Muda wa kumuonesha trafiki leseni ni mpaka siku tatu kama umesimamishwa na huna

Muda wa kumuonesha trafiki leseni ni mpaka siku tatu kama umesimamishwa na huna

Kusahau leseni kupo. Nadhani tahadhari nzuri ni kutoa copy ya leseni yako na kuweka garini sambamba na kadi ya gari ili ikitokea umesahau na ukasimamishwa na Trafiki umweleze kuwa umesahau leseni nyumbani na umwoneshe copy. Hapo akiendelea kukomaa ana lake jambo hata hivyo, ninamshauri mleta thread hii ambaye bila shaka na mwanasheria atuwekee (attach) hivi vifungu vya sheria hasa kifungu cha 77 (1)
 
Swali: Utamthibitishia vipi askari kwamba utarudi kumuonyesha leseni kabla ya muda wa kisheria haujapita, ilhali mmekutana tu barabarani?

Sent using Jamii Forums mobile app

nami nilitaka kuuliza hili swali na je askari anaweza kuzuia chombo ulichonacho ili ukamletee leseni uliyoisahau nyumbani?
 
Nawashangaa sana wengi wenu humu munaendesha magari na hamjui hili.
Mimi moja ya mbinu ya kukwepa faini namuambia traffic police nimesahau leseni home. Wakati ninayo mfukoni. Kwa nn nafanya hivi, hawa ni wajinga sana. Akiishika leseni yako anaanza kukuandikia.
Sasa basi nikiwa nawaambia sina leseni sheria inasema ninatakiwa niilete leseni ndani ya masaa 48 (correct me if I am wrong hapa). Sema wengi wananiambia inabidi niwache gari kituo cha polisi (nadhani hii nayo ni sheria japo sijahakikisha).
Hivyo basi usumbufu unaoweza kupata ni huu tu wa mtuke hapo muelekee kituoni mkawache gari ndio uende home ukalete leseni. Camooooon sijawahi Fanya huu upupu huwa tunamalizana kiutuuzima baada ya hapo, if u noo warra amm seingi
 
944dce79c40d360daa84f627171cd6b1.jpg
waooooo, ahsante sana mkuu
 
Nawashangaa sana wengi wenu humu munaendesha magari na hamjui hili.
Mimi moja ya mbinu ya kukwepa faini namuambia traffic police nimesahau leseni home. Wakati ninayo mfukoni. Kwa nn nafanya hivi, hawa ni wajinga sana. Akiishika leseni yako anaanza kukuandikia.
Sasa basi nikiwa nawaambia sina leseni sheria inasema ninatakiwa niilete leseni ndani ya masaa 48 (correct me if I am wrong hapa). Sema wengi wananiambia inabidi niwache gari kituo cha polisi (nadhani hii nayo ni sheria japo sijahakikisha).
Hivyo basi usumbufu unaoweza kupata ni huu tu wa mtuke hapo muelekee kituoni mkawache gari ndio uende home ukalete leseni. Camooooon sijawahi Fanya huu upupu huwa tunamalizana kiutuuzima baada ya hapo, if u noo warra amm seingi
gerara hia
 
Hilo la kupiga leseni picha kwa simu nimelipenda. Sijawahi kusahau simu hata siku moja ila leseni nasahau mara nyingi tu..👍🏾
 
=========
ILANI: Makala hii hailengi wale wasio na leseni kabisa. Aidha, unashauriwa kupiga picha leseni yako ili angalau uwe na kumbukumbu ya namba ya leseni
=========​

Kusimamishwa na trafiki barabarani, na ukawa huna leseni mfukoni kwa muda huo sio kosa. Mwambie huyo trafiki kuwa hilo sio kosa. Sheria inatutaka kutembea na leseni tunapoendesha vyombo vya moto, lakini pia haisemi kuwa utakapokuwa hauna pale unapoombwa na trafiki basi ni kosa.

Tunaongelea Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168. Wapo watu wameandikiwa faini kisa wameombwa leseni wakasema hawana, au wakasema wamezisahau majumbani. Hawa waliotozwa faini katika mazingira kama haya wameonewa. Na wanastahili kurudishiwa fedha walizotoa haraka.

Ni kweli kifungu cha 77 cha Sheria ya Usalama Barabarani kinamtaka kila mwendesha chombo cha moto kutembea na leseni barabarani. Ni kweli askari anayo mamlaka kumsimamisha mwendesha chombo cha moto. Na ni kweli pia kuwa askari anayo mamlaka ya kumtaka mwendesha chombo cha moto aoneshe leseni yake. Lakini sio kweli hata kidogo kuwa mwendesha chombo cha moto asipoonesha leseni kwa wakati huo basi tayari ametenda kosa. Sio kweli.

