Kung'ang'ania kifo cha Yesu ni uoni finyu
HAKUNA aya hata moja ya Biblia inayomtaja mtu yeyote aliyeona sura ya Yesu hasa wakati akifa pale msalabani.
Yesu alidhaniwa tu kuwa ni Yesu aliyeuawa msalabani, lakini baada ya siku chache Yesu huyo akaonekana yu hai, wala hakurudi kama pepo (ghost)! Kung'ang'ania kuwa ni Yesu aliyeuawa pale msalabani ni utani mgonjwa, hususan tukizingatia ushahidi wote huo hapo nyuma, vipofu na hata kuwafufua watu.
Kwa upande mwingine twaambiwa eti kumtesa Yesu kwa kumpiga, kumchoma kwa ncha kali, na kumpigilia misumari mtini eti ilitosha kumuuwa Yesu.
Hii haiingii akilini kimantiki labda kwa kuiamini tu kiupofu (blindly).
Isitoshe, Yesu angalisubuliwa kweli, ingekuweko aina moja tu ya msalaba aliouliwa. Lakini Catholic Encyclopaedia peke yake ina aina 40 za misalaba.
Kwa sababu zisizo dhahiri, msalaba ule wa vipande viwili vinavyosigana yaani +, ndio umependelewa zaidi na Waingereza wakauita "Cross", ingawa neno la awali la msabala kwa Kigiriki ni "Stauros" ambalo halina dhana ya vipande viwili ila kimoja tu.
Biblia chache tu kama ile ya Mashahidi wa Yehova ndio imetaja waziwazi kuwa Yesu aliangikwa kwenye mti (stauros) na usulubisho kwao wao sio "cricifixion" bali "stafixion".
Dhehebu jingine limesema Yesu aliangikwa kwenye mti wenye umbo la T. Ke bado Wakristo wengine wanauabudu msalaba huo wa alama ya kujumlisha +.
Gazeti la Newsweek la Aprili 4, 1994 liandika: "Kifo cha Yesu - Fikra mpya za siku zake za mwisho". Limesema kuwa, kama Yesu kweli aliuliwa msalabani, basi lazima iweko aina moja tu ya msalaba.
Katika gazeti hilo hilo, Padri wa Kikatoliki Raymond Brown kaandika kitabu chake, "The Death of the Messiah (Kifo cha Masihi)". Doubleday na wanaseminari wenziwe 2000 amesema kuwa hadithi za Yesu kuhusu kuhubiri, kuponya wagonjwa, kufanya miujiza, hizo zaweza kuwa kweli; lakini hadithi nyingine (kama ya kusulubiwa Yesu) hazina usahihi wa kihistoria (historical accuracy).
Hii anasema ni kwa sababu waandishi wote wa Injili hawakuwa mashahidi wa macho (eye witnesses) kushuhudia hata moja ya yale wayoyaandika mnamo miaka 35-70 baada ya Kristo; na mpaka leo hatuna hakika ni nani hasa aliyeandika Injili zote hizo, ambazo kila inatofuatiana na yenzie.
Yesu asingekosa kutabiri kuuliwa kwake msalabani, akatabiri juu ya kuteswa tu:
"Mt 23:35 Hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habil, yule mwenye hakika hata ... Zakaria ... mliyemuua kati ya patakatifu".
"Lk 22:15 ... Nimetamani sana kula pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa