Mtu kama huyu ni binadamu au shetani? Anaombeaje Corona ifike Tanzania. Kuiombea nchi yako majanga, sio zaidi ya uendawazimu? Huu sio ushetani?

Mtu kama huyu ni binadamu au shetani? Anaombeaje Corona ifike Tanzania. Kuiombea nchi yako majanga, sio zaidi ya uendawazimu? Huu sio ushetani?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi

Japo kwa kawaida usiku ni wakati wa kulala na kupumzika, ila kwa watu ma jobless wakiwemo kada yangu ya watu wa "mishe mishe", moja ya usiku ngumu sana, huwa ni usiku wa Jumapili kuamkia Jumatatu ambayo umeipitisha weekend kwa mazabe mazabe, halafu blue Monday inakuja!, usingizi huwa unakata mapema sana, by saa 9:00 usiku, usingizi umekata, hivyo huna jingine lolote la kufanya zaidi ya kushuka JF, ndipo unakutana na taarifa za Corona, usingizi unakata kabisa unakuwa full awake!, hivyo kushuka na makala hii "Kwa Maslahi ya Taifa".

Hii ni thread ya swali tu linalohusu uzalendo na kutanguliza mbele maslahi ya taifa, nikiuliza, hivi mtu kama huyu ni binadamu mwenzetu au shetani? Anaombeaje ugonjwa wa Corona ufike nchini kwetu Tanzania ili kuikomoa serikali? Mtu kama huyu ni mzima kweli au ni mwendawazimu? Kuiombea nchi yako majanga, sio ni zaidi ya uendawazimu? Huu sio ushetani huu?!

Hivi kweli kuna Watanzania wenzetu wenye akili zao timamu kabisa, kwa vile wao sio CCM hivyo wana chuki ya ajabu na serikali ya Magufuli mpaka kufikia hatua ya kuiombea nchi yetu majanga kwa kuomba janga la ugonjwa wa Corona litue nchini mwetu ili kuikomoa serikali kwa kuona jinsi itakavyo kabiliana nalo?!

Corona ikija, atakayeteseka ni serikali au ni mwana CCM pekee?!

Swali hili ni kufuatia nilikuwa nafuatilia thread fulani humu JF, nikakutana na mchango wa ajabu sana wa mwana jf fulani

Korona ije kwanza ili serikali isipoteze rasimali kupambana na Chadema bora izo nguvu wazitumie kupambana na korona kukosa majanga ya kitaifa kunaifanya nchi kubweteka na viongozi kufanya mambo ya kipumbavu ugonjwa huu uje tuone investment yake.
Duh...!. Kweli is this what you wish for your beloved country Mama Tanzania?.

Huu sio zaidi ya uendawazimu? huu sio ni ushetani kabisa huu?

Pamoja na vitendo vya kiendawazimu na vya kishetani wapinzani wanavyotendewa na serikali yetu, kweli tumefikia kiwango cha Watanzania wenzetu kukosa utu na kugeuka wanyama kwa kuombea majanga yalikumbe taifa letu eti kwa sababu tuu kuna wendawazimu fulani serikalini wanafanya vitendo vya kiendawazimu na kishetani kwa wapinzani, hivyo sasa kuombea ushetani huu utokee kwa serikali yetu kuadhibiwa na janga la ugonjwa wa Corona? Hivi hii Corona ikiingia, atakayeathirika ni serikali ya CCM au ni Watanzania wote akiwemo mwendawazimu huyu?

Nasisitiza ule wito wangu wa siku zote kwenye hizi makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa", kwenye issues za kitaifa yakiwemo majanga mbalimbali, Watanzania tusimame pamoja kwa uzalendo, umoja, upendo na mshikamano na serikali yetu kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa, regardless political affiliations zetu, sisi Watanzania lets pray and stand as one against Corona.

Mungu tuepushie mbali hili janga la ugonjwa wa Corona.

Mungu Ibariki Tanzania.

Nawatakia Jumatatu Njema
Paskali
Updates.
IMG-20200317-WA0086.jpg

JF has impact, ukisikia taarifa ya serikali kuhusu mitandao ya kijamii, ujue ni jf.
Rejea
Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao huumba!

Uzalendo wa ajabu wa watanzania, unafurahije wakati nchi yako imepata majanga. Hawa ni ma nunda, ma sadist or what?

