malembeka18
JF-Expert Member
- Jan 26, 2018
- 3,266
- 3,698
Habar wakuu msaada wenu wa mawazo binti yangu ana miezi saba kamili sasa.
Awali ya yote tangu ijumaa kaanza kuugua malaria akapewa doze ya mseto, sasa tangu alfajiri ya leo kaanza kuharisha na na tumbo kulisikia kama linatoa sauti. Kaharisha mara 13 tangu alfajiri.
Asubuh tukachukua jukumu la kumpeleka zahanati alipotibiwa akaangaliwa dokta akashauri amalizie dozi ya malaria
Sasa kufika saa kumi jion bado akawa anaharisha tukamrudisha zahanati tena kwa dokta,
Akapimwa malaria, ikaonekana malaria imeshuka toka 9 hadi 5 ila mtoto akawa na joto sana ikabidi achomwe sindano yakushusha joto. Dokta akashauri apewe dawa ya kukata kuharisha pia akashauri aanzishiwe sindano kwa ajili ya malaria.
Pia dokta akakagua choo cha mtoto akasema mtoto anaharisha maziwa ya mama ni machafu ikabid mama mtoto akamue maziwa yatoke machafu kwa ushauri wa dokta walau mtoto apate maziwa fresh zoezi lilifanyika tukarud nyumba
Sasa mtoto akapewa dawa ya kukata kuharisha mida hii ya saa kumi na mbili lakini mtoto baada ya dakika 15 mtoto akaicheua dawa yote pamoja na chakula chote alichokula pia baada ya kama nusu saa akaharisha tena.
Msaada wenu wakuu hii, Hali ya kuharisha na pia mtoto kushindwa kuinywa dawa anaicheua nifanyaje?
Maana hii kuhara mtoto mara zaidi ya kumi naona anapoteza maji mwilini, nahisi hatari nisije nikamkosa mtoto wangu nahitaji ushauri wenu wakuu
Awali ya yote tangu ijumaa kaanza kuugua malaria akapewa doze ya mseto, sasa tangu alfajiri ya leo kaanza kuharisha na na tumbo kulisikia kama linatoa sauti. Kaharisha mara 13 tangu alfajiri.
Asubuh tukachukua jukumu la kumpeleka zahanati alipotibiwa akaangaliwa dokta akashauri amalizie dozi ya malaria
Sasa kufika saa kumi jion bado akawa anaharisha tukamrudisha zahanati tena kwa dokta,
Akapimwa malaria, ikaonekana malaria imeshuka toka 9 hadi 5 ila mtoto akawa na joto sana ikabidi achomwe sindano yakushusha joto. Dokta akashauri apewe dawa ya kukata kuharisha pia akashauri aanzishiwe sindano kwa ajili ya malaria.
Pia dokta akakagua choo cha mtoto akasema mtoto anaharisha maziwa ya mama ni machafu ikabid mama mtoto akamue maziwa yatoke machafu kwa ushauri wa dokta walau mtoto apate maziwa fresh zoezi lilifanyika tukarud nyumba
Sasa mtoto akapewa dawa ya kukata kuharisha mida hii ya saa kumi na mbili lakini mtoto baada ya dakika 15 mtoto akaicheua dawa yote pamoja na chakula chote alichokula pia baada ya kama nusu saa akaharisha tena.
Msaada wenu wakuu hii, Hali ya kuharisha na pia mtoto kushindwa kuinywa dawa anaicheua nifanyaje?
Maana hii kuhara mtoto mara zaidi ya kumi naona anapoteza maji mwilini, nahisi hatari nisije nikamkosa mtoto wangu nahitaji ushauri wenu wakuu