Hee Mkuu, sistahli hayo kwa maoni kidogo kama haya. Napaswa kuwajibika zaidi kupata mtazamo wako kama huu ulio very positive. Hata hivyo asante sana.Baraka zake Mungu baba mwenyezi, Baba, Mwana na Roho mtakatifu, zikae nawe mleta mada daima na milele. Amina.
Tunahitaji hili lifikishwe Bungeni, maana linazidi kupamba moto sasa imekuwa vurugu. Nasikia majina ya mitaa watu hata walitoa fedha ili mitaa iitwe kwa majina yao. Yaani kuna ufisadi mkubwa umefanyka kwenye kutoa majina ya mitaa kwenye huu mradi wa anuani za makazi. Ujinga mwingine huu wa watu kupenda kutukuzwaNili shangaa hilo Daraja kuli ita Mfugale (mita 300 tu) na vibao vyake vipo. Wakati hilo ni Daraja la kawaida tu wala siyo Fly over wala siyo Express Road.
Tembelea majirani zetu Kenya. Hivyo ni vitu vya kawaida. Fly over zao zina run 2KM to 10Km.
Pia @TANROADS tuna omba muendeleze utamaduni wa kuandika majina ya Vijiji au Mitaa barabarani. Ina pendeza kwa utalii. Siyo kusumbua kuuliza uliza watu kwenye gari.
Shule zote, madaraja, Majengo, nk majina yake yawe ya eneo husika kutunza Historia ya maeneo. Siyo eti LUKUVI, TULIA, akati mchango wao ktk nchi una zidiwa na Mwl wa Primary aliye staafu kwa Heshima.
USA kuna uwanja wa ndege unaitwa JFK, jina la rais wao aliyeuwawa mwaka 1963.Nachukia sana hili suala la kuiita miundombinu kwa majina ya watu binafsi, kama maraisi au watu wengine wanasiasa na wengineo. Kinachoniudhi zaidi ni kwamba mapendekezo ya majina haya mara nyingi hufanywa na watu ambao wana ajenda ya kujipendeke kwa raisi au wengineo.
Sikatai kwamba hawa watu, kwa mfano maraisi, wanakuwa wamesimamia vizuri mambo fulani. Lakini tujiulize, hivi kuna raisi au kiongozi yeyote ambae anasimamia hayo mambo kwa utashi wake, au anayafanya kama wajibu wake kwa kutumia kodi na tozo zinazolipwa na wananchi?
Tuchukue kwa mfano Mfugale Flyover, ambayo ilipewa jina la Mfugale kwa sababu wakati huo alikuwa ndio Mkurugenzi wa TANROADS. Sawa alifanya kazi nzuri, labda ni kweli, maana ndivyo alivyosema Magufuli, lakini nani alikuambia hakuna Mkurugenzi wa TANROADS atakae kuja kufanya kazi nzuri zaidi ya Mfugale? Kwa nini tuiite hii flyover jina la Mfugale kama vile yeye ndio amevunja rekodi ya Tanzania ya wakurugenzi bora wa TANROADS na hakuna atakaetokea kuwa bora zaidi yake?
Hivyo hivyo kwa maraisi. Mwinyi kile sijui, Mkapa hiki sijui, Kikwete hapa, Magufuli pale sijui, na sasa watu wanaanza kupendekeza Samia nini sijui. Kwa nini? Kwani hawa watu wanafanya hizi kazi kwa utashi wao au wajibu wao? Wanatumia fedha zao toka mfukoni au fedha zetu za kodi na tozo? Kwa nini tuwatukuze kwa kutimiza wajibu wao kwa kutumia kodi na tozo zetu?
Hili jambo liwekwe wazi, kwamba majina ya miundombinu ambayo tutayaacha ni ya Nyerere na Karume tu, waasisi wa Tanzania. Na ndio maana tulikubaliana kuwa hakuna picha ya raisi mwingine itawekwa kwenye fedha. Na iwe hivyo kwa miundombinu pia. Tuache hii tabia ya kujipendekeza kwa viongozi.
Tunaondoa majina yenye umaana mkubwa kihistoria kwa sababu tunataka kujipendekeza kwa raisi aliyeko madarakani. Kwa mfano daraja la Wami. Nani anajua historia ya jina Wami hadi tuamue halitufai na labda tuliite daraja la Samia?
Nakusihi Samia usikubali huu ujinga wa kutukuzwa, kama kweli kazi unayofanya kama raisi unaiona kama wajibu wako wa kikatiba na sio favor unayotufanyia Watanzania. Kama Samia unataka tuite kitu kwa jina lako, labda basi jitolee fedha zako kukijenga ili tukuenzi, lakini sio utimize wajibu wako kama raisi, utumie kodi na tozo tunazolipa kwa maumivu makubwa, halafu mwishowe tukiite kitu fulani ulichosimamia kwa jina lako.
Na pia ninapendekeza kwamba majina ya miundo mbinu iliyopewa viongozi zaidi ya Nyerere na Karume yabadilishwe mara moja!
Tuondokane na huku kujipendekeza kwa kuwatukuza watu, wanadamu kama sisi. Kwanza inawakatisha tamaa watu ambao wanachapa kazi zaidi hata ya raisi, the unsung heroes, wao watatukuzwaje?
Na pia Samia, kwa taarifa yako tu, kwenye mradi wa anuani za makazi watu wametoa fedha ili mitaa iitwe kwa majina yao, ujinga mwingine huu.
Wanapopenda kutukuzwa wewe binafsi unapungukiwa na nini?. Maisha haya ni mafupi sana na hakuna ajuaye ataondoka lini juu ya uso wa dunia.Tunahitaji hili lifikishwe Bungeni, maana linazidi kupamba moto sasa imekuwa vurugu. Nasikia majina ya mitaa watu hata walitoa fedha ili mitaa iitwe kwa majina yao. Yaani kuna ufisadi mkubwa umefanyka kwenye kutoa majina ya mitaa kwenye huu mradi wa anuani za makazi. Ujinga mwingine huu wa watu kupenda kutukuzwa
Mkuu acha kunisikitisha. Tunafanya hivi kwa kuwa USA, Senegal na kwingineko wanafanya hivi, ndio sababu? Kwa nini tunakataa ushoga basi, ambao USA, Canada, nk nk wanafanya?USA kuna uwanja wa ndege unaitwa JFK, jina la rais wao aliyeuwawa mwaka 1963.
Senegal wana uwanja mkubwa wa mpira unaitwa Leopold Senghor ni wa miaka na miaka.
Huwezi kukwepa kuipa mitaa au barabara majina ya watu maarufu, jitahidi ulitazame suala hili kwa mtazamo chanya utaelewa kwa kina kwanini majina yanatumika katika kutambulisha vitu vyenye umuhimu.
Angeendelea kuwepo hata jina la nchi lingebadilishwa na kitwa Jamuhuri ya Magufuli, mwanzili wa hiyo kampeni angekuwa Job Ndugai pale mjengoni na meza zingegongwa kwa kusindikizwa na nderemo, vifijo na vigeregere.Magufuli alikaa madarakani kwa miaka 5 tu ila ana karibia vitu 10 tayari vina majina yake
Kuna daraja linaitwa Magufuli huko Morogoro, Stendi ya Magufuli, kuna mji wa Serikali unaitwa Magufuli City, kuns kivuko cha Busisi nacho wanakiita Magufuli
Vitu vinafanywa na watu na ndio wamiliki wa hayo majina. Usilitazame hili suala kwa mtazamo wa kisiasa wa ndani ya TZ, litazame kidunia. Ushoga na suala la majina ni vitu viwili tofauti kabisa.Mkuu acha kunisikitisha. Tunafanya hivi kwa kuwa USA, Senegal na kwingineko wanafanya hivi, ndio sababu? Kwa nini tunakataa ushoga basi, ambao USA, Canada, nk nk wanafanya?
Yaani kama nchi hatuwezi kuwa na msimamo wetu ili kina USA na Senegal watuige?
Ila nimedokeza, majina ya kikoloni tuyaache. Ila tusiendeleze hii tabia.
Kwanini iitwe Mkwawa kwani Dar haikuwa na machifu wake wa kiazararamo na Kikwere????!!! Mara mia ingeitwa Kikwete flyover kidoooooogo ingeleta maana, au unaonajeHata ile fly over ya John Kijazi ibadilishwe, iitwe Mkwawa flyover kutambua mchango wake wa kupambana na Wakoloni
Mkuu, watu wenye maswali kama haya ni mzigo katika jamii. Kama yeye amebaka mtoto wewe unapungukiwa ninii? Siku moja utaniambia kama mke wangu amebakwa wewe unapungukiwa nini?Wanapopenda kutukuzwa wewe binafsi unapungukiwa na nini?. Maisha haya ni mafupi sana na hakuna ajuaye ataondoka lini juu ya uso wa dunia.
Hee, vipi tukimuita mke wako Mrs wa jina la mwanaume wa kwanza alietembea nae, si lojiki hiyohiyo?Injinia aliyejenga flyover ya kwanza nchini, kuna ubaya gani akaendelea kuheshimika kwa aliyoyafanya kupitia jina lake?. Punguza hizi siasa nyingi jikite kwenye uzalendo.
Niliweka uzi humu kupinga jambo lileHiyo ya Mfugale mi ndo iliniacha hoi
Mfugale anastahiki,kasanifu na kusimamia madaraja zaidi ya buku nchini..nyerere aliyepewa uhuru na wazungu vitu kila Kona anapewa yeye,akina mkwawa,milambo,kinjekitile,isike,abushiri,kheri,Sykes nk hawapewi chochoteHiyo ya Mfugale mi ndo iliniacha hoi