Mteja azimia NMB Buzuruga, ni baada ya kukaa kwenye foleni masaa manne

Mteja azimia NMB Buzuruga, ni baada ya kukaa kwenye foleni masaa manne

MSAGA SUMU

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2015
Posts
6,661
Reaction score
21,656
Katika hali isiyo ya kawaida mgonjwa mmoja aliyekuwa akitaka kutoa hela kwa ajili ya matibabu alijikuta akizimia baada ya kukaa foleni kwa muda mrefu.

Katika benki ya NMB iliyopo Buzuruga plaza, yenye madirisha matano ya tellers, ni madirisha mawili tu yalikuwa yakifanya kazi, na katika madirisha hayo mawili dirisha moja lilimuhudumia mteja mmoja kwa zaidi ya masaa mawili huku dirisha moja lililobaki lilifungwa kuanzia majira ya saa 7 mpaka mishale ya kuelekea saa 9 na muhudumu huyo alisema ameenda kupata lunch nzito.

Kwa mbali niliwasikia mateller hao wakilalamika udogo wa mishahara ndio chanzo cha kufanya kazi kwa kusua sua.

Natoa ombi kwa mtu yoyote anayetaka kutumia NMB ajaribu matawi mengine, asije kusema hakuambiwa.

NMB Buzuruga ina watu wengi wa usafi na ulinzi kuliko wafanyakazi wa benki mpaka mmtu anijiuliza hivi hapa G4S au NMB?

Ili kupunguza matumizi inabidi NMB wapange jengo dogo kuendana na idadi ya mateller walionao, labda wafikirie kuchukua fremu hata Buzurga stendi- maana serikali nayo inasubiri gawio lake.
 
Hakuna Benk ya Maajabu Kama NMB Yaan bora CRDB, Kwa diaspora ndo huduma hupati hadi urudi mwenyewe bongo ,

wana mambo ya ajabu sana

mashangaa NMB unampa mtu kadi ya Visa na MasterCard alafu unasema afanye application ya kufanya manunuzi online au eti kutoa Pesa internationale napo ufanye application what a shit 💩 , Yaan NMB wajinga sana
 
Heri yake alikuwa amekaa kwenye foleni....angekuwa amesimama angekata roho kabisa....this africa
 
Hakuna Benk ya Maajabu Kama NMB Yaan bora CRDB, Kwa diaspora ndo huduma hupati hadi urudi mwenyewe bongo ,

wana mambo ya ajabu sana

mashangaa NMB unampa mtu kadi ya Visa na MasterCard alafu unasema afanye application ya kufanya manunuzi online au eti kutoa Pesa internationale napo ufanye application what a shit 💩 , Yaan NMB wajinga sana
Maajabu ,nimefanya application ya kufanya manunuzi online hadi leo (wiki ya pili) mastercard haikubali online transaction.
 
Hakuna Benk ya Maajabu Kama NMB Yaan bora CRDB, Kwa diaspora ndo huduma hupati hadi urudi mwenyewe bongo ,

wana mambo ya ajabu sana

mashangaa NMB unampa mtu kadi ya Visa na MasterCard alafu unasema afanye application ya kufanya manunuzi online au eti kutoa Pesa internationale napo ufanye application what a shit 💩 , Yaan NMB wajinga sana
Ukiwa Ulaya fungua account ya Barclays, ukiwa Bongo unapeta tu.
 
Alikuwa anataka kufanya muamala wa zaidi ya milioni sita?
 
Maeneo mengi changamoto ya foleni ipo,ukitembelea mahospitalini ndio utachanganikiwa zaidi; wahitaji wa huduma ni wengi kuliko watoa huduma au vitendea kazi
 
Hakuna Benk ya Maajabu Kama NMB Yaan bora CRDB, Kwa diaspora ndo huduma hupati hadi urudi mwenyewe bongo ,

wana mambo ya ajabu sana

mashangaa NMB unampa mtu kadi ya Visa na MasterCard alafu unasema afanye application ya kufanya manunuzi online au eti kutoa Pesa internationale napo ufanye application what a shit 💩 , Yaan NMB wajinga sana
Wewe ni mshamba we ulitaka upewe card ikiwa tayari imeactivatiwa online banking mimi nikipewa hiyo kazi umaskini bye bye lazima uaccept na uactivate mwenyewe sema wabongo washamba
 
Huwa wanasemaga CRDB wana huduma mbovu ila mimi kuna siku walinihudumia vizuri tawi la UDSM hadi nikashangaa.
Yaani hadi muda wa kazi ukaisha wakafunga mlango na watu wa usafi wakaanza kudeki nikaambiwa tu ndugu mteja hamia huku! walihangaika hadi kuwasiliana na tawi lingine ili mradi tu tatizo langu liishe na likaisha baada ya nusu saa hivi baada ya benki kufungwa.

Muda mwingine ukitaka huduma nzuri na za haraka bank muwe mnafahamiana na staff wa bank, wewe hata foleni zitakuwa hazikuhusu ingawa sasa utakuwa unawaonea wateja wenzako.
 
Back
Top Bottom