Mtu aliyesoma akaelimika akakombolewa kifikra hawezi Kutoa au kutolewa Mahari

Mtu aliyesoma akaelimika akakombolewa kifikra hawezi Kutoa au kutolewa Mahari

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Elimu Kazi yake kûbwa ni kumkomboa Mtu ndiye Mwanamke na Mwanaume kifikra.

Haiwezeniki Mtu kafika chuo Kikuu, amesoma degree au katika chuo cha Kati akasoma stashahada akaibusti Akili Yake Akaelimika alafu Wakati wa kuchumbia au Kuoa au kuolewa akakubali Kutoa au kutolewa mahari.

Mtu aliyesoma au Mtu yeyote àmbaye akili yake Iko Huru na inachaji hawezi kushindwa kujua kuwa mahari ni biashara haramu ya kumnunua Mwanamke

Sisi Watibeli hata kusingekuwa na shule Kabisa, tusingeshindwa kujua kuwa Mahari ni biashara haramu àmbayo Watu hawapaswi kuifanya. Tunajua Jambo hili Kwa sababu ya haki, ukweli, maarifa na upendo.

Huwezi mnunua Mtu bhana tenà Mtu unayempenda Kwa Kile ambacho Mila na desturi potofu zilikiita Mahari ili kupumbaza Watu.

Wanawake hawawezi kuwa na Haki Sawa na Wanaume ilhali waô wananunuliwa kimafungu kama Mbuzi.

Sisi Watibeli hatufanya Vitu kuridhisha Watu hata kama Watu hao ni wazazi wetu, Watoto wetu, ndugu zetu, wake zetu ilhali Vitu hivyo tunajua NI dhulma, ukatili, udhalilishaji, na uovu.

Nafahamu Watu wengi wanajua kuwa Mahari ni biashara haramu lakini hawanabudi kufanya ili kuridhisha Wazazi na ndugu na Mila. Jambo hilo Kamwe Sisi Watibeli hatutafanya.

Watoto wàngu, Jambo lolote ambalo mnajua ni ovu na siô Haki Kamwe msilifanye Kwa lengo la kuniridhisha Mimi Baba Yenu au kumridhisha Mama Yenu.

Wazazi Bila aibu mnakaa mnajadili na kupanga bei ya Binti Yenu. Kisha kijana naye anakuja kutajiwa bei Kisha ati mnashushana bei mara Milioni nne. Mwanaume anasema Nina Milioni Mbili unusu, ooh mnamwambia tatu mwisho kama mnauza tukutuku.

Mimi kama Mtibeli siwezi kufanya wala kujadili uharamu wa namna hiyo.

Kama tunajadili kuhusu kununua Ng'ombe Sawa lakini kununua Mtu sijui Mwanamke alafu mnaleta unafiki kuwa hamuuzi ila NI Mahari sijui shukrani. Shukrani gàni inapangwa na Mpokeaji?

Kwamba ati uniletee Laki tisa kama Shukrani ya kumchukua Binti yàngu. Hivi Akili zenu zinafanya Kazi Sawasawa.

Huyo siô Mimi, hao siô Watibeli. Watibeli hawatoi Mahari wala Binti zetu hawatolewi Mahari. Kwa sababu Binti zetu ni Watu Huru, hawanunuliki.Hatuwezi kuwathaminisha ati huyu nipe kiasi kadhaa nikupatie awe Mkeo.

Mmekubaliana Huko njooni Kwetu Wazazi mjitambulishe, tuwaone na kuwajua, mtujue, tufurahi. Tuwabariki. Full stop!

Watibeli tunatambua adhabu Kwa Watoto wetu. Ikiwa Watoto watakiuka Baadhi ya Sheria mfano wamekutana juu Kwa juu Huko wakabebeshana Mimba pasipo kûja nyumbani kutambulishana ni ruhusa Kwa Wazazi kuwapa adhabu na hiyo adhabu lazima iwahusu watoto wôte wawili, yàani Kijana na Binti wôte lazima wawajibike na siô kumpa adhabu Mtu mmoja. Hiyo ndîo haki.

Kumpa adhabu kijana pekee ni dhulma, ukatili, uonevu na hii humfanya kijana awe katika mazîngira ya kuona anammiliki Binti Jambo ambalo siô kwèli. Hii hufanya unyanyasaji na ukatili baadaye utokee.

Wamepeana Mimba, wôte wamekosea, kama adhabu NI kutoa Pesa, Basi wôte watoe Pesa mmoja kama ni Laki tano Basi kîla Mtu atoe Laki Mbili unusu. Wakiamua kushirikiana siô kesi Acha washirikiane. Hizô Pesa zipelekwe Kwa familia ya upande Binti na familia ya kijana Nusu Kwa Nusu.

Watu walale Kwa starehe zào Kwa mapenzi Yao alafu ninyi mseme ati Binti Yenu ameharibiwa hivi mnaakili Sawasawa. Binti anayeharibiwa NI Yule àmbaye hajafikia Umri wa Ûtu uzima. Huyo kaharibiwa na Sheria lazima zichukue mkondo wake.

Mabinti msikubali kutolewa Mahari. Vijana msikubali Kutoa Mahari. Wazazi msiuze mabinti zenu.

Unakuta familia inamnyanyasa Binti Kisa ilimnunua Kwa Milioni Moja.

Binti Fanya Kazi. Kazi ndîo Ûtu wako. Kazi itakufanya uheshimike. Usikubali kutolewa mahari. Ikiwa alikutolea mahari, na unaona anatumia uanaume wake kukunyanyasa, mrudishie mahari Yake.

Usikubali Kupewa talaka Kabla hujarudisha Mahari ya Watu kama alikutolea mahari. Huo ni utapeli. Wewe ulinunuliwa tuu Rudisha mahari ya watu

Oooh! Nilimzalia Watoto hivyo sirudishi Pesa. Ndivyo Akili za Watumwa zilivyo. Mtu Huru au mwenye Akili zilizotimia Huwezi kuongea maneno ya ajabu na hovyo namna hiyo. Kwamba ulinunuliwa ili ukazae Sasa Kazi ushafanya hivyo hudaiwi.

Ndîo maana Wanaume Huona Watoto ni haki Yao Kwa sababu waliwanunua. Mtoto ni Baba na Mama. Kisayansi na Kiroho. Hata kihaki Ipo hivyo Ila kibiashara Mtoto ni Wa baba Kwa sababu alishamnunua Mwanamke. Kwa wale Wanaofanya hizô biashara haramu.

Hakufanya ubaya na Jambo ambalo tunaliona halipo Sawa kumridhisha yeyote.

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
 
Biashara ya utumwa isiyo haramu.

Binti unauzwa bei chee

Unaenda unafurahi

Kumbe umenunuliwa kwa bei ya jumla ndogo sana

Bora ujiuze mwenyewe rejareja ukusanye faida kubwa kwa bidhaa hiyohiyo
 
Huu uzi wa ki-feminism haf ukaongelewa 'na mwanaume ni upuuzi, Tunakuomba uhudhurie vizur ratiba ya vikao vya kiume huenda ukawa full -package masculine.
'na sisi wafia dini hautuhusu maana mahari ni amri kutoka kwa muumba sisi tunatii , kama we ni atheist sawa! Ila kama una dini andaa jibu la kumjibu mola siku ukikutana naye maana umepngana naye au utamuulza huo siku mbinguni kwann kuweka mahari 'na utoe hizi hoja ukiwa unaiona jahannamu..
Pia umekiuka mila za mababu kwahiyo unapotea kama ambavyo huwa mnasema kufuata dini ni utumwa kutoka kwa watu weupe.

MAHARI NI LAZIMA ,USIPOTOSHWE!
NI UTARATBU WA BINADAMU WOTE HTA HAO CIVILIZED WA WESTERN !
MABABU WALITOA MAHARI JAPO HAWAKUWA NA AMRI YA MUNGU YOYOTE!
MAHARI NI KUMUHESHIMISHA MWANAMKE NA KUMUONA NI MTU MWENYE THAMANI NA SO MTUMWA!

GET ME POSTED ON THIS THREAD OF HOCUS POCUS.
 
Huu uzi wa ki-feminism haf ukaongelewa 'na mwanaume ni upuuzi, Tunakuomba uhudhurie vizur ratiba ya vikao vya kiume huenda ukawa full -package masculine.
'na sisi wafia dini hautuhusu maana mahari ni amri kutoka kwa muumba sisi tunatii , kama we ni atheist sawa! Ila kama una dini andaa jibu la kumjibu mola siku ukikutana naye maana umepngana naye au utamuulza huo siku mbinguni kwann kuweka mahari 'na utoe hizi hoja ukiwa unaiona jahannamu..
Pia umekiuka mila za mababu kwahiyo unapotea kama ambavyo huwa mnasema kufuata dini ni utumwa kutoka kwa watu weupe.

MAHARI NI LAZIMA ,USIPOTOSHWE!
NI UTARATBU WA BINADAMU WOTE HTA HAO CIVILIZED WA WESTERN !
MABABU WALITOA MAHARI JAPO HAWAKUWA NA AMRI YA MUNGU YOYOTE!
MAHARI NI KUMUHESHIMISHA MWANAMKE NA KUMUONA NI MTU MWENYE THAMANI NA SO MTUMWA!

GET ME POSTED ON THIS THREAD OF HOCUS POCUS.

Sawa embu jaribu Kutumia Akili yako ya kawaida kumueleza Mtu asiyeamini katika Dini yako, na anayeamini katika HAKI.

Eleza ulazima wa Mahari(biashara ya kumnunua Mwanamke) katika mahusiano.

Nasubiri
 
Mahari ni zawadi kwa mwanamke sio kumnunua, mahari inampa hadhi na thamani mwanamke. Tena mahari ni amri ya Mwenyenzi Mungu, maana ukikataa mahari isiwepo unakua unampinga Mwenyenzi Mungu moja kwa moja.
 
Je kwa mm nliyetoa fungu la tende na masaafu, maana kwa dini yangu nimeruhisiwa kuvitoa kama mahari🙃
 
Je kwa mm nliyetoa fungu la tende na masaafu, maana kwa dini yangu nimeruhisiwa kuvitoa kama mahari🙃

Hata hao wanaotoa Ng'ombe, mbuzi, Pesa na Mali zingine kama exchange na Mwanamke wameelekezwa na Dini( mil na desturi zao)
 
Mimi ni Mtibeli

Nimekuambia chukulia Hakuna Dini, chukulia hujasoma kabisa.
Tumia Akili yako ya kuzaliwa kuelezea ulazima wa Mahari (kumnunua Mwanamke) na umuhimu wake.

Hivyo tuu.

Au unategemea mawazo ya Wengine katika Hilo?
Kaka mi so mtibeli Basi jadili na watibeli wenzio ,maana Mimi Nina misingi tofaut ya kupima usahihi wa mambo na nyinyi mna misingi yenu ya kitibeli huko kupima mambo .
Mfano, Mimi Jambo ili liwe sahihi au sio sahihi Cha kwanza likubaliane na anvyotaka aliyeniumba, halafu Kama aliyeniumba amelichia huru bila kuliwekea Sheria au amri Basi ndo akili yangu itafuata kujiuliza .
Ila naona nyinyi watibeli mnatanguliza akili kwanza kwenye kila ktu Mana na Mimi ningewaiga nisingeweza hta kuwatii wazazi ,Mana Kuna mambo hta hayana Tija Ila walikuwa wanatufosi.
Huu Uzi wa kitibeli siuwezi, watibeli endeleeni.
I'm a couch potato when it's come on brainstorming but for really mtibeli you're a bad apple🍎.
 
Apatae mke kapata kitu chema, kuna watu wanatolewa hiyo mahari mara mbili, yaani baada ya kuishi na mtu anaona kama ya mwanzo haikutosha.
 