Rejea za Mandiko ya The Same Author Kuhusu Janga la Corona
  1. Mtu kama huyu ni binadamu au shetani? Anaombeaje Corona ifike Tanzania. Kuiombea nchi yako majanga, sio zaidi ya uendawazimu? Huu sio ushetani? - JamiiForums
  2. Corona: Japo ni janga, pia ni fursa. Tanzania bado hakuna maambukizi, tupunguze panic, tuongeze Elimu. WB kumwaga mihela, tuchangamkie fursa - JamiiForums
  3. Corona inatufundisha Tanzania tuna tatizo kuchanganya siasa na professionalism. Hongera Prof. Janabi kwa elimu uliyotoa, so far you are the best! - JamiiForums
  4. RC Makonda, Dar ni jiji la wote, vyama vyote. Mbowe sio mwanasiasa uchwara aliyefilisika, Zitto sio mshirikina. Tunakupenda, heshimu wote uheshimiwe - JamiiForums
  5. Je, ni kweli kuna Waziri anaugua Corona inafanywa Siri? Tunaficha nini? Hala hala kisa cha mficha maradhi! Truth & Transparency the only way out! - JamiiForums
  6. Star TV: Msemaji Mkuu wa Serekali, Dr. Hassan Abbas, azungumzia wajibu wa vyombo vya habari kuripoti janga la Corona - JamiiForums
  7. Ama kweli nabii hakubaliki nyumbani!. Je Magufuli ni nabii? Tanzania wanambeza, Afrika wanamlilia! Tanzania yapigiwa mfano Magufuli awe Rais wa Afrika - JamiiForums
  8. Vita Janga la Corona: Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas, Naibu Waziri wa Afya, Dr. Faustine Ndungulile, kesho watakuwa live JLNH-Star TV - JamiiForums
  9. Star TV: Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas na Naibu Wazuri wa Afya Dr. Faustine Ndungulile, Wanazungumzia Corona - JamiiForums
  10. Mungu ni Omnipresent. Kufuatia Local Transmission ya Corona. Je, Sasa Tushinikize Watu Wasalie Majumbani Mwao, ila Sadaka Ndio Itumwe Kwa M-Pesa? - JamiiForums
  11. Nabii Malisa: Mungu ameniambia Corona ni April tu, May hakuna Corona na hakuna atakayekufa!. - JamiiForums
  12. Kwa Kasi Sasa, Jee Tuendelee Ushujaa wa Ka-Corona, Tusitishane, Tuchape Kazi Tukiteketea, Au Sasa Tubadili Msimamo Tusitisishe Mikusanyiko Tuokoke? - JamiiForums
  13. TBC - Mjadala wa Role of The Media kwenye mapambano ya Corona, Je, Media Inatimiza Wajibu Wake Ipasavyo? - JamiiForums
  14. Live on Star TV: Corona Kushika Kasi Ndio Habari Kubwa Tanzania, Jee Media ya Tanzania, Inatimiza Wajibu Wake Ipasavyo? - JamiiForums
  15. Corona: Tusinyoosheane vidole. Kama unaweza kusaidia, please do. Usisubiri uombwe - jitokeze saidia, vinginevyo nyamaza! - JamiiForums
 
Najua P Mayalla una lengo la kuwa expose wengi zaidi. Hujaacha kile ulichomfanyia Kabendera.

Lengo lako ni comments kama hizo zitiririke hapa upeleke file huko.

Una roho mbaya sana, ila watu tu hawakujui.
 
Kwahiyo wew ulitakaje, serikali yako iendelee kutesa upinzani na kuwavunja mikono.. Si bora uje ili hao police na serikali yako iogope kuwashika upinzani na ipambane na corana na ikiwezekana watu Wa ccm waupate huo ugonjwa ili waache kuwatesa na kuwavunja mikono wapinzani.. Tena na wewe ulivyo mnafiki uupate ili uache unafiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
For people who like data:

82,000 People are sick with Coronavirus at the moment,
of which 77,000 are in China.
This means that if you are not in or haven't recently visited China, this should eliminate 94% of your concern.

If you do contract Coronavirus, this still is not a cause for panic because:
81% of the Cases are MILD
14% of the Cases are MODERATE
Only 5% of the Cases are CRITICAL

Which means that even if you do get the virus, you are most likely to recover from it.

Some have said, “but this is worse than SARS!”. SARS had a fatality rate of 10% while COVID-19 has a fatality rate of 2%

Moreover, looking at the ages of those who are dying of this virus, the death rate for the people UNDER 50 years of age is only 0.2%

This means that:
if you are under 50 years of age and don't live in China - you are more likely to win the lottery (which has a 1 in 45,000,000 chance)

Let’s take one of the worst days so far, the 10th of February, when 108 people in CHINA died of Coronavirus.

On the same day:
26,283 people died of Cancer
24,641 people died of Heart Disease
4,300 people died of Diabetes
Suicide took 28 times more lives than the virus did.

Mosquitoes kill 2,740 people every day, HUMANS kill 1,300 fellow humans every day, and Snakes kill 137 people every day.
 
unataka kumsemelea huyu kama kabendera?
Wanabodi

Japo kwa kawaida usiku ni wakati wa kulala na kupumzika, ila kwa watu ma jobless wakiwemo kada yangu ya watu wa "mishe mishe", moja ya usiku ngumu sana, huwa ni usiku wa Jumapili kuamkia Jumatatu ambayo umeipitisha weekend kwa mazabe mazabe, halafu blue Monday inakuja!, usingizi huwa unakata mapema sana, by saa 9:00 usiku, usingizi umekata, hivyo huna jingine lolote la kufanya zaidi ya kushuka JF, ndipo unakutana na taarifa za Corona, usingizi unakata kabisa unakuwa full awake!, hivyo kushuka na makala hii "Kwa Maslahi ya Taifa".

