Muelekeo wa Uwekezaji nchini chini ya uongozi wa Prof. Mkumbo, Tunatokaje tulipo?

Muelekeo wa Uwekezaji nchini chini ya uongozi wa Prof. Mkumbo, Tunatokaje tulipo?

Dola- Kiswahili - Daulatt- Kiarabu- Sovereignty - kingereza.

Mkuu pata maana yake kwanza mbona unaogopa sana Dola.

Sovereignty means some persons, assembly of group of persons in every independent state have the final legal authority to command and enforce obedience.
Hii maana yako ya kwenye makaratasi una hakika ndivyo inavyomaanishwa kwa vitendo? au wewe ni mgeni Tz hujawahi kusikia/kuona hilo neno hutumika vipi? umewahi kusikia kauli "vyombo vya dola" huwa ina maanisha nini? au kwa akili zako za kukariri ndio humaanisha sovereignty? wacha kufundisha werevu ujinga.
 
Hii wizara kama angekabidhiwa Prof Mkenda, Bashe ama Kimei nafikiri tungeona ubunifu fulani.
Are you sure? Tatizo la JF wengi njaa zinawasumbua. Kufanikiwa kupata wawekezaji ni sera na sio mtu. Wacheni majungu kosoeni sera sio kuwashambulia individuals. Wekeni mawazo mbadala na mifano if possible.

Mtu analalamika ati kodi sio rafiki ulitaka shangazi yako ndio alipe kodi na wengine wasilipe? Kodi ndio kila kitu, tena kodi za Tanzania bado zipo chini. Ili nchi iendelee lazima kodi ziangaliwe upya na ikibidi zingine ziongezwe. Hatuwezi kupiga hatua kama kodi zetu zitadumaa.
 
MMECHANGIA WENGI NI MICHANGO YA KILA MTUU AONAVYO, LAKINI HAKUNA HATA MMOJA ALIYE ADDRESS SAWA SAWA TATIZO AMBALO BIASHARA ZETU ZINAPAMBANA NAZO.

KWA PROJECTION YA MKUU LABDA AONGEZE KUKUSANYA KODI NA WAKATI HUO HUO A PRINT PESA NA KUTOSHA KUPAMPU KWENYE MZUNGURUKO WA SASA.

Tatizo pesa ama mitaji haipo huria, kwa hiyo biashara huria Haito wezekana.

Biashara huria bila mitaji huria ni sawa na gari lá bila mafuta yakuliendesha. Pesa iliyo nunua madege, meli za maziwa karibu yote, barabara zinazo jengwa na makontrakta wa njee, Ujenzi wa Bwawa lá Nyerere wamelipwa malipo yao na wamepeleka kwao zaidi ya billion 15 USD ( kama trillion 43 )zimenyofolewa kutoka kwenye mzunguuko wa pesa zetu, jee tumebaki na nini?
Are you serious?
 
By the way as long as Magufuli ana exist kwenye kile kiti hakuna chochote kipya kwenye uwekezaji kitakachofanyika na hata kikifanyika hakita kuwa na umuhimu sababu uwekezaji Tanzania umerudishwa nyuma na Sera zake za miaka 47 za kutaka serikali kuhodhi kila kitu.

Ukiachana na huo,kuna kuna uwekezaji wa MTU moja moja ambapo Watanzania wengi walikuwa wamisha anza kupiga hatua Kibiashara hence maisha binafsi ya watu kustawi hapa napo katurudisha hatua 1000 nyuma.Mchawi wa maendeleo ya Watanzania kila Siku mnampamba na kumsifia bado tunasubiri miujiza-poor Tanzanians.
JK alifika sehemu akawa drop, mtu anafika ulaya anaanza kuomba msaada wa arv, oh mie nalea viwete na mataahira, who wants all those stories!
 
Unamzungumzia mkumbo huyu aliehojiwa juzi na ITV?sina hakika sana kama kuna la maana atakaloliibua mkumbo ndani ya muda atakao kuwepo katika hiyo wizara mfano mzuli ni majuzi anaacha kuzungumzia changamoto za wizara na namna mpango kazi wa namna ya kuzitatua anapoteza muda kuwashambulia chadema yaani unawaza huyu nae ni professor?
Mawaziri wetu Bhana. Mh Molel aliulizwa kama kuna Corona. Jibu alilotoa ni kwamba Lissu alikuja akafanya mikutano bila barakoa.
 
Kuna msemo kuwa ili kupata matokeo yasiyo ya kawaida, ni lazima kwanza kufanya kitu kisichokuwa cha kawaida .

Sote tunakubaliana kuwa ili kukuza uchumi wetu, kwa vyovyote vile ni lazima tukuze uwekezaji wa kutoka nje lakini pia wa ndani ya nchi.

