Nambie kaka
Ila ile kesi ya babu seya nimesikia sikia kuwa ilikuwa ya kutengeneza tu na haikuwa na ukweli ndani yake ndio maana raisi kawatoa. Ila wabakaji na walawiti huwa wanapata msamaha wa raisi?
Wenyewe wanafikiri usafi wa mwanasiasa ni kuwa chama flani.UKAWA ni Nzi wa kijani iliyozubaa ukitaka kujua hilo leo hii Jiwe akisema anahamia upinzani watamshangilia na kumpa kila Aina ya sifa unafiki wa Watanganyika hauna kifani dunia hii.
Mleta mada umeandika mengi, ila binafsi hebu nitulie hapo kwa Magufuli na Tundu Lissu.
Umesema binafsi hauna chama, good; umeanza kuzungumzia tukio la Tundu Lissu kwa kulaumu uovu ule aliofanyiwa.
Baadae umesogea zaidi ukazumgumzia uhasama uliopo kati ya Lissu na Magufuli ( kwa mtazamo wako).
Halafu ukaja hapo chini kumlaumu Lissu kwa kuichafua Tanzania, hapa sasa ndio nataka unisome vizuri unijibu;
Tanzania kwa mtazamo wako ni nini?
a) Rais Magufuli
b) Eneo la ardhi linalounda nchi yetu.
Kama jibu lako ni (a) iko hivi;
Rais Magufuli akiwa kama kiongozi wa taifa la Tanzania, tukubaliane kwa nafasi yake alikuwa na uwezo wa angalau kuagiza uchunguzi ufanyike juu ya tukio lile la kushambuliwa Tundu Lissu. Lakini hakuwahi kufanya hivyo, huku sio kuichafua Tanzania, ni kusema ukweli juu ya maovu yanayotokea Tanzania chini ya uongozi wa Rais Magufuli.
Sasa unapomshambulia Tundu Lissu anaichafua Tanzania kwenye hili ningependa kujua umetumia vigezo gani, na ningependa pia kujua wewe kwa upande wako ulitaka Lissu afanyaje kama wale wenye mamlaka ya kufanya kitu waliamua kukaa kimya?
Kama jibu lako ni (b) kwamba Tanzania ni eneo la ardhi, binafsi sijaona popote Lissu akilaumu kitu hicho, bali hulaumu yale yafanywayo ndani ya eneo hilo huku viongozi wake wenye mamlaka ya kuzuia hali hiyo wakiwa kimya, na hapa ndipo Lissu hu-base malalamiko yake.
Mara nyingi Lissu hutumia maneno; "Tanzania chini ya Rais Magufuli" akiwa anamaanisha Tanzania kama nchi, chini ya uongozi wa Rais Magufuli, kwamba huyu kiongozi ndie mwenye mamlaka ya kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia wake, bila kujali itikadi, rangi, dini, wala kabila.
Sent using Jamii Forums mobile app
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂UKAWA ni Nzi wa kijani iliyozubaa ukitaka kujua hilo leo hii Jiwe akisema anahamia upinzani watamshangilia na kumpa kila Aina ya sifa unafiki wa Watanganyika hauna kifani dunia hii.
Naomba nirudi tena hapo kwenye Siasa za Upinzani:
Unadai siku hizi wapinzani hawasemi watajenga madarasa, hospitali n.k. hivyo kazi yao imebaki kulaumu tu.
Nikwambie jambo, kazi ya upinzani sio kujenga shule, hospitali, na vinginevyo. Kazi ya upinzani ni kuisukuma serikali iwapelekee wananchi maendeleo. Wapinzani hawakusanyi kodi.
Hivyo, ulivyosema Magufuli anajenga reli, barabara, hospitali, kwanza umekosea, Magufuli hatoi fedha zake mfukoni kujenga hivyo vitu, ni fedha zinazotokana na kodi za wananchi, na kama huwa unamsikiliza Magufuli vizuri huwa anasema fedha za watanzania.
