Muelekeo wa Uwekezaji nchini chini ya uongozi wa Prof. Mkumbo, Tunatokaje tulipo?

Muelekeo wa Uwekezaji nchini chini ya uongozi wa Prof. Mkumbo, Tunatokaje tulipo?

Uko sahihi sana mkuu. Katika mazingira hayo sasa, ndio unapoonekana zaidi umuhimu wa kutengeneza wawekezaji wa ndani kwa wingi, ambapo mbele ni tutajadili ni kwa vipi hilo linawezekana kwa kwa kufanya mabadiliko flani flani kwenye mfumo wa elimu na kujenga uwezo kwenye maeneo flani flani.

.
... hata hao wa ndani wakiwekewa makodi makubwa makubwa ya kukomoana lazima watafunga shughuli zao. Kodi za kukomoana ni miongoni mwa matatizo makuu ya uwekezaji.
 
Unamzungumzia mkumbo huyu aliehojiwa juzi na ITV?sina hakika sana kama kuna la maana atakaloliibua mkumbo ndani ya muda atakao kuwepo katika hiyo wizara mfano mzuli ni majuzi anaacha kuzungumzia changamoto za wizara na namna mpango kazi wa namna ya kuzitatua anapoteza muda kuwashambulia chadema yaani unawaza huyu nae ni professor?
... bora Prof. Mkenda yeye anaongoza jeshi kuwasambaratisha nzige waliovamia Kaskazini kutokea nchi jirani. At least that's something tangible kwa mwananchi wa kawaida.
 
Huyu mzee hana ubuni wowote yeye anachowaza ni CHADEMA unaitwa kwenye kipindi kwenye TV badala ya kuongelea mipango wewe unakomaa na CHADEMA mwanzo mwisho, Wizara haina Waziri ina kivuli pekee
Yaani alishangaza wengi kwa kweli, muda wote ni yeye na chadema tu, hapo ndipo tunapohoji elimu za hawa wanaojiita maprofesa,
Anatakiwa atolewe kwenye hiyo nafasi haraka sana.

Maana hana uwezo wa kufanya chochote zaidi ya mipasho.
Atafutiwe kazi ya kuiponda CDM huko kwenye chama cha sisemu
Hana mbinu,maarifa,maono wala mikakati ya kuisongesha sector ya uwekezaji,
Sana sana huko kwenye hiyo sector,atawatafuta wawekezaji wanaoiunga mkono CDM awafungie shughuli zao, ndio mawazo yake hayo
 
... Covid-19 imeathiri uwekezaji duniani kote sio Tanzania peke yake japo Tanzania haina Corona kwa mujibu wa wataalamu wetu. Pili sheria za kodi nazo ni tatizo; Wizara ya Prof. Mkumbo ni mwathirika wa hayo.
Atatumbuliwa soon
 
Kwa maoni yangu, kulingana na mazingira ya kisiasa nchini, kazi hii inaweza kuwa na ufanisi ikiwa kitengo/ mfumi huu utaundwa ndani ya chama kinachoongoza dola, na humo wakawekwa watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri, kuchanganua mambo na kubuni solutions za matatizo mbalimbali ya kiuwekezaji.
.
Mada yako ni nzuri ila nilipofika hapa nikachoka kabisa...... Huwezi tegemea chama tawala kilichopitisha ilani ndio hiko hiko kifanye scrutiny kwa makosa yaliyozalishwa na serikali/TRA ambao ni zao lao!!
Nadhani ifike mahala Private sector ishirikishwe kabisa maana wao ndio wanajua wanataka nini..... tume zipo kibao kuanzia ya ushindani, baraza la uwezeshaji uchumi, Financial intelligence unit n.k lakini ufanisi wao umesaidia nni?

Ifike kipindi private sector nao watoe maoni na miongozo ya nni kifanyike sio kuwapangia tu. Kma ni timu ikiundwa basi nusu wachaguliwe na waziri na nusu watoke Private sector maana wao ndio wanajua kadhia yote but kuingiza vyama na serikali kujikagua wenyewe ni ngumu mnoo.

