Mtu hawezi kufa akafufuka, Stori za Watu waliokufa kuonekana ni uongo, na zinafanana kwa asilimia kubwa

Mtu hawezi kufa akafufuka, Stori za Watu waliokufa kuonekana ni uongo, na zinafanana kwa asilimia kubwa

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Kuna habari zinazoendelea hapa nchini hasa kanda ya ziwa na huko kanda ya magharibi ya nchi yetu kuhusu Watu waliokufa kuonekana tena , kurudi na juzi kuna mmoja amepiga simu ati kuwatakia ndugu zake mwaka mpya mwema.

Ni jamii ya kijinga inayoamini kuwa mtu akifa tena akazikwa anaweza kufufuka na kurudi tena.
Jamii zilizogizani, familia zenye mambo ya kishirikina na Uchawi, familia zenye elimu duni ndio zinazoweza kuamini na kutokewa na matukio kama hayo ya uongo.

Habari hizo ukizifuatilia kwa umakini utagundua ya kuwa zinafanana kwa namna hii;
1. Marehemu alipata ajali mbaya na uso wake haukuwa rahisi kuutambua,
Kuharibika kwa mwili na uso kwa marehemu wengi hupelekea Watu kuzika mtu asiye sahihi. Na hiyo kupelekea mtu sahihi ambaye hajafa akirudi waseme Amefufuka jambo ambalo sio kwéli.

Ukichukua DNA ya marehemu aliyefariki ambaye bila shaka yupo kaburini kwani alizikwa haziwezi kufanana na ndugu wa marehemu.

Kuhusu zile stori za mtu kufa alafu wakazika kisha kaburi likichimbwa wakakuta Mgomba ni stori za Watu wajinga ambao upeo wao upo chini kabisa katika kufikiri mambo.

Mtu yeyote anayeamini habari hizo lazima awe na sifa zifuatazo;
1. Ametoka familia Maskini sana.
2. Ametoka familia inayoamini ushirikina na uchawi ambao kimsingi hauwezi kufanya kitu kama hicho.
3. Ametoka familia isiyo na elimu na yeye mwenyewe hana elimu.
4. Ametoka familia isiyomjua Mungu isipokuwa miungu na mizimu.

Nawatakia Sabato Njema

Robert Heriel
Taikon WA Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Watu wakubwa na wenye elimu nzuri wanaamini haya mambo ila kwa siri. Kumbuka maisha ni mchezo! Huamini katika misukule?? Ndugu yangu, watu wanaojua ulimwengu wa roho ndio wenye maisha mazuri hapa duniani, amini usiamini. Hata wewe ulieandika huu uzi, usipokuwa makini nyota yako itanyakuliwa na wajanja.
 
Watu wakubwa na wenye elimu nzuri wanaamini haya mambo ila kwa siri. Kumbuka maisha ni mchezo! Huamini katika misukule?? Ndugu yangu, watu wanaojua ulimwengu wa roho ndio wenye maisha mazuri hapa duniani, amini usiamini. Hata wewe ulieandika huu uzi, usipokuwa makini nyota yako itanyakuliwa na wajanja.

Labda hujui Watibeli ni Watu wa aina ipi.

Uliza waliojaribu hiyo michezo michafu nini kiliwapata
 
Kwema Wakuu!

Kuna habari zinazoendelea hapa nchini hasa kanda ya ziwa na huko kanda ya magharibi ya nchi yetu kuhusu Watu waliokufa kuonekana tena , kurudi na juzi kuna mmoja amepiga simu ati kuwatakia ndugu zake mwaka mpya mwema.

Ni jamii ya kijinga inayoamini kuwa mtu akifa tena akazikwa anaweza kufufuka na kurudi tena.
Jamii zilizogizani, familia zenye mambo ya kishirikina na Uchawi, familia zenye elimu duni ndio zinazoweza kuamini na kutokewa na matukio kama hayo ya uongo.