Hata hiyo sio tu kwamba kasi ya uwekezaji kwa ujumla wake hairidhishi sana bali pia kuna hoja ya kwamba mazingira ya uwekezaji hayavutii vya kutosha. Aidha, kuna hoja kuwa, biashara nyingi zinazoanzishwa huishia kufa na watanzania wengi wanashindwa kuwekeza kwa kukosa mitaji.

Pamoja na uwezo mkubwa ambao Prof. Mkumbo anao na hivyo kuleta matumaini kuwa kuna hatua tunaweza kupiga chini ya uongozi wake, vile vile yanahitajika mabadiliko makubwa ya kimifumo ili kupata mafanikio makubwa. Kwa leo nitagusia eneo moja kwa ufupi sana, maeneo mawili tutayagusia wakati mwingine.

Kwanza, kuhusu hoja ya kwamba hakuna mazingira rafiki ya uwekezaji. Hoja hii inajiekemeza kwenye suala la kwamba, kumekuwa na tozo na kodi nyingi bila kujali biashara zinatengeneza faida au laa jambo ambalo ni sawa na kumkamua ng'ombe bila kujali anakula au la! mwishowe anakufa.

Ni nini cha kufanya? Kwa kuwa TRA ni chombo cha serikali cha kukusanya kodi, kwa muundo wake hamna namna kinaweza kujikita sana kukuza biashara za wadau badala ya kukusanya kodi.

Hivyo ni vyema kuwa na mfumo mwingine ambao kazi yake itakuwa ni kufuatilia biashara 'interprises' mpyaa na zile za zamani ili kubaini changamoto zinazokabili biashara husika na kuzifikisha kwa wafanya maamuzi haraka bila urasimu ili zitatuliwe. Aidha, kutambua kama biashara husika zinaenda kwa hasara na kushauri wafanya maamuzi juu ya ' interventions' muhimu za kufanya ili kuokoa biashara husika ikiwemo pengine kupunguziwa kodi kwa kipindi maalum na na kutambua biashara ambazo zishatengemaa na kuongeza kodi kidogo kidogo kwa namna ambayo italeta 'win win situation'.k

Kwa maoni yangu, kulingana na mazingira ya kisiasa nchini, kazi hii inaweza kuwa na ufanisi ikiwa kitengo/ mfumi huu utaundwa ndani ya chama kinachoongoza dola, na humo wakawekwa watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri, kuchanganua mambo na kubuni solutions za matatizo mbalimbali ya kiuwekezaji.

Mfumo juu utaweka mazingira ya kuhakikisha kuwa, hakuna biashara 'interprises' inayokufa, na kuchukulia kuwa kufa kwa biashara hata moja tu bila kujali ukubwa wake ni kosa kubwa sana.

Mbinu hii imetunika China na ndio moja ya sababu moja ya sababu kubwa zilizosaidia kuibuka kwa biashara na kampuni nyingi kubwa na ndogo ndogo kuanzia miaka ya 90's hadi sasa ambazo zinaendeshwa kwa faida na kuiweka China kwenye kilele cha mafanikio ya kiuchumi kwa kutengeneza na kukuza wawekezaji wa ndani ya china na nje ya china waliowekeza China.

Mfumo huu utakuwa ni complement kwa mifumo iliyopo ya ukusanyaji kodi ambapo wakati wakusanya kodi watakuwa wanakamua maziwa, mfumo huu utakuwa unamlisha ng'ombe ili kwanza aweze kuwepo na kisha atoe maziwa.

Swali ni je? Kama watakaopewa kazi hiyo wataamua kuwa corrupt pengine wakawa wanafanya manipulation na wasitoe taarifa za kweli? Jibu ni kwamba mfumo huo utatakiwa kuwa na checks and balances ndani yake wenyewe na nje pia.

Nitaendelea sehemu ya pili itakayoeleza ni kwa vipi tunaweza kutengeneza wawekezaji wa ndani kwa wingi, kwa muda mfupi na kwa mafanikio makubwa na Sehemu ya tatu ambayo itaelezea ni nini Tufanye ili wawekezaji wa nje waje Tanzania na sio kwenda nchi nyingine duniani? Wakati dunia ina mamia ya nchi.
TRA inatakiwa kubadilika kabisa ili kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji.
Wazo langu kubwa kwa TRA ni kwamba wabuni njia za kukuza biashara ndogo na pia kutowa support kwa biashara kubwa ili kuwe na mzunguko wa pesa wakutosha kwa ajili ya wao kukusanya kodi na siyo kuweka kodi nyingi nyingi zinaso umiza na kusababisha biashara kufa.
 
Unamzungumzia mkumbo huyu aliehojiwa juzi na ITV?sina hakika sana kama kuna la maana atakaloliibua mkumbo ndani ya muda atakao kuwepo katika hiyo wizara mfano mzuli ni majuzi anaacha kuzungumzia changamoto za wizara na namna mpango kazi wa namna ya kuzitatua anapoteza muda kuwashambulia chadema yaani unawaza huyu nae ni professor?
Shida njaaa zinatumiza sana wafrica. Hizi njaa zinafanya mpka usaliti unakuwepo. Ndomana mimi nasema africa amna siasa bali ni filam tupu. Huyu katoka huku huyu karudi huku. Ni ukicha.
Ma proffesor njaa nao sijuwi ni uprofessa gani apa bongo huo amna innovation zozote tu kazi kusagia siasa.
 
