Mtazamo: Kuhusu MCC kusitisha msaada wa MCC 2 na shughuli zake Tanzania

Mtazamo: Kuhusu MCC kusitisha msaada wa MCC 2 na shughuli zake Tanzania

Nonda #87

Ubutu wa kufikiri ni tatizo kubwa nchini. Muungano upo naturally, ni kuweka misingi ya kuimarisha uwepo usiwepo tutakuwa pamoja iwe iwavyo.

Muungano haulindwi na maderaya.USSR isingesambaratika, Shah wa Iran asingefia ughaibuni. Itafika mahali haitawezekana

Mfano, kauli ya Sitta katika video imelenga kudhoofisha muungano badala ya kuujenga

Wanaondoa suala la siasa katika majukwaa wanalipeleka katika imani.

Hawajifunzi, ktk mambo yote duniani, imani inaonekana inaunganisha watu kwa nguvu

Siku nguvu hiyo itakapotimia, dereya, mizinga vifaru havitakuwa na kazi.

Shah wa Iran anajua, Mfalame wa Hungary anaju, Gorbachev anajua hilo

Niachie hapo

Bilioni 5 kwa maagizo wakijua SMZ haitolewi kwa karatasi.
Ilihitaji nini basi kufanya uchaguzi na kutumia migharama yote hiyo? Jipu
Gharama za kuweka majeshi kule hazielezeki na sijui kama si jipu

Rais alisafiri na kuacha shughuli za umma achilia mbali gharama kwenda kuomba MCC.
Wakati huo walijua ili kupata lazima demokrasia ya watoaji itimie.

Walirudi na kutamba, tumepewa kwasababu ya utawala bora na demokrasia!

Leo wanarudi na hadithi za kipuuzi wakituma wapambe eti MCC isiingilie Demokrasia yetu.

Huko nyuma walisifia demokrasia yetu kama kigezo cha kupata MCC.

Unaweza kuona kwanini wazungu wanatuendesha!Hatujitambui. Tulienda kuomba! jipu

Wakatueleza miradi ni matokeo ya safari za Rais na Demokrasia nchini.
Leo wanaponda eti ''tunaweza bila misaada''!
Kwanini hatukuweza wakati ndege zinaruka kwenda NY kila subuhi?

Wanaona hasira za wananchi, wanatuma wapambe watushawishi uzalendo!
Huu ni utoto! Uzalendo leo! Uzalendo gani mapesa yametumika katika ze comedy ZNZ

Hakuna cha uzalendo, ukweli unabaki pale pale MCC wapo sahihi.
Tuliende kuomba wenyewe. Tumeshindwa kujisimamia sasa wakitusimamia tuna ng'aka

Tutaanza kulipia nguzo za umeme kwasababu hawana pesa, zilikuwa za MCC
Gharama hiyo wanatupambaza eti uzalendo

Hili tusimame pamoja, hatuwezi kuwa Taifa la watu 100 au 200 ni watu milioni 45 .

Hatuwezi kudanganywa na uzalendo wakati uzalendo umewashinda wao.

Hawawezi kufuja mapesa kwa ze comedy wakitushawishi ni uzalendo
 
- Gharama na utu wetu kama Taifa hauwezi kupimwa kwa Shillingi Trilioni Moja kwanza ni matusi makubwa sana, Wamarekani walupomuua Chief Abiola Nigeria kusudi waibe mafuta yao hatukusema kitu sio kwamba hatukujua, Walipoivamia Iraq walisema kuna Chemical Weapons mpaka leo hawajaziona, Walipomuibia kura Al-Gore hatukusema kitu, Walipomuua rafiki yao wa zamani Saddam Hussein hatukusema kitu,

- Zanzibar ni Taifa huru lenye Sheria na Katiba yake ambayo inasema kama kuna aliyedhulumiwa uchaguzi anatakiwa aende Mahakamani, Muungano wetu hauna uhusiano na Uchaguzi isipokuwa Ulinzi kwa waliochaguliwa na Serikali iliyochaguliwa, so

