Mtazamo: Kuhusu MCC kusitisha msaada wa MCC 2 na shughuli zake Tanzania

Huyu tangu awe nduwila kuwili na kupiga domo kwiiingi amepuuzika like a used toilet paper.
 

Misri wanapewa fedha kama Fidia ambayo waliahidiwa Kumaaliza Vita Na Israel, Misri wanapewa Fidia Kwa sababu Israel Iliwanyemelea kivita bila kuwatangazia Vita na Wakaharibu Vifaa vyao vya Kivita na Mali nyingi. Hayo yalikuwa ni Makubaliano ya Kupatikana amani kati ya Misri na Israel. Sio Msaada per ce
 
Anahalalisha walichokifanya Zanzibar.
 
Tumbo linatuponza wengi,unaweza kujitoa ufahamu bila aibu,mleta mada kwann wamesahau kukupa ukuu wa wilaya .mmelikoroga mlinnywe full stop mengine ni blah blah unaleta
 
Huwezi kukataa misaada yote, mingine ni yakistaarabu!

Sijaona ubaya wa MCC.
Wamefadhaika na uchaguzi Zanzibar.Sidhani kama kuna watanzania wengi waliofurahia uchaguzi ule.
Wamepigia kelele sheria ya utandawazi.Watanzania pia kwa ujumla wao walipinga sana hii sheria.
Ni ustaarabu gani unaozungumzia?
 
CCM ya sasa wanasema wataendelea na Katiba Pendekezwa,Polepole anasema waliokwamisha katiba ya Warioba wamehamia UKAWA,huyu mpumbavu aseme nini nimwamini
 
Sijaona ubaya wa MCC.
Wamefadhaika na uchaguzi Zanzibar.Sidhani kama kuna watanzania wengi waliofurahia uchaguzi ule.
Wamepigia kelele sheria ya utandawazi.Watanzania pia kwa ujumla wao walipinga sana hii sheria.
Ni ustaarabu gani unaozungumzia?
Haya ni mawazo yako usiwasemee watanzania wote! Kama ni watanzania wote mbona wengine wamepiga kura za marudio?
 
sawa je wakikuambia huruhusiwi kuruka 20,000ft kutoka usawa wa bahari na kusafiri zaidi ya 5km ndani ya bahari tutafanyaje maana hawashindwi ata kuleta yale mandege yao yapo kama popo yakawa yanakatiza kwenye anga letu je tunauwezo wa kupambana nao!!??
 
Pole pole sababu walizotaja MCC (dubious election in Zanzibar na Cybercrime) zina chembe ya ukweli au hakuna? Kama ukweli upo hakuna namna ya kukwepa lawama hapa. Kama wao ndo wametunyima kabla sisi hatujakataa basi hoja zako zinakosa nguvu.
Tatizo la msingi lipo ila tunarukiarukia vijisababu na historia tofauti. Tuna tatizo tulitafutie ufumbuzi siyo kujishauwashauwa. Yawezekana wana malengo yao mengine lakini tatizo tunalo tukubali hilo kwanza kabla ya kujitetea uwongo.

Tusikiuke misingi ya haki halafu tuseme tuna demokrasia yetu inayokua taratibu. Kama ndiyo hivyo tuachane na mambo ya kuwa na katiba haina haja. Maana tutasema katiba na sheria zetu zina historia ya ulaya au Asiatuachane nazo na tuifanye ndo demokrasia yetu. Viongozi wa Afrika wakibanwa kuhusu kukiuka misingi wanakimbilia this is African democracy.
 
Upo sawa ila hapo kwenye nyeusi ondoa kabisa hatupaswi kuuza mazao ghafi tuuze bidhaa zilizotokana na hayo mazao kwani hata sasa hatuuzi mazao nje si tunauza.
 
Huwezi kukataa misaada yote, mingine ni yakistaarabu!
Nchi za dunia ya tatu zinategemea wahisani na wafadhli kujikwamua kimaendeleo. Nchi zote zinazotoa misaada kuja kwa nchi masikini ni nchi za kibepari.

Sasa nitajie misaada yote na inapotoka kuwa huu ni wakistaarabu na huu si wakistaarabu kwa data rasmi na sababu ya kusema kwanini huu ni wakistaarabu au sio wakistaarabu.
 
Polepole nae msanii tu!Yaliyotokea zanzibar kuhusu mzozo wa kisiasa zijafurahishwa nayo kipi hujafurahishwa nacho si hamna tatizo asa mbona unaweweseka mara misri mara palestina hayo yanakujaje?Mhe. Kikwete alishawahi kusema wajinga ndo waliwao.........!
 
Tusubiri tuone hili picha la kihindi linaisha vipi..........Watanzania ni mabingwa wa kuandika riwaya
 
Upo sawa ila hapo kwenye nyeusi ondoa kabisa hatupaswi kuuza mazao ghafi tuuze bidhaa zilizotokana na hayo mazao kwani hata sasa hatuuzi mazao nje si tunauza.
sawa ataondoa je wakikuambia bidhaa yako haijakizi viwango ata kama we unajua imekidhi viwango wakakuambia inabidi waichome moto na petrol ambayo haijachakachuliwa kutoka kwa gadafi ambaya alikuwa na sauti ambayo ata baada ya miaka 200 tutakuwa hatujaifikia !! tutafanyaje?
tafakari chukuwa hatua!!
 
Haya ni mawazo yako usiwasemee watanzania wote! Kama ni watanzania wote mbona wengine wamepiga kura za marudio?
Hapo nimekuelewa.Naona kwa mtizamo wako Uchaguzi Vsiwani ulikuwa wa huru na haki na MCC walipaswa kutupa pesa yete kwa vile Dr Shein alipata ushindi wa kishindo wa asilimia 92%.Tupo pamoja!
 
Polepole amekuwa kichaa siku hizi coz anataka ukuu wa wilaya
 
Ovyo kabisa kama mliyaona hayo mapema kwanini msingezikata, kwanini leo wamegoma kutoa ndio mnaanza kutoa sababu za ovyo kuficha ukweli,suala la zanzibar na sheria ya makosa ya kimtandao wamesema uongo?au mnatafuta sababu ya kuwaambia wadanganyika,tuache kujifariji au mnataka mpaka mama ntilie alipe kodi,? Makusanyo ya 1.3 tr kwa mwezi hayatoshi kukidhi bajeti ya 25tr tungekuwa tunakusanya 3tr au 4tr kwa mwezi apo tungeringa lakini sasa ni porojo tu kila mtu anajidai mchumi
 
Misaada ya kistaarabu ni ile ambayo haiambatani na masharti. Unafahamu kwanini Baba wa Taifa alielekea China kuomba msaada wa kujenga reli ya TAZARA? Ni kwasababu nchi za magharibi wakati ule zilitoa masharti mengi ikiwemo kutounga mkono jitihada za nchi za Kusini kujipatia uhuru wao!
 
Hapo nimekuelewa.Naona kwa mtizamo wako Uchaguzi Vsiwani ulikuwa wa huru na haki na MCC walipaswa kutupa pesa yete kwa vile Dr Shein alipata ushindi wa kishindo wa asilimia 92%.Tupo pamoja!
Nimekuambia usiseme "watanzania"! Mimi na wengine kama milioni 30 hatuna mawazo kama ya kwako! Semea NAFSI yako na siyo kujumuisha watanzania wengine!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…