Ni vile tu mtasema sio uzalendo ila unaweza hta kuwapa tender kampuni za kikaguzi na consultancy za nje kma PwC kwa mkataba yaani wao kazi yao ni kufuatilia hayo yote na kutoa mapendekezo na ushauri wa kitaalam. Trust me ufanisi wao utakua mkubwa sababu wanaenda kibiashara zaidi ila haya ma-tume hayana faida zaidi ya vikao tu kutafuta umaarufu kwa matamko kwenye camera!
 
Kitila angekuwa na uwezo angeanzisha chama chake akijenge tukione badala ya kukimbilia CCM kama alivyofanya, he is nobody to me; hapo ulipotaka kuundwe chombo kitachojihusisha na masuala ya kodi kitakachokuwa nje ya TRA na kitatokana na watu toka ndani ya "chama dola", hapo ndipo sijakuelewa kabisa.

Hili neno "chama dola" kwanza mtambue sio sifa ndugu zanguni, mamlaka na nguvu ya chama chochote cha siasa siku zote lazima yatoke kwa wanachama na wapenzi wake, kutegemea nguvu toka nje ya hapo ni udhaifu, hicho chama hakifai kuongoza nchi.

Hali hii ndio husababisha CHADEMA waonekane wanaharakati, kwasababu kwa hali ya kawaida hawashindani na wanasiasa wenzao bali wanashindana na "chama cha siasa" jina tu kinachotegemea support ya kina Mambosasa.

Hiki ndicho husababisha Chadema wajivike uanaharakati ili kujaribu kwenda sawa na hiki chama kinachotegemea nguvu ya dola/polisi ili kupigania haki zao, mfano pale wanapotaka kuandama kisheria inaruhusiwa, lakini Mambosasa anakataa maandamano yao ili kuilinda CCM, hapa lazima Chadema wapiganie hali yao, ila wajinga huwaita wanaharakati bila kujua their motive behind.

Sasa ukishakuwa na chama dhaifu kama hicho kinachotegemea dola, hao watu "ma-genious" unaowataka wapewe hiyo task ya kufuatilia mambo ya biashara za watu watakuwa na nguvu gani kutekeleza majukumu yao kwa uhuru bila kupendelea maslahi ya chama chao, na/au kujipendekeza kwa kiongozi wao kwa kuwakandamiza wale wasio wa chama chao ili kumfurahisha bosi wao? hapa utaona hapatakuwepo na tofauti yoyote na haya tunayoshuhudia siku hizi.

Kwa mtazamo wangu mengi ya hayo uliyoandika hapo juu yanahitaji mtazamo na fikra mpya katika taifa letu ili kutekelezeka, na fikra hizo lazima ziongozwe na katiba mpya itakayompa kila mmoja wetu uwanja wake wa kutimiza majukumu yake kisheria zaidi (kwa uhuru), badala ya kusubiri fulani akupe kazi halafu uanze kufanya hiyo kazi kwa hofu bila weledi wowote ili umridhishe bosi wako.
mkuu nmefurahi na ww umeona hilo tatizo.... Sijaelewa kwanini anawaza chama dola ndio kisimamie masuala ya kitaalam kama haya. Siasa ikiingizwa huko utashangaa wanajazwa UVCCM kufuatilia biashara wakati ilipaswa iwe na professional consultants wasio na vyama tena wana experience kwenye field!!
 
Serikali nyingi hutumia pesa nyingi na muda mwingi kutengeneza sheria na miongozo ya kufanya biashara chakushangaza biashara huwa hazifanikiwi hufa
 
Mkumbo na Sosholojia yake na uwekezaji - ni mafuta na maji. Huyu anchojua ni porojo.

Badala ya kuingelea uwekezaji, anaongelea CHADEMA, huo si ujinga wa hali ya juu? Hakuna faida Taifa litapata kwenye uwekezaji kwa kumtegemea huyo unprofessional Prof.
 
