Muda umefika nchi za kiislamu na dunia iiambie Israel wacha na inatosha

Muda umefika nchi za kiislamu na dunia iiambie Israel wacha na inatosha

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
inachofanya Israel sasa kwenye jimbo la Gaza ni unyama ambao unapaswa kuzuiwa kivitendo na si kwa lawama za mdomo tu.

Kwa muda wote wa miezi 9 ya vita Israel imeachwa ifanye inavyopenda kwa watu wa Gaza.Wamehamishwa mara mia na sasa wamechoka na hata mikoba yao ya kuhama hama imewapotea.

Iwapo Israel inachotafuta haijakipata basi ni wakati wa kushikwa na kuambiwa inatosha na wacha.Ni kawaida ya binadamu kumzuia mtu katili anapoonekana anamuumiza mwengine kwa sababu yoyote ile.Hali ikifikia hapo huwa hatuanzi kuuliza nani mkosa bali tunazuia uovu na ukatili unaofanyika.

Hukumu za mahakama na lawama nyepesi hazina maana yoyote.Hata wale wanaojidai kuitambua Palestina hawajafanya lolote la maana kuwasaidia watu wa Gaza ambao hata sauti na machozi vimewakauka mwilini.
Bila kufanyika hivyo adhabu za kutoka kwa muumba tunaomba ziwashukie kila mmoja mwenye uwezo wa kuishika mkono Israel lakini amekaa kimya bila kufanya chochote cha maana.

Leo hii watu zaidi ya 70 wameuliwa eneo la Mawasi ambalo watu waliambiwa wakimbilie na ni sehemu salama.Watu na watoto wamebakia vipande vipande

1720887745249.png

An Israeli attack targeting the Hamas military commander kills at least 71 in southern Gaza

 
Kwani hao wapalestina na waarabu wanashindwa nini kuwaambia hamas wawaachilie hao mateka wa kiyahudi kadri wanavyoshikiliwa mateka ndio israel inapata kibali cha kuiponda ponda gaza cha msingi embu mateka waachiliwe maana wapalestina wanakufa kama kuku sioni faida ya kuwashikilia mateka 124 huku mnaendelea kuuawa
 
Kwani hao wapalestina na waarabu wanashindwa nini kuwaambia hamas wawaachilie hao mateka wa kiyahudi kadri wanavyoshikiliwa mateka ndio israel inapata kibali cha kuiponda ponda gaza cha msingi embu mateka waachiliwe maana wapalestina wanakufa kama kuku sioni faida ya kuwashikilia mateka 124 huku mnaendelea kuuawa
Netanyahu ameshasema hata mateka wakiachiliwa haitasaidia kitu.Huoni kuwa ameshakuwa kichaa na ni lazima ashikwe mkono afungwe kamba.
 
Wanaojiita 'civilized world ' walishakosea toka awali....wao walisema Israel ina haki ya kujilinda wakasahu huko kujilinda kuna mipaka yake.

Kwa unyama uliofanyika hapo Gaza sidhani kama kuna hiyo inayoitwa 'International law order ' bado ipo.
Imeisha kabisa. Sasa katika dunia kila mwenye nguvu hataweza kuzuiwa kimahakama.
Dunia inaelekea kuwa uwanja wa fujo.
 
Kuna taarifa huku mastermind Mohameid Deif aka paka mwenye roho saba pamoja na kamanda wa khan yunis wameuawa kwenye haya mashambulizi ya watu 71 waliokufa mbona mnaficha
Hatujadili habari za Mohammed Deif ambaye tangu hapo keshakufa mara kadhaa.Tunajadili unyama unaofanyika kupitiliza kwa kisingizio cha kumtafuta Deif.
 
Back
Top Bottom