Hii ni thread ya swali tuu linalohusu uzalendo na kutanguliza mbele maslahi ya taifa, nikiuliza, hivi mtu kama huyu ni binadamu mwenzetu au shetani?. Anaombeaje ugonjwa wa corona ufike nchini kwetu Tanzania ili kuikomoa serikali?. Mtu kama huyu ni mzima kweli au ni mwendawazimu?. Kuiombea nchi yako majanga, sio ni zaidi ya uendawazimu?. Huu sio ushetani huu?!.

Hivi kweli kuna Watanzania wenzetu wenye akili zao timamu kabisa, kwa vile wao sio CCM hivyo wana chuki ya ajabu na serikali ya Magufuli mpaka kufikia hatua ya kuiombea nchi yetu majanga kwa kuomba janga la ugonjwa wa Corona litue nchini mwetu ili kuikomoa serikali kwa kuona jinsi itakavyo kabiliana nalo?!.

Corona ikija, atakayeteseka ni serikali au ni mwana CCM pekee?!.

Swali hili ni kufuatia nilikuwa nafuatilia thread fulani humu jf, nikakutana na mchango wa ajabu sana wa mwana jf fulani


Duh...!. Kweli is this what you wish for your beloved country Mama Tanzania?.

Huu sio zaidi ya uendawazimu?, huu sio ni ushetani kabisa huu?.

Pamoja na vitendo vya kiendawazimu na vya kishetani wapinzani wanavyotendewa na serikali yetu, kweli tumefikia kiwango cha Watanzania wenzetu kukosa utu na kugeuka wanyama kwa kuombea majanga yalikumbe taifa letu eti kwa sababu tuu kuna wendawazimu fulani serikalini wanafanya vitendo vya kiendawazimu na kishetani kwa wapinzani, hivyo sasa kuombea ushetani huu utokee kwa serikali yetu kuadhibiwa na janga la ugonjwa wa Corona?. Hivi hii Corona ikiingia, atakayeathirika ni serikali ya CCM au ni Watanzania wote akiwemo mwendawazimu huyu?.

Nasisitiza ule wito wangu wa siku zote kwenye hizi makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa", kwenye issues za kitaifa yakiwemo majanga mbalimbali, Watanzania tusimame pamoja kwa uzalendo, umoja, upendo na mshikamano na serikali yetu kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa, regardless political affiliations zetu, sisi Watanzania lets pray and stand as one against Corona

Mungu tuepushie mbali hili janga la ugonjwa wa Corona.
Mungu Ibariki Tanzania.

Nawatakia Jumatatu Njema
Paskali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je anayeua watanzania kama sisimiZi kwa kuwapoteza, risasi etc unamsemaje? Wanatofauti gani na Corona, maana essense ni kupoteza uhai wa watanzania. Huyu anawaua kwa risasi, kuwapoteza etc. Huyu anawaua kwa corona, si wote ni mashetani? wauaji? Pascal, nitakusema siku zote maana una akili kidogo nowadays!
 
Binafsi ninapinga sana wanaombea kwamba Corona iingie nchini. Maana si jambo la kuchukulia poa.
Jambo la kujiuliza inakuwaje watu wafikie hali hiyo? Ukiacha wanaoombea Corona, kuna wale wanaoombea vita itokee, yaani nchi yetu ivamiwe na ipigwe. Matukio ya maafa kwa miaka mingi yamekuwa yakiwaunganisha watanzania na kujikuta wakiweka kando tofauti zao za aina yoyote ile.

Tumeona sasa hivi hata askari wetu wakipigwa ambush na kuuawa huko nje badala ya wengi wetu kushikwa na majonzi na kuombeleza, hali huwa kinyume chake, wengil hushangilia na kuhisi Mungu ameingilia kujibu 'maombi'.

Kwa hadhi yako Pascal Mayalla ulipaswa ujiulize na kulaumu beyond this point. Sasa hivi taifa siyo moja tena, taifa limesambaratika na mioyoni watu hawapo nalo, kuna watu wametufikisha hapa ni wakina nani hao? Kwa nini? Ili iweje? Nini kifanyike?

Kwa hali iliyopo Petrol imeshamwagika na kusambaa kote, akipita mwendawazimu na kipisi cha sigara yenye moto na kutupia au akawasha kiberete au akasababisha msyguano wowote ule basi Tanzania itakuwa imeshaanza rasmi safari ya kuzaliwa upya.
 
Back
Top Bottom