Hivyo kwa hapa sikubaliani na wewe.
Sent using Jamii Forums mobile app
Magufuli na Wananchi Wake:
Kama unasema Tanzania ni eneo jumlisha na watu waliopo, halafu unasema Lissu anaichafua Tanzania; binafsi sijawahi kumuona Lissu akiwalalamikia watanzania kwa kupigwa kwake risasi, siku zote Lissu analalamikia vyombo vya dola vilivyokuwa na jukumu la kuhakikisha ulinzi wake bali vikashindwa kutekeleza wajibu wao, na pia, Lissu anamlalamikia Magufuli, kwasababu kwa mamlaka yake alikuwa na uwezo wa angalau kuagiza uchunguzi ufanyike lakini hakufanya hivyo.Kwa mtazamo wangu sio (a) wala (b), kwangu Tanzania ni watu, eneo la ardhi likiwepo bila sisi kuwepo hapa pasingekuwa Tanzania. Kwa mtazamo wangu ukifanya jambo kuhusu Tanzania umelifanya kwa watu wa Tanzania na si kwa ardhi ya Tanzania kama unavyoona wewe. .
Binafsinaomba mnielewe siwezi kushangilia Tundu Lisu kupigwa risasi hata kama sina undugu nae tuna damu ya UTANZANIA kewa hiyo naelewa kushindwa hata mabeberu huko ulaya. .
Ila hapa inavyoonekana hili jambi linapelekwa kisiasa sana kana kwamba Magufuli anajua aliyempiga risasi Tundu Lisu. Hapo ndio naposhindwa ku argue na yeyote yule alafu mtu kufanyiwa uhalifu anaweza kuwa kafanyiwa na yeyote na tukiweka list ya nadharia ya watu wanaoweza kufanya vile ni wengi mno. .
Ila nchi hii ni mamlaka, na mamlaka katika mapana yake kunamamlaka chini yake. Hii nchi ina polisi na hata huko ughaibuni kuna polisi kama interpols si ndiyo? Unaweza kupeleka kesi yako popote pale kama umeona polisi wa Tanzania hawawezi kukusaidia. Tundu Lisu kagoma kutoa ushirikiano wowote kwa polisi wa Tanzania, Hapo Magufuli anafanyaje? Kwamba aamru polisi wafanye kazi yake? Au watu wanachotaka ni kuwaMagufuli acheze wimbo wa Lisu ili mseme kuwa si mnaona anacheza ule wimbo wake? Hana Imani na raisi alafu leo tushangae kuwa kwa nini Magu anaendelea na yake?
Mie sitaki kubishana kuhusu Lisu ila chukiyake ilikuwa kabla ya kupigwa risasi, kinachotokea hapa ni public sympathy. Nakumbuka siku Lisu anapigwa risasi nilisali sana kwa Yesu amtie nguvu na nimalaani sana kitendo hicho. Lakini haimpi sababu ya kufanya anayoyafanya na kuyaeleza huko ughaibuni huku akilenga kuharibu Tanzania (nikimanisha sisi ndio tunaoumia sio Magufuli) kwa chuki binafsi dhidi ya Magufuli. .
Huna hoja dogo zaidi ya kujikomba . Uzi umewafungulia wapinzani kuwananga as if wamemkwamisha mh Rais kutekeleza majukumu yake. Ukiomba kazi ya u Rais , wananchi wote ni wako. Wakupendao na wasiokupenda. Si kulipa visasi kwa wale wasiokukubali.“Siasa sio Matusi au Chuki, Hoja Hupingwa Kwa Hoja”
Hapo kwa Magufuli na Wananchi wake, umezungumzia chuki iliyopo baina ya makundi mawili, ningependa kwa mtazamo wako utuambie nini chanzo cha hiyo chuki?
