Mtazamo: Wanawake wengi wapo kwenye ndoa au mahusiano kwa sababu za kiuchumi zaidi na si mapenzi

Mtazamo: Wanawake wengi wapo kwenye ndoa au mahusiano kwa sababu za kiuchumi zaidi na si mapenzi

KikulachoChako

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2013
Posts
19,185
Reaction score
37,239
Habari za muda huu waungwana.

Mapenzi ni maisha na mapenzi ni sehemu kubwa ya maisha. Ni vigumu kuyaweka kando mapenzi kwani hata ukifanya hivyo moyo utakuamulia, hivyo basi hatuwezi kuyacha kuyajadili kwa mazuri na mabaya yake.

Nyakati za hivi karibuni kumeshamiri wimbi la hali ya uongo, usaliti, wizi, na ukatili kwenye ndoa. Wingi wa visa hivyo kumepelekea taasisi ya ndoa kupoteza maana mpaka mtu ukiamua kuoa watu wanakushangaa na kukuonea huruma kana kwamba unafanya jambo la kishetani.

Hasa nikiangazia upande wa wanawake walio kwenye ndoa unakutana na matukio ya usaliti wa kupindukia, unakutana na matukio ya wanawake kuwaibia waume zao au kufanya mambo yao kwa siri pasi na mume kujua kuamua kuachana na mumewe pindi tu anapopata uwezo wa kiuchumi na kuweza kujitegemea.

Vipo vilio vya wanaume wengi waliojaribu kwa namna moja au nyingine kuwainua wanawake zao kiuchumi kwa nia njema kabisa lakini matokeo yake yamekuwa machungu.

Wingi wa mtiririko wa matukio haya ya wanawake kukithiri kwa vilio hivi kwa wanaume kuongezeka kwa taraka na kukimbiana baada ya mke kujiona kuwa anaweza kujimudu yote inadhihirisha ukweli kuwa wanawake walio wengi wapo kwenye ndoa au mahusiano kwa sababu za kiuchumi zaidi kuliko mapenzi.

Kuna uwezekano mkubwa huyo unayemuita mkeo au mpenzi wako yupo na wewe kwa kuwa kwa muda huu ni wewe pekee unayeweza kusimamia vyema matatizo yake ya kiuchumi. Nguzo ya upendo haipo moyoni mwake.

Hatukatai kwamba mwanaume lazima utoe huduma kwa mkeo lakini kwanza yatangulie mapenzi kwani kwenye maisha kuna nyakati nyingi hasa si uungwana kuwa na mtu ndoani kwa sababu fulani kwani inawezekana sababu hiyo siku moja ikaondoka.

Ingawa hali ni ngumu na ni vigumu kutambua maana waigizaji ni wengi sana wanapoona kuwa kuna uwezekano wa kupata chochote kitu kwenye muunganiko huo tusijisahau wanaume wenzangu. Lazima ufanye jitihada za kumjua mwenzako ni mtu wa namna gani ili ujiandae kisaikolojia kukabiliana na unalolijua.

Word is enough for the wise.
 
Naunga mkono wanawake wanaokua kwenye mahusiano kwa sababu ya uchumi, viumbe vyote duniani vya jinsia ya kike vinapenda kuwa kwenye mahusiano kwa sababu yenye nguvu kama hiyo kwa maslai mapana ya kizazi chake.
 
Naunga mkono wanawake wanaokua kwenye mahusiano kwa sababu ya uchumi, viumbe vyote duniani vya jinsia ya kike vinapenda kuwa kwenye mahusiano kwa sababu yenye nguvu kama hiyo kwa maslai mapana ya kizazi chake.
Mwanamke anayeingia kwenye ndoa kwa Sababu za kiuchumi maana yake ni kuwa huyo ni mpita njia iko siku sababu hiyo ikaondoka atakuacha either kwa kupata kazi au biashara inayoweza kumuendeshea maisha yake......
 
Mwanamke anayeingia kwenye ndoa kwa Sababu za kiuchumi maana yake ni kuwa huyo ni mpita njia iko siku sababu hiyo ikaondoka atakuacha either kwa kupata kazi au biashara inayoweza kumuendeshea maisha yake......
Mwanamke hajawahi kupenda tu bure bure bila kuangalia kwanza maslai yake hasa ya kiuchumi 🤔
 
Ndio unafahamu Leo ? 99% mwanamke yupo na wewe kwa maslahi yake binafsi hivo kaa kijanja usijiachie Sana maana hatakiwi akusome na asijue hata Una kias gani cha pesa, wewe kaa nae kwa akili mbona ilishaandikwa
 
Tujiangalie na sisi Wanaumme! Je,tuko waaminifu katika ndoa zetu na wake zetu au mahusiano yetu na hawala zetu ?
Huenda chanzo cha hayo yote ni sisi Wanaumme!
Just imagine skandali ya Baltazar huko Eq.Gin!
Wanawake 400 huku ana mke!
 
