Mtemi Ng'wanamalundi (Mwanamalundi) - Yesu wa Afrika?

Mtemi Ng'wanamalundi (Mwanamalundi) - Yesu wa Afrika?

hakuna kitu kitu kibaya kama kujidharau sasa hawajamaa walichofanya ni kuwafanya waafrika wajidharau na kujiona hawaposahihi kwenye yale wanayoyafanya katika maisha yao..
RIP watemi wote wa kiafrika
 
WanaJF, kuna watu maarufu waliowahi kuvuma katika historia za bara letu, na mmojwapo ni huyu MWANAMALUNDI kutoka kabila la wasukuma. Niliwahi kusoma kitabu kilichokuwa kinaelezea historia yake kwa ufupi na maajabu aliyowahi kufanya wakati wa uhai. Moja ya maajabu ni pamoja na kupona wagonjwa, kupita katikati ya ziwa huku maji yakiacha njia, kuacha nyao zake kwenye mawe, kukausha miti kwa ajili ya kuni nk.

Nimekuwa nikijiuliza sana, maajabu/uwezo aliokuwa nao huyu MWANAMALUNDI si ndiyo ule ule aliokuwa nao Bwana YESU kristo? Basi kama ni kweli, MWANAMALUNDI ndiye haswa YESU WA AFRIKA. Kutokana na kuwa nyuma kimaendeleo, wazee wetu hawakuweza kujiandikia mambo mengi kuhusu huyu bwana na pengine leo hii tungekuwa hatumuabudu YESU bali angekuwa ni huyu yesu wetu MWANAMALUNDI.

WanaJF, mwenye kitabu au historia zaidi au maoni zaidi kuhusu MWANALUNDI na maisha yake, amwage hapa ili tuweze kuelimishana.

Kwa nini umfananishe NG'WANAMALUNDI na yesu, mwache yesu abaki kuwa yesu na ng'wanamalundi abaki kuwa yeye. usijaribu kuwalinganisha
 
Kwa nini umfananishe NG'WANAMALUNDI na yesu, mwache yesu abaki kuwa yesu na ng'wanamalundi abaki kuwa yeye. usijaribu kuwalinganisha
Mkuu Baba V, fuatilia comments za wadau utapata kitu si bure. Pengine unaweza ukawa na jibu zuriiii.
 
hakuna kitu kitu kibaya kama kujidharau sasa hawajamaa walichofanya ni kuwafanya waafrika wajidharau na kujiona hawaposahihi kwenye yale wanayoyafanya katika maisha yao..
RIP watemi wote wa kiafrika
Hilo ndilo neno haswaaa, ukienda Asia na maeneo mengine ya karibu karibu kama Australia, wanaimani zao pamoja na baadhi ya watu kukubali masimulizi ya wazee wa kiyahudi lakini bado kundi kubwa linaamini katika tamaduni zao, dini, mila na desturi zao. Na hata utakuta kuna maeneo mengi ya yenye kumbukumbu nyingi za tamaduni zao, hawazitupi wala kuchoma moto, watu wanazisoma na kuhitimu. Kuna mambo mengi sana ambayo sisi bado tunayaona ni mambo ya ajabu kumbe ni lulu, ni neema kwa vizazi vijavyo. Siku hizi watoto badala ya kukaa chini na mabibi au mababu wapate hadithi za kale na simulizi kuhusu tamaduni za koo zao au kabila zao, wanakalishwa kwenye TV na kuangalia Cartoons au mieleka (a 5 years old kid watching cartoon or restling). Ni mambo mengi, ila kwa kuanza tu ni hii ya historia ya MWANAMALUNDI.
 
VITA VYA USUKUMANI.
[FONT=Times New Roman,Times New Roman][FONT=Times New Roman,Times New Roman]Baada ya siku chache Kapela aliporudi nyumbani kwake, kutoka Ikonongo, Mirambo alituma habari kwa mjomba wake Kapela kuwa ajiandae maana anakuja kumsaidia kuwpigana na maadui wake.Kapela alikubali kupewa msaada huo. Mirambo alikuja na jeshi lake hadi Ukune katika Ikulu. Akapiga kambi yake katika mlima wa Mangua. Kapela akamwambia Mirambo kuwa safari yao ni kuelekea Usukumani kupita Ukamba, Luhombo na Tinde.
Walipofika katika mpaka wa Tinde na Usanda, Mirambo alisema kuwa yeye atapitia njia ya Shinyanga na Kapela apitie Nindo na kukutania Usumau. Mirambo alikuwa na fununu kuwa sehemu za Usia kuna ngombe wengi wa Wasukuma.Hivyo alikusudia kuteka nyara ng'ombe hao. Kapela alimwambia Mirambo kuwa ukifika Usanda asipige eneo hilo kwa kuwa huko kuna wajomba zake .Safari ya Mirambo haikuwa na mafanikio yoyote kwa kuwa Wasukuma walikuwa wamepata habari kuwa Mirambo atapita kuchukua ngombe wao. Wasukuma waliwaficha ng'ombe wao porini, Mirambo akaambulia wanawake tu. Akaendelea mpaka Seka huko alikuta kundi kubwa la ngombe ambao walikuwa ni wa Mwanamalundi, mtu maarufu sana kwa uchawi. Mirambo akashindwa kuwachukua na askari wake wengi wakafa kwa madawa ya mchawi huyo na kwa sababu ya njaa. Mirambo alienda moja kwa moja mpaka Usumau ambako waliahidiana kukutana na Kapela sehemu iitwayo Bungulwa . Kapela alifanikiwa kuteka ngombe wengi akiwemo ngombe dume wa mizimu wa Msukuma wa Nela .Ngombe huyo alikuwa anaitwa Ilindilo, yaani ngombe wa kulinda nchi. Mirambo akamwambia Kapela kuwa nimemkuta Msukuma moja huko ni mchawi kamaliza askari wangu Akamsimulia habari zote za Mwanamalundi. Mirambo aliona wivu kuwa yule ngombe dume na kuapa kuwa lazima amchukue. Kapela na Mirambo walikaa muda mrefu Usukumani Nela, Usumau na Uhungukila. Na walifaulu kuteka mali nyingi ng'ombe wengi pamoja na watu pia.
[/FONT]
[/FONT]
 