Hapo ndio utajua hao unaowaona wana chuki, je, wanasababu ya msingi kuwa na hiyo chuki ama hawana, but usilazimishe watu kuwa na furaha bila kuwa na sababu ya kuwa nayo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama unasema Tanzania ni eneo jumlisha na watu waliopo, halafu unasema Lissu anaichafua Tanzania; binafsi sijawahi kumuona Lissu akiwalalamikia watanzania kwa kupigwa kwake risasi, siku zote Lissu analalamikia vyombo vya dola vilivyokuwa na jukumu la kuhakikisha ulinzi wake bali vikashindwa kutekeleza wajibu wao, na pia, Lissu anamlalamikia Magufuli, kwasababu kwa mamlaka yake alikuwa na uwezo wa angalau kuagiza uchunguzi ufanyike lakini hakufanya hivyo.
Sijui unafahamu tukio la siku Lissu anapigwa risasi ulinzi uliondolewa nyumbani kwake?
Na kamera za CCTV nazo ziliondolewa?
Kwa matendo hayo wewe binafsi unaweza vipi kuwa na imani na vyombo vya ulinzi?
Hata suala la Lissu kuwa na chuki hata kabla ya kupigwa risasi ni hisia zako tu, mtu kukemea uovu sio chuki, huwezi lazimisha kusifiwa hata pasipostahili.
Hivyo, argument yako kwamba Lissu anaichafua Tanzania (ukimaanisha watu na ardhi kama ulivyojibu mwenyewe) umekosea.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi binafsi sina chama, si kwa sababu nataka iwe ivyo, ni kwa sababu sijaona chama Tanzania chenye misimamo nayotaka mimi.
Rais Magufuli na Bunge:
Kwa mtazamo wangu nadhani si kwamba raisi Magufuli anapinga mhimili wa bunge, hili limedhihirishwa na mkataba alioingia Muheshimiwa Kangi Lugola. Kwa kauli yake kupinga mkataba ule Kwa kuwa haukushirikisha bunge wala serikali yake wala wizara nyingine husika Kama Wizara Ya Fedha. Nafikiri tu kwa raisi magufuli kukubali kupeleka mambo mengi ambayo anafanya sasa bungeni basi hayo mambo yangebaki kwenye ubishani yasingefanyika.
Kupeleka majadiliano bungeni inakuwa Kama mbwa ukimshika mkia hata afanye vipi atafanya unavyotaka wewe. Serikali yetu ingekuwa imeshikiliwa mkia ingebweka tu ila bunge lingekuwa linapoteza mda mwingi kwenye mabishano ya kisiasa yasiyo zaa matunda na mambo mengi yangesimama kama tulivyoona serikali zilizopita. Hapa tuna kubwa la kujifunza, kutokuwa Na uwiano mzuri kati ya serikali Na bunge.
Raisi Magufuli na Misimamo Yake Kisiasa:
Nakumbuka raisi Magufuli alivyoingia madarakani katika mambo aliyoyafanya mwanzo Ni kupinga siasa zisifanyike wakati uchaguzi umepita. Kwa wapinzani waliona Kama wananyimwa kuwa huru kisiasa kiasi cha kumwita Magufuli Ni ditekta. Upande wa pili kwa raisi Magufuli alipinga hili ili kupisha maendeleo yafanywe na wale viongozi waliochaguliwa, akisisitizia, siasa za majukwaa zimepita sasa waliochaguliwa wafanye siasa za ktekeleza yale waliyoyaimba kwenye majukwaa. Lakini kitu ambacho nakiwaza tu Ni kuwa raisi Magufuli aliruhusu waliochaguliwa wawe wapinzani au awe CCM anaruhusiwa kufanya siasa kwenye jimbo lake hususani madiwani Na wabunge.
Mimi binafsi niko wilaya ya Ubungo Na nimepita sana Pwani huko na hata mkoani Kilimanjaro ambapo ni nyumbani, lakini sijaona madiwani au wabunge walioita mikutano kujadili lipi lifanyike kuleta maendeleo (nimeuliza maeneo mengi ila hiki ndicho kinachoendelea). Nani kaenda kufanya mikutano ya hadhara kakataliwa kwenye jimbo lake?
