Muamala kutoka CRDB kwenda NBC unachukua muda gani?

Muamala kutoka CRDB kwenda NBC unachukua muda gani?

raslimali

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2014
Posts
1,958
Reaction score
1,744
Wakuu kuna mahali nadai senti zangu sasa asubuhi nilitaarifiwa kwamba wametuma muamala kutoka akaunti yao ya CRDB kuja akaunti yangu ya NBC. Nimepita mchana kwa wakala pesa haijaingia. Nikapiga customer care NBC wakasema muamala haujawasili. Namuuliza mdada wa customer care kwa kawaida inachukua muda gani ananijibu inategemea imetumwa kwa njia gani. Sikumuelewa. Kule ninakodai nimeshindwa kumpata hewani mchana huu. Mwenye uzoefu na transactions kutoka CRDB kwenda NBC anijuze hutumia muda gani. Shukran.
 
Aliyekutumia itakua kakudanganya. Muamala ni fasta tu au muombe akupe slip ya muamala
 
Aliyekutumia itakua kakudanganya. Muamala ni fasta tu au muombe akupe slip ya muamala
Kwa kweli na mimi nimewaza hivyo. Maana ingekuwa ni kutoka nje ya nchi ndiyo huchukua siku mbili. Naona hapa kuna kitu
 
Wakuu kuna mahali nadai senti zangu sasa asubuhi nilitaarifiwa kwamba wametuma muamala kutoka akaunti yao ya CRDB kuja akaunti yangu ya NBC. Nimepita mchana kwa wakala pesa haijaingia. Nikapiga customer care NBC wakasema muamala haujawasili. Namuuliza mdada wa customer care kwa kawaida inachukua muda gani ananijibu inategemea imetumwa kwa njia gani. Sikumuelewa. Kule ninakodai nimeshindwa kumpata hewani mchana huu. Mwenye uzoefu na transactions kutoka CRDB kwenda NBC anijuze hutumia muda gani. Shukran.
Pole sana ndugu. Nakusii hachana na benki hiyo, hakika utakuja nishukuru baadae. By the way, una uhakika kuwa hawajafirisiwa na kuwa chini ya uangalizi wa BOT?
 
Jibu alilotoa mhudumu WA bank ni kweli,inategemea na njia iliyotumika kutuma.
Kutuma muamala bank moja kwenda nyingine inachukua saa 24,hii kama ni siku za kazi isiwe weekend.
 
In 2 hours time transaction inatakiwa iwe imekamilika, otherwise ka request then wahudumu wa remitter bank hawaprocess au katumia app pengine mtandao una shida
vyema ukamuomba evidence, km screenshot ya transaction au received document from bank
 
In 2 hours time transaction inatakiwa iwe imekamilika, otherwise ka request then wahudumu wa remitter bank hawaprocess au katumia app pengine mtandao una shida
vyema ukamuomba evidence, km screenshot ya transaction au received document from bank
Ninaidai kampuni siyo mtu binafsi
 
Epuka kabisa kupitisha pesa benki tofauti kama unamishe ya haraka..
 
Epuka kabisa kupitisha pesa benki tofauti kama unamishe ya haraka..
Niliwaambia wanitumie Tigo pesa ambayo siku zote inakuwa instant ila nashangaa this time transaction was declined!
 
Huwa nafanya transactions kwa hizo benki mbili ulizotaja na mara zote miamala imekua ikifika papo hapo
 
Back
Top Bottom