[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
YESU HAWEZI KUWA KAFARA :
Jambo la mwisho lakini la maana ni kwamba Yesu angewezaje kuzaliwa akiwa hana dhambi ilhali alikuwa na mama wa
kibinadamu?
Kama dhambi ya Adamu na Hawa ilikwisha kichafua kizazi cha hao wawili wenye bahati mbaya, basi matokeo yake ni kwamba wazao wao wote wa kiume na wa kike walirithi maelekeo ya kufanya dhambi katika kuzaliwa kwao.
Labda wanawake wakarithi zaidi shauku ya kutenda dhambi kwa sababu Hawa ndiye aliyetumiwa na shetani ili kumbembeleza Adamu kutenda dhambi.
Kwahiyo, Hawa anahusika na dhambi moja kwa moja kuliko pengine Adamu.
Katika habari ya kuzaliwa Kristo, binti wa Hawa alihusikana zaidi. Swali linalozuka kwa nguvu sana ni kwamba je, Yesu alirithi kromosom zenye vijine, (genes) kutoka kwa mamake binadamu ama hapana?
Kama ndiyo, hapo haikuwezekana kwa Yesu kuepukana na dhambi ya lazima ya kurithiwa. Kama hakuirithi kromosom yoyote kutoka kwa mamake wala kwa Mungu Baba, hapo kuzaliwa kwake kutakuwa mwujiza maradufu. Mwujiza pekee yake unaweza kuzalisha mwana asiyehusikana na baba yake wala mamake.
Jambo lisiloeleweka ni kwamba kwa nini kromosom za Hawa hazikumtilia mwanaye Yesu maelekeo ya kiasili ya kutenda
dhambi. Tukidhani kwamba ilikuwa hivyo kwa vyovyote na Yesu alikuwa safi asiye na dhambi - jambo ambalo ni lazima ili
kujichukulia dhambi za wanadamu sharti wamwamini, hapo swali jingine litazuka: Walikuwaje, mtu aweza kuuliza, waliokufa
miongoni mwa wazao wa Adamu na Hawa kabla haujafika Ukristo?
Mabilioni mangapi ya watu hao waliwahi kutawanyika duniani kote katika mabara matano kizazi baada ya kizazi.
Lazima waliishi na wakafa pasipo kutumaini bali pasipo uwezekano wa kusikia habari ya Kristo, Mwokozi wao, ambaye alikuwa
hajazaliwa.
Kwa hakika wanadamu wote waliokuwapo baina ya Adamu na Kristo wanaonekana waliangamia kwa kudumu. Kwa nini hao hawakupewa nafasi walau hafifu sana ya kusamehewa?
Je, hao watasamehewa na Yesu Kristo kwa kutumia kanuni ya kafara kwa waliopita kabla ya kanuni hiyo kuundwa?
Kama ndiyo, kwa nini?
Katika sehemu nyingine za dunia zilizo kubwa zaidi kuliko Uyahudi ilivyo ndogo sana, haikupata kusikika habari za Ukristo hata katika zama za uhai wa Yesu Kristo; watu hao watakuwaje?
Maana hawakuamini 'Uana' wa Yesu Kristo wala hawangeweza.
Je, wataadhibiwa kwa madhambi yao ama hapana na kwa hoja gani? Walikuwa na nafasi gani kwa vyovyote? Walikuwa hoi
kabisa. Maana mbovu iliyoje hiyo ya Uadilifu!