Huyu mzee hana ubuni wowote yeye anachowaza ni CHADEMA unaitwa kwenye kipindi kwenye TV badala ya kuongelea mipango wewe unakomaa na CHADEMA mwanzo mwisho, Wizara haina Waziri ina kivuli pekee
Wawekezaji wakubwa hawataki sijui nn? Wao wanataka predactibility. Haya mambo ya kulipishana mafaini kwa mashirika ya Madini mlizani mnawakomoa kina Lisu???
 
Kuna msemo kuwa ili kupata matokeo yasiyo ya kawaida, ni lazima kwanza kufanya kitu kisichokuwa cha kawaida .

Sote tunakubaliana kuwa ili kukuza uchumi wetu, kwa vyovyote vile ni lazima tukuze uwekezaji wa kutoka nje lakini pia wa ndani ya nchi.

Hata hiyo sio tu kwamba kasi ya uwekezaji kwa ujumla wake hairidhishi sana bali pia kuna hoja ya kwamba mazingira ya uwekezaji hayavutii vya kutosha. Aidha, kuna hoja kuwa, biashara nyingi zinazoanzishwa huishia kufa na watanzania wengi wanashindwa kuwekeza kwa kukosa mitaji.

Pamoja na uwezo mkubwa ambao Prof. Mkumbo anao na hivyo kuleta matumaini kuwa kuna hatua tunaweza kupiga chini ya uongozi wake, vile vile yanahitajika mabadiliko makubwa ya kimifumo ili kupata mafanikio makubwa. Kwa leo nitagusia eneo moja kwa ufupi sana, maeneo mawili tutayagusia wakati mwingine.

Kwanza, kuhusu hoja ya kwamba hakuna mazingira rafiki ya uwekezaji. Hoja hii inajiekemeza kwenye suala la kwamba, kumekuwa na tozo na kodi nyingi bila kujali biashara zinatengeneza faida au laa jambo ambalo ni sawa na kumkamua ng'ombe bila kujali anakula au la! mwishowe anakufa.

Ni nini cha kufanya? Kwa kuwa TRA ni chombo cha serikali cha kukusanya kodi, kwa muundo wake hamna namna kinaweza kujikita sana kukuza biashara za wadau badala ya kukusanya kodi.

Hivyo ni vyema kuwa na mfumo mwingine ambao kazi yake itakuwa ni kufuatilia biashara 'interprises' mpyaa na zile za zamani ili kubaini changamoto zinazokabili biashara husika na kuzifikisha kwa wafanya maamuzi haraka bila urasimu ili zitatuliwe. Aidha, kutambua kama biashara husika zinaenda kwa hasara na kushauri wafanya maamuzi juu ya ' interventions' muhimu za kufanya ili kuokoa biashara husika ikiwemo pengine kupunguziwa kodi kwa kipindi maalum na na kutambua biashara ambazo zishatengemaa na kuongeza kodi kidogo kidogo kwa namna ambayo italeta 'win win situation'.k

Kwa maoni yangu, kulingana na mazingira ya kisiasa nchini, kazi hii inaweza kuwa na ufanisi ikiwa kitengo/ mfumi huu utaundwa ndani ya chama kinachoongoza dola, na humo wakawekwa watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri, kuchanganua mambo na kubuni solutions za matatizo mbalimbali ya kiuwekezaji.

Mfumo juu utaweka mazingira ya kuhakikisha kuwa, hakuna biashara 'interprises' inayokufa, na kuchukulia kuwa kufa kwa biashara hata moja tu bila kujali ukubwa wake ni kosa kubwa sana.

Mbinu hii imetunika China na ndio moja ya sababu moja ya sababu kubwa zilizosaidia kuibuka kwa biashara na kampuni nyingi kubwa na ndogo ndogo kuanzia miaka ya 90's hadi sasa ambazo zinaendeshwa kwa faida na kuiweka China kwenye kilele cha mafanikio ya kiuchumi kwa kutengeneza na kukuza wawekezaji wa ndani ya china na nje ya china waliowekeza China.

Mfumo huu utakuwa ni complement kwa mifumo iliyopo ya ukusanyaji kodi ambapo wakati wakusanya kodi watakuwa wanakamua maziwa, mfumo huu utakuwa unamlisha ng'ombe ili kwanza aweze kuwepo na kisha atoe maziwa.

Swali ni je? Kama watakaopewa kazi hiyo wataamua kuwa corrupt pengine wakawa wanafanya manipulation na wasitoe taarifa za kweli? Jibu ni kwamba mfumo huo utatakiwa kuwa na checks and balances ndani yake wenyewe na nje pia.

Nitaendelea sehemu ya pili itakayoeleza ni kwa vipi tunaweza kutengeneza wawekezaji wa ndani kwa wingi, kwa muda mfupi na kwa mafanikio makubwa na Sehemu ya tatu ambayo itaelezea ni nini Tufanye ili wawekezaji wa nje waje Tanzania na sio kwenda nchi nyingine duniani? Wakati dunia ina mamia ya nchi.
Mazingira ya uwekezaji siyo RAFIKI kabisa kwa mtu kuja kuwekeza Tanzania. Ndiyo maana hakuna hata muwekezaji mmoja aliyetokea kuja Tanzania baada ya Magufuli kuingia. Mwekezaji wa mwisho mwenye mtaji unaogusa uchumi wa nchi ni DANGOTE tu aliyekuja mwaka 2014 wakati wa JK akatumbukiza Dollars 0.5Trillion.

Wachawi wa mazingira ya uwekezaji Tanzania ni sheiria zetu tunazoandika kila siku, TRA, TAKUKURU na Mkuu wa nchi mwenyewe
 
Kibongo bongo ni moja ya watu smart sana, kulingana na samples zilizopo. Kwa hiyo akipata support anaweza kuleta mafanikio makubwa kwenye eneo la uwekezaji.

Tatizo ni pale tunapojilinganisha na kina Musk, bila kukumbuka wabongo tunajijua tu wenyewe hahahahah
Eti watu smart sana...
Mbona nyie wabongo mnapenda kusema
Mtu fulani bwana smart sana
Mtu akijua kupiga tantalila mtaskia aise jamaa
Smart sanaaa

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Hii sekta ngumu hasa kipindi hiki cha korona lakini bado kuna mambo mazuri yanayoweza kufanyika kama mifumo ikiboreshwa
Wewe achana na mambo ya korona, huko ni kuzunguka zunguka na kudeflect blames sehemu isiyohusika. Uwekezaji nchi hii umeanza kusua sua tangu 2016, korona imeingia 2019.

Takwimu za Tz kupokea wawekezaji wakubwa zipo, na juhudi zimerudi nyuma sana katika huu utawala wa awamu ya tano, Huyu baba alipoapishwa tu alianza kudeal na watu fulani fulani, Mfano ni yule mfanyabiashara mkubwa aliyeweka mtaji mkubwa na kuajiri maelfu ya waTz. Wamemharass we hadi akahamisha mtaji wake kwingine. Dunia nzima inafahamu alichofanyiwa yule mfanyabiashara, kufikiri wenye mitaji wataendelea kumiminika ni kujitoa ufahamu. Infact, Tz haijapokea mfanyabiashara mwenye mtaji mkubwa kama Dangote kipindi hiki cha Dk,Mtukufu, mheshimiwa sana Magufuli sababu ya mazingira ya uwekezaji kutokuwa rafiki na mabavu.

Tatizo la kiongozi wetu ni kudhani dunia inatuhitaji kuliko tunavyoihitaji, Mkiwaharass wafanyabiashara watapeleka mitaji yao kwa majirani zetu wakenya, uganda, Zambia etc. Tutakosa kodi na ajira za watu wetu.
 
Kitila hiyo nafasi siyo ya kupiga porojo, mazingira ya kufanya biashara ni mabovu na yanatakiwa kuboreshwa ili kuwawezesha wafanyabiashara waliopo ndani wawe na imani ya mitaji yao kukua na kupanua biashara zao. Kama wawekezaji wa ndani hawana imani na sera ya biashara, wafanya biashara wa nje hawatataka hata kusikia neno tanzania. Nani atakuja kama waliopo ndani wanachechemea na kufunga biashara zao?
 