- Wabaki na misaada yao, Tulikuwa watumwa once sio wakati wote!!

le Mutuz
 
- Gharama na utu wetu kama Taifa hauwezi kupimwa kwa Shillingi Trilioni Moja kwanza ni matusi makubwa sana, Wamarekani walupomuua Chief Abiola Nigeria kusudi waibe mafuta yao hatukusema kitu sio kwamba hatukujua, Walipoivamia Iraq walisema kuna Chemical Weapons mpaka leo hawajaziona, Walipomuibia kura Al-Gore hatukusema kitu, Walipomuua rafiki yao wa zamani Saddam Hussein hatukusema kitu,

- Zanzibar ni Taifa huru lenye Sheria na Katiba yake ambayo inasema kama kuna aliyedhulumiwa uchaguzi anatakiwa aende Mahakamani, Muungano wetu hauna uhusiano na Uchaguzi isipokuwa Ulinzi kwa waliochaguliwa na Serikali iliyochaguliwa, so

- Wabaki na misaada yao, Tulikuwa watumwa once sio wakati wote!!

le Mutuz
Kuna nini basi hata hao wasimamizi wa kimataifa wakashindwa kuyaona hayo mapungufu unayoyasema wewe?

Nakwanini hawaku complain chochote juu ya uchaguzi wa Tanzania Bara?

Kikwete alipokwenda MCC hakujua vigezo vya democrasia iliyozungumziwa?
 
tufike sehemu tujikubali,,ipo siku watatuonea wivu,,ndipo misaada yao haitakuwa na mashart makali,,mcc safar njema natambua ipo siku mtarud kwa jina lingine namsipe nafas kirahis kama mlivyo ingia.
Hivi unajua kuna misaada ya aina ngapi kutoka marekani? MCC ni misaada ilionza kutolewa baada ya kuanzishwa taasisi ya MCC mwaka 2004 na serikali ya marekani. sifa ya kupewa msaada huu ni utawala bora na demokrasia. Kwahiyo kuna misaada mingi tuu huo mmoja ndio umefutwa.
 
Na ili nchi yetu ipige hatua katika nyanza zote tunahitaji misaada ya utaalamu zaidi kuliko fedha ili tuweze kujitegemea
Na km mataifa haya wanayojiita wahisani wangekuwa na nia njema wangekuwa wamewekeza ktk elimu ambayo pekee ingelikwamua bara la Afrika badala yake wamekuwa mstari wa mbele kuinyang'anya afrika wataalamu wote na kuwaweka katika taasisi zao za kinyonyaji zinazoitwa za kumataifa
Sera ya deindustrialization pekee ni pigo kubwa ambalo AFrika tungekuwa na uhuru wa kulazimisha bidhaa zinazozalishwa kutokana na malighafi inayopatikana afrika viwanda vyake vijengwe afrika . Afrika ndo lingekuwa bara lenye viwanda vingi kukiko yote
(OMBA OMBA HAJAWAHI KUTAJIRIKA)
(HAKUNA UTUMWA MBAYA KM UTUMWA WA AKILI)
 
- Gharama na utu wetu kama Taifa hauwezi kupimwa kwa Shillingi Trilioni Moja kwanza ni matusi makubwa sana, Wamarekani walupomuua Chief Abiola Nigeria kusudi waibe mafuta yao hatukusema kitu sio kwamba hatukujua, Walipoivamia Iraq walisema kuna Chemical Weapons mpaka leo hawajaziona, Walipomuibia kura Al-Gore hatukusema kitu, Walipomuua rafiki yao wa zamani Saddam Hussein hatukusema kitu,

- Zanzibar ni Taifa huru lenye Sheria na Katiba yake ambayo inasema kama kuna aliyedhulumiwa uchaguzi anatakiwa aende Mahakamani, Muungano wetu hauna uhusiano na Uchaguzi isipokuwa Ulinzi kwa waliochaguliwa na Serikali iliyochaguliwa, so

- Wabaki na misaada yao, Tulikuwa watumwa once sio wakati wote!!

le Mutuz
Hizi story mnazileta Leo baada ya kunyimwa msaada.
Kwanini maneno haya hamkua mkiyasema wakati tukipokea misaada?
Ni katiba ipi inayotoa nafasi ya kwenda kupinga matokeo ya urais mahakamani?

