Mtemi Ng'wanamalundi (Mwanamalundi) - Yesu wa Afrika?

Mtemi Ng'wanamalundi (Mwanamalundi) - Yesu wa Afrika?

Hivi alifariki mwaka gani? Na nini chanzo cha kifo chake? Je kaburi lake liko wapi? Au naye alichukuliwa na gari la moto linalovutwa na farasi kama nabii Elia Mtishibi?
Alifariki miaka ya 1940's sikumbuki mwaka exactly hata ugonjwa wake sikumbuki kutokana na hicho kitabu, alizikwa kwao ambayo kwa sasa ni eneo la wilaya ya Kwimba-Mwanza, na inasemekena baada ya Mazishi yake kulikuwa na manyunyu na yalivyokatika moshi ukawa unatoka kwenye kaburi lake watu wakajiridhisha kwamba Ng'wanamalundi kaenda mbinguni.

Alishitakiwa kwa kosa la kuua watu pamoja na mifugo na mazao ya watu, kulikuwa na mashindano ya ngoma (mbina) wakati mashindano yanaendelea wakaja wasaidizi wake waliokuwa wanashughulika na kupika na kumwambia hawakuwa na kuni sasa yeye alichofanya ni kunyanyua mkono kuelekea upande kulikokuwa na miti na kuamrisha umagi pye abing'we akiwa na maana vyote vilivyokuwa upande kule alikoelekeza mkono wake vikauke ili wapate kuni, badala ya miti pekee kukauka kila kitu kilichokuwa upande ule kilikauka.
 
Njia ya kuelekea Musoma ukitokea Mwanza kuna kitongoji ambacho jina silikumbuki lakini kutoka barabarani unaweza kuona alama za unyayo wa huyu Bwana kwenye jiwe. Yumkini alikuwa mtu wa ajabu. Kuna vitabu vinaelezea historia yake.

Tiba
Kwenye hiyo njia uliyotaja hamna kitu kama hicho mkuu, labda kuna makumbusho ya Bujora ambapo unaweza kupata historia yake.

Alama za nyayo zake nadhan zinaweza kupatikana wilaya za Kwimba, Maswa, Sengerema labda na Geita au Kahama.
 
Kuna simulizi za watu wengine kama Ng'wanagasasala, Samike, na kuna mwingine nimemsahau jina alikuwa na uwezo wa kuruhusu mwili wake ujae na kufiti chumba, kuna simulizi zingine za visima kuwa na uwezo wa kumeza watu na kuwatoa baada ya siku kadhaa wakiwa hai, simulizi za maajabu ni nyingi sana.
Je na hawa ntapata wapi vitabu vyao?
 
Je na hawa ntapata wapi vitabu vyao?
Mkuu hizi simulizi zingine hata mimi sijawahi kuona document zake, hizi nyingi zinzpitishwa verbally, kama inayohusu visima mimi alinisimulia bibi yangu na yeye ilimtokea bibi yake live.

kuhusu hao watu wengine kama huyo Ng'wanagasasala ukipata watu wazima kidogo hasa wa maeneo ya Kwimba na Magu story zake nyingi wanazijua, Samike huyu sana sana maeneo ya Maswa au Shinyanga.
 
mwengine alikuwa anaitwa Mawombekelo, huyu alikuwa alikuwa na uwezo wa kujaa ndani pindi anapogundua pombe anayokunywa ni tamu, kama ndani kuna watu wengi anajaa peke yake chumba kizima.
 
Ni kweli mkuu ulichokisema hata mimi hicho kitabu nilikisoma miaka ya mwanzo ya tisini na kama ulivyoelekeza akienda Bujora lazima atakipata.

Hata hivyo usukumani kuna simulizi za watu wengi sana zaidi ya Ng'wanaMalundi. Kuna simulizi za watu wengine kama Ng'wanagasasala, Samike, na kuna mwingine nimemsahau jina alikuwa na uwezo wa kuruhusu mwili wake ujae na kufiti chumba, kuna simulizi zingine za visima kuwa na uwezo wa kumeza watu na kuwatoa baada ya siku kadhaa wakiwa hai, simulizi za maajabu ni nyingi sana.

Wewe Masuke ni wa-Ng'wiswe wewe!!

Ni kweli masimulizi ni mengi na yalikuwa ya kutisha na watu wanashuhudia kwamba waliyaona hayo. Aliyekuwa anajaa kwenye chumba kama sijakosea alikuwa anaitwa Ibamba Ngulu. Inasemekana huyu bwana siku moja wajanja walimkomesha wakaweka pombe kwenye nyumba iliyokandikwa kwa udongo (siyo ya tofari), jamaa alivyoingia ndani akataka kuwafukuza watu ili afaidi pombe peke yake hivyo akajaa kweye hicho kijumba watu wakakimbia kumbe tumbo lake likavimba na minyama ikatokeza kwenye hicho kijumba. Maana ule udongo ulimomonyoka hivyo minyama ikawa imechukua nafasi ya ule udongo, kuku walivyoona hivyo wakaanza kumdonoa mpaka wakamtoa utumbo nje.

Lakini inasemekana walikuwa ni kuku wa ki-mazingara. Hivyo ndo ukawa mwisho wa Ibamba Ngulu. Kuhusu visima ni kweli tulikuwa tunasimuliwa hivyo eti kukutoa mpaka wafanye tambiko la kuchinja ng'ombe mweupe usoni ndo urudi. Simulizi ni nyingi kiasi kwamba akipatikana mwananchi wa kuandika vitabu ataleta burudani ya pekee na kuonesha jinsi wazungu walivyotupumbaza!!
 
Alifariki miaka ya 1940's sikumbuki mwaka exactly hata ugonjwa wake sikumbuki kutokana na hicho kitabu, alizikwa kwao ambayo kwa sasa ni eneo la wilaya ya Kwimba-Mwanza, na inasemekena baada ya Mazishi yake kulikuwa na manyunyu na yalivyokatika moshi ukawa unatoka kwenye kaburi lake watu wakajiridhisha kwamba Ng'wanamalundi kaenda mbinguni.

Alishitakiwa kwa kosa la kuua watu pamoja na mifugo na mazao ya watu, kulikuwa na mashindano ya ngoma (mbina) wakati mashindano yanaendelea wakaja wasaidizi wake waliokuwa wanashughulika na kupika na kumwambia hawakuwa na kuni sasa yeye alichofanya ni kunyanyua mkono kuelekea upande kulikokuwa na miti na kuamrisha umagi pye abing'we akiwa na maana vyote vilivyokuwa upande kule alikoelekeza mkono wake vikauke ili wapate kuni, badala ya miti pekee kukauka kila kitu kilichokuwa upande ule kilikauka.

Alifariki mwaka 1932. Mjukuu wake ndiye aliyekuja kuanzisha Jeshi la SunguSungu miaka ya 1980's kama watu wa Usukumani mtakuwa mnakumbuka (Jeshi lililotaka kurudisha nidhamu katika jamii ya Wasukuma).

Ni kweli aliua watu wengi sana siku hiyo ya ngoma. Katika uganga alioupata kwa yule bibi alikuwa amezuiliwa asinyooshe mkono wake vinginevyo upande aliolekezea mkono wake vitu vyote vitakauka. Hivyo siku hiyo aliyokuwa anapambana kwenye ngoma na yule mpinzani wake wa jadi (Mwanamke - Gindu Nkima) aliletewa taarifa na wapishi wakidai hawana kuni, hivyo jamaa akajisahau akanyoosha mkono wake akisema "Batemagi pye abenaba" yaani yakateni yote haya. Hivyo vitu vyote vilivyokuwa upande huo viakakuka (Watu, Mifugo, miti na kila kiumkbe chenye uhai).

Ndipo mtemi akatoa amri ya kwamba akamatwe na kupelekwa kwenye vyombo vya sheria.
 
hili jina la ng'wana malundi ni jina ambalo alipewa mdogo wetu na marehemu baba yetu..
kwa hiyo mkuu umenikumbusha mbali sana...
 
Wewe Masuke ni wa-Ng'wiswe wewe!!

Ni kweli masimulizi ni mengi na yalikuwa ya kutisha na watu wanashuhudia kwamba waliyaona hayo. Aliyekuwa anajaa kwenye chumba kama sijakosea alikuwa anaitwa Ibamba Ngulu. Inasemekana huyu bwana siku moja wajanja walimkomesha wakaweka pombe kwenye nyumba iliyokandikwa kwa udongo (siyo ya tofari), jamaa alivyoingia ndani akataka kuwafukuza watu ili afaidi pombe peke yake hivyo akajaa kweye hicho kijumba watu wakakimbia kumbe tumbo lake likavimba na minyama ikatokeza kwenye hicho kijumba. Maana ule udongo ulimomonyoka hivyo minyama ikawa imechukua nafasi ya ule udongo, kuku walivyoona hivyo wakaanza kumdonoa mpaka wakamtoa utumbo nje.

Lakini inasemekana walikuwa ni kuku wa ki-mazingara. Hivyo ndo ukawa mwisho wa Ibamba Ngulu. Kuhusu visima ni kweli tulikuwa tunasimuliwa hivyo eti kukutoa mpaka wafanye tambiko la kuchinja ng'ombe mweupe usoni ndo urudi. Simulizi ni nyingi kiasi kwamba akipatikana mwananchi wa kuandika vitabu ataleta burudani ya pekee na kuonesha jinsi wazungu walivyotupumbaza!!
Asante mkuu kwa share hizi memory kupitia JF.
 
Alifariki mwaka 1932. Mjukuu wake ndiye aliyekuja kuanzisha Jeshi la SunguSungu miaka ya 1980's kama watu wa Usukumani mtakuwa mnakumbuka (Jeshi lililotaka kurudisha nidhamu katika jamii ya Wasukuma).

Ni kweli aliua watu wengi sana siku hiyo ya ngoma. Katika uganga alioupata kwa yule bibi alikuwa amezuiliwa asinyooshe mkono wake vinginevyo upande aliolekezea mkono wake vitu vyote vitakauka. Hivyo siku hiyo aliyokuwa anapambana kwenye ngoma na yule mpinzani wake wa jadi (Mwanamke - Gindu Nkima) aliletewa taarifa na wapishi wakidai hawana kuni, hivyo jamaa akajisahau akanyoosha mkono wake akisema "Batemagi pye abenaba" yaani yakateni yote haya. Hivyo vitu vyote vilivyokuwa upande huo viakakuka (Watu, Mifugo, miti na kila kiumkbe chenye uhai).

Ndipo mtemi akatoa amri ya kwamba akamatwe na kupelekwa kwenye vyombo vya sheria.

Asante mkuu kwa masahihisho, haya ni majina ambayo kusahaulika sio rahisi.

Sungusungu ilikuwa noma full displine mtu unataja makosa yako mwenyewe, kuna mwaka Sungu sungu walitoka Sengerema kuja kutemya Magu sehemu moja inaitwa Itumbili, ile sehemu kwa uchawi ni balaa wenyeji wenyewe ikishafika jioni wanaogopa kutoka, lile jeshi la Sungusungu walikuwa na kawaida ya kuchinja ng'ombe na kupika nyama kwenye mapipa, iliwachukua zaidi ya masaa mawili bado nyama inatoka damu mbichi ilibidi waahirishe kutemya mpaka wakarudi baadaye.

WanaJF naomba kutoa hoja, tuwatafute Sungusungu wa kipindi hicho waje watemye hawa mafisadi, mtu kama Jairo lazima ataje watu wote waliochukua zile hela.
 