Habari hizo ukizifuatilia kwa umakini utagundua ya kuwa zinafanana kwa namna hii;
1. Marehemu alipata ajali mbaya na uso wake haukuwa rahisi kuutambua,
Kuharibika kwa mwili na uso kwa marehemu wengi hupelekea Watu kuzika mtu asiye sahihi. Na hiyo kupelekea mtu sahihi ambaye hajafa akirudi waseme Amefufuka jambo ambalo sio kwéli.

Ukichukua DNA ya marehemu aliyefariki ambaye bila shaka yupo kaburini kwani alizikwa haziwezi kufanana na ndugu wa marehemu.

Kuhusu zile stori za mtu kufa alafu wakazika kisha kaburi likichimbwa wakakuta Mgomba ni stori za Watu wajinga ambao upeo wao upo chini kabisa katika kufikiri mambo.

Mtu yeyote anayeamini habari hizo lazima awe na sifa zifuatazo;
1. Ametoka familia Maskini sana.
2. Ametoka familia inayoamini ushirikina na uchawi ambao kimsingi hauwezi kufanya kitu kama hicho.
3. Ametoka familia isiyo na elimu na yeye mwenyewe hana elimu.
4. Ametoka familia isiyomjua Mungu isipokuwa miungu na mizimu.

Nawatakia Sabato Njema

Robert Heriel
Taikon WA Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Taikon, usi-conclude kirahisi hivyo. Kufufuka unaona ni kitu cha ajabu? Mbona kuna Yesu mwana wa Yussuf alifariki huko Israel sijui Palestina na akafufuka baada ya siku 3? Nafikiri ingekuwa bora tufukue kaburi tuone kweli kama hakuna mtu. Kama yupo mtu kaburini tufanye vipimo tuone ulinganifu wao. Mambo tunayoyatambua ulimwenguni ni machache sana.
 
Watu wakubwa na wenye elimu nzuri wanaamini haya mambo ila kwa siri. Kumbuka maisha ni mchezo! Huamini katika misukule?? Ndugu yangu, watu wanaojua ulimwengu wa roho ndio wenye maisha mazuri hapa duniani, amini usiamini. Hata wewe ulieandika huu uzi, usipokuwa makini nyota yako itanyakuliwa na wajanja.
Una hakika anayo nyota? Ooooh.... Nimekuelewa. Yeye nyota yake kuliwa ni maamuzi yake tu. Maana siku hizi mnaruhusu sana kuliwa nyota.
 
Kwema Wakuu!

Kuna habari zinazoendelea hapa nchini hasa kanda ya ziwa na huko kanda ya magharibi ya nchi yetu kuhusu Watu waliokufa kuonekana tena , kurudi na juzi kuna mmoja amepiga simu ati kuwatakia ndugu zake mwaka mpya mwema.

Ni jamii ya kijinga inayoamini kuwa mtu akifa tena akazikwa anaweza kufufuka na kurudi tena.
Jamii zilizogizani, familia zenye mambo ya kishirikina na Uchawi, familia zenye elimu duni ndio zinazoweza kuamini na kutokewa na matukio kama hayo ya uongo.

Habari hizo ukizifuatilia kwa umakini utagundua ya kuwa zinafanana kwa namna hii;
1. Marehemu alipata ajali mbaya na uso wake haukuwa rahisi kuutambua,
Kuharibika kwa mwili na uso kwa marehemu wengi hupelekea Watu kuzika mtu asiye sahihi. Na hiyo kupelekea mtu sahihi ambaye hajafa akirudi waseme Amefufuka jambo ambalo sio kwéli.

Ukichukua DNA ya marehemu aliyefariki ambaye bila shaka yupo kaburini kwani alizikwa haziwezi kufanana na ndugu wa marehemu.

Kuhusu zile stori za mtu kufa alafu wakazika kisha kaburi likichimbwa wakakuta Mgomba ni stori za Watu wajinga ambao upeo wao upo chini kabisa katika kufikiri mambo.

Mtu yeyote anayeamini habari hizo lazima awe na sifa zifuatazo;
1. Ametoka familia Maskini sana.
2. Ametoka familia inayoamini ushirikina na uchawi ambao kimsingi hauwezi kufanya kitu kama hicho.
3. Ametoka familia isiyo na elimu na yeye mwenyewe hana elimu.
4. Ametoka familia isiyomjua Mungu isipokuwa miungu na mizimu.

Nawatakia Sabato Njema

Robert Heriel
Taikon WA Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Mkuu kuna kitu umekwenda sawa na kuna mahali umekosea.

Labda nikuulize, duniani kuna uchawi au hakuna.

Tuanze na swali hilo na majibu utakayojaza yawe ya kitafiti na siyo kishabiki.

Je wanaosemwa wamefufuka ni kutoka katika wafu kifo cha asili au ni kurejea walikochukuliwa kichawi baada ya nguvu za maombi kushinda?
 
Taikon, usi-conclude kirahisi hivyo. Kufufuka unaona ni kitu cha ajabu? Mbona kuna Yesu mwana wa Yussuf alifariki huko Israel sijui Palestina na akafufuka baada ya siku 3? Nafikiri ingekuwa bora tufukue kaburi tuone kweli kama hakuna mtu. Kama yupo mtu kaburini tufanye vipimo tuone ulinganifu wao. Mambo tunayoyatambua ulimwenguni ni machache sana.

Mtu akifa hawezi kufufuka. Hiyo ipo kisayansi na kiimani
 
Mkuu kuna kitu umekwenda sawa na kuna mahali umekosea.

Labda nikuulize, duniani kuna uchawi au hakuna.

Tuanze na swali hilo na majibu utakayojaza yawe ya kitafiti na siyo kishabiki.

Je wanaosemwa wamefufuka ni kutoka katika wafu kifo cha asili au ni kurejea walikochukuliwa kichawi baada ya nguvu za maombi kushinda?

Hizo ni hadithi tuu Mkuu.
Mtu akifa hawezi kufufuka.
 
Mtaa wa Manzese Beston kuliwahi kutokea na mkasa kama huo, kuna kijana alikuwa mwizi alieshindikana. Ukapita muda mrefu bila kuonekana nyumbani kwao, zikaja taarifa kuwa ameuwawa kwenye tukio la wizi na mwili wake umehifadhiwa chuma cha maiti.
Ndugu zake walivyokwenda hospital ili kuutambua mwili kama ni yeye au sie wakagundua kuwa ni yeye. Wakauchukua na kufanya taratibu zote za mazishi, wakazika.
Baada ya muda kidogo kupita kuna kijana anaeishi mitaa hiyo alikuwa na mishemishe zake kariakoo akawa na soo akakamatwa na polisi akapelekwa Msimbazi police. Ile kuingia selo anamuona mtu ambae sio kwamba aliambiwa amekufa bali alishiriki kikamilifu mazishi yake.
Ndani ya selo likazuka timbwili lisilo la kawaida yule kijana anataka kutolewa ndani ya selo anasema huyu si binadamu ni msukule au mzimu nimeshiriki msiba wake ameshakufa huyu.
Polisi walijaribu kumtuliza hadi kumpiga lakini yeye alisema nina uhakika na ninachosema mnipige hadi mniue lakini nipelekeni selo nyingine humu sikai. Ikabidi ufanywe utaratibu wa kuleta ndugu wa yule anaedaiwa kufa.
Ndugu walipokuja walistaajabu kumkuta ndugu yao yupo pale na walithibitisha ni kweli alikufa na alizikwa. Uchunguzi wa kina ulipofanyika ulibaini kuwa walizika mtu ambae si ndugu yao ila kwa vile alikuwa ameharibika sana kwa kupigwa na hisia za za uvumi za ndugu yao kuuwawa kwenye tukio la wizi zilisababisha hivyo.
Yule kijana aliedaiwa kufa na kuzikwa akafanyiwa dua na mila za kwao ili kumuweka sawa na mpaka leo ameacha wizi kabisa.
 
Back
Top Bottom