Wehu wa CCM leo mtaharisha viwavi jeshi vyote ila kwenye hili la MCC hampindui.
 
Stupid Kama sio marekani ku_subsidise dawa za ukimwi tungelikuwaje afrika hasa tanzania
 
Polepole hina tofauti ns dada poa wanaouza utu wao kwa pesa. Njaa na ussliti vinakusumbua. Ulale mahali pema peponi na usaliti wako
 
"Rai yangu kwa Vyama vya upinzani nchini jaribuni kuweka utaifa kwanza na siasa baadae" kwa yaliyofanywa zanzibar tutakuwaje wazalendo? never ever!
 
Humphrey Polepole, ishukuru sheria ya makosa ya mtandao! Natetea sana nchi kujenga uwezo wa kujitegemea na kuthamini uhuru wake bila kuingiliwa na taifa lingine kwa kisingizio cha misaada. Lakini yule anayejaribu kuupotosha ukweli kwa maslahi yake au ya kikundi flani kwa makusudi ni mmbaya zaidi.
 
KUHUSU MCC KUSITISHA MSAADA WA MCC 2 NA SHUGHULI ZAKE TANZANIA: MTIZAMO

Nianze na nukuu hizi mbili kuntu za Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere- Mwenyezi Mungu amrehemu.

“Democracy is not a bottle of Coca-Cola which you can import. Democracy should develop according to that particular country”. June 1991 in Rio De Janeiro, Brazil

"Demokrasia sio chupa ya Coca-Cola ambayo unaweza kuagiza. Demokrasia lazima ikue na kuendelezwa kulingana na nchi husika". Juni 1991 Rio De Janeiro, Brazil (Tafsiri ni yangu)

“No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people”. From ‘A Peaceful New Year’ speech, Tanzania, January 1968

"Hakuna Taifa lina haki ya kufanya maamuzi juu ya Taifa lingine; wala watu juu ya watu wengine ". Hotuba ya Amani ya Mwaka Mpya, Tanzania, Januari 1968 (Tafsiri ni yangu)

Hili la Marekani na uamuzi wa MCC ni jambo la mpito na haliwezi kuua mahusiano yetu na Marekani. Tanzania na Marekani zinashirikiana kwa mambo mengi na MCC ni sehemu tu tena ni eneo jipya la ushirikiano. Uamuzi huu ni jaribio kwa uhuru wa Taifa letu. Hakuna namna nyingine ila kushinda hili kama tulivyoshinda mengine huko nyuma. Kwa wale ambao wameuona umri watakumbuka namna tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi 1964 pale walipotaka kuwa na kauli hasi dhidi ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi baada ya kutaka kuingilia Uhuru wa Mataifa Mawili huru yaliyoamua kuungana na kuunda Nchi Mpya ambayo leo tunajivunia, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 1965 Tulivunja uhusiano na Uingereza kufuatia na kitendo cha wazungu wachache kujitangazia Uhuru (Unilateral Declaration of Independence) kule Rhodesia na uingereza kukaa kimya na kushindwa kuchukua hatua stahiki.

Tulivunja Uhusiano na Uingereza kuieleza Dunia kwamba Uhuru wa nchi za Afrika ni kipaumbele muhimu kwa Tanzania. Jambo tunalopaswa kufahamu ni kuwa MCC 2 toka mwanzo imekuwa ni mtihani dhidi ya uhuru wetu. Napenda ieleweke kwamba kipindi hiki kilichotokea sio kuvunjika kwa uhusiano wetu na Marekani bali taasisi ya MCC ndio imesitisha msaada wao kwetu, lakini mahusiano yetu na marekani bado yako pale pale, na si Marekani au Tanzania inayoweza kuugharimu uhusiano wetu.