Mkuu kwakweli nimekumbuka mbali sana. Nakumbuka kulikuwa na vitabu vya huyu ndugu yetu Ng'wanamalundi katika shule za msingi miaka ya nyuma na nilibahatika kuvisoma. Historia inakaliwa na watawala wetu. REJEA: Kipindi cha Kambi Popote cha Clauds TV utatamani kulia. Na wengi wetu ni mashahidi wa utajiri wa kihistoria tulionao Watanzania karibia ktk kila mkoa. Kuanzia historia ya Uumbaji na hata ile ya kikoloni. Inauma Saaana!
 
Asante mkuu kwa masahihisho, haya ni majina ambayo kusahaulika sio rahisi.

Sungusungu ilikuwa noma full displine mtu unataja makosa yako mwenyewe, kuna mwaka Sungu sungu walitoka Sengerema kuja kutemya Magu sehemu moja inaitwa Itumbili, ile sehemu kwa uchawi ni balaa wenyeji wenyewe ikishafika jioni wanaogopa kutoka, lile jeshi la Sungusungu walikuwa na kawaida ya kuchinja ng'ombe na kupika nyama kwenye mapipa, iliwachukua zaidi ya masaa mawili bado nyama inatoka damu mbichi ilibidi waahirishe kutemya mpaka wakarudi baadaye.

WanaJF naomba kutoa hoja, tuwatafute Sungusungu wa kipindi hicho waje watemye hawa mafisadi, mtu kama Jairo lazima ataje watu wote waliochukua zile hela.

Mkuu hapo umenikumbusha mbali sana na hayo mambo ya "Kutemya" yaani kusimika jeshi la Sungu Sungu kwenye kijiji.

Nakumbuka Mwaka 1986 ndo nilikuwa nimemaliza shule ya msingi, kijiji kikatukalia kooni kwamba mpaka tujiunge na jeshi la Sungu Sungu! Hivyo nikalazimika kujiunga na hilo jeshi kwa muda wa miezi kama 3 hivi. Hii ilikuwa baada ya shule yetu kuwa imeadhibiwa na Idara ya Elimu (M) eti tutakaa miaka 10 bila kupeleka mtoto sekondari (Ulikuwa unyama na ushenzi enzi hizo). Basi Mkuu nikashiriki katika kusimika jeshi kwenye vijiji zaidi ya 10 (Nyamatembe, Shigalla, Busega, Nyangiri, Masanga, Mkula, Lukungu, Lamadi, Malili, Chabutwa, n.k.). Mkuu viboko vilikuwa vinatembea usiombe! Siyo jambazi, siyo mchawi wote walikuwa wanatubu wenyewe mpaka wachawi walikuwa wanaenda kuonesha misukule yao usipime!

Lakini baadaye nilikuja kujinasua baada ya kufanya mtihani wa shule za Private na kukimbilia huko. Ila kwa kweli lile jeshi kama lingeboreshwa lilikuwa linafanyakazi, mpaka hata polisi wenyewe wala rushwa viboko vilikuwa vinawaka mpaka wanatubu!! Wote wenye mali yenye mashaka mashaka walikuwa wanacharazwa viboko mpaka wanakili waliipataje hiyo mali. Naamini kama lingeruhusiwa hata hawa mafisadi sasa hivi wangetubu wenyewe.

Wanahistoria sijui wako wapi? Maana naamini kama wangefuatilia haya mambo wangekiachia kizazi kijacho mambo mengi sana ya maana na ya kukumbukwa!
 
Mkuu hapo umenikumbusha mbali sana na hayo mambo ya "Kutemya" yaani kusimika jeshi la Sungu Sungu kwenye kijiji.