Magufuli na Tundu Lisu:
Kwanza kabisa nasikitika Sana kwa mheshimiwa Tundu Lisu kupigwa risasi mchana kweupe na jambo hili kupelekwa kisiasa. Ila nimeona jambo ndani ya Mheshimiwa Tundu Lisu na chuki yake dhidi ya raisi Magufuli. Binafsi wanasiasa wanachukiana ila chuki zao ni za kisiasa wakiwa kwenye mziki wanacheza pamoja, binafsi sijui chuki hizi zililetwa na nini ila wao binafsi wanaelewa kindaki ndaki sio tunashabikia tu. Ila nasikitika sana kitendo cha mheshimiwa Tundu Lisu kwenda kuichafua Tanzania ili tusipewe misaada kwa chuki yake binafsi dhidi ya raisi, bila kujali anachikiomba anawaathiri vipi wa Tanzania.
Mheshimiwa Tundu Lissu anazunguka sehemu nyingi duniani kutaka wajitenge Na Tanzania wakati familia yake, ndugu zake Na ukoo wake wapo Tanzania. Amezunguka akiomba mabeberu watunyime misaada kitu ambacho hajui kingemuathiri kila mTanzania. Amediriki kukubaliana Na mabeberu tena nimesikitika Sana kusikia mheshimiwa Tundu Lisu akisapoti ushoga kabisa kwa mdomo wake mwenyewe na kuikandia serikali ya Tanzania ka kukataa ushiga ilihali anajua tamaduni hizi kwetu hazipo. Mbali na kuichafua Tanzania hao mabeberu bado wamekuwa mstari wa mbele kuleta misaada na kuikopesha Tanzania.
Mheshimiwa Tundu Lisu amekosa uzalendo kuhusu Tanzania juu ya chuki yake dhidi ya Magufuli. Kama alikuwa na mashtaka binafsi juu ya Magufuli sikatai ila hana ulazima wa kuichafua Tanzania na kuchinganisha na nchi rafiki, hata Magufuli akitoka madarakani uhusiano uliopo kati ya Tanzania na nchi nyingine utabaki, anapotaka kuuvuruga hata aje raisi mwingine lile doa litakuwepo tu ..
Raisi Magufuli hata Kama anayoyafanya analazimisha Kwa wananchi wa Tanzania na yatabaki kwa wananchi wa Tanzania. Hizo ndege si zake Ni za waTanzania, Na juhudi hizi zinaonekana ni za kujenga Tanzanua; huku Tundu Lisu anabomoa kile kinachojengwa kwa wa Tanzania. Tanzania inasonga mbele Kwa shida kwa raha ila inasonga mbele.
Siasa na Taaluma:
Kwa mtazamo wangu tu nchi yetu imeshindwa kutofautisha siasa na taaluma, hapo mwanzo tulikuwa tuko kwenye shimo dogo tu ila kwa sasa tuko kwenye shimo kubwa sana. Raisi Magufuli kwa kuchagua viongozi wenye taaluma zao kwa asilimia kubwa ameua nguvu nzito kwenye taaluma yetu. Kila m Tanzania sasa amekuwa mwanasiasa kitu ambacho kimekuwa sana katika utawala huu wa awamu ya tano. Ukienda chuoni, mashuleni, jeshini na maofisini watu wengi wamekuwa wanaacha taaluma zao na kuingia kwenye siasa. Baadhi ya viongozi au taaluma (mfano maprofesa, madokta, wanajeshi) ambao wamechaguliwa na raisi wetu wangeweza kuwa walimu wazuri wazalishe wanasiasa wazuri ila wameacha kuzalisha wanasiasa na wamekuwa ndio wanasiasa wakubwa. Sasa kumekuwa na taaluma mbovu kwa sababu ya siasa za kupita, ila manufaa ya taaluma si ya kupita.