MCC 1 ilikuwa ni chambo cha kutuvuta na tulipewa bila masharti tena hela nyingi dola milioni 698 na ni fedha tulizopewa moja kwa moja na kupewa uhuru wa kuamua tuzitumieje. Tanzania ilitakiwa kuainisha maeneo kisha wao wanatoa hela. Ndio maana miradi kama ile barabara ambazo hazikuwa zikipata ufadhili kwa kuwa hazikuonekana ni za kiuchumi na miradi ya maji ya Morogoro na kwingineko iliingizwa humu na kupata ufadhili. MCC 2 sio hivyo. Kwenye MCC 2 walengwa wakubwa ni sekta binafsi ya Marekani, hapa kuna mtego hapa, hapa ni biashara hapa.

Mchakato wa MCC 2 ulipoanzishwa, wafanyabiashara kwa kushirikiana na Maseneta wakaanzisha hoja kuwa kwanini Marekani inatoa fedha kwa ufadhili katika nchi ambazo China ndio wenye kufaidika na fedha hizo? Wakaleta hoja ya kuwa Serikali ya Marekani ifanye jitihada ya kuweka fedha kwa kusaidia Sekta Binafsi ya Marekani kupenya Afrika.

Ukaitishwa mkutano wa US-Africa Summit na agenda kubwa ikawa Power Africa. Katika Power Africa, Marekani ikalichagua eneo la Nishati (si uzalishaji viwanda) kwa kutambua kuwa ndio eneo pekee wanaloweza kushindana na wachina. Wakasema wataelekeza fedha huko kuisaidia Afrika kutatua tatizo la nishati ambalo ndio pembejeo ya viwanda. Wakaweka sharti kuwa fedha hizo na miradi hiyo itatekelezwa na Sekta Binafsi ya Marekani.

Ndio sababu wengi wenu mtakumbuka hata Rais Obama alitangazia dhamira ile pale Ubungo kwenye Mitambo ya Symbion Power na sio kwamba alipenda kwenda kutembea Ubungo. Kuanzia hapo kumekuwepo na shinikizo kubwa sana na masharti magumu na yenye kuhamahama (shifting goal post) kutaka kuibaka sekta ya nishati nchini ikiwemo mageuzi ya TANESCO. Zikaainishwa hatua kadhaa,ambazo utekelezaji wake baadhi ni kisheria na kisera na hivyo haziwezi kwenda kwa deadline walizotaka. Kila bodi ikikutana wanaibua hiki na kile lakini wakisema hela watatoa. Hela hizi zikawa zimeshikiliwa kama chambo ukisogelea zinasogea, ni sawa na ule mchoro wa Mpanda Punde aliyeshika fimbo yenye majani na akiielekeza mbele ya punda, kwamba punda ataendelea kuyafuata majani akidhani atayafikia kumbe ndio anaupiga mwendo. Hatimaye wakasema wanasubiri uchaguzi mkuu jambo ambalo halihusiani na madai ya mwanzoni. Baada ya uchaguzi wakaibuka na suala la Zanzibar.

Hivyo, uamuzi wao wa leo ni uamuzi uliotarajiwa. Pia ni uamuzi wenye madhara kwa sekta binafsi ya Marekani pia ambayo ndio ilikuwa itekeleze miradi hiyo. Kama Taifa ni muhimu kulinda utu na uhuru wetu. Ndio msingi wa sera yetu ya nje toka mwanzo na hata sasa. Tumetofautiana na Marekani katika hili tutapatana katika mengine. Ndio uhai wa maisha ya diplomasia.

Wao nao wanayo hadhira ya wapiga kura wao wanayojaribu kuituliza huko nchini kwao kwa uamuzi huu. Tunapaswa kuheshimu uamuzi wao kama ambavyo wanapaswa kuuheshimu wetu. Hatimaye baadae tutapatana. Marekani inaihitaji Tanzania zaidi na Tanzania inaihitaji Marekani. Marekani inahitaji MCC 2 zaidi hali kadhalika Tanzania inahitaji MCC 2.

