Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7

Ndo maana braza Hamza akaamua kufanya yake.
Wakampa na cheo Cha ugaidi.
Nadhani sasa wabadili jina lingine la kesi ya kubambikia, hilo la ugaidi limewashinda. Kesi ya Mbowe pia wameumbuka kwa kubambikia kesi yenye jina hilo.
 
Laiti police wangemdhibiti aliyemtolea nape bastola, mfanyabiashara wa madini asingeuwawa.
 
Jeshi la Polisi lifumuliwe lote kuanzia IGP mpaka mfumo wake wote. Ni wazi, kuna uozo (saratani) usiopona.

Tatizo husababishwa na wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya (kamati za ulinzi) hata Rais au mawaziri wenye dhamana kubwa kubwa wanapolitumia jeshi la polisi kama nyenzo yao binafsi ya kufanyia watu "extortion".

Hata uwe mkuu vipi, ukishampa na kumuachia polisi akufanyie na au akufichie dhambi zko, inakuwa umeshampa yeye mpini na wewe umeshayashika makali. Umeshamfanya kuwa jambazi wewe mwenyewe, kwa dhambi zako tu.

Tuwaiteni Waingereza waje kuliunda na kulinoa upya jeshi la polisi, walipoondoka nnaamini hawakutuachia uozo huu.
 
Mawazo yako mazuri lakini bila kuwatenganisha police na wanasiasa, police wataendelea kulaumiwa Sana kwa kutii maagizo ya wanasiasa.
Kama mwanasiasa ndie Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama police watakuaje huru sasa. Na Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ni lazima uwe ccm Ili mshirikiane na wakuregenzi kuiba kura.
Kumbuka ukiwa police ni marufuku kuhoji, kupinga amri yeyeto toka juu uwe unapenda upendi.
 

bibi upooooo!!
 
Nasisitiza ukiwa na shida ukaenda polisi kupata haki yako yaweza kuwa mauti yako.
Maharamia na majangili kabisa hawa…
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…