Magufuli na Wananchi Wake:
Kwa mtazamo wangu kuna wananchi wanakubali Sana kazi na mwenendo wa serikali ya raisi Magufuli. Ila pia kuna wananchi wanachukia sana mwenendo wa serikali hii ya awamu ya tano kwa mitazamo yao mingi tu. La kusikitisha kipindi hiki cha miaka mitano wananchi wamepandikizwa chuki mbaya ambazo Ni kinyume Na utamaduni wetu Kama waTanzania. Chuki hizi zinaonekana mpaka baina ya ndugu Na ndugu huku watu wakiwa wamesahau siasa si chuki. Mfano tu humu ndani ya JF nimesoma nyuzi nyingi humu ndani watu wameshindwa kabisa kubishana kwa hoja majibu yao yanakuwa mfano “nenda kachukue buku saba lumbumba”, huku jukwaa hili la siasa likikosa sifa kabisa kwa kuwa na matusi mengi ambayo nashindwa kuyaandika hapa kwa maadili yangu yalivyo. Nahimiza tu watu wawe CCM, CHADEMA, au chama chochote kile siasa sio ‘Matusi’ “Hoja Hupingwa Kwa Hoja”
Siasa za Upinzani:
Kwa mtazamo wangu tu siasa zimebadilika Sana Kwa wapinzania Kwa sasa zile siasa za kusema tutajenga mashule, hospitali, barabara, tutaleta maji nk Kwa sasa hazisikiki. Nimekuwa najiuliza Sana Kwa nini hazisikiki? Nimegundua kuwa Kwa sasa vitu vingi vimejengwa au kuboreshwa Na serikali hii ya awamu ya Tano. Wapinzani wa raisi Magufuli kwa asilimia kubwa kazi zao zimekuwa ni kuponda tu huku huku hawawi mbele kusema kipi kifanyike. Kwa akili ya kawaida tu huwezi kuwa mmekaa kibarazani aje mwenye nyumba awaulize ‘mmekula nataka kuwaletea chakula’ alafu mmoja wenu ajibu “sie tumeshiba” huku mnakuta wengine wana njaa kali amewasemea bila kuwauliza kama wanahitaji kula. Kwa sasa siasa zimekita kwenye udikteta wa raisi Magufuli na kuponda yale anayofanya huku wakiwa hawasemi nini kifanyike tusonge mbele..
Kwa mtazamo wangu tu Wapinzani kuleta maendeleo si lazima wawe wamechaguliwa: Kwa jinsi nilivyoona wapinzani wakiwa msatri wa mbele kuomba michango ya kuwatoa wenzao gerezani au kuomba hela za hospitali za mheshimiwa Tundu Lisu basi wangeweza kutumia njia hizo hizo kukusanya michango kwa waTanzania ili kuleta maendeleo. Hata Kama hili lingepingwa wapinzani hawa wangeweza kuanzisha utaratibu Kwa viongozi waliowachaguliwa ndani ya upinzani kuleta maendeleo Kwa michango ya wananchi wenyewe ILA zingeonekana Ni juhudi zao ndio zimeleta maendeleo. Wapinzani wanaonekana kuwa wamesahau kabisa kuwa ‘Maendeleo Hayana Chama”
La mwisho ningependa sana kuona siku moja upinzani umeshika madaraka Tanzania ila si kwa upinzani huu naouona sasa. Na ningependa sana kuona CCM inavunjwa Na kuanzishwa chama kipya chenye wanasiasa mahiri wanaoweza kuleta mabadiliko ya kweli Tanzania Kwa wananchi wake. Ningependelea sana kuona siasa zenye tija na maendeleo kwa waTanzania wote bila kujali wametokea vyama gani vya siasa. .
Wewe umechukua ambacho kimekugusa ila nimeelezea mtazamo wangu tu sifanyi siasaHuna hoja dogo zaidi ya kujikomba . Uzi umewafungulia wapinzani kuwananga as if wamemkwamisha mh Rais kutekeleza majukumu yake. Ukiomba kazi ya u Rais , wananchi wote ni wako. Wakupendao na wasiokupenda. Si kulipa visasi kwa wale wasiokukubali.