Nakumbuka Mwaka 1986 ndo nilikuwa nimemaliza shule ya msingi, kijiji kikatukalia kooni kwamba mpaka tujiunge na jeshi la Sungu Sungu! Hivyo nikalazimika kujiunga na hilo jeshi kwa muda wa miezi kama 3 hivi. Hii ilikuwa baada ya shule yetu kuwa imeadhibiwa na Idara ya Elimu (M) eti tutakaa miaka 10 bila kupeleka mtoto sekondari (Ulikuwa unyama na ushenzi enzi hizo). Basi Mkuu nikashiriki katika kusimika jeshi kwenye vijiji zaidi ya 10 (Nyamatembe, Shigalla, Busega, Nyangiri, Masanga, Mkula, Lukungu, Lamadi, Malili, Chabutwa, n.k.). Mkuu viboko vilikuwa vinatembea usiombe! Siyo jambazi, siyo mchawi wote walikuwa wanatubu wenyewe mpaka wachawi walikuwa wanaenda kuonesha misukule yao usipime!

Lakini baadaye nilikuja kujinasua baada ya kufanya mtihani wa shule za Private na kukimbilia huko. Ila kwa kweli lile jeshi kama lingeboreshwa lilikuwa linafanyakazi, mpaka hata polisi wenyewe wala rushwa viboko vilikuwa vinawaka mpaka wanatubu!! Wote wenye mali yenye mashaka mashaka walikuwa wanacharazwa viboko mpaka wanakili waliipataje hiyo mali. Naamini kama lingeruhusiwa hata hawa mafisadi sasa hivi wangetubu wenyewe.

Wanahistoria sijui wako wapi? Maana naamini kama wangefuatilia haya mambo wangekiachia kizazi kijacho mambo mengi sana ya maana na ya kukumbukwa!

Mkuu itabidi nikuPM inaonekana wa kwetu maana vijiji vyote ulivyovitaja navifahamu isipokuwa Masanga ndo sijawahi kukisikia.
 
Naona angekuwepo ombi la kwanza ni kuita mvua mtera ifule maji tuondokane na sound za wanamagamba
 
Mashujaa wapo kila kabila, ila ukoloni ulio athiri akili zetu unatufanya tuwape kisogo na kujivunia kina carl peters
 
Mkuu itabidi nikuPM inaonekana wa kwetu maana vijiji vyote ulivyovitaja navifahamu isipokuwa Masanga ndo sijawahi kukisikia.
Hata mimi nimemkumbuka jinsi walivyokuja kututemya pale Mkula miaka ile.
 
WanaJF, kuna watu maarufu waliowahi kuvuma katika historia za bara letu, na mmojwapo ni huyu MWANAMALUNDI kutoka kabila la wasukuma. Niliwahi kusoma kitabu kilichokuwa kinaelezea historia yake kwa ufupi na maajabu aliyowahi kufanya wakati wa uhai. Moja ya maajabu ni pamoja na kuponya wagonjwa, kupita katikati ya ziwa huku maji yakiacha njia, kuacha nyao zake kwenye mawe, kukausha miti kwa ajili ya kuni nk.

Nimekuwa nikijiuliza sana, maajabu/uwezo aliokuwa nao huyu MWANAMALUNDI si ndiyo ule ule aliokuwa nao Bwana YESU kristo? Basi kama ni kweli, MWANAMALUNDI ndiye haswa YESU WA AFRIKA. Kutokana na kuwa nyuma kimaendeleo, wazee wetu hawakuweza kujiandikia mambo mengi kuhusu huyu bwana na pengine leo hii tungekuwa hatumuabudu YESU bali angekuwa ni huyu yesu wetu MWANAMALUNDI.

WanaJF, mwenye kitabu au historia zaidi au maoni zaidi kuhusu MWANALUNDI na maisha yake, amwage hapa ili tuweze kuelimishana.
 
Sitaki kunfananisha mtu mwenye nguvu za kiganga na Bwana Yesu. Ng'wana malundi unaijua vizuri historia yake? Je unajua alipewa nguvu zake na mwanamke? Hebu nenda usukumani kwanza kamjue Ng'wanamalundi kisha uje hapa ukiwa kamili
 
Back
Top Bottom