Mtwara: Jinsi Askari Polisi akiwemo Mkuu wa Kituo na Upelelezi walivyoshiriki Mauaji ya Mfanyabiashara wa Madini

Siku zote nasemaga wabongo ni makatili sana,huyo anayesemaga
Kuna amani ni muongo
Narudia kusena,kama unavipesa
Hakikisha hawa jamaa wasijuwe
Maana kuna kundi maalum wao kazi yao kuwatisha watu na kuwatemesha pesa...

Ova
Harafu hilo kundi linataka hela nyingi balaa sio chenji na ndio maana wanaoshindana nao lazima wakutwe mtaroni...
 
Huyu Tajiri Mussa Hamisi Hamisi atakuw amtu mzito na mtu wa chama.

Sio rahisi kesi yake kusimama hivi. Kama tulivyozoea.

Vinginevyo tunawapongeza Jeshi la Polisi na Serikaki kusimamia haki.
Hapa ndipo sasa tatizo linapoanzia. Unawapongeza wanaosababisha matatizo. Mpaka siku tukijua mzizi wa tatizo ni nini, ndiyo haya mauaji yatapungua.
 
Siku zote nasemaga wabongo ni makatili sana,huyo anayesemaga
Kuna amani ni muongo
Narudia kusena,kama unavipesa
Hakikisha hawa jamaa wasijuwe
Maana kuna kundi maalum wao kazi yao kuwatisha watu na kuwatemesha pesa...

Ova
Huyo dr wa polisi Msuya anajaribu kujitoa kwenye kundi la mauaji kiaina baada ya kuona limevunda. Inakuwaje umchome mtu sindano ya usingizi ili eti akiamka ndiyo aseme kila kitu. Alijua kabisa marehemu atafanywa nini baada ya kuchomwa sindano.
 
Hatari sana Polisi wetu
 
Ndugu yangu ni hivi: haya ni baadhi ya matukio machache sana yanayojulikana. Mengi yanaishia chini kwa chini. Tulitakiwa tuwe na tume huru ya kupokea na kuchunguza malalamiko kutoka kwa wananchi.
 
Hii kesi ngumu sana na Kuna watu wanaenda kula nyundo za kutosha mana ingekuwa ameuliwa mtu ambae Hana connection yoyote ingekuwa kesi ishazimwa na wangesema mtuhumiwa bwana hamis kajinyonga mwenyewe.!

Lakin hata kosa alilofanya mpaka wakamuuwa hawalisemi kafanya Nini.

Polisi wakitaka kukutia hatiani kwanza wanakupa jina baya kama hawakuita unatumiwa na magaidi basi watakupa hata kesi za bangi na unga !

Huyu mchizi alikuwa na Hela na alikuwa na ushamba flani hivi mana kapata Hela ukubwani alafu za haraka haraka sasa akawa anaruka majoka sana .Nasikia alikuwa anatoka na kibegi Cha Hela kwenda kula Bata ndio wale wajomba wakatonywa kuwa Kuna mchizi anatamba huko viwanja na kibegi Cha Hela

Tatizo likaanzia hapo.

Polisi wengi Huwa hawana roho za kibinadamu kabisa .wao wanaishi kama wanyama

Wanahisi wakishakutoa roho ni kama ndio wamemaliza maisha yako. Wasichokijua ni kuwa kufa sio mwisho WA maisha.!
 
Unaikumbuka kesi ya kuuawa kwa wafanyabishara wa madini ya 2006 ya ACP Abdallah Zombe na wenzake kumi na moja?

Ni kweli kwamba Ephraim Sabinus Chigumbi, Sabinus Chigumbi, Juma Ndugu (dereva tax) na Mathias Lunkombe waliuawa wakiwa mikononi mwa polisi.

Magafu alikuwa ndiyo aliyesimama pale kati. Na unajua nini kilitokea baada CPL Saad Alawi kutoweka kabla ya kukamatwa?

Unajua kilichotokea baada ya DC Rashid Lema kuugua ghafla akiwa mahabusu, siku moja kabla ya kutoa ushahidi wake mahakamani, na baadaye kufariki?

Nikukumbushe, Zombe na wenzake waliachiwa huru. Baadaye Bageni pekee alinaswa kwenye rufaa.

Na huko Mtwara tayari mtuhumiwa moja ameshafariki kwa kujinyonga. Ukiona Magafu yuko kwenye kesi anazoziweza zaidi, usibet.

Ova
 
Ndugu yangu ni hivi: haya ni baadhi ya matukio machache sana yanayojulikana. Mengi yanaishia chini kwa chini. Tulitakiwa tuwe na tume huru ya kupokea na kuchunguza malalamiko kutoka kwa wananchi.
Upo sahihi na hiyo Tume huru iwepo kila mkoa maana unaona kabisa pana wahuni wapo busy kuua Raia kwa kutumia Kodi za Wananchi inaumiza sana ujue watu wanapambana kupata pesa wakipata harafu wanakuja wahuni kuua ili watoke na hizo hela huku Wabunge wakiwa kimya kuangalia maslahi yao tu huko Bungeni...
 
Ile taarifa ya mauaji ya yule kijana iliniumiza sana mtu unapambana hustle zako zinajibu shimo linatema wanakuja watu na njaa zao wanakubambikizia kesi wachukue pesa zako wanaona haitoshi wanaamua kufanya ukatili wa mauaji..
Inaumiza sana
 
Jina siyo tatizo per se. Tatizo ni CCM. CCM inawatumia polisi kukandamiza wananchi ili iendelee kutawala. In turn lazima iwaachie wafanye watakavyo ili isiwaudhi. Polisi inayotumiwa na serikali kufanya maovu ni lazima nayo ifanye uhuni kwani inajua kabisa watawale ni wahuni.
 
Taasisi nyingi za serikali wanakwambia ‘system’ haifanyi kazi mtandao uko chini unadhani police watashindwa kuzima hizo camera ili wafanye yao? Na hawashindwi kukata umeme kabisa ili watimize yao.
Ninafanya kazi ya kukusanya mapato kwa kutumia mashine za serikali.

Hili suala la system kutokufanya kazi ni la kweli na huwa linatokea.

Sitetei wala kukataa kwamba kuna wanaodanganya, ila binafsi huwa linanitokea katika majukumu yangu ya kazi.
 
Ninafanya kazi ya kukusanya mapato kwa kutumia mashine za serikali.

Hili suala la system kutokufanya kazi ni la kweli na huwa linatokea.

Sitetei wala kukataa kwamba kuna wanaodanganya, ila binafsi huwa linanitokea katika majukumu yangu ya kazi.


Sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…