Kuhusu Ibada ya Sanamu. Kabla uvumilivu haujanishinda nikakushushia Misumari ya moto. em eleza wewe Mwenyewe:
1. Lile Jiwe pale Ka'aba mnalobusu la kazi gani?.
2.Dunia nzima mnaelekeza vichwa huko..Mungu yupo Arabuni peke yake?
3. Alama ya Mwezi na Nyota ya kazi gani misikitini?.
Make sure you're Smart.
4. Kulingana na ibada za Mungu Baali( Hubaal) za waquraish alikua na alama hiyo ya Mwezi.
Eleza mwenyewe tofauti ya allah na huyu Allah baali.
Be brief. Tafadhali.
NB: Sitaki povu wala gazeti.
Ubatizo
Hii pia ni ibada kuu na ya msingi katika dini ya Kikristo ambayo hata watoto wachanga nao huusishwa nayo pia!
Kwa ujumla wake, ibada hii (ya ubatizo) imeshamiri sana katika Ukristo.
Hata hivyo, pamoja na kuwemo katika orodha ya ibada za Kikristo, lakini kwa mujibu wa maelezo ya Biblia tukufu, asili ya ibada hiyo (ya ubatizo) imetokana na dini ya kipagani.
Uthibitisho wa hayo tunaupata katika maelezo ya Biblia yafuatayo:
"Ibada ya (ubatizo) kutosa mwili majini ni mfano wa utakaso au wakujitengeneza upya. Ibada kama hiyo ilijulikana na kutendeka katika dini za kale za kipagani na dini ya Kiyahudi pia (kama ubatizo wa waongofu Mdo 2:10; Waesseni)'. (Tazama Biblia ya Wakatoliki, Imprimatur M. Mihayo Archbishop of Tabora, February, 1967, kwenye maelezo ya Mathayo 3:6 uk. 879).
Maelezo hayo ya Biblia hapo juu yanathibitisha wazi kwamba ibada hiyo ya ubatizo inatokana na dini za kale za kipagani na kamwe haitokani na dini ya Yehova.
Nasema ibada hiyo (ya ubatizo ya kipagani) katu haitokani na Yehova, kwa sababu tangu mapema Yehova alikwishawakataza na kuwaonya wanadamu kutenda ibada yoyote (kama hiyo ya ubatizo) ya watu wa mataifa (yaani wapagani) kama asemavyo (Yehova) katika maandiko yafuatayo:
"Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako, usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale". (Kumbukumbu la Torati 18:19).
BWANA, Mungu wako, atakapoyakatalia mbali hayo mataifa mbele yako, huko uingiako kuyamiliki, nawe ukawatwaa, na kuketi katika nchi yao, ujiangalie, usije ukanaswa ukawafuata, wakiisha kuangamizwa mbele yako, wala usije ukauliza habari za miungu yao, ukasema, mataifa haya waitumikiaje miungu yao? Nami nifanye vivyo". (Kumbukumbu la Torati 12:29-30)
Kulingana na maandiko hayo juu, hapo Yehova kwa ujumla anawataka wanadamu wajiepushe mbali kabisa na ibada ya watu wa mataifa au wapagani.
Na kwa kuwa Biblia tukufu inakiri kwamba ibada ya ubatizo ni ya kipagani, ni dhahiri kuwa ibada hiyo nayo i miongoni mwa machukizo kwa Yehova ambayo hataki wanadamu kuyatenda.
Pamoja na makemeo hayo ya Yehova dhidi ya yeyote anayetenda ibada za watu wa mataifa au wapagani (kama hiyo ya ubatizo), lakini muasisi wa Ukristo, Bwana Paulo kwa kuwa tangu mapema alidhamiria na hatimaye kuamua kufuata mia kwa mia dini ya kipagani, alisema kama ifuatavyo kuhusu ibada hiyo ya ubatizo:
"Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima". (Warumi 6:3-4).
"Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja". (1Wakoritho 12:13).
Kwa uchache, anachokiri Bwana Paulo katika maelezo yake hayo juu ni kwamba, yeye binafsi pamoja na wafuasi wake wote (Wakristo) huifanya ibada hiyo (ya ubatizo). Kwa lugha nyingine anakiri kwamba ibada hiyo imo katika orodha ya taratibu za dini yake ya Kikristo.
Miaka 36 mpaka 45 baada ya Paulo kuifundisha ibada hiyo (ya ubatizo), waandishi wa Agano Jipya nao katika kuuandikia Ukristo wa 'mwalimu wao' (Paulo), walisherehesha mafundisho yake hayo (ya ubatizo) ambayo wamethubutu hata kutunga katika Injili zao kuwa Bwana Yesu naye eti aliwahi kutenda ibada hiyo ya kipagani kwa kubatizwa na Yohana katika mto wa Yordani! (Tazama Mathayo 3:13-17; Marko 1:9-11; Luka 3:21-22; Yohana 1:31-34).
Nasema waandishi hao (Wainjilisti) wametunga kwa kuwa kama tulivyoona Biblia tukufu ielezeavyo kwamba ibada ya ubatizo imetokana na dini za kale za kipagani, ni dhahiri kuwa Nabii Yesu na Nabii Yohana kamwe hawawezi kutenda ibada potofu za wapagani (kama hiyo ya ubatizo) ambazo zimekemewa vikali na Yehova aliyewatuma (rejea Kumbukumbu la Torati 18:9).
Na hata ukiyasoma masimulizi ya waandishi hao juu ya nadharia hiyo ya Yesu na Yohana kubatizana, licha ya maelezo yao kutofautiana na hivyo kutojua ni mwandishi gani anayeelezea kiusahihi, bado utaona kuna utata mkubwa na wa kimsingi wa kutendeka kwa tukio hilo.
Kwa mfano, waandishi hao wamesimulia kuwa ubatizo wa Nabii Yohana (a.s.) waliouelezea kuwa ni wa maji, ulikuwa ni kwa ajili ya utakaso wa kumwondolea mtu dhambi (tazama Marko 1:4-5).
Kwa shuhuda hiyo, waandishi hao wasingeonekana kuwa wanasherehesha ibada ya Paulo (ya ubatizo) iwapo wangetusimulia katika Injili zao kuwa Nabii Yohana (a.s.) alipombatiza Yesu (a.s.) Yehova alisahau kumjulisha kuwa ubatizo wake haukumstahili Yesu kwa kuwa (Yesu) hakuwa na dhambi (tazama Yohana 8:45-46).
Aidha, kauli inayosimuliwa na waandishi hao kutolewa na Nabii Yohana (a.s.) akimshangaa Yesu (a.s.) alipomjia hapo katika mto wa Yordani ili ambatize kwa kumwambia: " Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?", Kisha Yesu (a.s.) eti akamjibu Yohana (a.s.) na kumwambia: "Kubali hivi sasa, kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote" (Mathayo 3:13-14), inaonyesha Yesu hapa akipinga wazi maelekezo ya Nabii Yohana (a.s.) jambo ambalo kamwe haliwezi kufanywa na Yesu (a.s.) kwani Yesu (a.s.) anajua wazi kuwa Nabii yoyote wa kweli (kama Yohana) hasemi neno ila ni wahyi (ufunuo). (Tazama 2 Petro 1:21).
Aidha, kumpinga Nabii kama Yohana (a.s.), Bwana Yesu (a.s.) anajua pia kuwa ni kukiuka ile ahadi yake kwamba: "Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua Torati wala Manabii..." Tazama Mathayo 5:17-19)
Kwa upande mwingine wa masimulizi ya waandishi hao, yaonyesha kwamba, kumshangaa kwake kule Yesu (a.s.), Nabii Yohana (a.s.) hakujua alitendalo hata ikabidi Yesu amkosoe kwa kupinga maelekezo yake (Yohana) yale! Jambo ambalo siyo kweli. Kwani Nabii kama Yohana kamwe hawezi akathubutu kutoa maelekezo ya uongo kama hayo anayodaiwa (katika masimulizi ya waandishi hao) kuwa eti alisema kwamba "alitakiwa Yesu ndiye ambatize yeye (Yohana) na kukosolewa kwa kupingwa vikali na Yesu!
Kwa uchache, huo ndio utata wa kimsingi unaotia shaka kuwepo (kutendeka) kwa tukio la kubatizana Yesu na Yohana (a.s.) katika mto wa Yordani kama isimuliwavyo na waandishi wa Agano Jipya katika Injili zao.
Tukiachilia mbali utata huo, jambo la kuzingatia ni kwamba ibada hiyo (ya ubatizo) kama Biblia ielezavyo imetokana na wapagani.
Kwa shuhuda hiyo ni dhahiri kuwa Bwana Yesu (a.s.) na Nabii Yohana (a.s.) kamwe hawawezi kutenda ibada hiyo kwa kuwa ni ibada ya kipagani ambapo Yehova aliyewatuma amewakataza wanadamu kutenda ibada zote za wapagani.
Na ni wazi kuwa Wakristo kutenda ibada hiyo ni uthibitisho kuwa hawamwabudu Yehova, Mungu wa Nabii Ibrahimu, Ismaili, Isaka, Yakobo, Muhammad na Manabii wengine wote.