - mbuga za wanyama, mlima wenye barafu south of equator, olduvai gorge alipopatikana binadamu wa kwanza,Mauritius hawana vivutio vya maana kama hivi lakini bado wanapokea watalii wengi kuliko Tanzania kwa zaidi ya asilimia ishirini. Kwa mfano, Takwimu za World Tourism Organization zinaonyesha Tanzania hupokea watalii 700,000, na Mauritius watalii 900,000.

Pia katika "Doing Business Report", inayoangalia ease of doing business/ubora wa mazingira ya kufanya biashara, Mauritius is 17th in the world, sisi Tanzania na ukubwa wetu wa pua, we are 131st.

Mauritious ina GDP ambayo ni nusu tu ya Tanzania (kama USD 12 Billion, compared na ya Tanzania inayovuka USD 25 Billion sasa), lakini bado wananchi wa mauritious wana maisha bora kwa mbali sana ikilinganishwa na Watanzania. Wananchi wa mauritious ni miongoni mwa wananchi wenye hali bora za maisha sio afrika tu bali katika nchi zinazoendelea. Isitoshe, na udogo wao, hawapo tena katika low income countries bali middle income. Tanzania na ukubwa wetu wa pua, hii bado ni ndoto licha ya matumaini mengi wanayotoa wanasiasa kwa wananchi.

Tusiwatishe wazanzibari, bali tuwape moyoo kuelekea autonomy and self determination kwani hivyo ndivyo na Tanganyika itapatikana na kupelekea uwepo wa muungano unaoendeshwa kwa ushindani and with less waste of resources tofauti na mfumo mbovu wa ccm na serikali zake mbili zisizo na tija.

Wazanzibari should be inspired by the likes of Mauritious, tusiwakatishe tamaa, tusiwatishe. Isitoshe, wakiamua kufungua kesi ya madai ya uchakachuaji wa mali na akiba zake nilizojadili, ndani ya serikali ya ccm hapatatosha.

Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.
Mtanganyika, Bongolander, MwanaDiwani, ZeMarcopolo, zomba, Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Wakuu nadhani tunazunguka mbuyu tuu hapa na theories nyingi sana. Serikali mbili so far zimekuwa sustainable (japokuwa kuna kasoro nyingi) serikali yenu ya tatu mnayoitaka ni assumption tupu, ni model ambayo imejaa assumption na Ifs. Na model yenu haingalii "hayo matakwa ya Wanzazibar". Jana tuu Maalim Seif amesema wanataka serikali ya mkataba. They need contractual union. Kwa nini hamtaki kujadili hili wanalo litaka?

Honest, mimi sio mshabiki wa huu muungano toka mwanzo sababu ya gharama na hauna economical au strategical benefit kwetu Tanzania bara, other than assumption za militarily advantage. Sasa lets cut the chase, tuambieni kwa nini tuangaike na muungano ambao hautakuwa sustainable?

Mchambuzi, hiyo analysis yako kuhusu Zanzibar economic growth ni kutokana na 1963 assumption kabla Tanzania Bara hamjawapa more spending oxygen. Sasa wanafanya all kind of projects kutokana na tax payer wa mchinga na nachingwea na mkisema wajiendeshe wenyewe mtatuleta disaster kama ya Ugiriki.

Mimi nasema kama hatuwezi kuboresha hizi mbili TUVUNJENI muungano, why mnaogopa kusema neno ambalo wote mnalitaka kulisema VUNJA. Msilete hadithi za Hablakadabla, Zanzibar economic growth yake sio sustainable kama sio Tanzania bara subsidy, ukiwaacha wajiendeshe is a recipe for disaster. Pato lao la taifa halifiki hata 1B USD, budget ya Zanzibar ni 650million USD. 50% of that ni government speeding on salary na mambo ya chai.

Kama mlikubali tangu 1964 kubeba msalaba nadhani it's too little too short kuja na agenda ya kuongeza serikali ya 3 ambayo itaendelea kubebesha vizazi vyetu deni zaidi ya hili. Hivyo kuliko kwenda that route nasema tugawaneni mbao as JK said.
 
Wakuu nadhani tunazunguka mbuyu tuu hapa na theories nyingi sana. Serikali mbili so far zimekuwa sustainable (japokuwa kuna kasoro nyingi) serikali yenu ya tatu mnayoitaka ni assumption tupu, ni model ambayo imejaa assumption na Ifs. Na model yenu haingalii "hayo matakwa ya Wanzazibar". Jana tuu Maalim Seif amesema wanataka serikali ya mkataba. They need contractual union. Kwa nini hamtaki kujadili hili wanalo litaka?

Honest, mimi sio mshabiki wa huu muungano toka mwanzo sababu ya gharama na hauna economical au strategical benefit kwetu Tanzania bara, other than assumption za militarily advantage. Sasa lets cut the chase, tuambieni kwa nini tuangaike na muungano ambao hautakuwa sustainable?

Mchambuzi, hiyo analysis yako kuhusu Zanzibar economic growth ni kutokana na 1963 assumption kabla Tanzania Bara hamjawapa more spending oxygen. Sasa wanafanya all kind of projects kutokana na tax payer wa mchinga na nachingwea na mkisema wajiendeshe wenyewe mtatuleta disaster kama ya Ugiriki.

Mimi nasema kama hatuwezi kuboresha hizi mbili TUVUNJENI muungano, why mnaogopa kusema neno ambalo wote mnalitaka kulisema VUNJA. Msilete hadithi za Hablakadabla, Zanzibar economic growth yake sio sustainable kama sio Tanzania bara subsidy, ukiwaacha wajiendeshe is a recipe for disaster. Pato lao la taifa halifiki hata 1B USD, budget ya Zanzibar ni 650million USD. 50% of that ni government speeding on salary na mambo ya chai.

Kama mlikubali tangu 1964 kubeba msalaba nadhani it's too little too short kuja na agenda ya kuongeza serikali ya 3 ambayo itaendelea kubebesha vizazi vyetu deni zaidi ya hili. Hivyo kuliko kwenda that route nasema tugawaneni mbao as JK said.
Muungano wa serikali 2 umesema ni sustainable.
Vipi leo kuna vurugu za kutaka kubadili?

Mara nyingine tena umekubali kuwa znz inapata subsidy, vipi utaondoa malalamiko yao kuwa Tanganyika imejificha katika koti na wananyonywa ili hali wao wanapata subsidy na hawaelewi.

Tatu, kuna nchi kama Comoro, Haiti, Syechelles n.k. zenye maeneno na chumi ndogo au sawa na znz. Hujatueleza vipi zinajiendesha na kwanini udhani znz hawawezi nawanapaswa subsidy.

Tunaomba utueleze malalamiko ya znz kuhusu mamlaka kamili unayamalizaje katika hali iliyopo.

Kuhusu suala la mkataba, hilo tumekujibu kuwa wznz hawawezi ku define mkataba ni nini na wa nini, kwanini na kwa faida gani.

Kwanini tujadili unknown? Labda kama una idea tufahamishe ili tujadili, kama huna, nao hawana na hakuna cha kujadili.

Mkataba hauwezi kujadiliwa kwasababu nani ametoa mandate kuwa znz wana prerogative ya kuamua muungano

Kwa mantiki hiyo kwanini unadhani wao wanapaswa na si serikali 3 za Watanganyika mamilioni.

Kuhusu kuvunja jahazai na kugawana mbao , mbona siku nyingi sana tumelisema?
1. Serikali 3 yenye mambo machache
2. Vunja jahazi

Serikali 2 hazijatoa jawabu miaka 50 na wanaotaka hawana majawabu.
Wakiullizwa wanasema tuboreshe. Kuboresha ni neno, tunaboresha nini hawana jibu.

Serikali 2 zinambebesha Mtanganyika zigo zito lisilo na maana. Muda wa kutua zigo is long overdue.
 
Muungano wa serikali 2 umesema ni sustainable.
Vipi leo kuna vurugu za kutaka kubadili?

Mara nyingine tena umekubali kuwa znz inapata subsidy, vipi utaondoa malalamiko yao kuwa Tanganyika imejificha katika koti na wananyonywa ili hali wao wanapata subsidy na hawaelewi.

Tatu, kuna nchi kama Comoro, Haiti, Syechelles n.k. zenye maeneno na chumi ndogo au sawa na znz. Hujatueleza vipi zinajiendesha na kwanini udhani znz hawawezi nawanapaswa subsidy.

