Mtu asiyepokea simu au kujibu ujumbe wa simu ana maana gani?

Mtu asiyepokea simu au kujibu ujumbe wa simu ana maana gani?

Mengine ni madeni bro, Kuna siku nipo ofisini sasa Kuna mwamba aliacha simu yake chaji hapo hapo akawa ametoka mara ikaanza kuita na aliweka mlio mkubwa unakera mpaka hata inaharibu attention ya kazi... Ikaita mara ya kwanza, ya pili, ya tatu... Ya nne nkasema acha nipokee nimwambie bwana mwenye simu hayupo amcheki badae... Aisee najuta kupokea hiyo simu.. jamaa alinitukana akasema nimepangwa na mwenye simu nimzuge.. akaniambia basi nilipe Mimi hilo deni maana nina shobo na masiara na deni la watu... Akasema KADI ya bank jamaa ameiacha na mshahara ametoa wote simbanking kabla jamaa hawajachukua Chao.. alifoka mshikaji katukana sana... Saiv simu hata ikiita mara mia.. siwezi kuigusa kama ni kelele Bora kazi nifanyie kwenye vimbweta vya watoto
🤣🤣daah aisee nmecheka sana japo stori inasikitisha sana. pole mkuu
 
Eti wakuu

Mtu anayeuchuna mazima baada ya kuwa umempigia simu au kumtumia meseji ni kwamba
yupo bize sana kiasi hana kabisa muda wa kuona simu au meseji zilizoingia?

Au anaona simu na meseji ila anapokea na kujibu jumbe zile za muhimu tu na ivyo ukiona yako haijapata majibu ujue ni miongoni mwa zile zisizo muhimu au ndo inawezekana keshakuona hata wewe mwenyewe hauna umuhimu?

Au inakuwa ni nini hasa kinatokea hapo?
Mfano mimi siyo mtu wa kuizingatia cm naweza maliza siku nisiishike, ila nikikuta nimepigiwa huwa napiga
 
Katika sim ambayo naizingatia sana ni namba ngeni, sim ambazo sizizingatii kivile ni sim Toka kwa ndg aisee mtanisamehe sana kwa hilo
 
Hutakiwi kuumiza kichwa jambo la wazi ni kuwa huyo mtu hataki mawsiliano na wewe......

Unatakiwa akili yako ilijue hilo na kukaa naye mbali ili kulinda heshima yako
 
Kama ukiwa karibu nae huwa yupo busy na simu mara zote. Bhasi jua call au text yako haina umuhimu maana kama ingekuwa nao bhasi angekutafuta baada ya kutoka katika hali inayomtatiza au kupokea simu kwa wakati
 
Hakuna anaye enjoy kuchat na wewe asijibu wala kupokea simu yako,
Acha usumbufu, fanya mambo yako mengine tu
 
Back
Top Bottom