Kifungu cha 77(1) cha Sheria ya Usalama Barabarani kinasema kuwa mtu hatatiwa hatiani, kwa maana ya kulipa faini au kuandikiwa kosa au kuadhibiwa na chombo chochote ikiwamo mahakama, kwasababu tu hakubeba, au hakutoa/kuonesha leseni pale alipotakiwa kufanya hivyo, isipokuwa ana siku tatu za kutoa au kuonesha leseni hiyo tokea siku hiyo aliposimamishwa.

Tafsiri iko wazi kuwa unaposimamishwa, ukaombwa kuonesha leseni, ukawa huna kwa mda huo, unazo siku tatu mbele za kutakiwa kuleta na kuonesha. Anachotakiwa kufanya askari sio kukuandikia kosa, laa hasha, bali ni kukutaka umuoneshe leseni hiyo ndani ya siku tatu tokea siku hiyo. Ukishindwa kufanya hivyo ndani ya siku hizo hapo ndipo linaweza kuwa kosa.

Watu wasionewe. Wapo askari wengine pia hawajui hizi sheria. Hawa sisi madereva tuwaelimishe. Unaweza kudhani askari anakuonea kumbe naye hajui. Kwahiyo kazi unayo wewe kuhakikisha unamweleza huyo askari kuhusu kifungu hiki na namna kinavyotaka. Wewe ndiye mtetezi wa kwanza wa haki yako kabla ya kutetewa na mtu mwingine.

Na kama itatokea ukaandikiwa adhabu kwa lazima kwa kitu kama hiki, basi unayo haki ya kukataa kulipa na kuomba kufikishwa mahakamani ili sheria ikatafsiriwe. Mwambie “Sitalipa nataka sheria ikatafsiriwe mahakamani”.

Kukataa kulipa sio kosa au ukorofi na hivyo huna haja ya kukhofu. Kukataa kulipa ni haki katika haki ulizonazo ukihisi umeonewa. Na kama umeshalipa au ulilipa huko nyuma katika mazingira ya jambo kama hili na unao ushahidi basi unayo haki ya kudai hela uliyolipa. Unaweza kuidai huko ulikotozwa au mahakamani.

Sheria imetoa ahueni hii ikizingatia mazingira ya ubinadamu. Huwezi kila unapoamka asubuhi ukakumbuka leseni. Huwezi kila unapokuwa na safari ukakumbuka leseni. Safari nyingine ni za ghafla na za kushtua, mfano kuitiwa msiba, ugonjwa, matatizo kazini, bila kusahau msongo/stress za ada na kodi. Atapata wapi muda wa kukumbuka leseni mtu huyu?

Mwingine amebadilisha nguo na hivyo leseni kubaki kwenye nguo iliyovuliwa, mwingine amebadilisha gari na hivyo leseni kubaki kwenye gari jingine. Na mazingira mengine kama hayo. Zote hizi ni dharula za kibinadamu zilizowafanya watunga sheria kuweka muda wa siku tatu kwa ajili ya kutoa au kuonesha leseni.

Basi wote tubadilike, madereva na askari wasimamia usalama barabarani. Dereva asiwe mkorofi, kadhalika askari asimwonee dereva
Mkuu shida hapa hawa jamaa ukiwa huna lesseni wanakutaka ukalipaki gari kituoni kwao hadi utakapowakubali leseni. Hii kisheria imekaaje, na kama ikinitokea ni nn nnachotakiwa kufanya?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nipe elimu kidogo maana sasa hivi unaandikiwa tu police hachukui cash mkjibishana mpaka siku saba faini inaongezeka kwenye systems hapa inakuwaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawezi kukuandikia bila kumpa leseni kwakuwa lazima aweke kumbukumbu zako kwenye document anayokuandikia so kama hana leseni hana particulars zako
 
Japo cjaspma comments nyingi lkn sasa ukimwambia sheria inataka ndani ya siku 3 uwe umeshamuonyesha askari! Sasa huyu askari MTAACHANAJE pale wakati wewe unakwenda kufuata leseni?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
=========
ILANI: Makala hii hailengi wale wasio na leseni kabisa. Aidha, unashauriwa kupiga picha leseni yako ili angalau uwe na kumbukumbu ya namba ya leseni
=========​

Kusimamishwa na trafiki barabarani, na ukawa huna leseni mfukoni kwa muda huo sio kosa. Mwambie huyo trafiki kuwa hilo sio kosa. Sheria inatutaka kutembea na leseni tunapoendesha vyombo vya moto, lakini pia haisemi kuwa utakapokuwa hauna pale unapoombwa na trafiki basi ni kosa.

Tunaongelea Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168. Wapo watu wameandikiwa faini kisa wameombwa leseni wakasema hawana, au wakasema wamezisahau majumbani. Hawa waliotozwa faini katika mazingira kama haya wameonewa. Na wanastahili kurudishiwa fedha walizotoa haraka.

Ni kweli kifungu cha 77 cha Sheria ya Usalama Barabarani kinamtaka kila mwendesha chombo cha moto kutembea na leseni barabarani. Ni kweli askari anayo mamlaka kumsimamisha mwendesha chombo cha moto. Na ni kweli pia kuwa askari anayo mamlaka ya kumtaka mwendesha chombo cha moto aoneshe leseni yake. Lakini sio kweli hata kidogo kuwa mwendesha chombo cha moto asipoonesha leseni kwa wakati huo basi tayari ametenda kosa. Sio kweli.

Kifungu cha 77(1) cha Sheria ya Usalama Barabarani kinasema kuwa mtu hatatiwa hatiani, kwa maana ya kulipa faini au kuandikiwa kosa au kuadhibiwa na chombo chochote ikiwamo mahakama, kwasababu tu hakubeba, au hakutoa/kuonesha leseni pale alipotakiwa kufanya hivyo, isipokuwa ana siku tatu za kutoa au kuonesha leseni hiyo tokea siku hiyo aliposimamishwa.

Tafsiri iko wazi kuwa unaposimamishwa, ukaombwa kuonesha leseni, ukawa huna kwa mda huo, unazo siku tatu mbele za kutakiwa kuleta na kuonesha. Anachotakiwa kufanya askari sio kukuandikia kosa, laa hasha, bali ni kukutaka umuoneshe leseni hiyo ndani ya siku tatu tokea siku hiyo. Ukishindwa kufanya hivyo ndani ya siku hizo hapo ndipo linaweza kuwa kosa.

Watu wasionewe. Wapo askari wengine pia hawajui hizi sheria. Hawa sisi madereva tuwaelimishe. Unaweza kudhani askari anakuonea kumbe naye hajui. Kwahiyo kazi unayo wewe kuhakikisha unamweleza huyo askari kuhusu kifungu hiki na namna kinavyotaka. Wewe ndiye mtetezi wa kwanza wa haki yako kabla ya kutetewa na mtu mwingine.

Na kama itatokea ukaandikiwa adhabu kwa lazima kwa kitu kama hiki, basi unayo haki ya kukataa kulipa na kuomba kufikishwa mahakamani ili sheria ikatafsiriwe. Mwambie “Sitalipa nataka sheria ikatafsiriwe mahakamani”.

Kukataa kulipa sio kosa au ukorofi na hivyo huna haja ya kukhofu. Kukataa kulipa ni haki katika haki ulizonazo ukihisi umeonewa. Na kama umeshalipa au ulilipa huko nyuma katika mazingira ya jambo kama hili na unao ushahidi basi unayo haki ya kudai hela uliyolipa. Unaweza kuidai huko ulikotozwa au mahakamani.

Sheria imetoa ahueni hii ikizingatia mazingira ya ubinadamu. Huwezi kila unapoamka asubuhi ukakumbuka leseni. Huwezi kila unapokuwa na safari ukakumbuka leseni. Safari nyingine ni za ghafla na za kushtua, mfano kuitiwa msiba, ugonjwa, matatizo kazini, bila kusahau msongo/stress za ada na kodi. Atapata wapi muda wa kukumbuka leseni mtu huyu?

Mwingine amebadilisha nguo na hivyo leseni kubaki kwenye nguo iliyovuliwa, mwingine amebadilisha gari na hivyo leseni kubaki kwenye gari jingine. Na mazingira mengine kama hayo. Zote hizi ni dharula za kibinadamu zilizowafanya watunga sheria kuweka muda wa siku tatu kwa ajili ya kutoa au kuonesha leseni.

Basi wote tubadilike, madereva na askari wasimamia usalama barabarani. Dereva asiwe mkorofi, kadhalika askari asimwonee dereva
Ama kweli 'ignorance of the law is not an excuse' Jamaa hawa wanachukua advantage ya ujinga wetu.
Ahsante sana kwa elimu.
 
Back
Top Bottom