Sasa hata kwa sisi wanawake tukipata wanaume waaminifu na wapole tunaanzaje kuwa wajeuri na wakorofi?Sasa mke kama Madam S unaanzaje kumsaliti aisee, mtoto anajua nini kitu mapenzi namna hio. Hapo mida ya jiji letu tu nipo mjengoni yani nacheza na mdoli wangu.
Kwani mimi naitafsiri vipi na wewe unaitafsiri vipi? Hebu naomba nifafanulie."mgawanyo wa majukumu" hii line unaipenda sana ila jinsi unayoitafsiri huwa napatwa na bumbuwazi.
Uamuzi upi sasa hebu nisaidie? Siwezi kuchukua uamuzi wowote kwa sababu kwa wakati huo anakuwa hana matatizo hivyo anakuwa hahitaji msaada wangu ila namsubiri siku akipata matatizo na kuhitaji msaada wangu ndipo nitamuomba aende kwa huo mchepuko wake ukampe msaadakwanini na wewe usichukue uamuzi sahihi mapema pale unapoona unanyanyasika sababu ya hela zake na badala yake unakaa unavumulia manyanyaso weweeee, halafu siku akiingia matatizoni ndio unaona ni wakati wako wa ku retaliate unavyojua wewe?
Oh, Sasa hili litakuwa nje ya mada kidogo mana hapa tunaongelea tabia ya kukomoana na kuto kutiana moyo kipindi cha hali ngumu ya maisha.
Ok kwa hilo siwezi kutetea hilo ni kosa na kwa nionavyo Mimi sio sahihi, kwasababu hakuna mtu asiye fanya kosa, mwanamke anapaswa kumheshimu mume na kumtii lakini si kuwa mtumwa kwa mume, mwanaume anapaswa kumpenda mkewe, kumpenda mtu Kuna maana kubwa sana ikiwa ni pamoja na kumheshimu na kumjali, kwa hivyo huwezi mfanya awe mtumwa kwako kwa kumfanyia mabaya kwa makusudi.
Iliposemwa uishi na mke kwa akili ilikuwa ni pamoja na kutambua majukumu yako kama mwanaume lakini pia uwe kiongozi kwa huyo mwanamke na familia yako kwa ujumla ndio maana ikasemwa kuwa mume ni kichwa cha familia.
Note, hili linawezekana kwa mwanamke anayekubali kuongozeka lakini kwa mwanamke mshindani halita wezekana.
Mhh ' na wewe leo unataka kuni 'nywesha chai?Sio kweli.
Tangu mwanzo nilikwambia kuwa usipende sana kujihesabia haki na kuwaona wanaume kuwa ndio chanzo cha matatizo. Unaposema wanaume wa siku hizi unatakiwa kukumbuka pia Kuna wanawake wa siku hizi, sijui kama unajua hilo?Hakuna mwanamke anayefurukuta mbele ya mwanaume mwenye sifa hizo ulizozielezea labda awe karogwa ila sasa ndo ujiulize ni wanaume wangapi wenye sifa hizo ulizozielezea? Ukishapata jibu ndo utajua kwanini wanawake wengi wa sasa wapo hivi walivyo
Mimi nadhani vitu vingine msitulaumu sana wanawake ila mjichunguze kauli na tabia zenu hasa wanaume wa siku hizi yaani siku hizi hakuna mapenzi tena ni tamaa na utapeli tu kwa kwenda mbele na haya mambo walianzisha wanaume sasa kwanini na wanawake waendelee kukubali kuwa victims wa haya maovu kila siku?
Sawa nimekuelewa!Tangu mwanzo nilikwambia kuwa usipende sana kujihesabia haki na kuwaona wanaume kuwa ndio chanzo cha matatizo. Unaposema wanaume wa siku hizi unatakiwa kukumbuka pia Kuna wanawake wa siku hizi, sijui kama unajua hilo?
Mwanaume anapokutana na mwanamke wa siku hizi, hatakubali heshima yake kama mwanaume ipotee lazima atatafuta namna ya kumuadabisha huyo mwanamke ili kurudisha heshima yake.
Na mwanamke akikutana na mwanaume wa siku hizi kama mwenyewe unavyowaita basi lazima atateseka hata kama tabia yake ni nzuri.
Lakini pia wanaume bado na wanawake wanaoa jitambua wapo wengi tu ndio maana wakati wengine wakilalamika kuna wengine huku mitaani wazeeka pamoja sasa na ndoa zao.
Narudia tena,mwanaume atambue majukumu yake, na mwanamke pia akubali kuongozeka asiwe mshindani hapo watafika mbali.
Co km shda n kuhudumia....shda n pale mambo yakienda kombo....mishe haziwezi kunyooka siku zoteSaa kama huwezi kuhudumia mke kwa nini uoe?