Mimi kama Mtibeli siwezi kufanya wala kujadili uharamu wa namna hiyo.
utamaduni

mila, asili, jadi na desturi za kundi la jamii fulani


mahari

mali au fedha inayotolewa na mwanamume kupewa mwanamke au wazazi wa mwanamke anayetaka kumuoa


dowry

in some societies, an amount of money or property that a woman's parents give to the man she
marries

dowry​


the money, goods, or estate that a woman brings to her husband in marriage

2 The King and Queen’s Marriage: Dowry, Infertility, and Adultery​



Wewe ni :

dikteta

mtu mwenye tabia ya kutaka lifanywe lile analosema bila ya kupingwa

 
Kaka mi so mtibeli Basi jadili na watibeli wenzio ,maana Mimi Nina misingi tofaut ya kupima usahihi wa mambo na nyinyi mna misingi yenu ya kitibeli huko kupima mambo .
Mfano, Mimi Jambo ili liwe sahihi au sio sahihi Cha kwanza likubaliane na anvyotaka aliyeniumba, halafu Kama aliyeniumba amelichia huru bila kuliwekea Sheria au amri Basi ndo akili yangu itafuata kujiuliza .
Ila naona nyinyi watibeli mnatanguliza akili kwanza kwenye kila ktu Mana na Mimi ningewaiga nisingeweza hta kuwatii wazazi ,Mana Kuna mambo hta hayana Tija Ila walikuwa wanatufosi.
Huu Uzi wa kitibeli siuwezi, watibeli endeleeni.
I'm a couch potato when it's come on brainstorming but for really mtibeli you're a bad apple🍎.

Kama Hiki ulichoandika ndîo hoja yako àmbayo umeiona NI kûbwa Basi nakupongeza
 
utamaduni

mila, asili, jadi na desturi za kundi la jamii fulani


mahari

mali au fedha inayotolewa na mwanamume kupewa mwanamke au wazazi wa mwanamke anayetaka kumuoa


dowry

in some societies, an amount of money or property that a woman's parents give to the man she marries

dowry​


the money, goods, or estate that a woman brings to her husband in marriage

2 The King and Queen’s Marriage: Dowry, Infertility, and Adultery​



Wewe ni :

dikteta

mtu mwenye tabia ya kutaka lifanywe lile analosema bila ya kupingwa


Aiseeh!

Sijui Kwa nini weñye hoja Zenye mashiko wanawaachia ninyi.

Kwa nini hamuwezi kutetea upande mliopo Kwa hoja zilizonyooka?
Jibu NI Kwa sababu mpo upande wa Uongo.
 
Apatae mke kapata kitu chema, kuna watu wanatolewa hiyo mahari mara mbili, yaani baada ya kuishi na mtu anaona kama ya mwanzo haikutosha.

Kwamba kama umenunua Ng'ombe Ikawa inatoa maziwa na faîda ya kutosha unawaza hiyo Ng'ombe ungetoa zaidi ya Pesa uliyomnunulia huyo Ng'ombe?

Mke hatolewi mahari (hanunuliwi) ila mtumwa ananunuliwa
 
Sasa mtu kaweka hoja kulingana na imani yake unamuita yuko upande wa uongo, unataka watu wakubali hoja yako ili waitwe wa kweli? utoaji wamahari kwanza ni utamaduni, kila kabila lina namna yake wanavyotoa
 
Huu uzi wa ki-feminism haf ukaongelewa 'na mwanaume ni upuuzi, Tunakuomba uhudhurie vizur ratiba ya vikao vya kiume huenda ukawa full -package masculine.
'na sisi wafia dini hautuhusu maana mahari ni amri kutoka kwa muumba sisi tunatii , kama we ni atheist sawa! Ila kama una dini andaa jibu la kumjibu mola siku ukikutana naye maana umepngana naye au utamuulza huo siku mbinguni kwann kuweka mahari 'na utoe hizi hoja ukiwa unaiona jahannamu..
Pia umekiuka mila za mababu kwahiyo unapotea kama ambavyo huwa mnasema kufuata dini ni utumwa kutoka kwa watu weupe.

MAHARI NI LAZIMA ,USIPOTOSHWE!
NI UTARATBU WA BINADAMU WOTE HTA HAO CIVILIZED WA WESTERN !
MABABU WALITOA MAHARI JAPO HAWAKUWA NA AMRI YA MUNGU YOYOTE!
MAHARI NI KUMUHESHIMISHA MWANAMKE NA KUMUONA NI MTU MWENYE THAMANI NA SO MTUMWA!

GET ME POSTED ON THIS THREAD OF HOCUS POCUS.
 
Back
Top Bottom