Tujiangalie na sisi Wanaumme! Je,tuko waaminifu katika ndoa zetu na wake zetu au mahusiano yetu na hawala zetu ?
Huenda chanzo cha hayo yote ni sisi Wanaumme!
Just imagine skandali ya Baltazar huko Eq.Gin!
Wanawake 400 huku ana mke!
Hakika hata sisi wanaume sio wakamilifu tunafanya madudu mengi sana...lakini leo tunaangazia wanawake
 
Ndio unafahamu Leo ? 99% mwanamke yupo na wewe kwa maslahi yake binafsi hivo kaa kijanja usijiachie Sana maana hatakiwi akusome na asijue hata Una kias gani cha pesa, wewe kaa nae kwa akili mbona ilishaandikwa
Asante ndugu.....
Ndio maana nimejaribu kutoa mtazamo wangu hapa ili iwe kama ukumbusho kwa wengine
 
Waacheni sasa wametosha imekuwa ni wanawake wanawake tu na mods wanachekelea hawajui kuwa hz threads ndio zinaharibu jamii,ukiwa jf itakufanya uogope wanawake

Jf inapromote watu kuishi kihuni bila ndoa
Hakuna aliye promote kufanya hivyo ndugu pengine ni mtazamo wako.... isipokuwa tunakumbushana kwenye kuchagua wenza tuwe makini.....kuhusu watu kuishi kihuni ni utashi wao wenyewe.....
 
Jukwaa la mapenzi mkuu na mapenzi ni kati ya mwanamke na mwaume mkuu 🤔
Pamoja na hayo mkuu," mada dhidi ya wanawake zimekuwa nyingi mno. Kwanini wanaume tumekuwa watu wa kulia lia tu dhidi ya hawa viumbe? Tumesahau kuwa sisi ndio tunapaswa kuwaongoza hawa. Ukute huko mbinguni Mungu anatushangaa yale mamlaka aliyetupa dhidi ya hawa viumbe tumeyatupa wapi?
 
Tena nawasihi kabisa. Usijiumize kiuchumi kwa lengo eti la kumfanya mwanamke atulie. My brother hilo liko nje ya uwezo wako. Hata umtoe kwenye chumba cha 50,000 Vingunguti Relini ukampangie nyumba ya 700,000 Mikocheni, haimzuii kwenda kuliwa na bodaboda, muuza genge, mpaka rangi za kucha n.k. Acha kabisa kuongozwa na hisia. Hawa wanawake asilimia 98 wanajiuza either directly or indirectly. Acha kutumika kwa maslahi yao.
 
Pamoja na hayo mkuu," mada dhidi ya wanawake zimekuwa nyingi mno. Kwanini wanaume tumekuwa watu wa kulia lia tu dhidi ya hawa viumbe? Tumesahau kuwa sisi ndio tunapaswa kuwaongoza hawa. Ukute huko mbinguni Mungu anatushangaa yale mamlaka aliyetupa dhidi ya hawa viumbe tumeyatupa wapi?
Hayo mamlaka ulipewa lini mkuu na Mungu yupi na mbinguni ni wapi?
 
Pamoja na hayo mkuu," mada dhidi ya wanawake zimekuwa nyingi mno. Kwanini wanaume tumekuwa watu wa kulia lia tu dhidi ya hawa viumbe? Tumesahau kuwa sisi ndio tunapaswa kuwaongoza hawa. Ukute huko mbinguni Mungu anatushangaa yale mamlaka aliyetupa dhidi ya hawa viumbe tumeyatupa wapi?
Hapana mkuu wanaume hatulii isipokuwa tunawekana sawa.....

Rejea hasara ya mwanamume kwenye mahusiano umebeba mambo matatu......
1) Muda
2)Uchumi
3)Moyo

Kuna asilimia kubwa kwa mwanaume kuyaharibu maisha yake Kwa kufanya machaguo mabaya ya kuoa na huenda asiinuke tena kwenye maisha.... rejea kesi za taraka.......

Hivyo wingi wa mada kunaonyesha wingi wa mabaya na hivyo tunatakiwa kuwa makini
 
Tena nawasihi kabisa. Usijiumize kiuchumi kwa lengo eti la kumfanya mwanamke atulie. My brother hilo liko nje ya uwezo wako. Hata umtoe kwenye chumba cha 50,000 Vingunguti Relini ukampangie nyumba ya 700,000 Mikocheni, haimzuii kwenda kuliwa na bodaboda, muuza genge, mpaka rangi za kucha n.k. Acha kabisa kuongozwa na hisia. Hawa wanawake asilimia 98 wanajiuza either directly or indirectly. Acha kutumika kwa maslahi yao.
Asante mjumbe....

Ndio maana tupo hapa kukumbushana kwenye masuala ya msingi kama haya......
 
Back
Top Bottom