Tunaomba utueleze malalamiko ya znz kuhusu mamlaka kamili unayamalizaje katika hali iliyopo.

Kuhusu suala la mkataba, hilo tumekujibu kuwa wznz hawawezi ku define mkataba ni nini na wa nini, kwanini na kwa faida gani.

Kwanini tujadili unknown? Labda kama una idea tufahamishe ili tujadili, kama huna, nao hawana na hakuna cha kujadili.

Mkataba hauwezi kujadiliwa kwasababu nani ametoa mandate kuwa znz wana prerogative ya kuamua muungano

Kwa mantiki hiyo kwanini unadhani wao wanapaswa na si serikali 3 za Watanganyika mamilioni.

Kuhusu kuvunja jahazai na kugawana mbao , mbona siku nyingi sana tumelisema?
1. Serikali 3 yenye mambo machache
2. Vunja jahazi

Serikali 2 hazijatoa jawabu miaka 50 na wanaotaka hawana majawabu.
Wakiullizwa wanasema tuboreshe. Kuboresha ni neno, tunaboresha nini hawana jibu.

Serikali 2 zinambebesha Mtanganyika zigo zito lisilo na maana. Muda wa kutua zigo is long overdue.

Mkuu naomba kwanza niseme hivi, kama Zanzibar watakubalia kurudi mezani na kujadili agenda za muungano kama watu wazima na sio watoto walionyimwa pipi, basi ni mara million kuwa na serikali mbili kuliko kuleta mzigo wa Jaji Warioba wa serikali tatu.

Lalamiko la kwanza Tanganyika imejificha ndani ya koti la Tanzania inapigwa na wanasiasa wachache ambao wapo unguja ambao hawajui madhara halisi ya janga wanalolitaka. Na kuna kila haki ya msingi Wazanzibar wakaelemishwa kuhusu madhara wanayoyataka, na kisha wakaambiwa wapige referendum vote ya kuwa na mfumo huu huu au kuondokana nao na kuwa nchi huru. Hatuwezi kutengeneza mfumo mpya ili tuu kuwafuraisha watu 1.2 Million katika nchi ya watu 44Million. Yaani tutengeneze serikali ya tatu kwa 3% ya population. Na hili nyinyi ndugu zangu mnalipigia kelele kabisa kwamba eeh tulifanye. Jee inangia akilini kuanzisha new system just to sustain 3% of the people?

Lapili, ukweli ni kwamba matumizi ya Tanzania kwa Zanzibar yanaweza kuwa insignificant kama kweli tutazama namba zinasemaje. Pato la taifa ni 5.8 Billion Dollar kwa mwaka 2012 na tukakopa 4.2 Billion Dollar ili kufidia budget deficit, hivyo kwa mwaka 2012 tumekopa cent 42 kwenye kila shillingi tuliyotumia. Jee ni kiasi gani hapa tumepeleka Zanzibar? Total Zanzibar Budget ni 650 Million Dollar ukiangalia na total Tanzania budget hiyo ni 6% ya Budget yetu yote. Sasa mnataka tutengeneze serikali nyingine kupigania 3% ya watu ambao wanatumia 6% ya total budget? Tell me kama mnaona fikira za swala hili ni logic.

Sasa turudini mezani, pato la taifa limekuwa likiongezeka kwa takribani 15% kwa miaka 5 iliyopita likewise na matumizi yamekuwa yakiongezeka hasahasa kwenye recurrent expenditure ambayo ni 70% ya matumizi yote wakati 30% ndio mipango ya maendeleo. Maana kwenye kila shilling basi senti 30 ndio inakwenda kwenye mipango ya maendeleo, senti 70 inakwenda kwenye mambo mengine, military spending, ndege ya raisi, VX, chai, sambusa na mambo kama hayo. Sasa niambieni kwamba jee serikali ya 3 itapunguza haya matumizi? Na kama mlivyoona hapo juu Zanzibar wanatumia less than 7% ya Total Tanzania spending, sasa niembieni jee tukiweka serikali ya tatu haya yatapungua kwa asilimia ngapi? Tatizo tulilonalo sasa ni matumizi mabaya huku kwetu bara tunakopa centi 42 kwenye kila shillingi na 70% ya mkopo tunanunulia chai na vitu vingine ambavyo sio vya maendeleo na 93% of that inatumika Tanzania bara.

Nguvi03 umejikita sana kwenye Watalii wa Dodoma, lakini hiyo ni pocket change, sidhani kabisa kama tunatakiwa hata tujadili. Tuangalie vitu kama military spending ambayo kwa asilimia kubwa ni jeshi letu la Tanzania bara ndio linalotafuna pesa. Kama kweli mnataka tuzungumzie matumizi mabaya ya pesa ya taifa sidhani kabisa Zanzibar wanaweza hata kusogeza mizani. Balaa lipo kwetu huku Bara.

Sasa twendeni kwenye reality, jee serikali yenu ya Tanganyika itakuwa na ukubwa gani? Jee Muungano utaongozwa kwa fund gani? Jee Raisi wa Muungano atatoka upande gani (FYI 3% ya watu hawawezi hata siku moja kutoa raisi wa 97%)? na kama muungano utapata fund kwa kuchangia jee Zanzibar watachanga kiasi gani? Jee kwa nini kuwe na Bunge la Muungano ambalo litatumia pesa ambazo Tanganyika ndio atachangia by majority, so kwa nini Tanganyika isijifanyie maamuzi yake yewenyewe? Jee raisi wa Muungano atakuwa na nguvu kiaisi gani?
Kwanini tuingie kwenye complexity zote za fund wakati wao wapo 3% ya total population? Hili bunge la muungano mnalolipendekeza ni la nini? Kwa nini tuitaji bunge la muungano wakati kila nchi itakuwa inajiendesha yenyewe. Unaona jinsi hili swala mnalolitaka linavyoweza kuwa complex? Yaani mnataka tuumize vichwa kwa 3% of the population spending 6% ya budget ya taifa?

Ukiangalia hisabati utakubaliana na mimi kwamba serikali ya tatu ni kuongeza matumizi tuu, ili hawa vigogo na familia zao waendelee kuendesha VX za walipa kodi, wawapeleke vimada wao Dubai shopping. Hakuna justification. Jaji Warioba angesema ukweli kwamba sijui hesabu za serikali mpya ambayo ninataka muanzishe. Tukisema eti tufanye vipimo vya suti wakati hatuna kitambaa tutakuja kushikana mchawi tukaipeleka hii nchi pabaya zaidi ya hapa ilipo. Kuliko kumsikiliza Mboe na Wenzie ambao wapo kisiasa zaidi turudi mezani na tujumlishe.

Kusema kweli the math doesn't add up. Mimi nasema kama kweli Wanzanzibar hawataki kurudi mezani na kuchanachana ile katiba yao ya 2010, basi tugawaneni mbao. Wala msiombe kabisa kuongeza serikali ya tatu, kwani matumizi mliyonayo leo hayataondoka bali mtaongeza at least 2 Billion Dollar in spending na kuongeza gharama za nchi hii kwa at least 17%.

Mimi ningesema kweli mmejikita katika maendeleo kama mgekuja na Kauli Mbiu ya kulazimisha Katiba iweke kikomo cha kukopa pesa nje kuja kununua VX za wabunge tuu huku kwa kusupport Matumizi Ndani ya Uwezo wetu( balanced-budget amendment). We need balance budget clause ndani ya Katiba, na kwa wote wanaolilia serikali ya 3 this will be more beneficially kuliko hadithi za kuongeza makarani na watu wenye degree za diplomasia.
 
Mtanganyika,

Hakuna mtu aliyechambua jinsi gani muungano ni mzigo kwa Tanganyika kama Nguruvi3, lakini pia hakuna mtu aliyekuja na hoja mbadala kujadili gharama kutetea serikali mbili au moja, HAKUNA. Ingekuwa vyema sana iwapo upande wa pili wa hoja mngekuwa mnachukua hoja zake moja baada ya nyingine na kuzijadili katika mfumo mnaoupigia debe. Vinginevyo kurusha usha tu numbers and terminologies hakuleti maana yote katika kutatua matatizo tuliyonayo hapa. Lugha, namba na mifano ya nguruvi3 inaeleweka hata kwa mtu asiyekuwa na elimu ya form six; nakaa na kuwaelewesha watu vijiweni na wanaelewa vizuri sana; na nyie mngekuja na lugha, mifano na takwimu za kueleweka kwa wananchi walio wengi ambao hawajui FY au GDP ni nini, mngekuwa mnafanya la maana sana. So far, hampo huko. Hoja zenu ni za kuelimishana wenyewe waelewa kwenye board rooms, tena kwa takwimu ambazo hazijibu swali kwanini Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.

Maswali yako yote tulishayajibu, ni kwamba tu haujashiriki mijadala yetu mingine;nikipata muda nitakurudia na takwimu kama ulivyofanya;vinginevyo unashangaza sana unaposema kwamba serikali tatu ni theory na kwamba haiwezekani in practice;unasahau kwamba serikali mbili hata in theory haipo, na in practice ndio imetufikisha hapa; dunia imetucheka sana na hii constitutional arrangement;

Huko nyuma nilijadili sura kuu tatu za mahusiano ya kimataifa baina ya nchi mbili au zaidi:

1. Serikali moja.
2. Serikali ya matangamano ya majimbo.
3. Serikali ya shirikisho.

Nikaweka bayana kwamba mkataba wa muungano ulilenga shirikisho, na hata Nyerere in his Panafricanist vision alijadili juu ya umuhimu wa mfumo wa shirikisho;mfumo huu upo practiced nchi nyingi zikiwemo za africa na zimekuwa efficient;leo unasema federalism is only theoritical and wishful thinking?

Unapopinga federalism na kuunga mkono unitary system, ni lazima ujadili faida na hasara za kila mfumo kwa kutumia takwimu unazozileta hapa. Those numbers can't speak for themselves; nilijadili kwa mtindo huu huko nyuma, nikipata nafasi ntarudia tena; kwa kuanzia, naomba ujadili:

1. Mkataba wa muungano ulilenga mfumo wa aina gani na kwanini.
2. Zipi ni faida za mfumo wa unitary kiuchumi na kisiasa dhidi ya mfumo wa shirikisho.

Itakuwa vyema sana ukitumia numbers zako katika haya kuliko kuzirushia rushia tu kama unavyofanya sasa.

Vinginevyo kama nilivyojadili awali, usiitazame zanzibar kwa jicho la post 1964, itazame kwa jicho la kipindi cha kabla ambapo uchumi wake performed better kuliko hata uchumi wa Tanganyika. Pia angalia visiwa vyenye ukubwa wa zanzibar or less, na vyenye less resources and less advantage in terms of strategic location, je havina uwezo wa kujiendesha? Na katika suala la muungano kufuatana na mapendekezo ya tume na masuala saba, ainisha gharama za muungano na ujadili kwanini zanzibar hawataweza changia. Achana na gharama za kuendesha Tanganyika kwani hizo zimekuwepo tangia 1964 ambapo Tanzania bara ndio imekuwa Tanzania, na huko nyuma tukaonyesha jinsi gani mfumo wa sasa have more leakages than injections in the circular flow of income;

Ukijadili haya, tutakuwa sasa on par level kwani tutakuwa na vitu vya kufananisha. Tembelea nyuzi zangu za mwaka jana na mwaka juzi ambapo nimejadili sana takwimu. Lakini kama unaona itakupa shida to start to dig in, nitazirudia. Ila kwa kuanzia naomba ujadili niliyokuomba hapa juu ili tuwe na framework of analysis. So far hoja zako zipo so erratic, na numbers unazotumia hazileti sana maana katika kutafuta majibu ya suala lililo mbele yetu. Kumbuka haya matatu/mawili wakati unarudi na hoja zako:

1. Importance of devolution/why devolution.
2. Misingi ya muungano wowote ule baina ya sovereign states - what makes a union efficient and effective.
3. Demokrasia and its role on 1 and 2, above.





Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Wakuu nadhani tunazunguka mbuyu tuu hapa na theories nyingi sana. Serikali mbili so far zimekuwa sustainable (japokuwa kuna kasoro nyingi) serikali yenu ya tatu mnayoitaka ni assumption tupu, ni model ambayo imejaa assumption na Ifs. Na model yenu haingalii "hayo matakwa ya Wanzazibar". Jana tuu Maalim Seif amesema wanataka serikali ya mkataba. They need contractual union. Kwa nini hamtaki kujadili hili wanalo litaka?

Honest, mimi sio mshabiki wa huu muungano toka mwanzo sababu ya gharama na hauna economical au strategical benefit kwetu Tanzania bara, other than assumption za militarily advantage. Sasa lets cut the chase, tuambieni kwa nini tuangaike na muungano ambao hautakuwa sustainable?

Mchambuzi, hiyo analysis yako kuhusu Zanzibar economic growth ni kutokana na 1963 assumption kabla Tanzania Bara hamjawapa more spending oxygen. Sasa wanafanya all kind of projects kutokana na tax payer wa mchinga na nachingwea na mkisema wajiendeshe wenyewe mtatuleta disaster kama ya Ugiriki.

Mimi nasema kama hatuwezi kuboresha hizi mbili TUVUNJENI muungano, why mnaogopa kusema neno ambalo wote mnalitaka kulisema VUNJA. Msilete hadithi za Hablakadabla, Zanzibar economic growth yake sio sustainable kama sio Tanzania bara subsidy, ukiwaacha wajiendeshe is a recipe for disaster. Pato lao la taifa halifiki hata 1B USD, budget ya Zanzibar ni 650million USD. 50% of that ni government speeding on salary na mambo ya chai.

Kama mlikubali tangu 1964 kubeba msalaba nadhani it's too little too short kuja na agenda ya kuongeza serikali ya 3 ambayo itaendelea kubebesha vizazi vyetu deni zaidi ya hili. Hivyo kuliko kwenda that route nasema tugawaneni mbao as JK said.

Mtanganyika hapa naona kuna harufu fulani ya unafiki, lakini at the same time naona kuwa hata wewe unafiki unakushinda. Na hii ni trend kwa wabara wengi kwa sasa. Wengi ambao tuko in favour of muungano tuna swali moja ambalo serikali haitupi jibu. Kwanini tuwe na muungano ambao tunaulipia? tunaulipia kwa maana kuwa hatunufaiki chochote na muungano huo zaidi ya sifa za kisiasa na kumantain legacy ya Mwalimu na Karume.

Mkuu Nguruvi3 huwa anaeleza wazi kabisa kuwa muungano huu ni bomu, na ubomu wake ni kuwa unatugharimu na hautunufaini hata kidogo. Kama kweli una manufaa kwa wabara ingekuwa vizuri tuorodheshewe manufaa hayo, ili kama kuupigania tuupinaganie kwa nguvu, lakini so far CCM haitaki kusema hayo, zaidi ya Kusema Mwalimu na Karume waliunganisha nchi mbili. It is very unintelligent answer and absurd at best.

Suggestion that two governments are self sustainable is misleading. Economic realities proves otherwise, we are sustaining a useless union by footing a huge bill, and getting nothing in return.

Anayesema serikali mbili kwa sasa kimsingi anatudanganya, au anataka tuendelee kugharamia kitu ambacho hakitunufaishi. Mimi suggestion yangu ni serikali moja, yaani Zanzibar ife kama Tanganyika. Kama hilo haliwezekani serikali tatu zitaondoa ule mzigo ambao tumeubeba kwa muda mrefu, na zitaifanya Zanzibar iache malalamiko na iwe mchangiaji wa kweli wa muungano kuliko kuwa parasite.

Sioni kama kwa sasa ni dhambi kusikia neno VUNJA na wala usione aibu kulitaja, we are free to express our opinion.

kwa sasa realistic options za muungano ni: 1. serikali moja 2. serikali tatu. 3 kama hizo mbili haziwekeani kujna lugha nzuri ya nguruvi3...kila mtu abebe mbao zake.

Option ya mbili kwa style ya sasa inayolalamikiwa, au kusema tuondoe kero za muungano kwa style ya kurudi kwenye serikali mbili as per articles of union kama mwalimu na karume walivyofanya, in my opinion ni kudanganyana tu.

Uzuri ni kuwa serikali imeanza kutambua ukweli huu, ndio maana wanataka kufanya ujanja bunge la katiba lisimalize kazi yake, na kuweka kiporo kazi ya katiba.
 
Mkuu naomba kwanza niseme hivi, kama Zanzibar watakubalia kurudi mezani na kujadili agenda za muungano kama watu wazima na sio watoto walionyimwa pipi, basi ni mara million kuwa na serikali mbili kuliko kuleta mzigo wa Jaji Warioba wa serikali tatu.
Lalamiko la kwanza Tanganyika imejificha ndani ya koti la Tanzania inapigwa na wanasiasa wachache ambao wapo unguja ambao hawajui madhara halisi ya janga wanalolitaka. Na kuna kila haki ya msingi Wazanzibar wakaelemishwa kuhusu madhara wanayoyataka, na kisha wakaambiwa wapige referendum vote ya kuwa na mfumo huu huu au kuondokana nao na kuwa nchi huru. Hatuwezi kutengeneza mfumo mpya ili tuu kuwafuraisha watu 1.2 Million katika nchi ya watu 44Million. Yaani tutengeneze serikali ya tatu kwa 3% ya population. Na hili nyinyi ndugu zangu mnalipigia kelele kabisa kwamba eeh tulifanye. Jee inangia akilini kuanzisha new system just to sustain 3% of the people?

Lapili, ukweli ni kwamba matumizi ya Tanzania kwa Zanzibar yanaweza kuwa insignificant kama kweli tutazama namba zinasemaje. Pato la taifa ni 5.8 Billion Dollar kwa mwaka 2012 na tukakopa 4.2 Billion Dollar ili kufidia budget deficit, hivyo kwa mwaka 2012 tumekopa cent 42 kwenye kila shillingi tuliyotumia. Jee ni kiasi gani hapa tumepeleka Zanzibar? Total Zanzibar Budget ni 650 Million Dollar ukiangalia na total Tanzania budget hiyo ni 6% ya Budget yetu yote. Sasa mnataka tutengeneze serikali nyingine kupigania 3% ya watu ambao wanatumia 6% ya total budget? Tell me kama mnaona fikira za swala hili ni logic.

Sasa turudini mezani, pato la taifa limekuwa likiongezeka kwa takribani 15% kwa miaka 5 iliyopita likewise na matumizi yamekuwa yakiongezeka hasahasa kwenye recurrent expenditure ambayo ni 70% ya matumizi yote wakati 30% ndio mipango ya maendeleo. Maana kwenye kila shilling basi senti 30 ndio inakwenda kwenye mipango ya maendeleo, senti 70 inakwenda kwenye mambo mengine, military spending, ndege ya raisi, VX, chai, sambusa na mambo kama hayo. Sasa niambieni kwamba jee serikali ya 3 itapunguza haya matumizi? Na kama mlivyoona hapo juu Zanzibar wanatumia less than 7% ya Total Tanzania spending, sasa niembieni jee tukiweka serikali ya tatu haya yatapungua kwa asilimia ngapi? Tatizo tulilonalo sasa ni matumizi mabaya huku kwetu bara tunakopa centi 42 kwenye kila shillingi na 70% ya mkopo tunanunulia chai na vitu vingine ambavyo sio vya maendeleo na 93% of that inatumika Tanzania bara.

Nguvi03 umejikita sana kwenye Watalii wa Dodoma, lakini hiyo ni pocket change, sidhani kabisa kama tunatakiwa hata tujadili. Tuangalie vitu kama military spending ambayo kwa asilimia kubwa ni jeshi letu la Tanzania bara ndio linalotafuna pesa. Kama kweli mnataka tuzungumzie matumizi mabaya ya pesa ya taifa sidhani kabisa Zanzibar wanaweza hata kusogeza mizani. Balaa lipo kwetu huku Bara.

Sasa twendeni kwenye reality, jee serikali yenu ya Tanganyika itakuwa na ukubwa gani? Jee Muungano utaongozwa kwa fund gani? Jee Raisi wa Muungano atatoka upande gani (FYI 3% ya watu hawawezi hata siku moja kutoa raisi wa 97%)? na kama muungano utapata fund kwa kuchangia jee Zanzibar watachanga kiasi gani? Jee kwa nini kuwe na Bunge la Muungano ambalo litatumia pesa ambazo Tanganyika ndio atachangia by majority, so kwa nini Tanganyika isijifanyie maamuzi yake yewenyewe? Jee raisi wa Muungano atakuwa na nguvu kiaisi gani?
Kwanini tuingie kwenye complexity zote za fund wakati wao wapo 3% ya total population? Hili bunge la muungano mnalolipendekeza ni la nini? Kwa nini tuitaji bunge la muungano wakati kila nchi itakuwa inajiendesha yenyewe. Unaona jinsi hili swala mnalolitaka linavyoweza kuwa complex? Yaani mnataka tuumize vichwa kwa 3% of the population spending 6% ya budget ya taifa?

Ukiangalia hisabati utakubaliana na mimi kwamba serikali ya tatu ni kuongeza matumizi tuu, ili hawa vigogo na familia zao waendelee kuendesha VX za walipa kodi, wawapeleke vimada wao Dubai shopping. Hakuna justification. Jaji Warioba angesema ukweli kwamba sijui hesabu za serikali mpya ambayo ninataka muanzishe. Tukisema eti tufanye vipimo vya suti wakati hatuna kitambaa tutakuja kushikana mchawi tukaipeleka hii nchi pabaya zaidi ya hapa ilipo. Kuliko kumsikiliza Mboe na Wenzie ambao wapo kisiasa zaidi turudi mezani na tujumlishe.

Kusema kweli the math doesn't add up. Mimi nasema kama kweli Wanzanzibar hawataki kurudi mezani na kuchanachana ile katiba yao ya 2010, basi tugawaneni mbao. Wala msiombe kabisa kuongeza serikali ya tatu, kwani matumizi mliyonayo leo hayataondoka bali mtaongeza at least 2 Billion Dollar in spending na kuongeza gharama za nchi hii kwa at least 17%.

Mimi ningesema kweli mmejikita katika maendeleo kama mgekuja na Kauli Mbiu ya kulazimisha Katiba iweke kikomo cha kukopa pesa nje kuja kununua VX za wabunge tuu huku kwa kusupport Matumizi Ndani ya Uwezo wetu( balanced-budget amendment). We need balance budget clause ndani ya Katiba, na kwa wote wanaolilia serikali ya 3 this will be more beneficially kuliko hadithi za kuongeza makarani na watu wenye degree za diplomasia.
Nimelazimika kunukuu habari yako ili kujibu hoja zako nzuri na za kupotosha kama ifuatavyo;

Bajeti ya znz ni takribani Bilioni 700, ya JMT ni trillion 11. kwa hesabu zako ni karibia asilimia 6.3
Kiasi hicho siyo insignicant kama unavyosema. Kukimeza ni sawa na kuua bajeti ya wizara nzima.
Tafuta bajeti ya wizara ya utalii ulinganishe ni kiasi gani cha bajeti ili uone kama ni kiasi kidogo.

Senti 70 ulizosema zinakwenda katika mambo mengine, unasahau mambo hayo ni yale 22 ambayo umetaja baadhi kama ulinzi na usalama.

Kwa kupunguza mambo 22 na kubaki na 7 maana yake senti 70 itakuwa na thamani zaidi hasa Tanganyika kwa vile mambo 7 tu ya tume ya Warioba ndiyo yatamega senti 70 tena kwa kuchangiwa.


Matumizi mabaya ya fedha na ufisadi haihalalishi znz kupata subsidy.
Matumizi mabaya ni pamoja na kuelekeza fedha kule zisipohitajika kwenda ambao ni znz.

Hayo mengine ni jukumu la Watanganyika. Narudia hakuna uhalali wa znz kupata ruzuku kwasababu kuna vibaka Tanganyika.
Hapa tunaongelea nchi na nchi, katika usawa wa mbia wa muungano.


Muungano utapata fund kutoka kwa washirika. Washirika ni znz ambayo inapata asilimia 4 za pato la taifa, inapata asilimia 20 ya ajira, inapata free ride ya ulinzi na mambo 22.
Mshirika mwingine ni Tanganyika.


Kila nchi iyakuwa na vyanzo vyake vya mapato kama alivyoainisha Warioba.

Lakini jiulize kwasasa nani anachangia serikali ya muungano?
Vipi znz wakichangia kiasi chao, huoni inapunguza mzigo?


Bunge la muungano litakuwa na wabunge 75 tu. Wabunge hao ni wachache kuliko idadi ya Watalii wa znz Dodoma kwasasa ambao ni 81.

Bunge la muungano kila mshairika atachangia gharama za wabunge wake.

Kwasasa watalii 80 wanachangiwa na Tanganyika peke yake.

Zanzibar watachangia kiasi gani?
Jibu ni kuwa watachangia kama walivyofanya wakati wanadai mgao wa pato la taifa.

Walianza na 4 sasa ni 7% na walitaka 11%. Hesabu hazina tatizo, tatizo ni kuchangia na hilo linawezekana.

Watakuwa na uwezo wa kukopa na kupata misaada kama nchi huru, vipi uone hawana uwezo?

Rais wa muungano atakuwa na nguvu kwasababu ndiye mwenye jeshi, ndiye mdhamini wa washirika, ndiye mwenye mahakama ya juu.
Ndiye atakuwa alama ya nchi akiwa na katiba kuu ya muungano na mambo ya nje.

Katiba za washirika zitakuwa chini ya katiba ya muungano, unless wznz waendelee na kiburi kama cha 2010.

Bunge la muungano linashughulikia mambo 7 tu. Ni lazima mambo hayo yashughulikiwe na bunge la muungano kwavile hayapo kwa washirika. Hapo bunge litajadili mambo 7 na si 22 ya sasa ambayo miongoni mwao 15 hayawahusu watalii kutoka znz

Umesema katika senti 42 za misaada znz inapata kiasi gani.
Hili ndilo linatumika kupotosha ukweli kwa kuifanya Tanganyika kama mfadika ili kuhalalisha subsidy kwa nchi ya jirani.

Niatakupa mfano tu, narudia mfano tu wa jinsi senti 42 zinavyotumika.
Assume watalii 80 wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na 37
Wafanyakazi asilimia 20 wa muungano wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 32
Ulinzi na usalama (jeshi na mambo ya ndani) wanapata senti 10, Tanganyika inabaki na senti 22
Mishahara inayotoka hazina wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 17
Wizara ya mambo ya nje na balozi zetu, wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 12
Elimu ya juu, wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 7
Pato la taifa wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 2
Mchango bajeti ya znz, wanapata senti 5, Tanganyika tunadaiwa senti 3(minus)

Kwa haraka haraka wznz wanapata senti 40 kwa mambo machache sana.
Tukiweka yote 22 zikiwemo Tanganyika sijui itabaki na senti ngapi

Indirect benefit pengine ni nyingi kuliko hizo gharama nilizotaja.

Hivyo suala la misaada haliangaliwi kwa kiasi gani kimepatikana bila kuangalia mambo yanayoambatana na misaada.

Mwenyewe umesema wanapata subsidy, sasa unadai hawapati kitu katika senti 42. Tumekuonyesha kwa takwimu zisizo za kitaalamu ili kila mmoja aelewe.

Tukizungumzia GP,GDP, Import export na kuingia kwa Investment tutachanganya umma.
Hebu twende taratibu na hesabu za mifano ya darasa la 2B.


Serikali 3 haziongezi gharama, kwa Mtanganyika zinapunguza sana.
Kama kuongeza gharama ni kwa znz hilo sina utetezi.


Nikupe mfano, Watalii 80 tu waokuja Dodoma wanakula milioni 10 kwa mwezi kila mmoja ambazo ni sawa na milioni 800 kwa mwezi na bilioni 9.6 kwa mwaka.

Hapo achilia mbali Utalii katika kamati na makando kando mengine.

Hizo bilioni takribani 10 ni zigo la Mtanganyika.
Jiulize mkoa wa Singida wamepata mgao wa keki ya taifa kiasi gani?


Ukiacha watalii na kuingia kwa hesabu halisi ni wazi kuwa tunapoteza karibu trilioni moja.
Wao wanapoteza nini?

Kwasasa tuna serikali 2, hebu tuambie zikiwa na mambo 22 zinapunguzaje gharama.
 
Nimelazimika kunukuu habari yako ili kujibu hoja zako nzuri na za kupotosha kama ifuatavyo;

Bajeti ya znz ni takribani Bilioni 700, ya JMT ni trillion 11. kwa hesabu zako ni karibia asilimia 6.3
Kiasi hicho siyo insignicant kama unavyosema. Kukimeza ni sawa na kuua bajeti ya wizara nzima.
Tafuta bajeti ya wizara ya utalii ulinganishe ni kiasi gani cha bajeti ili uone kama ni kiasi kidogo.

Senti 70 ulizosema zinakwenda katika mambo mengine, unasahau mambo hayo ni yale 22 ambayo umetaja baadhi kama ulinzi na usalama.

Kwa kupunguza mambo 22 na kubaki na 7 maana yake senti 70 itakuwa na thamani zaidi hasa Tanganyika kwa vile mambo 7 tu ya tume ya Warioba ndiyo yatamega senti 70 tena kwa kuchangiwa.


Matumizi mabaya ya fedha na ufisadi haihalalishi znz kupata subsidy.
Matumizi mabaya ni pamoja na kuelekeza fedha kule zisipohitajika kwenda ambao ni znz.

Hayo mengine ni jukumu la Watanganyika. Narudia hakuna uhalali wa znz kupata ruzuku kwasababu kuna vibaka Tanganyika.
Hapa tunaongelea nchi na nchi, katika usawa wa mbia wa muungano.


Muungano utapata fund kutoka kwa washirika. Washirika ni znz ambayo inapata asilimia 4 za pato la taifa, inapata asilimia 20 ya ajira, inapata free ride ya ulinzi na mambo 22.
Mshirika mwingine ni Tanganyika.


Kila nchi iyakuwa na vyanzo vyake vya mapato kama alivyoainisha Warioba.

Lakini jiulize kwasasa nani anachangia serikali ya muungano?
Vipi znz wakichangia kiasi chao, huoni inapunguza mzigo?


Bunge la muungano litakuwa na wabunge 75 tu. Wabunge hao ni wachache kuliko idadi ya Watalii wa znz Dodoma kwasasa ambao ni 81.

Bunge la muungano kila mshairika atachangia gharama za wabunge wake.

Kwasasa watalii 80 wanachangiwa na Tanganyika peke yake.

Zanzibar watachangia kiasi gani?
Jibu ni kuwa watachangia kama walivyofanya wakati wanadai mgao wa pato la taifa.

Walianza na 4 sasa ni 7% na walitaka 11%. Hesabu hazina tatizo, tatizo ni kuchangia na hilo linawezekana.

Watakuwa na uwezo wa kukopa na kupata misaada kama nchi huru, vipi uone hawana uwezo?

Rais wa muungano atakuwa na nguvu kwasababu ndiye mwenye jeshi, ndiye mdhamini wa washirika, ndiye mwenye mahakama ya juu.
Ndiye atakuwa alama ya nchi akiwa na katiba kuu ya muungano na mambo ya nje.

Katiba za washirika zitakuwa chini ya katiba ya muungano, unless wznz waendelee na kiburi kama cha 2010.

Bunge la muungano linashughulikia mambo 7 tu. Ni lazima mambo hayo yashughulikiwe na bunge la muungano kwavile hayapo kwa washirika. Hapo bunge litajadili mambo 7 na si 22 ya sasa ambayo miongoni mwao 15 hayawahusu watalii kutoka znz

Umesema katika senti 42 za misaada znz inapata kiasi gani.
Hili ndilo linatumika kupotosha ukweli kwa kuifanya Tanganyika kama mfadika ili kuhalalisha subsidy kwa nchi ya jirani.

Niatakupa mfano tu, narudia mfano tu wa jinsi senti 42 zinavyotumika.
Assume watalii 80 wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na 37
Wafanyakazi asilimia 20 wa muungano wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 32
Ulinzi na usalama (jeshi na mambo ya ndani) wanapata senti 10, Tanganyika inabaki na senti 22
Mishahara inayotoka hazina wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 17
Wizara ya mambo ya nje na balozi zetu, wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 12
Elimu ya juu, wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 7
Pato la taifa wanapata senti 5, Tanganyika inabaki na senti 2
Mchango bajeti ya znz, wanapata senti 5, Tanganyika tunadaiwa senti 3(minus)

Kwa haraka haraka wznz wanapata senti 40 kwa mambo machache sana.
Tukiweka yote 22 zikiwemo Tanganyika sijui itabaki na senti ngapi

Indirect benefit pengine ni nyingi kuliko hizo gharama nilizotaja.

Hivyo suala la misaada haliangaliwi kwa kiasi gani kimepatikana bila kuangalia mambo yanayoambatana na misaada.

Mwenyewe umesema wanapata subsidy, sasa unadai hawapati kitu katika senti 42. Tumekuonyesha kwa takwimu zisizo za kitaalamu ili kila mmoja aelewe.

Tukizungumzia GP,GDP, Import export na kuingia kwa Investment tutachanganya umma.
Hebu twende taratibu na hesabu za mifano ya darasa la 2B.


Serikali 3 haziongezi gharama, kwa Mtanganyika zinapunguza sana.
Kama kuongeza gharama ni kwa znz hilo sina utetezi.


Nikupe mfano, Watalii 80 tu waokuja Dodoma wanakula milioni 10 kwa mwezi kila mmoja ambazo ni sawa na milioni 800 kwa mwezi na bilioni 9.6 kwa mwaka.

Hapo achilia mbali Utalii katika kamati na makando kando mengine.

Hizo bilioni takribani 10 ni zigo la Mtanganyika.
Jiulize mkoa wa Singida wamepata mgao wa keki ya taifa kiasi gani?


Ukiacha watalii na kuingia kwa hesabu halisi ni wazi kuwa tunapoteza karibu trilioni moja.
Wao wanapoteza nini?

Kwasasa tuna serikali 2, hebu tuambie zikiwa na mambo 22 zinapunguzaje gharama.

Nguvu na kaka Mchambuzi. Kwanza data hizi nimezitoa kwenye Budget ya Tanzania 2012/2013, nilichofanya hapo ni kuweka nyama kwenye mifupa, kuchambua kiasi ambacho hata kijana mdogo anaweza kufahamu.

1. Mjadala huu naomba ujikite kwenye ukweli zaidi na tuweke pembeni maoni ambayo mengi hayana tija ni kelele tuu. Kwanza nimesema 6.3% amabyo ndio matumizi ya Zanzibar katika budget ya Tanzania sio 100% yote wanayopata kutoka Tanzania Bara wao wenyewe wanakusanya kodi na non tax revenue ambayo ni sawa na 38% ya gharama, hivyo msaada unaotoka bara ni 62% ya gharama yao nzima ya kuendesha Zanzibar. (Tafadhari rejea kwenye budget ya Tanzania 2012/2013 Jeduwali la kwanza kwenye hadidu za rejea na Zanzibar – Public Financial Management Performance Report ambayo ni public data). Hivyo kusema kwamba tunawapa 100% ya budget yao nadhani ni kukinza ukweli.

2. Unapotazama ulinzi na usalama na ukatazama resource allocation katika sehemu hii kiasi kinachokwenda Zanzibar ni tone kwenye bahari. Sidhani kama tunaweza jikita kwenye kujadili matumizi ya millioni shillingi kwenye billion transaction. Nadhani hizo ni kelele. Katika upande mwingine wa shillingi, budget ya serikali ya Zanzibar ina allocate fund kwenye kila maeneo ambayo yako katika Zanzibar Provence.

3.Mmekuwa mkisema kwamba Serikali ya Muungano haitakuwa na gharama za juu, leo hapa mmeweka wazi, kwamba kutakuwa na Raisi ambae atakiwa apatiwe Ikulu, msafara wa ving'ora, na staff cabinet nzima ambayo hakuna aliyekuja hapa kusema itakuwa na ukubwa gani. Vilevile hamna hata uhakika kwamba Zanzibar watakubali katiba shiriki za hizi nchi za kusadikika ziwe chini ya Katiba ya Muungano. Ni lipi mnaloliamini kwamba Wazanzibar watafanya amendment ya katiba yao ya sasa? Umeona jinsi mnavyokuwa watu wa nchi ya kusadikika? Hizi zote ni assumption tupu.

3. Hawa watalii wa Dodoma ambao wanakupa pressure gharama yao yote ni 0.00009% ya gharama yote ya Tanzania. Sasa kama nilivyosema tujikite kwenye ukweli na tuache maoni. Hivyo, sidhani kabisa hili swala la Wabunge wa Baraza la Wawakilishi kuja Dodoma linaongeza au kupunguza chochote.

Ni ukweli usio pingika na mungu anaona na ni shahidi, Sio Jaji Warioba wala nyinyi ambao mnafahamu kabisa gharama za hii serikali ya tatu. Wote mmetengeneza ukuta wa kusema kwamba gharama zake zitakuwa za kawaida. Lakini ukweli upo pale pale kwamba hili litaongeza gharama tafadhali angalia uchambuzi ufuatao.

(a) Sehemu kubwa ya matumizi ya recurrent expenditure inakwenda Tanzania Bara. Najua utarudi kwenye yale mambo 7, lakini ukweli ni kwamba katika hayo mambo 7 tukiangalia ratio ya salaries and wages expenses at least 90% ya Wafanyakazi wanatoka bara na either una muungano au hauna muungano bado utalipa salaries and wages ni 21% ya budget yako. Hii ni SUNK COST. Hakuna njia yoyote ile unaweza ipunguza laba mfuate ushauri wa balance budget amendment. Vilevile kama nilivyosema mwanzo Jeshi ndio linakula sana pesa, lakini jee ni resource kiasi gani za jeshi zipo allocated ZNZ? Utaona ni peanuts tuu.

(b) Zanzibar mnasema itachangia kwenye muungano, kwa sasa gharama za kuendesha hayo mambo 7 ni karibu na 2.5 Billion dollar. Zanzibar pato lao ni 200 Million dollar, ukisema uwape Zanzibar wachangie 11% utakuwa umewaambia watoe 71% ya pato lao la taifa kuweka kwenye muungano. Jee unadhani wataweza? Mnasema waende wakakope, hakuna development bank yoyote ile duniani ambayo itakupa mkopo katika ratio ya 1:1 revenue/debt. Hivyo hilo la kusema tutawapa Zanzibar asilimia 11 halipo.

(c) Serikali ya Tanganyika bado matumizi yake yapo palepale, kwamba at least 9 Billion Dollar ndio total expenditure na revenue yetu ni 58% of that. Na hapa sababu sasa tunachangia muungano kwa 2.36 Billion Dollar tutajikuta tunakopa sasa 60% ili kuweza kujikimu na kubalance budget.

Kusema kweli kama kweli mnataka maendeleo basi option ni Wanzibar warudi kufanyia marekebisho ile katiba yao, tuweke clause ya Balance Budget Amendment kwenye katiba mpya. Na tuje na proportional representation. Au turudi kwenye the best Option Vunja Muungano sababu hatuwezi kujiingiza kwenye gharama zisizo na kichwa wala miguu.

Ndio maana wenzetu kabla hawajaingia kwenye mambo haya wanafanya study. Hapa hakuna study wala nini mnataka tukanunue kitambaa ndio fundi afanye vipimo?
 
Mtanganyika, twende taratibu kwa hesabu rahisi ili kila mmoja aelewe.
Ninasema ukianza mambo ya Dow Jones,Nikkei, GDP etc ni njia rahisi ya kuwaacha baadhi nje.
Hili ni suala la kitaifa twende taratibu.

Kuhusu Watalii wa znz Dodoma, unasema gharama zao ni kidogo.
Well, Bilioni 10/mwaka ni revenue collection ya znz kwa mwezi.
Kwamba gharama za watalii 81 ni sawa na kuendesha SMZ/mwezi katika miezi 12.

Hii maana yake ni nini
1. Subsidy unayoongelea ndiyo inafanya kazi. Jiulize mkoa wa Singida umepata kiasi kwa mwaka.
Kama mkoa mmoja utapata kiasi kinachokaribiana na watalii 81, hizo ni gharama kidogo?

Bilioni 10 zinatosha kudhamini wanafunzi elimu ya juu wapatao 1,000 kwa kiwango cha Tsh 10milioni kwa kila mmoja.Badala ya kusomesha wanafunzi 1,000 tunawapa Watalii 81 Dodoma.
Watalii wa serengeti huleta Dollar, hawa kutoka znz wanachukua Dollar.