Kwa nini umfananishe NG'WANAMALUNDI na yesu, mwache yesu abaki kuwa yesu na ng'wanamalundi abaki kuwa yeye. usijaribu kuwalinganisha

Swali dogo tu kulingana na ufahamu na uelewa wako; Yesu ni nani? na Ngw'anamalundi ni nani?
 
Kwenye hiyo njia uliyotaja hamna kitu kama hicho mkuu, labda kuna makumbusho ya Bujora ambapo unaweza kupata historia yake.

Alama za nyayo zake nadhan zinaweza kupatikana wilaya za Kwimba, Maswa, Sengerema labda na Geita au Kahama.

Sihitaji kuendeleza ligi hapa, nilionyeshwa hizo nyayo kwenye jiwe na mwenyeji wa eneo hilo na mimi nilizishuhudia!!!! Sasa ubishi wa nini?

Tiba
 
Missionaries brought the Bible.They ordered us to close our eyes for prayers. When we opened our eyes, they had grabbed all our fertile land, taken our minerals and in return left us with the Bible. Nenda Ulaya, brothers, you will be surprised there are some families that has never had the name JESUS!!!
 
Missionaries brought the Bible.They ordered us to close our eyes for prayers. When we opened our eyes, they had grabbed all our fertile land, taken our minerals and in return left us with the Bible. Nenda Ulaya, brothers, you will be surprised there are some families that has never had the name JESUS!!!

Na zile families za ulaya ambao hadi leo wanaendelea kumwamini na kumhubiri Yesu?
 
MWANAMALUNDI hakua na uwezo kama KRISTO kwa sababu kuna mambo ambayo aliyafanya ambayo hayampendez Mwenyezi MUNGU. Kama kukausha watu na kuwachoma kama kuni wakati wa mashindano ya ngoma za asili
 
mwana malonde hakuacha nyayo aliye acha nyayo aliitwa ibhambangulu, hizonyayo ndizo anazo tudanganya nazo babu wa loliondo alikuwa akitembea kila mahari, pia kulikuwa na luhanga mawe, na kiboko ya wachawi kasasala nikipata mda nitasimlia habari zake.

Ibambangulu alikuwa akitembelea wafalme ote na kushauliana nao,alitembea na mbwa na mkuki, akienda kwa mfalme alifikia mlimani, alipokanyaga yeye,mbwa wake na alipokita mkukiwake nyayo na alama ya mkuki vilibaki, alichonga bao kwenyejiwe kwa kutumia mikono.ndiyo mabao yote ya kwenye mawe na nyayo zote unazo zisikia popote tanzania. wasukuma tukojuu sana tupeni nchi tuwaongoze.
 
Ibambangulu alikuwa akitembelea wafalme ote na kushauliana nao,alitembea na mbwa na mkuki, akienda kwa mfalme alifikia mlimani, alipokanyaga yeye,mbwa wake na alipokita mkukiwake nyayo na alama ya mkuki vilibaki, alichonga bao kwenyejiwe kwa kutumia mikono.ndiyo mabao yote ya kwenye mawe na nyayo zote unazo zisikia popote tanzania. wasukuma tukojuu sana tupeni nchi tuwaongoze.
 
Anaitwa KESHOSHA MALUNDE, waulizeni masai yero wanamjua sana
 
ilitabiliwa kuwa siku za mwisho kutatokea wapinga kristo wengi sana,na haya twayaona sasa
 
Mkuu Baba V, fuatilia comments za wadau utapata kitu si bure. Pengine unaweza ukawa na jibu zuriiii.

Hapa tunaendeleza "inferiority complex" kwanini YESU ndo asiitwe Mwanamalundi wa Mashariki ya kati!!
 
hiyo historia ya Mirambo na kapela nimeipenda, itaendelea!!? Pale mwanza kuna eneo la nela (kituo cha daladala) kuna uhusiano wowote? maana niliwahi sikia nela ni jina la mtemi
Sp
 
Back
Top Bottom