Kitila angekuwa na uwezo angeanzisha chama chake akijenge tukione badala ya kukimbilia CCM kama alivyofanya, he is nobody to me; hapo ulipotaka kuundwe chombo kitachojihusisha na masuala ya kodi kitakachokuwa nje ya TRA na kitatokana na watu toka ndani ya "chama dola", hapo ndipo sijakuelewa kabisa.

Hili neno "chama dola" kwanza mtambue sio sifa ndugu zanguni, mamlaka na nguvu ya chama chochote cha siasa siku zote lazima yatoke kwa wanachama na wapenzi wake, kutegemea nguvu toka nje ya hapo ni udhaifu, hicho chama hakifai kuongoza nchi.

Hali hii ndio husababisha CHADEMA waonekane wanaharakati, kwasababu kwa hali ya kawaida hawashindani na wanasiasa wenzao bali wanashindana na "chama cha siasa" jina tu kinachotegemea support ya kina Mambosasa.

Hiki ndicho husababisha Chadema wajivike uanaharakati ili kujaribu kwenda sawa na hiki chama kinachotegemea nguvu ya dola/polisi ili kupigania haki zao, mfano pale wanapotaka kuandamana kisheria inaruhusiwa, lakini Mambosasa anakataa maandamano yao ili kuilinda CCM, hapa lazima Chadema wapiganie hali yao, ila wajinga huwaita wanaharakati bila kujua their motive behind.

Sasa ukishakuwa na chama dhaifu kama hicho kinachotegemea dola, hao watu "ma-genious" unaowataka wapewe hiyo task ya kufuatilia mambo ya biashara za watu watakuwa na nguvu gani kutekeleza majukumu yao kwa uhuru bila kupendelea maslahi ya chama chao, na/au kujipendekeza kwa kiongozi wao kwa kuwakandamiza wale wasio wa chama chao ili kumfurahisha bosi wao? hapa utaona hapatakuwepo na tofauti yoyote na haya tunayoshuhudia siku hizi.

Kwa mtazamo wangu mengi ya hayo uliyoandika hapo juu yanahitaji mtazamo na fikra mpya katika taifa letu ili kutekelezeka, na fikra hizo lazima ziongozwe na katiba mpya itakayompa kila mmoja wetu uwanja wake wa kutimiza majukumu yake kisheria zaidi (kwa uhuru), badala ya kusubiri fulani akupe kazi halafu uanze kufanya hiyo kazi kwa hofu bila weledi wowote ili umridhishe bosi wako.
Dola- Kiswahili - Daulatt- Kiarabu- Sovereignty - kingereza.

Mkuu pata maana yake kwanza mbona unaogopa sana Dola.

Sovereignty means some persons, assembly of group of persons in every independent state have the final legal authority to command and enforce obedience.
 
MMECHANGIA WENGI NI MICHANGO YA KILA MTUU AONAVYO, LAKINI HAKUNA HATA MMOJA ALIYE ADDRESS SAWA SAWA TATIZO AMBALO BIASHARA ZETU ZINAPAMBANA NAZO.

KWA PROJECTION YA MKUU LABDA AONGEZE KUKUSANYA KODI NA WAKATI HUO HUO A PRINT PESA NA KUTOSHA KUPAMPU KWENYE MZUNGURUKO WA SASA.

Tatizo pesa ama mitaji haipo huria, kwa hiyo biashara huria Haito wezekana.

Biashara huria bila mitaji huria ni sawa na gari lá bila mafuta yakuliendesha. Pesa iliyo nunua madege, meli za maziwa karibu yote, barabara zinazo jengwa na makontrakta wa njee, Ujenzi wa Bwawa lá Nyerere wamelipwa malipo yao na wamepeleka kwao zaidi ya billion 15 USD ( kama trillion 43 )zimenyofolewa kutoka kwenye mzunguuko wa pesa zetu, jee tumebaki na nini?
 
Back
Top Bottom