Heheh mtu anajichepusha afu ategemee akipata shida nimtie moyo subutuu...Wanaume vipi ninyi huwa mnawatia moyo wake zenu wakiwa katika nyakati ngumu maana naona mnalalamika sana.
Inategemea na wewe huwa unanicomfort vipi mda nikiwa na shidaStephen King ,mtu maarufu kwa uandishi wa Vitabu duniani aliwahi kukataliwa Kazi zake Mara nyingi.
Aliwahi kwenda kwa wachapishaji (Publishers) wa Vitabu 30 wakikataa Kazi zake kwamba hazikuwa na ubora .
Hali hii ilimfanya aanze kukata tamaa na mafanikio.
Akiwa katika hali ya kukata tamaa aliambiwa neno kubwa na mke wake " *Mume wangu ,tusikate tamaa tuendelee kutafuta wachapishaji wengi ipo Siku tutafanikiwa tu* "
Kutokana na hilo neno la mke wake lililomtia nguvu na ujasiri aliendelea kutafuta hatimaye akapata.
Stephen King ameandika vitabu 58 na stori fupi zaidi ya 200 .
Stephen King ameshauza nakala za vitabu milioni 350 duniani mpaka sasa .
Tafiti zinaonesha kwamba Stephen King ni tajiri wa 5 katika waandishi wa vitabu duniani mwaka 2019 , akiwa na dolla million 400.
Hakika hakuna safari isiyo na changamoto katika maisha isipokuwa lazima uangalie aina ya mtu unayesafiri naye.
Mke wa Stephen King alimwambia mume wake hivi akafanikiwa
[emoji1377]
*Mume wangu ,tusikate tamaa tuendelee kutafuta wachapishaji wengi ipo siku tutafanikiwa tu*
Je, mke wako anakwambiaje unapokwama , mume wako anakwambiaje ukikwama ? Ndugu, jamaa na rafiki zako wanakwambiaje ukikwama?
Hakikisha unasafiri na mtu anayeona matatizo kwa jicho la mafanikio.
*You're the Sperm that won the race*
#Nanauka
Kweli, heko zake mama...Kimsingi amezaa mtu kweli kweli. Najiskia raha napoona hekima zako kupitia comment unazotoa humu. Wapo watakaojifunza kupitia wewe naiman.Hapana siombi hata kubadilika na the way nilivyo na ninavoishi najiona nina amani siwez kua mwengine kwa kweli na unavoniona hivi ni mama yangu mtupu
Ni kweli kabisa.tupoo sema nyi mna vigezo vya macho zaidi ndomana......POLENI.
Mkuu umewahi kumsoma mara ngapi huyu bibie Madame S ??? Believe me humu kuna wanawake wako njema sana sana sana!et "mpo" ... nyie wanawake wa jamiiforum ambao kila muda tunawasoma humu na mentality zenu za ovyoo sijui mambo yakienda mrama ndani ya familia mume ndio chanzo!! kuwa na aibu hata kama tunatumia fake ids
You are one of the best!Hiyo ni mentality umejiekea siwez kukubadili
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣ahahahaha.... nimecheka sana bro!
wao wamemsajiri Edelyn sisi hatujasajiri mtu na tunaenda nao tit for tat..hahaha.
Mkuu ni kweli hayo yapo ila si kwa wote. Tuepuke ku-generalize vitu kwa kweli. Wapo wanawake very smart in here ndugu yanguNyie wanawake wa humu kila Leo tunasoma comments zenu jinsi mnavyoyachukulia mahusiano na hasa kuhusiana na situation anayoelezea mleta mada, wengi mnafanana kimaono.
Sikumbuki ni mara ngapi nimesoma huu mstari "ukiona mambo hayaendi vizuri ndani ya ndoa/mahusiano basi ujue mwanaume ameshindwa kusimama vizuri kwenye nafasi yake"
Sasa kwa mwanamke mwenye mawazo kama haya saa ngapi atakuwa na akili ya kumu encourage mume wake pale anapoanguka!?? sana sana si atamkimbia tu huku akimshtumu kuwa ameshindwa kuwa mwanaume ndio maana akaanguka eboo acha unafiki binti.
Heaven Sent pia????Ha ha ha hio list ya #TeamPasuaKichwa balaa! Kocha mchezaji Heaven Sent
Mmh, kama kuna wanaume wanalizwa basi ni aina ya Ben Pol. Mwanamke wa kibongo akipata mtu mpole kama Ben anaanza vituko vya abuja yani. Mara ajiskilizie mara kiburi kiburi ilimradi tu kero. Mwishowe huwa wanasaliti penzi maana ukiwa mpole mwenye mapenz mwanamke wa kiswahili anakuona kama Zoba tu au zezeta. Wengi hawanaga tabia ya ku appreciate upendo.Sasa hata kwa sisi wanawake tukipata wanaume waaminifu na wapole tunaanzaje kuwa wajeuri na wakorofi?