Sijajua kama ulikuwa unaniuliza unataka nikujibu au unatoa ufafanuzi [emoji1745]
Wafanyabiashara wa Madini na yule Dreva Tax wote waliuawa kwa kupigwa Risasi tena za SMG,Askari wote 11 waliokuwepo kwenye tukio lile ilionekana siku ya tukio ni Silaha moja tu SMG ya Koplo Saad Ally ndio ilitumika(actually namfahamu sana maana tulikuwa nae pale Oysterbay).
Maana unapoingia kazini kama unabeba SMG maana yake unapewa na Risasi zake 30 kwenye Magazine,na kama unabeba Bastola(Chinese Pistol)maana yake unahesabiwa na Risasi zake 8. Wale Askari walipomaliza zamu na kurudisha Silaha na Risasi,Askari wote walirudisha Silaha na Risasi zikiwa sawa isipokuwa Koplo Saad tu ndie ambaye alirudisha Risasi pungufu hivyo aliandika maelekezo kwa nini amerudisha Risasi pungufu na pia kwenye Armoury Register(Kitabu cha Makabidhiano ya Silaha na Risasi)taarifa hiyo iliandikwa(Mahakamani Kitabu kile kilikuwa sehemu ya vielelezo upande wa Mashtaka). Ndio maana Jaji aliwaachia Huru watuhumiwa wote na akawaambia upande wa Mashtaka wamlete Koplo Saad maana hakuwahi kukamatwa mpaka leo na ndie ambaye Silaha yake ilitumika.
Upande wa Mashtaka ulipokuja kukata Rufaa ndio Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya(OC CID Christopher Bageni)akaangukiwa na jumba bovu akahukumiwa Kunyongwa. Na hata alipokata Rufaa bado Majaji wakatupilia mbali Rufaa yake hivyo yupo Jela mpaka leo.
Sababu ya Bageni kukutwa na Hatia na Majaji wa Mahakama ya Rufaa ni kwa kwamba yeye ndie alikuwa Incharge wa Upelelezi Wilaya hivyo mtiririko mzima wa tukio hilo alikuwa anaujua hivyo alikuwa na uwezo wa kuzuia Mauaji yale lakini hakufanya hivyo maana mpaka Mabwepande alienda na kile Kikosi kukamilisha Mauaji. Zombe kama Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa alikuwa anapewa taarifa tu na Bageni na hakuwepo eneo la Mauaji.
Hivyo kitendo cha Mhusika Mkuu aliyefyatua trigger kuua wale jamaa wanne kutokuwepo Mahakamani ndio ikawa pona ya wengine.
Kuhusu kifo cha Rashid Lema akiwa Mahabusu ni kwamba yeye aliona kama kukamatwa alionewa maana hakuhusika,hivyo kwenye ile Tume iliyoundwa alinyoosha Maelezo A to Z kama alivyonyoosha huyu Daktari na yule A/Inspekta aliyefia Mahabusu. Hivyo kwa vyovyote mnavyokuwa na tatizo watu watano kwa mfano,ni lazima mkae mpangane nini cha kuongea,lakini inapotokea mwenzenu anakuwa tofauti na nyie maana yake anataka kuwachoma,hivyo mwisho wa siku lazima nae mumpoteze tu.
Ninategemea kwenye Kesi hii huyo Daktari atanyoosha maelezo A to Z maana haya ushahidi wa huyo ACP Mgonja umeegemea kwenye maelezo waliyoyapata kutoka kwa huyo Daktari na yule Askari aliyefia Mahabusu.
Kesi hii labda hao Watuhumiwa wote wakane kuhusika akiwemo huyo Daktari akane maelezo ambayo huyo Shahidi ACP Mgonja anadai aliambiwa na Daktari. Kisha wote wamuangushie jumba bovu Marehemu Askari aliyefia Mahabusu kwamba ndie aliyeua. Lakini hapohapo huyu Gilbert ndie alikuwa na Cheo kikubwa kuliko wote,swali ni kwa nini alishindwa kuzuia Mauaji hayo kama Incharge??
Anyway,Kesi ni nzuri,tusubiri tuone
Nadhani ulianza kufuatilia suala hili baada ya kuanza kesi, pengine huna story ya moja kwa moja kabla ya kesi kwenda mahakamani.
Nasema hivi kutokana na story yako kwa DC Lema. Kwamba alionewa kukamatwa, wakati yeye alijisalimisha mwenyewe.
Ni kwamba, Lema ndiye aliyeendesha gari iliyopeleka miili ya waliuawa kwenye chumba cha kuhofadhia maiti, Muhimbili.
Lema ndiye aliyetoa ushahidi mzito uliofanya ACP Zombe aingizwe kwenye kesi na kuwa mshitakiwa namba moja.
Ilikuwa hivi,
Tukio lilitokea wakati Zombe akikaimu nafasi Kanda Maalum, wakati ambao Tibaigana alikuwa likizo. Yakatokea ya kutokea.
Zombe akaibuka na press akisema marehemu walikuwa majambazi. Na kwa wakati huo CPL Saad Alawi na DC Rashid Lema walishatoroka.
Saad aliwafyatulia risasi na Lema alipeleka miili Muhimbili. Baada ya kelele nyingi, Rais Jakaya Kikwete akaunda tume.
Tume iliongozwa na Jaji Ramadhan Kipenka, na ikatangaza kwa umma mwenye ushahidi aende nao. Hadi wakati huo Zombe yuko uraiani.
Lema alienda kwao Arusha, na huko akasimulia wazazi wake. Kutokana na uchamungu wa wazazi wakagoma kumwelewa.
Wakamshinikiza akatoe ushahidi kwa tume ya Kipenka. Ndipo hapo kila kitu kwenye kesi kikabadilika, alinyoosha kama huyo daktari wa Mtwara.
Na msingi wa kesi uliundwa zaidi kwa ushahidi wa Lema, kama ya Mtwara ilivyoundwa kwa ushahidi wa daktari.
Hadi suala la Msitu wa Pande ni Lema alileta. Ndiyo maana Lema alikuwa shahidi muhimu katika ile kesi na kifo chake kilitoa ahueni ya kesi.
Saad na Lema ndiyo waliokwenda kufyatua risasi hewani kwenye misitu ya Bunju ili kuunda ushahidi hewa wa kuwa wajibizana kwa risasi na marehemu.
Tume ya Kipenka ilipokea ushahidi hadi wa wezi halisi waliofanya tukio la ujambazi ambalo Zombe alisema kwenye press kuwa lilifanywa na marehemu.
Kwa hiyo;
Haya maelezo yaliyotolewa na daktari yanabaki kama msingi wa kesi huku daktari akiwa ndiye shahidi muhimu kama Lema.
Sasa tuifuatilie hii kesi hadi mwisho, na tuwe na kalamu na karatasi ya kunakili maswali ya Magafu kwa hao mashahidi ili tusichanganyikiwe na hukumu.
Ila naendelea kushauri, Magafu yuko hapo. Tusibet.
Ova