Mahusiano ya Tanzania na Marekani hayakuanza na hayataisha na MCC. MCC imeyakuta na itayaacha.

Kama marudio ya uchaguzi wa Zanzibar ndio kigezo, basi Marekani isingekuwa inatoa zaidi ya Dola Bilioni 3 kila mwaka kwa Egypt iliyo chini ya utawala wa kijeshi kwa sababu ya kuununua ugomvi wa Egypt na Israel na isingetoa kiasi cha dola bilioni 6 kwa Israel kila mwaka kwa yale wanayoyafanya dhidi ya Wapalestina.

Huu ni wakati ambao Taifa linawaita Wazalendo wake. Wazalendo wasimame na kusema 'Nchi yangu KWANZA, iwe Sahihi au Imekosea" na Makuwadi watashangilia na kusema "si mnaona sasa kiko wapi?".

Huu ni wakati wa kujifunga mikanda na kulinda heshima yetu kama Taifa letu. Tuna vyanzo vya mapato vingi sana ambavyo hatujaanza kukusanya mapato, tuwe wabunifu na tusibweteke na kutegemea mapato yataongezeka maradufu kwa vyanzo vile vile.

Niseme kwa uchache, sababu walizotoa MCC, na ieleweke aliyetoa tamko ni MCC, heri lingetoka tamko hili Wizara ya Mambo ya Nje au Ikulu ya Marekani, moja ni Zanzibar na pili ni Sheria ya Makosa ya Mitandao (Cyber crimes Act).

Sasa hebu tujadili kidogo, hivi kule Zanzibar tulitaka kitokee nini pale ambapo wanasiasa walikuwa hawataki kujadiliana? Tume ile ile ya Uchaguzi ambayo bado ilikuwa na uhalali wa kikatiba na kisheria kuuitisha, kuufuta na kuuitisha tena uchaguzi ikachukua nafasi yake. Wanasiasa wasio makini wakaishia kuhamishia malumbano mitandaoni badala ya kuitafuta suluhu ya kisiasa na pale siasa iliposhindikana basi wangeitafuta suluhu katika mahakama za Zanzibar. Mezani wakashindwa, mahakamani hawakwenda. Tume ikachukua uongozi, uchaguzi ukaitishwa Wananchi wakapiga kura na sasa huko Zanzibar kuna serikali na baraza la wawakilishi. Hata mimi sifurahii sana njia waliyoichukua Zanzibar lakini ilibidi siasa za madaraka zisite ili tuanze kufanya siasa za maendeleo. Je wamarekani walitaka muujiza gani utokee huko.?

Kuhusu Sheria ya Mitandao, hata mimi siipendi, si twende mahakamani, bunge litaanza vikao muda si mrefu je wabunge si wapeleke hoja ya kuifanyia marekebisho sheria hii. Sasa Marekani (MCC) inapoweka shinikizo kwa suala la Sheria ambayo ni jambo la ndani na linaloweza kujadilika, sijaelewa. Mbona sie hatujapiga kelele Yule jamaa yao Trump alipotutusi waafrika na kusema sisi stahili yetu ni kuwekwa tena chini ya ukoloni (hapa nimechomekea tu).

INDHARI

Ni aibu kwa viongozi wa kisiasa kufurahia jambo hili, ni ishara ya ukuwadi wa kisiasa na ambao uko tayari kukumbatia mahusiano yanayotweza Uhuru wetu. It is now high time kufanya siasa safi za maendeleo (politics of development) na sio kujikita katika katika siasa za madaraka (Politics of Power).

Mwandishi, Ndg. Humphrey Polepole amenufaika na uelewa wa watu wenye uzoefu wa mahusiano ya Tanzania na nchi za Nje. Aidha, ni mnufaikaji (alumni) wa programu ya uongozi chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani.
Mkuu Polepole nani asekufahamu?me sijaelewa wanunuliwa bei gani.Lijapo suala la utaifa tuache unafik na kuganga njaa.
 
hivi Karibuni utapewa U-DC , ukifika huko waambie wananchi kuwa hawatapata umeme walioahidiwa kwa sababu pesa ya MCC uliikataa. Usisahau kufagilia Sheria ya Makosa ya Mtandao na Ukiukwaji wa Demokrasia.
mpaka sasa sijui kilichokusibu ppole. Haiwezi kuwa njaa!!!
 
Polepole ndugu yangu hata mie ni CCM kama wewe, lakini ukweli suala la ukandamizaji wa demokrasia Zanzibar ni suala ambalo ni gumu sana kulitetea kwa kutumia akili timamu, let us be honest! utazunguka kote huko! na ni ujinga kudhani kuwa MCC haitaharibu uhusiano wetu na USA
Kada mweleze huyo mjinga hajielewi pambaf
 
Msikilize mtu anasema hataki msaada wakati hata matangazo ya siku ya choo yanafadhiliwa na watu wa Marekani
Je makusanyo ya Magu yatanunua dawa za ARV wanazopewa waathirika nchi nzima bure kwa msaada wa wahisani,wakati malaria inaua watu wengi kuliko ukimwi na hakuna dawa ya bure
Aah!...yako mengi mengine
Ahahahaha umeongea ya moyoni sna umenipa raha unajua sana ila magu ajue zile barabara alizokua anatamba amejenga na serikali yake sasa cjui alikua ajui ni mcc matambo ya musa yalimkosti kwa mungu sasa musa magu kumbuka tena na mabango ujayatoa kule ya msaada wa watu wa marekani au ndo anahisi ashavuka mto na wachina wake njaa tutapata wote lkn chama kitalaumiwa akumbuke hilo ndugu ndugu tuendelee kuwakumbusha sana wasilale
 
MCC walichokifanya si kizur sana lakini ni kizuri coz wametuonesha madhara yakuwategememezi . Watanzania tunapaswa kujitahidi sana tufanyekazi sana ili tuongeze kipato kwetu na taifa kwa ujumla. America inatufundisha somo na hayo ndio madhara yakutegemea. Watz tupigeni kazi tuuze bidhaa na mazao nje.
 
Wewe Mawazo yako yanaona Leo tu wala si hata kesho? Nani kakwambia kuwa msaada uliositishwa utakuwa wa MCC tuu?

Hebu usiwe Na Mawazo mgando huu ni mwanzo tuu misaada mingine itasitishwa Kwa awamu Kama ilivokua inatolewa.

Na cha kushangaza zaid wewe si lolote si chochote Kwa Tanzania, Waziri analialia ambaye anajua athari Kwa wazungu hapo ujue hakuna kitakachotoka.
 
Tatizo nilionalo hapa ni tafsiri ya kile Marekani inachomaanisha.
Kama Marekani yupo kimaslahi zaidi je,huu hautakuwa mwanzo wa mvutano mkubwa zaidi kati yetu na hawa mabwana wakubwa na wenzao?
Kama ndivyo,je,tumejiandaa kwa vita hii ya kimaslahi na Marekani?
Je,wale wanaotupa kiburi(naona watu wanajivunia mchina humu jf)wanao uwezo na dhamira ya kutusaidia pale wakubwa hawa watakapoamua kutushughulikia?
Je,ni lazima sana kutofautiana na mmarekani kwa wakati huu na kwa sababu zilizopo za masuala ya Zanzibar na cybercrime?
Hatuna njia nyingine ya kidiplomasia ya kuishi na hawa wakubwa huku maslahi yao na yetu yakienda sambamba bila ugomvi?
Ni lazima sana kukingiana kifua na mmarekani kwa sasa?Itatusaidia au itatuumiza?
Hekima inahitajika kuliko nguvu hapa.
Magufuli my friend,be very very veeery careful na hili suala..nakutahadharisha sana,now you need your head.
 
Back
Top Bottom