Mtifuano mkali kati ya Wizara ya Afya na vyuo vya afya juu ya kubadili qualifications za kujiunga pharmacy ngazi ya cheti

Mtifuano mkali kati ya Wizara ya Afya na vyuo vya afya juu ya kubadili qualifications za kujiunga pharmacy ngazi ya cheti

Mshikeshike, mtifuano unaendelea kuhusu kubadili sifa za kujiunga na astashahada kutoka D mbili za Chemistry na Biology kwenda C mbili au zaidi za Chemistry na Biology!

Kiukweli, sifa zinazopendekezwa na serikali zitaathiri vyuo vya afya vinavyotoa hii kozi! C mbili za Chemistry na Biology ni kubwa mno kwa wanafunzi wetu, hivyo wizara haitendi haki kwa wanafunzi wetu waishio Tanzania.

Na mpaka sasa wizara haijatoa tamko lolote maana kikao kilikuwa na mtimtimti kikahairishwa kama si kuvunjika kabisa!

Serikali ya CCM, chama langu, muwasikilize Watanzania!
Unaendaje hospitali kuhudumiwa na mtu mwenye D mbili kwa mfano?
 
Unaendaje hospitali kuhudumiwa na mtu mwenye D mbili kwa mfano?
Unaendeshwaje kwasi na darasa la saba na hupati ajali?

Okay kuna maxingira penginepo yalikuwa sababu kwa watu hawa kupata D mbili!
Je hao waliopo mahospitali hao maCO watawapelrka wapi na wengi wao wana D mbili kwa madomo ya Bios na Kemia!
 
Kiukweli kwa kozi za Afya kupewa D2 kunashusha thamani na ubora wa wanafunzi. Angalau warudishe kama zamani hizo C2 ambazo ni lazima.
Tatizo la elimu yetu haliko kwenye grades. Kuna wahitimu wengi sana ambao wana hata grade A lakini knowledge yao haiendani na grade wanazopata. Hii ni kwa sababu wanafunzi na wanavyuo wanasoma kwa kukariri. Njia sahihi ilikuwa ni kufumua kwanza mfumo wa elimu na kuja na utaratibu unaojali zaidi kuelewa na siyo kupata grade nzuri. Hpa san sana wanazidisha zaidi tatizo kwani wanafunzi badala ya kusoma ili waelewe watakuwa wanatafuta njia za kuongeza grades wanazopata bila kujali knowledge. Pia wanaweza ku-introduce entrance examination ambazo zitapima zaidi maarifa na siyo ukariri.
 
D2 kwa somo la fani maalum ni dharau kwa fani husika.

Haya mambo tuwaachie wanajeshi na polisi wao matokeo ya vyeti hayana maana ktk kozi zao,ni afya timamu na akili timanu.
unakuwaje na akili timamu katika D mbili??? Ndo maana Polisi wanafanya mambo ya hovyo hovyo maana huwezi kuwa na utimamu wa akili ktk D mbili.
Mwanangu wewe una madini mimi naona wangeweka C Kabisa maana ni kudharau fani alaf pharmacy ni kozi nyeti ya Afya
 
Back
Top Bottom