Salaam wakuu.
Kwa wale wakazi wa Dar es Salaam, na maeneo ya jirani kwa leo(15.01.2014) tumeweza kushuhudia foleni ilivyoweza kuwa kubwa, kiasi kwamba barabara takribani zote toka asubuhi muda saa kumi na mbili na nusu hivi hadi muda huu, barabara zilikuwa "hazipitiki'..Sijajua kama ni "wikiendi" ndefu(kuambatana na mapumziko na siku kuu, au labda kufunguliwa kwa shule,n.k.
Lakini hii ikanifanya kutafakari muda tunaoupoteza tuwapo katika foleni. Mfano, iwapo mtu anapoteza masaa mawili(2) kwa siku yaani wastani wa masaa kumi kwa wiki, mtu huyu hupoteza masaa 500 kwa mwaka ambayo ni sawa na takribani siku 21(WIKI TATU).
Je, kwa wale wenye mizunguko zaidi, au wenye kupoteza masaa zaidi ya mawili kwa siku, muda huu tunautambua?
Kwa wale tulio/tunaoishi Dar es Salaam kwa miaka kadhaa tumepoteza miaka mingapi?