Bilioni 10 ni sawa na kiwango kilichotolewa kudhamini wanafunzi 1,000 wa znz.
Tanganyika inalipia bilioni 10 kwa wanafunzi 1000 wa znz na bilioni 10 kwa watalii 81.
Ukiweka jumla hiyo ni bilioni 20 kwa wznz 1081.Kiasi gani kilikwenda Kigoma kwa shughuli za maendeleo.

Kama kuna jambo linalowatisha wznz ni ulinzi na usalama.
Hajatokea mznz yoyote kusema ulinzi na usalama usiwe muungano.
Unasikia mkataba hawasemi wazi,tunajua ni kuhusu ulinzi na usalama.

Ulinzi na usalama peke yake unakula zaidi ya 10% ya pato la znz ukiwa nje ya muungano.
Kwa pato ni 200milioni Dollar, ina maana 20milioni ni ulinzi. Kwasasa hizo 20million Dollar hawana zinalipiwa na Tanganyika.

Income ya wznz wanaielekeza katika shughuli za maendeleo na income ya Mtanganyika inaelekezwa katika kumsaidia mznz ili aelekeze pesa zake kunakohitajika.

Hata kama ni bilioni 1 bado tujiulize bilioni 1 zinaweza kufanya nini.
Kwa hesabu ya kawaida sana, kwa nyumba ya milioni 20, Bilioni 1 inajenga nyumba 50 za Walimu.
Kiasi hicho ni kidogo kivipi. Na kwanini udhani ni kidogo ili hali anayekihitaji anakiogopa.

Znz wanasema ni wabia sawa wa muungano na wanahitaji heshima, hadhi na mgawanyo sawa wa madaraka.Unaposema hawawezi kuchangia ni kwenda tofauti na mawazo yao.

Kwasasa wanapata 7% ya pato la taifa na wanadai ifike 11%. Vipi utuaminishe kuwa hawawezi kuchangia hata 4 ikiwa wana uhuru wa kukopa na misaada?

Malalamiko ya wznz ni kunyimwa uhuru wa kukopa na misaada.
Tume imewapa uhuru, kwanini udhani hawawezi na kuwa serikali 2 zitabaki salama bila mizozo.

Wznz wamekimbia kutoa mafuta na gesi ili wapate vyanzo vya mapato,vipi leo utuambie hawawezi kuchangia?

Sasa kama hawawezi kuchangia kwanini wanataka kuwa nchi yenye bendera, wimbo wa taifa, mipaka n.k. Kwanini wasiwe mkoa ili tujue ni sehemu ya mikoa yetu kama Ruvuma.

Orodha ya mambo Tanganyika inayabeba juu ya znz kwa jumla ni zaidi ya bajeti ya wizara moja.
Hivi unawezaje kusema gharama za wizara moja ni tone la maji.

Tumekuuliza kuwa kama serikali 3 ni gharama basi tueleze serikali 2 zinapunguzaje gharama katika comperative analysis.

Landa nikuonyeshe kwanini serikali 3 zitapunguza gharama.

1. Kila mshirika atakuwa responsible kwa mapato na matumizi yake.
Kwa mfano, SMZ ipo responsible ndiyo maana BLW lina wajumbe 50.
Lakini kwa kujua Tanganyika itabeba mzigo, watalii wa znz katika bunge la JMT ni 81.
Kwa serikali 3 hawa hawatahudumiwa na Tanganyika.

2. Bunge la shirikisho litakuwa na wabunge 75. Kila mshirika atahudumia wabunge wake bila kupitisha gharama kwa mwenzake.

3. Ofisi ya Rais wa shirikisho itakuwa ndogo kwasababu ya udogo wa shughuliza shirikisho.
Gharama zitachangiwa na washirika. Mfano, wafanyakazi wa muungano watalipwa na serikali husika kwasasa zigo anabeba Mtanganyika
Znz inataka usawakwa kujua zigo la gharama atalibeba Msukuma, mbondei na Mnayakyusa.

4. Kila nchi itashughulikiwa mambo yasiyo ya muungano bila bughudha.
Kwa mfano, suala la elimu ya juu litakuwa kwa washirika tofauti na sasa ambako zigo la wanafunzi wa znz linabebwa na Myao, Mjita na muha.

Wakati watoto wa Wamakonde, warangi na wahaya wakitakiwa kurudisha mikopo wenzao wanachukua pesa za bure. Resource hizo zitaelekwezwa kwa washirika bila athhri kwa mwingine. ZNZ wanaleta wanafunzi wengi wakijua zigo anabeba Mzaramo asiye na mtetezi

5. Kutakuwa na nidhamu kwa washirka. Tanganyika itaamua ukubwa wa bunge lake na taasisi zake. Kwasasa ukubwa unaamuliwa kisiasa ndiyo maana tuna watalii 81 wengine wakiwakilisha watu 1000. Gharama hizi zilizokwepwa na SMZ zitakwepwa na Tanganyika.

6. Kila nchi itasimamia taasisi zake. Leo tunalipa ada IMO, znz wanakusanya mapato kuipitia ZMO.
Leo kuna wajumbe wa bodi ambao ni watalii wa aina nyingine.

Hivi mzanzibar anafanya nini NECTA ili hali wana baraza lao?
Hivi kwanini bodi zote zimejaa wznz ili hali wana taasisi zao. Gharama hizo Tanganyika itazikwepa na kumrudishia mzanzibar. Hatuwezi kulipa Watalii pensheni kwa kazi zisizowahusu.

Hayo ni kwa urahisi na ujumla, lakini tukiangia kwa undani utaona mfumo wa serikali 2 maana yake ni kumtupia mznz Mbeleko.

Mtanganyika hana mtetezi na ndio maana wamefikia mahali siku hizi wanadai vyeo tu kwasababu gharama za vyeo na mambo yao ni zigo la mnyamwezi, Mpogoro na Mkinga.
Nani atawaongelea hawa? Hawana serikali.

Tukuombe utupe mchanganuo wa serikali 2 zitakazojibu gharama na malalamiko ambayo ni ya pande zote bila mmoja kuwa mgongoni mwingine akicheza msewe.
 
Mtanganyika, twende taratibu kwa hesabu rahisi ili kila mmoja aelewe.
Ninasema ukianza mambo ya Dow Jones,Nikkei, GDP etc ni njia rahisi ya kuwaacha baadhi nje.
Hili ni suala la kitaifa twende taratibu.

Kuhusu Watalii wa znz Dodoma, unasema gharama zao ni kidogo.
Well, Bilioni 10/mwaka ni revenue collection ya znz kwa mwezi.
Kwamba gharama za watalii 81 ni sawa na kuendesha SMZ/mwezi katika miezi 12.

Hii maana yake ni nini
1. Subsidy unayoongelea ndiyo inafanya kazi. Jiulize mkoa wa Singida umepata kiasi kwa mwaka.
Kama mkoa mmoja utapata kiasi kinachokaribiana na watalii 81, hizo ni gharama kidogo?

Bilioni 10 zinatosha kudhamini wanafunzi elimu ya juu wapatao 1,000 kwa kiwango cha Tsh 10milioni kwa kila mmoja.Badala ya kusomesha wanafunzi 1,000 tunawapa Watalii 81 Dodoma.
Watalii wa serengeti huleta Dollar, hawa kutoka znz wanachukua Dollar.

Bilioni 10 ni sawa na kiwango kilichotolewa kudhamini wanafunzi 1,000 wa znz.
Tanganyika inalipia bilioni 10 kwa wanafunzi 1000 wa znz na bilioni 10 kwa watalii 81.
Ukiweka jumla hiyo ni bilioni 20 kwa wznz 1081.Kiasi gani kilikwenda Kigoma kwa shughuli za maendeleo.

Kama kuna jambo linalowatisha wznz ni ulinzi na usalama.
Hajatokea mznz yoyote kusema ulinzi na usalama usiwe muungano.
Unasikia mkataba hawasemi wazi,tunajua ni kuhusu ulinzi na usalama.

Ulinzi na usalama peke yake unakula zaidi ya 10% ya pato la znz ukiwa nje ya muungano.
Kwa pato ni 200milioni Dollar, ina maana 20milioni ni ulinzi. Kwasasa hizo 20million Dollar hawana zinalipiwa na Tanganyika.

Income ya wznz wanaielekeza katika shughuli za maendeleo na income ya Mtanganyika inaelekezwa katika kumsaidia mznz ili aelekeze pesa zake kunakohitajika.

Hata kama ni bilioni 1 bado tujiulize bilioni 1 zinaweza kufanya nini.
Kwa hesabu ya kawaida sana, kwa nyumba ya milioni 20, Bilioni 1 inajenga nyumba 50 za Walimu.
Kiasi hicho ni kidogo kivipi. Na kwanini udhani ni kidogo ili hali anayekihitaji anakiogopa.

Znz wanasema ni wabia sawa wa muungano na wanahitaji heshima, hadhi na mgawanyo sawa wa madaraka.Unaposema hawawezi kuchangia ni kwenda tofauti na mawazo yao.

Kwasasa wanapata 7% ya pato la taifa na wanadai ifike 11%. Vipi utuaminishe kuwa hawawezi kuchangia hata 4 ikiwa wana uhuru wa kukopa na misaada?

Malalamiko ya wznz ni kunyimwa uhuru wa kukopa na misaada.
Tume imewapa uhuru, kwanini udhani hawawezi na kuwa serikali 2 zitabaki salama bila mizozo.

Wznz wamekimbia kutoa mafuta na gesi ili wapate vyanzo vya mapato,vipi leo utuambie hawawezi kuchangia?

Sasa kama hawawezi kuchangia kwanini wanataka kuwa nchi yenye bendera, wimbo wa taifa, mipaka n.k. Kwanini wasiwe mkoa ili tujue ni sehemu ya mikoa yetu kama Ruvuma.

Orodha ya mambo Tanganyika inayabeba juu ya znz kwa jumla ni zaidi ya bajeti ya wizara moja.
Hivi unawezaje kusema gharama za wizara moja ni tone la maji.

Tumekuuliza kuwa kama serikali 3 ni gharama basi tueleze serikali 2 zinapunguzaje gharama katika comperative analysis.

Landa nikuonyeshe kwanini serikali 3 zitapunguza gharama.

1. Kila mshirika atakuwa responsible kwa mapato na matumizi yake.
Kwa mfano, SMZ ipo responsible ndiyo maana BLW lina wajumbe 50.
Lakini kwa kujua Tanganyika itabeba mzigo, watalii wa znz katika bunge la JMT ni 81.
Kwa serikali 3 hawa hawatahudumiwa na Tanganyika.

2. Bunge la shirikisho litakuwa na wabunge 75. Kila mshirika atahudumia wabunge wake bila kupitisha gharama kwa mwenzake.

3. Ofisi ya Rais wa shirikisho itakuwa ndogo kwasababu ya udogo wa shughuliza shirikisho.
Gharama zitachangiwa na washirika. Mfano, wafanyakazi wa muungano watalipwa na serikali husika kwasasa zigo anabeba Mtanganyika
Znz inataka usawakwa kujua zigo la gharama atalibeba Msukuma, mbondei na Mnayakyusa.

4. Kila nchi itashughulikiwa mambo yasiyo ya muungano bila bughudha.
Kwa mfano, suala la elimu ya juu litakuwa kwa washirika tofauti na sasa ambako zigo la wanafunzi wa znz linabebwa na Myao, Mjita na muha.

Wakati watoto wa Wamakonde, warangi na wahaya wakitakiwa kurudisha mikopo wenzao wanachukua pesa za bure. Resource hizo zitaelekwezwa kwa washirika bila athhri kwa mwingine. ZNZ wanaleta wanafunzi wengi wakijua zigo anabeba Mzaramo asiye na mtetezi

5. Kutakuwa na nidhamu kwa washirka. Tanganyika itaamua ukubwa wa bunge lake na taasisi zake. Kwasasa ukubwa unaamuliwa kisiasa ndiyo maana tuna watalii 81 wengine wakiwakilisha watu 1000. Gharama hizi zilizokwepwa na SMZ zitakwepwa na Tanganyika.

6. Kila nchi itasimamia taasisi zake. Leo tunalipa ada IMO, znz wanakusanya mapato kuipitia ZMO.
Leo kuna wajumbe wa bodi ambao ni watalii wa aina nyingine.

Hivi mzanzibar anafanya nini NECTA ili hali wana baraza lao?
Hivi kwanini bodi zote zimejaa wznz ili hali wana taasisi zao. Gharama hizo Tanganyika itazikwepa na kumrudishia mzanzibar. Hatuwezi kulipa Watalii pensheni kwa kazi zisizowahusu.

Hayo ni kwa urahisi na ujumla, lakini tukiangia kwa undani utaona mfumo wa serikali 2 maana yake ni kumtupia mznz Mbeleko.

Mtanganyika hana mtetezi na ndio maana wamefikia mahali siku hizi wanadai vyeo tu kwasababu gharama za vyeo na mambo yao ni zigo la mnyamwezi, Mpogoro na Mkinga.
Nani atawaongelea hawa? Hawana serikali.

Tukuombe utupe mchanganuo wa serikali 2 zitakazojibu gharama na malalamiko ambayo ni ya pande zote bila mmoja kuwa mgongoni mwingine akicheza msewe.

Mkuu kwanza sio kweli 10 Billion shillingi haindeshi serikali ya Zanzibar kwa mwezi. Kuendesha serikali ya znZ kwa mwezi ni kati ya 50-55 Million dollar kwa mwezi tafadhali rejea Znz budget 2012.

Mkuu naona unakimbia hoja, mimi nakuchambulia kutokana na economic reality sababu that is my concern, wewe unaongelea 10 Billion shillingi ambayo ni 0.00009% ya government expenditure. Nimekwambia kwamba gharama ya kuendesha muungano kama tukaiweka at low benchmark ni 2.5 Billion dollar, Zanzibar mnasema wachangie 11% hiyo 71% ya pato zila la Zanzibar, niambie watachangiaje. Znz wana budget deficit ya 400 Million USD ambayo ni 62% ya budget yao, jee watachangia vipi?

Achana na hadith za hao watalii, mnataka tujadili namba twende kazi. Mimi sitaki mpotoshe umma na story zenu za serikali tatu. Tujikite kwenye HISABATI.

Leo mmeanza story za Zanzibar wana mafuta, just to disclose mkuu mimi nafanya kama analyst kwenye kampuni ya Mafuta, na Zanzibar haipo hata kwenye world petroleum reservoir plan. Hivyo hadith za mafuta ni longolongo, sio kila penye bahari panamafuta ndio maana hujawai sikia Boston wamengundua mafuta.
 
Serikali mbili za sasa gharama ni 10 Billion dollar na nimechambua hapo juu kwamba 92% ya gharama hizi ni sunk cost ama tuwe na muungano au tusiwe na muungano haziendi kokote. Gharama ambazo tunaweza kuziondoa ni za ZNZ ambazo hazizidi 8% ya gharama zote. Mkituongezea serikali za tatu mnaleta 2.5 billion dollar new cost ambayo ni increase ya gharama kwa 21%.

Mimi nasema tuvunjeni muungano, acheni kuleta story. Jaji Warioba na genge lake wamekimbia kufanya hisabati. Haya tumejidolea kufanya hesabu hapa. Mimi sio CCM lakini kwa hili nasema asante Mungu CCM are majority. Kama kweli mnataka tuwekeni balance budget clause kwenye katiba kukomesha overspending ya hawa viongozi walevi wa madaraka.
 
Mtanganyika,
Nakusoma sana na takwimu zako za ki-serengeti advisors ambazo hazitoi hata chembe za majibu ya hoja zetu kwamba: sio kweli znz hawatakuwa na uwezo wa kuchangia gharama za muungano katika yale mambo saba na hilo limeshajadiliwa kwa hoja lakini anaamua kubaki mbugani serengeti. Pili ni hoja yetu kwamba Kwa mfumo wenu, mnatuumiza walipa kodi kwani mfumo wenu una:Ya muungano, ya Tanzania bara na ya mchaganyiko; sasa kwa vile mnatuelewa, sasa mmekuja na baraza la wawakilishi wa Tanzania bara, which means mabunge matatu, serikali mbili. Kwa kweli mmelewa sana ukada. Nitakuja na takwimu zangu tena kama bado haujatembelea threads zangu za nyuma.vinginevyo una kiporo cha maswali yangu kwako haujajibu.

Na swali kwamba mfumo wa sasa ni nafuu kwa mlipa kodi kuliko serikali tatu, tuonyesheni namba? Mnajificha mbugani serengeti.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom