Mtu akifa anaenda wapi?

Mtu akifa anaenda wapi?

Hili bara la kijinga sana mkuuu werevu kama wewe au mimi ni wachache mno ....wakutafuta na tochi.....
Kwasasa napata picha kwanini philosophers kama kina SOCRATES na wengine walikuwa wanauwawa,...kuwa miongoni mwa watu kama hawa pia ni hatari kwa usalama sio wa akili tu, bali pia kwa uhai wako kwa ujumla....
 
Naamini nitakuwa sijui lolote kama ambavyo nilikuwa sijui kabla ya hata shahawa kutungwa
 
Ikiwa mtu ni wa milele maana yake pia alikuwepo hata kabla hajazaliwa, na pia atakuwepo hata baada ya kufa....

sasa wewe una kumbuka ulikuwa wapi kabla hujazaliwa?...
Kaa chini ufundishwe,

(Yeremia 1:5)
"Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla ya Kutoka tumboni nalikutakasa,nimekuweka kuwa Nabii wa mataifa."

Ndipo ujue maisha ya mwanadamu hayaanzi tumboni au anapozaliwa, ni way back.

Kuthibitisha Hilo, tangu Leo, ulalapo uwe unatilia Umakini ndoto unazoota.

Ukiwa katika Ulimwengu wa Roho wa NDOTO, hakuna time,

Unaweza kuona future na past Kwa pamoja,Sema tu lugha ya ndoto Huwa ya mafumbo.

Tafuta sana Maarifa, usijizungushie uzio.
 
Kaa chini ufundishwe,

(Yeremia 1:5)
"Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla ya Kutoka tumboni nalikutakasa,nimekuweka kuwa Nabii wa mataifa."

Ndipo ujue maisha ya mwanadamu hayaanzi tumboni au anapozaliwa, ni way back.

Kuthibitisha Hilo, tangu Leo, ulalapo uwe unatilia Umakini ndoto unazoota.

Ukiwa katika Ulimwengu wa Roho wa NDOTO, hakuna time,

Unaweza kuona future na past Kwa pamoja,Sema tu lugha ya ndoto Huwa ya mafumbo.

Tafuta sana Maarifa, usijizungushie uzio.
Mkuu, maisha ya kiimani za kiroho na maisha nje ya imani za kiroho ni tofauti mno. Mmoja anatumia ubongo na mwingine anatumua hisia za imani.

Unapoishi kiroho unakuwa na mambo kama haya unayosema ila kama unaishi kwa kutumia akili ya mwanadamu huwezi kuwa na hayo mambo utaona ni ujinga.

Ukielewa hilo utajua namna ya kujadili hoja na mtu asiyeishi kiroho anayetumia akili ya kawaida ya binadamu na utaelewa kuwa kabla ya kutumia biblia kama ref basi kwanza una kazi ya kuigeuza akili ya unayemwelewesha kuamini mambo ya rohoni.

Kinyume na hapo hiyo biblia kwake ni hadithi za kutunga kwa watu wajinga.
 
Ukifata imani ndivyo ilivyo. Ila ukiiweka imani pembeni wewe na kunguni hamna tofauti. Mpo duniani kula, kunya na kufa, mengine mbwembwe.

Hata hivyo, Nje ya imani ubongo wa binadamu kupitia sayansi unafanya kazi kwa upekee sana. Pengine ukaja na dawa ya kutokufa huko mbeleni.

Nje ya imani wewe ni nani?

Wewe ni kumbukumbu ya yale uliyofanya na yale uliyofanyiwa na wengine.

Hizo kumbukumbu zimebebwa na mashine iitwayo mwili yenye kifaa maalum kiitwacho ubongo.

Sasa siri hapa ni namna ya kuzihamisha hizo kumbukumbu kwenye vifaa visivyoharibika au vifaa vingine tofauti na mwili au kuhakikisha kile kinachochakaza mwili hakichakazi.

Wanasayansi wapo kazini. Wameshafanikiwa kiasi kwenye uchakavu wa umbile la nje yaani sura. Sasa hivi ukiwa na pesa unaweza kuwa na miaka 60 ila ukaonekana kama una upo 20's.

Tunavyojadili hapa kuna program za kulipia za kugandisha mwili ikiaminika kwamba miaka mingi mbeleni tech itakuwa imekuwa juu kiasi cha kuurudisha mwili hai tena, hivyo si lazima uzikwe ukiwa na pesa, unaweza lipia ukagandishwa kwa vifaa maalum. Au kama ni mgonjwa na sasa hakuna dawa unaweza lipa ukasubiri miaka 200 ijayo dawa ikipatikana.
kama kuna kitu sina mashaka nacho basi ni SCIENCE, maana there is a logic behind every idea, na pia inakubali kukosolewa na kupingwa kupitia TAFITI,....


shida ya hizi imani waliozishikilia ukiwapiga maswali hawawezi kujibu, hawataki kukosolewa wala kupingwa, na Wakati huo hawana uthibitisho wowote ule....
 
Wapiramu ndiyo wakina nani?
Anajaribu kuwatusi wale asiowapenda sababu hawaamini kama yeye; wao wanamuabudu Mungu tu na si kina deacon sijui beacon.....sijui. Nikiangalia maelfu ya miaka ya mahangaiko ya kuwafuta watu hao na imani yao, tena kutoka kwa watu wenye akili na uwezo, bila madankkio; natamani nimshauri achukue jembe tu akalime.
 
kama kuna kitu sina mashaka nacho basi ni SCIENCE, maana there is a logic behind every idea, na pia inakubali kukosolewa na kupingwa kupitia TAFITI,....
Upo sawa
shida ya hizi imani waliozishikilia ukiwapiga maswali hawawezi kujibu, hawataki kukosolewa wala kupingwa, na Wakati huo hawana uthibitisho wowote ule....
Shida ya watu msio na imani za kiroho ni kuwa mnataka kujadili masuala ya kiroho kwa kutumia logic ya akili ya kawaida ya binadamu. HAIWEZEKANI. Haya mambo ya kiimani na akili ya kutengeneza logic hayaendi pamoja.

Wewe ni Logic gani utatengeneza kwenye binadamu kujaza wanyama, wadudu na ndege wawili wawili kwenye meli moja ya mbao na lami?

UKITAKA KUFAHAMU MAMBO YA ROHONI, ACHANA NA LOGIC SIJUI AKILI KUBWA. KWENYE MAMBO YA KIROHO NI MIUJIZA MIUJIZA, IMANI, MAMBO YASIYOWEZEKANA KATIKA ULIMWENGU WA LOGIC YA AKILI YA BINADAMA WA KAWAIDA.
 
HABARI YA PASAKA JF,Je Ulishawahi Kujiuliza Unaenda Wapi Ukisha kufa? Fuatana na Mimi Asubuhi Upate Elimu.

MTU AKIFA ANAENDA WAPI?
Mwili hushushwa ardhini baada ya pumzi kurudi kwa muumba,yaani baada ya nafsi kufa!

Kifo kinauma sana,na ukizingatia wengi hatujui nini kinafuatia baada ya kifo.Hatujui kama wapendwa wetu wanaunguzwa kwenye moto,wamepumzika paradisoni au wanahangaika peponi.Haya maswali yanasumbua watu wengi,mtu akifa nini kinafanyika?Lakini kwa bahati nzuri majibu tunayo....ebu tujifunze.

Tunakwenda wapi tukifa? Mbinguni? Jehanum? Toharani? (Toharani ni mahali ambapo baadhi ya watu hudai marehemu hupitia kupata mateso ili aruhusiwe kuingia ahera) au Ahera? Ndugu zetu waliokufa wako wapi? Je, tunaweza kuwaona?Hata Biblia linauliza hili swali, “Mtu akifa, je! atakuwa hai tena?” (Ayubu 14:14).

Lakini pia Biblia linatupa jibu thabiti ambalo halina utata. Majibu yake yanaeleweka, yanaridhisha, na zaidi ya yote, yanafariji.

MTU ANAPOKUFA, HUWA KUNATOKEA NINI?
“Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.” Mhubiri 12:7.Tukumbuke kitu kimoja hapa, neno "roho" iliyotumika hapa haina tofauti na "pumzi".Mara nyingi sana imetumika neno hilo roho kwenye Biblia kama tafasiri ya neno "spirit" pamoja na neno "breath".Yaani neno breath limetumika mara chache....

Mwili huyarudia mavumbi na pumzi/roho humrudia Mungu aliyeitoa. Pumzi ya mtu aliyekufa, awe mwenye haki au mwovu – humrudia Mungu wakati wa kufa,kwakuwa ni yeye aliitoa na sasa anakuwa ameitwaa.

ROHO AU PUMZI INAYOMRUDIA MUNGU NI KITU GANI?
Biblia inasema “Mwili pasipo roho(pumzi) umekufa.” Yakobo 2:26. “Roho(pumzi) ya Mungu i katika pua yangu.” Ayubu 27:3.

Roho inayomrudia Mungu wakati wa kufa ni ile pumzi ya uhai. Hakuna mahali katika Biblia ambapo tunaambiwa kuwa roho(pumzi) inakuwa na uhai, hekima au hisia baada ya mtu kufa. Ni “pumzi ya uhai”, na si ya kifo.Yaani kukosa pumzi matokeo yake ni KIFO!

NAFSI NI NINI?
“BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Mwanzo 2:7. Nafsi ni muunganiko wa vitu viwili: Mwili(nyama, mifupa, damu, mishipa n.k) na pumzi(roho). Nafsi haiwezi kuwepo bila mwili na pumzi kuunganishwa. Neno la Mungu linafundisha kuwa sisi ni nafsi.

NAFSI HUFA?
Ndiyo,nafsi hufa.
Biblia inathibitisha hili kwenye Warumi 7:24," Ole wangu, maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?" na kwenye Waebrania 9:16, "Maana agano la urithi lilipo, lazima iwepo mauti yake aliyelifanya."Pia Ezekiel 18:20,"Roho(spirit) itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa.”

Kulingana na Neno la Mungu, nafsi inaweza kufa! Sisi ni nafsi na nafsi zinaweza kufa. Mwanadamu hufa. Mungu pekee hapatikani na mauti (1 Tim. 6:15,16). Dhana ya nafsi isiyokufa inapingana na Biblia inayofundisha kuwa nafsi hazina budi kufa.

MTU ALIYEKUFA ANAWEZA KUJUA AU KUELEWA KITU?
Hapana! “Walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lo lote linalofanyika chini ya jua.” “Lolote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu (kaburini) uendako wewe.” Mhubiri 9:5,6,10. “Sio wafu wamsifuo Bwana.” Zab. 115:17.

Mungu anasema wafu hawajui kitu chochote.

WAFU WANAWEZA KUWASILIANA NA WALIO HAI?
Hapana! "Ni vivyo mwanadamu hulala chini, asiinuke; hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka, wala kuamshwa usingizini.” “Wanawe hufikiria heshima, wala yeye hajui; kisha wao huaibishwa, lakini yeye hana habari zao.” Ayubu 14:12,21. “Wala hawana sehemu tena katika jambo lolote lililofanyika chini ya jua.” Mhubiri 9:6.

Wafu hawawezi kuwasiliana na walio hai. Wamekufa. Mawazo yao yamepotea (Zab. 146:4).

SASA KWANINI SISI TUNAPATA NDOTO KUTOKA KWA WAFU KAMA HAWAELEWI KITU CHOCHOTE?
Natoa mfano hai kwenye Biblia,kwa sababu Biblia haifichi mambo. Mfalme Sauli na majeshi yake walikuwa vitani kaskazini mwa Israeli. Walikabili jeshi lenye kuogopesha la Wafilisti. Sauli alipoona majeshi ya Wafilisti, “akaogopa, na moyo wake ukaanza kutetemeka sana.” Wakati huo, Sauli alikuwa tyari ameacha ibada ya kweli. Kwa sababu hiyo, Yehova hakumjibu sala zake. Sauli angefanya nini ili apate msaada? Samweli, nabii wa Mungu naye alikuwa ameshafariki(1 Samweli 28:3, 5, 6).

Sauli aliamua kumtafuta mwongozo kutoka kwa mwanamke mmoja aliyekuwa na uwezo wa kuwasiliana na pepo huko En-dori. Alimsihi mwanamke huyo “nipandishie Samweli” kutoka kwa wafu. Mwanamke huyo alipandisha mzuka(mapepo) na kuweza kumuona “Samweli”. Na huyo Samweli aliyetokea aliongea na Sauli na kumwambia kuwa Wafilisti wangeshinda vita na kwamba Sauli na wanawe wangekufa vitani. (1 Samweli 28:7-19) Je, huyo alikuwa Samweli aliyeonekana alikuwa wa kweli aliyerudi kutoka wafu?Jibu ni hapana,lakini majibu ya huyo mama yalikuwa ya ukweli mtupu! Hii inawezekanaje?

Fikiria jambo hili kwa makini zaidi. Biblia inasema kwamba mtu anapokufa ‘anarudi kwenye udongo wake’ na kwamba “mawazo yake hupotea.” (Zaburi 146:4).Biblia haijichanganyi hata siku moja. Sauli na Samweli wote walijua kwamba Mungu anachukizwa sana na mawasiliana kati ya binadamu na mapepo(Mambo ya Walawi 19:31).

Kilichotokea,na kinachotokea mara kwa mara hata mpaka leo hio ni mawasiliano kupitia kwa malaika waasi,ambao ni viumbe vya kiroho(spirits),na ambao waliasi mamlaka ya Mungu mapema katika historia ya wanadamu(Mwanzo 6:1-4; Yuda 6). Mashetani hawa wanaweza kututazama na kuona binadamu hai.Wanajua mawazo yetu,uwezo wetu na madhaifu yetu.Pia wanajua ndugu zetu walikwisha kufa tangia walipokuwa hai,wanajua mahusiano kati ya hao marehemu na watu waliopo duniani. Kwa hiyo wanajua jinsi mtu alivyokuwa anazungumza, alivyotenda, na sura yake alipokuwa hai. Wanataka kuendeleza dhana kwamba Biblia na Mungu ni uwongo(dhana ambalo shetani alilianzisha tangia shamba la Edeni). Biblia inatuonya tusiwe na mawasiliano yoyote na roho kama hao! (Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Mashetani hao bado wanatenda kazi leo na wataendelea mpaka muda wao utakapoisha.

Sasa tunaweza kuelewa ni kwa nini wengi wanasema kwamba “wamewaona” wapendwa wao waliokufa au “kusikia” sauti yao. Ingawa wafu hao wanapotokea kama mizuka wanaweza kuonekana kuwa na nia nzuri, kumbuka kwamba roho waovu wameazimia kuwadanganya watu (Waefeso 6:12),hata kwa habari njema.

Kila binadamu anapokuwa hai hapa duniani,ni kiumbe cha kiroho ndani ya mwili wa nyama.Ni pumzi ndani ya mwili.Ndiyo maana anaweza kuwasiliana aidha na Mungu au shetani kiroho na siyo kimwili.Binadamu yuko huru kufanya mawasiliano kupitia roho mtakatifu wa Mungu au roho mtakavitu na chafu wa shetani.Mungu ni roho,na anataka tumuabudu kwa ROHO na KWELI (Yohana 4:24)"Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli."

Hii inamaanisha kuna kuabudu kwa ROHO na WONGO pia,right?Ni wewe uchague uko pande ipi....Mungu halazimishi ila matokeo ya chaguo lako hayaepukiki.

Kumbuka kwamba siyo ndoto zote ni mbaya au dhambi,kuna ndoto zinazotoka kwa Mungu kwajili ya watu wa Mungu.Alafu kuna ndoto zingine zinazotokea kwa ibilisi kwajili ya watu wake.Kuna mifano mingi mno ndani ya Biblia.

Ukisoma Matendo ya Mitume 2:17 inathibitisha kwamba hata siku za mwisho watu wataota ndoto kutoka kwa Mungu,inasema hivi,"Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto."

#MunguNiRoho
Haya mambo yamepitwa sana na wakati.
 
Upo sawa

Shida ya watu msio na imani za kiroho ni kuwa mnataka kujadili masuala ya kiroho kwa kutumia logic ya akili ya kawaida ya binadamu. HAIWEZEKANI. Haya mambo ya kiimani na akili ya kutengeneza logic hayaendi pamoja.

Wewe ni Logic gani utatengeneza kwenye binadamu kujaza wanyama, wadudu na ndege wawili wawili kwenye meli moja ya mbao na lami?

UKITAKA KUFAHAMU MAMBO YA ROHONI, ACHANA NA LOGIC SIJUI AKILI KUBWA. KWENYE MAMBO YA KIROHO NI MIUJIZA MIUJIZA, IMANI, MAMBO YASIYOWEZEKANA KATIKA ULIMWENGU WA LOGIC YA AKILI YA BINADAMA WA KAWAIDA.
kwahiyo ili uelewe imani ni lazima uwe empty-headed?🤧😆😅😂😂😂 sasa si wazimu huo, ubongo kazi nini tena kama sio kufikiri?....
 
Nenda kamuulize mama Yako alipokuzaa, kitovu chako alipokikata alikitunza wapi ndipo uje useme Ulimwengu wa Nuru na Giza ni story!!

Siku utakapolala umefunga milango na ukaamka uko kwenye majaruba ndio utajua uchawi upo au la!!

Ndio ninyi mnaenda shule Kisha mnamkataa hata Mungu na kuzidi kutokomea gizani kuliko kupata Nuru.

Sorry Kwa lugha ngumu!!
Wewe ni mpuuzi tu kama walivyo wapuuzi wengine.
 
kwahiyo ili uelewe imani ni lazima uwe empty-headed?🤧😆😅😂😂😂 sasa si wazimu huo, ubongo kazi nini tena kama sio kufikiri?....
Ndo fomula. Ili uishi kiroho lazima uamini wewe si lolote si chochote na option uliyonayo ni chaguzi kati ya nguvu mbili zenye uwezo wa kuendesha maisha yako na maisha yanaanzia rohoni ndipo yanatokea katika uhalisia wa mwili na haya maisha ya mwili ni temporary ili kujiandaa na maisha ya rohoni ambayo mfumo wake unategemeana na nguvu uliyoichagua iendeshe roho yako. Nguvu ni mbili tu, mwanga na giza, wema na ubaya, Shetani na MUNGU. Vyovyote utakavyoziita.

Au

Uishi kwa kutumia ubongo wako, utegemee sayansi, usiamini katika uwepo wa MUNGU wala shetani, kila kitu kwako kisicho na logic kiwe ni cha kufikirika na cha kukipuuza.

Binafsi naamini nguvu iliyotuumba ilitupa ubongo kwa sababu maalum. Nimeamua kuutumia ila kama jambo silielewi kabisa na ubongo umegoma kutengeneza logic silidharau na kusema halipo, ninachofanya ni kuliacha kama lilivyo kwanza.
 
kwahiyo ili uelewe imani ni lazima uwe empty-headed?🤧😆😅😂😂😂 sasa si wazimu huo, ubongo kazi nini tena kama sio kufikiri?....
Ni logic gani iliyopo Kwa wewe kuishi hapa Duniani?


I mean kwanini unaishi?
 
Mtu asiyemwamini Mungu ama mambo ya kiimani kwa usahihi ana jina lake la kitaalam nalo ni "Mshenzi"
 
Katika kipindi cha Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi katika Israel ila ni Naamani pekee aliyetakaswa wakoma wengi walikufa na ukoma wao kwa hiyo imani yako ndio itakayokuponya au kukuangamiza. Haijalishi unaamini life after or not you can not change the reality of life after death.
 
ukifa ndio umekufa hayo mengine ni masimulizi tu..
Tumia akili walau kidogo. Kama ukifa umekufa sasa nini lengo la sisi kuishi na kuwa hai. Akili iliyo salama unakataa hili.
 
Mtoa mada kaweka maandiko hapo ili kuhalalisha hoja zake ila turudi kwenye jambo moja. Katika Biblia kuna waandishi waliandika mitazamo yao na sio Neno kutoka kwa Mungu moja kwa moja bali ni mitazamo tu. Mfano Kitabu cha Mhubiri ni hekima za Suleimani na mitazamo yake mfano kila kitu kakiita ubatili na kujilisha upepo n.k.
Sasa katika mtizamo wa maisha mara baada ya kifo kila nabii alikuwa na mtizamo wake maana Biblia au Mungu alikaa kimnya na pengine kuzungumza kwa mafumbo. Mfano kitabu cha Mwanzo anapomlaani Adamu anamwambia " wewe ni mavumbi na mavumbini utarudi " hapohapo Kaini anamuuwa nduguye Abili na anapoulizwa na Mungu yuko wapi nduguye anamjibu Mungu shit kisha Mungu anamwambia "damu ya ndugu yako inanilia kutoka ardhini swali kama watu wakifa wanapotea au kurudi mavumbini hiyo damu iliyokuwa inatoa sauti Mungu alikuwa anasema na mzimu wa Abel?.

Kumbuka mwanadamu wa asili hawezi kuyatambua mambo ya rohoni kwani yanatambulika kwa jinsi ya roho. Hivyo wewe mwanadamu wa asili kamwe usijaribu mambo ya rohoni waachie wa rohoni.
 
Back
Top Bottom