Uchaguzi 2020 Mtihani mkubwa ulio mbele ya CHADEMA ni kupata fedha za kampeni za Urais. Chama hakina fedha na Mgombea hana fedha

Uchaguzi wa mwaka huu utawashangaza watanzania, afrika mashariki, afrika na dunia nzima. Tuombe uhai na afya njema.
Mtaona, kile kisichowezeka kitawezekana
 
Chadema hawajalalamika kuwa hawana hela ya kampeni,
chadema hawajatamani hela ya Nyarandu hadi wampitishe kugombea urais kisa ana hela, usenge huo ulikomea kwa EL

CDM imepandisha bendera na itasonga mbele Wadau tupo CDM inakwenda kutwaa nchi kwa kura zetu wala sio kwa pesa za wanyonyaji.


Fikisha habari hizi kwa jiwe fara wewe
 
Kuhusu pesa ccm ondoeni shaka, viongozi wetu wakifungua A/C bank asbh kuomba fedha ikifika jioni itakuwa tayari fedha zimetimia.
Wafanye hesabu, waliopiga kura2015 watu 6.8m×1000tshs. itatosha
Ongeza wenye chuki na ccm, wafanyakazi, wafanyabiashara, wanafunzi. NGOMA INOGILE
 
Kwani Magufuli ana pesa kiasi gani kwa ajili ya kampeni.....!!? Au kwa kuwa ameshikilia mfuko wa hazina ya serikali .... Na atakuwa anatanua na magari ya serikali!!
 
Ila we jamaa Lissu anakutoa kamasi sana khaa!
 
Elewa Tundu Lissu amezunguka nchi nyingi za ulaya. Huko alikuwa akienda kupiga kopo la msaada kwa ahadi ya kuwalipa akipata U-JPM. La kujiuliza ni kwamba atawalipa nini baada ya kupata urais?
 
Wasindikizaji
 

Sidhani kama watatumia ule ujuzi wa wakuwachangisha wanachama wao, watautumia, na wakifanya hivyo basi wanaweza pata mchango mzuri na kuendesha campaigne yao bila tatizo. Shida inakuja hapo ni wakati wa ukusanyaji na Utumiaji. Pesa zikielekezwa kwengine na campaign ika kwama au ikawa isoyo na nguvu, watu watavunjika nguvu na hata wasipige kura.
 
Wananchi nao hawana pesa ili wajikomboe?
 
Sasa kqma zimepigwa kimehemko wewe hufurahi kuona mgombea wako atashinda kiurahisi??, Mlimtaka Nyalandu ili mpate pakusemea??.

Ukweli hata 2015 km mgombea angekuwa tofauti na Eddo ukawa hawakuwa na sababu za kupiga kampeni, 2020 Lissu haihitaji kampeni kuubwaaaa maana anakubalika kwa waTz wote.
 
Tumemchangia Kamanda TL matibabu huko Ubelgiji baada ya serikali ya CCM kumnyima stahiki yake. Pia wanachama tumemchangia gharama zote za kujikimu kwa muda wote huu. Hii psa ya kampeni ni kitu kidogo sana, wala ksikuhangaishe wewe Yehodaya na CCM yenu! Mtahangaika saaana, lakini ngoma ndo inaanza!
 
Miaka yote hiki chama kinachangiwa na matajiri wa kichaga. Kwaiyo wachaga watachanga hata mwaka huu
 
Kwa hiyo watu wateuliwe kulingana na uwezo/utajiri wao wa fedha badala ya uwezo wao kuongoza na kukubalika myoyoni mwa wanachama na wananchi?
 
Siku tatu milioni zaidi ya mia3

Wewe kitulize tuu. kunywa mtori nyama ziko chini
 

Subiri kidogo utajuwa kama wana pesa,
Mabeberu wapo nyuma ya mgombea wao kwa hiyo pesa itapatikana tu.
 
Ingia jikoni kasonge ugali wanaume wakimaliza kikao waje wale, mtoto wa kike haya mambo hayakuhusu acha umbea! Kwanza kuchanga ni siku moja tu tunapitiliza hadi lengo.
 
Dhana ya uwakilishi ina lipi jipya?
Hujui kwamba asili ni kuchagua miongoni mwetu pasina kuangalia kipato au familia atokayo bali ni uwezo wa kuyaeleza Matatizo yetu, kujenga hoja na kuelekeza Serikali inapokosea na zaidi ni kushiriki katika kutengeneza sera kwaajili ya maendeleo yetu
 
Mtanyooka safari hii, naona mnahangaika kama mnataka kutaga YEHODAYA
Hakuna mtu anaehangaika na haya maigizo yenu. kama ulikua hujui, hili ndo suala ambalo toka mwanzo Mwenyekiti wenu lilikua likimuumiza kichwa kuchagua kati ya fedha na umaarufu wa mtu (ushawishi). Nyalandu ana fedha lakini hana umaarufu kumzidi Lissu. Ukifuatilia hotuba ya jana ya Lissu aligusia hili, kwamba chama lazima kichague mtu mwenye ushawishi ili kuweza kushinda uchaguzi. Kauli hii haikua ya bahati mbaya, alijua alichokua anakimaanisha. Lakini Uchaguzi kama alivyoeleza mleta mada una mambo mengi ambayo lazima utumie fedha kuliko umaarufu.

Mwaka 2015 bila kuangalia athari walizopata baadae, lakini naweza kusema CHADEMA ililamba dume, kwasababu mtu waliemchagua alikua ana sifa zote mbili yaani fedha na umaarufu (ushawishi) tena kuzidi alionao Lissu. Ndo maana walipata mafanikio kuliko wakati wowote ule ambao waliwahi kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Vyama vingi. Changamoto waliyonayo CHADEMA kwasasa, ni kwamba umaarufu wa Lissu unachagizwa sana na tukio baya lililompata tofauti na Lowassa ambapo umaarufu wake ulitokana na yeye mwenyewe (charismatic). Umaarufu unaotokana na charisma ya mtu ni jambo kubwa sana kisiasa, kwasababu popote anapotekea mtu wa namna hiyo anavutia watu lakini umaarufu unaotokana na matukio unategemea na jinsi watu walivyoguswa na tukio lenyewe. Siyo watu wote wanaweza kuwa na hisia zinazofanana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…