Hii habari nilishawahi kuisikia mahali, watu wanapeana tahadhari kutokubali kuwapa coins watu wasiowajua vyema. Pengine kuna substance ndani yake.
2014 nikiwa Mtwara, nilizunguka karibu maduka yote jion kutafuta chumvi nikatoka hola. Bahati nikakitana na mtu mtu wa kuja kwenye huo mji akaniambia ukisema chumvi jioni hakuna mtu atakayekupa hata ufanyeje.
Nikarudi nilipotoka, nikasema naomba DAWA YA JIKO fast nikapewa chumvi.
Mtwara na Lindi huko ndo kuna mafundi kwelikweli, kama mtu haamini haya mambo aende akaseme huko mbele zao haamini ndo ataelewa. Wala Sitanii