Mtoto wa miezi 7 kamili ameharisha mara 13, dawa akipewa anaicheua

Mtoto wa miezi 7 kamili ameharisha mara 13, dawa akipewa anaicheua

malembeka18

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2018
Posts
3,266
Reaction score
3,698
Habar wakuu msaada wenu wa mawazo binti yangu ana miezi saba kamili sasa.

Awali ya yote tangu ijumaa kaanza kuugua malaria akapewa doze ya mseto, sasa tangu alfajiri ya leo kaanza kuharisha na na tumbo kulisikia kama linatoa sauti. Kaharisha mara 13 tangu alfajiri.

Asubuh tukachukua jukumu la kumpeleka zahanati alipotibiwa akaangaliwa dokta akashauri amalizie dozi ya malaria
Sasa kufika saa kumi jion bado akawa anaharisha tukamrudisha zahanati tena kwa dokta,

Akapimwa malaria, ikaonekana malaria imeshuka toka 9 hadi 5 ila mtoto akawa na joto sana ikabidi achomwe sindano yakushusha joto. Dokta akashauri apewe dawa ya kukata kuharisha pia akashauri aanzishiwe sindano kwa ajili ya malaria.

Pia dokta akakagua choo cha mtoto akasema mtoto anaharisha maziwa ya mama ni machafu ikabid mama mtoto akamue maziwa yatoke machafu kwa ushauri wa dokta walau mtoto apate maziwa fresh zoezi lilifanyika tukarud nyumba

Sasa mtoto akapewa dawa ya kukata kuharisha mida hii ya saa kumi na mbili lakini mtoto baada ya dakika 15 mtoto akaicheua dawa yote pamoja na chakula chote alichokula pia baada ya kama nusu saa akaharisha tena.

Msaada wenu wakuu hii, Hali ya kuharisha na pia mtoto kushindwa kuinywa dawa anaicheua nifanyaje?

Maana hii kuhara mtoto mara zaidi ya kumi naona anapoteza maji mwilini, nahisi hatari nisije nikamkosa mtoto wangu nahitaji ushauri wenu wakuu
 
Habar wakuu msaada wenu wamawazo binit yangu wa miezi Saba kamili Sasa.awali ya yote tangu ijumaa kaanza kuugua malaria akapewa doze ya mseto Sasa tangu alfajiri ya leo kaanza kuharisha na natumbo kulisikia kama linatoa sauti...kaarisha mara13 tangu alfajiri ... asubuh tukachukua jukumu la kumpeleka zahanati alipotibiwa akaangaliwa dokta akashauri amalizie dozi ya malaria...Sasa kufika saa kumi jion Hali ikawa Bado anaharisha tukamrudisha zahanat Tena kwa dokta akapimwa malaria ilikua akakutwa malaria imeshuka toka9 Hadi 5 ila mtoto akawa na joto sana ikabidi achomwe sindano yakushusha joto...dokta akashauri apewe dawa kukata kuharisha akampa dawa pia akashauri aanzishiwe sindano kwa ajili ya malaria..pia dokta akakagua choo Iko Cha mtoto akasema mtoto anaharisha maziwa ya mama nimachafu ikabid mama mtoto akamue maziwa yatoke machafu kwa ushauri wa dokta walau mtoto apate maziwa fresh zoezi lilifanyika tukarud nyumba...Sasa mtoto akapewa dawa yakukata kuharisha mida hii yasaa kumi na mbili lakini mtoto baada ya dakika15 mtoto akaicheua dawa yote pamoja na chakula chote alichokula pia baada ya madakika kama nusu saa akaharisha Tena...msaada wenu wakuu hii Hali ya kuharisha kutokukata na pia mtoto kushindwa kuinywa dawa anaicheua nifanyaje wakuu.. maana hii kuhara mtoto mara Zaid ya kumi naona anapoteza maji mwilini nahis hatar nisije nikamkosa mtoto wangu nahitaji ushauri wenu wakuu
ORS vipi unampa
 

Attachments

  • IMG_20240929_195505.jpg
    IMG_20240929_195505.jpg
    229.1 KB · Views: 6
Mpeleke hospital kubwa fasta usichelewe mtoto amepoteza maji mengi
Mkuu jumapili uku hospital ya wilaya ya serikali na kituo cha afya hakuna huduma za vipimo vinavyofanyika zaid ya dripu tu nadawa
 
Pole sana...

Mpe
. Pedzinc 1*1*5/7
. Ors 1packet
. Kama anatapika sana muongezee na promethazine syrup 2.5ml *2*2/7
 
FBP
mchfuko wa damu huo nadhni
apige sindano ya ugonjwa,kushush homa(kma ipo) na kuzuia kutapika

wahi.hosp.chap
 
Pole sana...

Mpe
. Pedzinc 1*1*5/7
. Ors 1packet
. Kama anatapika sana muongezee na promethazine syrup 2.5ml *2*2/7
Mkuu hatapiki ila anaharisha..akipewa dawa akiinywa bas ndani ya dakika 2 dawa ataicheuwa yote Sasa hapa anatibikaje mkuu nishauri maana dawa yote anaicheuwa
 
Mkuu hatapiki ila anaharisha..akipewa dawa akiinywa bas ndani ya dakika 2 dawa ataicheuwa yote Sasa hapa anatibikaje mkuu nishauri maana dawa yote anaicheuwa
Hiyo dawa anayocheua ni dawa ipi mkuu?? Tuaze kwanza hapa??
 
Huyo mtoto amepimwa choo?
Mana isije ikawa ana infenction tumboni ndo inamsababisha aharishe
Nakushauri chukueni choo cha mtoto mkapime kwanza msomewe majibu na aanze dozi mapema mana inavyoonekana shida iko hapo
 
maana hii kuhara mtoto mara Zaid ya kumi naona anapoteza maji mwilini nahis hatar nisije nikamkosa mtoto wangu nahitaji ushauri wenu wakuu

pia dokta akakagua choo Iko Cha mtoto akasema mtoto anaharisha maziwa ya mama nimachafu ikabid mama mtoto akamue maziwa yatoke machafu kwa ushauri wa dokta walau mtoto apate maziwa fresh zoezi lilifanyika tukarud nyumba...
Kuuu huyu doc ni uchwara,,,, hakuna maziwa Machafu kutoka kwenye kwa mama, unless mama awe mchafu ndio atampa mtoto chuchu chafu,,,
Mtoto aneharisha ikifukia hatua hawezi kunywa dawa au ORS, yupo kwenye severe dehydration,,,, anatakiwa apate iv fluids( maji ya mishipani), ped. Zinci na pia matibabu yake ya malaria yaendelee,,,,
Nenda hospital haraka,,,,, mtoto atakuwa nahali mbaya zaidi ukichelewa.
 
Madhara ya mtoto kuoa mtoto wakazaa mtoto. Nyumba inakuwa na watoto watatu. Mtoto anaumwa anakuja Jf alaf anategemea madaktari wa Jf wamshauri.

Na madaktari wa Jf wanamuandikia dawa bila kumpima.

Mchi imevurugwa hii
 
Mkuu nimetoka hospital lakini Hali Bado ya mtoto Iko vilevile ndo nimekuja huku
Madhara ya mtoto kuoa mtoto wakazaa mtoto. Nyumba inakuwa na watoto watatu. Mtoto anaumwa anakuja Jf alaf anategemea madaktari wa Jf wamshauri.

Na madaktari wa Jf wanamuandikia dawa bila kumpima.

Mchi imevurugwa hii
Kuu
 
Mkuu jumapili uku hospital ya wilaya ya serikali na kituo cha afya hakuna huduma za vipimo vinavyofanyika zaid ya dripu tu nadawa
Si bora hata hizo drip,alfu siku ingine ukimpeleka mtoto zahanati maendeleo sio mazuri badili hospital,mfano hapo zahanati wanapima choo?
Mama aendelee kumyonyesha mara kwa mara
 
Ndugu kwani uko mkoa au Wilaya gani? Maana
 
Dawa yoyote dawa aliyopewa kuzuia kuharisha imeandikwa ciprofloxacin hydrochloride bp 500mg

Ciprofloxacin kwa mtoto wa miezi saba 🤨🤨🤨🤨🤨????



. Cha kwanza kabisa inabidi akatishe kuharisha kwanza.. Maana akiharisha sana maji mwilini yanapungua kwa haraka sana.
. Na mtoto anacheua dawa kwa sababu ni kali...

1. Tengeneza Ors ya kienyeji ( vijiko 4 vya sukari +kijiko kimoja cha chumvi kisha changanya kwenye lita moja ya maji. Au tumia hiyo Ors ya dukani, Kisha endelea kumpa.

2. Sitisha hiyo Ciprofloxacin, then mpe metronidazole syrup.

3. Pedzinc 1 *1 *5/7

3. Mpe na dawa ya kuzuia kichefuchefu ( promethazine syrup) hii ndo iwe ya kwanza kumpa ndo zifuate hizo zingine..


Then kesho amka mapema sana, mpeleke kituo cha Afya.
 
Dawa yoyote dawa aliyopewa kuzuia kuharisha imeandikwa ciprofloxacin hydrochloride bp 500mg
Mmh,hivi zahanati utakuta dawa gani?imagine mtoto anapewa cipro serious?
Nimehisi uchungu wa ghafla,wazazi kuweni serious kidogo,kitendo cha kukomaa na zahanati mda wote huo inaonesha jinsi gani hauko serious.
 
Mmh,hivi zahanati utakuta dawa gani?imagine mtoto anapewa cipro serious?
Nimehisi uchungu wa ghafla,wazazi kuweni serious kidogo,kitendo cha kukomaa na zahanati mda wote huo inaonesha jinsi gani hauko serious.
Hatari sana mkuu, Cipro ni dawa kali sana hii, na wasi wasi hata hiyo malaria walimbampika tu.. Ili wapate maokoto mengi.
 
Back
Top Bottom