After all siasa za ki democracy zipo kikatiba na hazitgemei hisani ya mtu, kuvunja au kutokuvunja katiba.
Sent using Jamii Forums mobile app
Samahani Mfiaukweli mataga ni nini?Samahani, ila propaganda zako zimeshindwa hata kabla hazijaanza. Kuna clip mataga mwenzako ameiweka hapa akidai kuwa Watanzania "tumebarikiwa" kwa kupata Rais "mnyenyekevu" wakati kwenye hiyo clip "Rais mnyenyekevu" anawatukana na kuwadhalilisha wasaidizi ALIOWATEUA yeye mwenyewe huku akikiri kuwa UCHUMI UMEDORORA.
Pole sana jomba.
“Siasa sio Matusi au Chuki, Hoja Hupingwa Kwa Hoja”
Hii chuki imepandikwa na siasa CHAFU kwa sasa Tanzania tumekuwa na siasa za watu wachache wanao influence asilimia kubwa ya watu kwa kuwapandikiza CHUKI ikiwa kama mbinu ambayo inakuwa inafatwa kuingia madarakani
Mimi nnaamini kabisa kama huna jambo la kusema juu ya kitu basi ni vyema mtu akakaa kimya ila watu kwa kutaka kuleta matabaka huwa wanapandikiza CHUKI. Kitu ambacho ni kibaya sana tena kwa vizazi vinavyokuja. .
WaTanzania tunatakiwa tubadlike twende na mabadiliko Ya kidunia. Watu wengi ni wavivu mpaka wa kufikiri na wengi wamesoma lakini elimu yao haijawakomboa. Nadhani watu wamekosa ubunifu na kutengeneza fursa za maisha, ili wajifurahishe lazima watafute wa kumlaumu wakati wa kujilaumu ni wao wenyewe. Siku zote ukiona yako hayaendi uatatafuta uyapeleke wapi kulaumu ila lawama hazikusogezi mbele je unachukua maamuzi gani kusonga mbele?
Unaona maisha magumu hapa Tanzania? Kweli hujatembea nchi za watu. Tanzania inabidi tutoe maoni yetu yapelekw bungeni na kwa serikali ili tujue tunatatua changamoto zetu vipi, ila tukianza kuweka lawama hakuna kitakachofanyika kikamfurahisha mwenye lawama. Wale waliotua lawama wanasonga mbele tu. .
Lakini ndivyo mahakama zetu zilivyowahukumu. Na hakuna hukumu nyingine iliyoiua hukumu ya jaji Mihayo !!Nambie kaka
Ila ile kesi ya babu seya nimesikia sikia kuwa ilikuwa ya kutengeneza tu na haikuwa na ukweli ndani yake ndio maana raisi kawatoa. Ila wabakaji na walawiti huwa wanapata msamaha wa raisi?
Nina wasiwasi kama wapinzani walivyokuwa wanasema watajenga mashule, barabara, n.k ulikuwa unawaelewa.Hujasoma nilichokiandika vizuri naomba ukasome tena
Nimeandika Upinzani kwa juhudi za kukusanya michango au kuwaleta wananchi pamoja wangeweza kuleta maendeleo mengi sana. Mfano wangeweza wakakusanya hela halafu wakanunua madawati, serikali ingekataa tu wananchi wangejua Upinzani unafanya kazi nyingi za kuleta maendeleo huku utawala unapinga huoni ingeleta tija kwa upinzani bila kutumia nguvu nyingi kushidana kwa kelele ambazo hazina msingi
Navyozungumza hivi naomba msininukuu vibaya mie napinga CCM kwa kuwa ni mbovu mno, hata viongozi wengi wanaochaguliwa ndani ya CCM na Magufuli wameonyesha udhaifu wa hali ya juu mbali na usomi wao .Ila vile vile napinga upinzani Pia kwa kunionyesha kuwa bado wanashindwa kuleta mabadiliko, hoja zao hata humu ndani ni matusi na kelele tu. .