Ni aina mojawapo ya maprofesor wa majalalani
Huwa naumia sana nikisikia proffesor yyote apa bongo anaongea nonsense yani naona kabisa hawana faida yoyote walio pata katk masomo yao zaidi yakuongeza ujinga tu.
 
Hivi kwanini hii wizara wasipewe watu walio fanikiwa kibiashara apa Tz ili watoe hizo mbinu zao kusaidia biashara ndogo ndogo kukua.
Mfano Bakhresa awe waziri wa viwanda na uwekezaji.
Katibu mkuu awe Mo dewiji ili watusaidie hapo swala zima la uwekezaji mana hao mawaziri wanao wekwa wengi elimu za vitabuni experience hawana. Hata biashara ya spea za magari hana sasa ndo waongoze uchumi wa Taifa zima
 
MMECHANGIA WENGI NI MICHANGO YA KILA MTUU AONAVYO, LAKINI HAKUNA HATA MMOJA ALIYE ADDRESS SAWA SAWA TATIZO AMBALO BIASHARA ZETU ZINAPAMBANA NAZO.

KWA PROJECTION YA MKUU LABDA AONGEZE KUKUSANYA KODI NA WAKATI HUO HUO A PRINT PESA NA KUTOSHA KUPAMPU KWENYE MZUNGURUKO WA SASA.

Tatizo pesa ama mitaji haipo huria, kwa hiyo biashara huria Haito wezekana.

Biashara huria bila mitaji huria ni sawa na gari lá bila mafuta yakuliendesha. Pesa iliyo nunua madege, meli za maziwa karibu yote, barabara zinazo jengwa na makontrakta wa njee, Ujenzi wa Bwawa lá Nyerere wamelipwa malipo yao na wamepeleka kwao zaidi ya billion 15 USD ( kama trillion 43 )zimenyofolewa kutoka kwenye mzunguuko wa pesa zetu, jee tumebaki na nini?

Mkuu unajua maana ya $15b, au umeandika ili kutishia wasiojua lolote? Ungesema hiyo ndio hela wangalau Tanzania inatarajia kutumia kwenye miradi yake ningekuelewa,na sio kusema hiyo hela yote imetolewa. Kama hizo $15b zingekuwa zimetolewa mpaka sasa, miradi ya SGR & SG respectively ingekuwa imekamilika kwa 100%. Rejea figure zako kwanza.
 
Are you sure? Tatizo la JF wengi njaa zinawasumbua. Kufanikiwa kupata wawekezaji ni sera na sio mtu. Wacheni majungu kosoeni sera sio kuwashambulia individuals. Wekeni mawazo mbadala na mifano if possible.

Mtu analalamika ati kodi sio rafiki ulitaka shangazi yako ndio alipe kodi na wengine wasilipe? Kodi ndio kila kitu, tena kodi za Tanzania bado zipo chini. Ili nchi iendelee lazima kodi ziangaliwe upya na ikibidi zingine ziongezwe. Hatuwezi kupiga hatua kama kodi zetu zitadumaa.

Kwa taarifa yako kuvutia wawekezaji huku kwetu Afrika ni mtu, hasa kiongozi aliye madarakani. Sera ni formalities tu, lakini imani waliyo nayo wawekezaji kwa kiongozi huwa ni first priority. Mfano mrahisi, wakati wa JK wangalau aliweza kuvutia wawekezaji wachache, lakini toka ameingia Magufuli madarakani, hakuna muwekazaji yoyote wa maana amekuja, ukiachia wachache waliopo iliobidi wakubaliane na mazingira mapya. Na hadi Magufuli atoke madarakani, sitegemei kama anaweza kupata muwekezaji wa kuwekeza mtaji kama wa Dangote kwa mfano.
 
Are you sure? Tatizo la JF wengi njaa zinawasumbua. Kufanikiwa kupata wawekezaji ni sera na sio mtu. Wacheni majungu kosoeni sera sio kuwashambulia individuals. Wekeni mawazo mbadala na mifano if possible.

Mtu analalamika ati kodi sio rafiki ulitaka shangazi yako ndio alipe kodi na wengine wasilipe? Kodi ndio kila kitu, tena kodi za Tanzania bado zipo chini. Ili nchi iendelee lazima kodi ziangaliwe upya na ikibidi zingine ziongezwe. Hatuwezi kupiga hatua kama kodi zetu zitadumaa.
Wewe ni mpuuzi kweli! Kodi za Tanzania zipo chini, unaota?

Katika Dunia, nchi zinazoongoza kwa kodi kubwa na nyingi ni Tanzania na South Africa.

Tanzania ndiyo nchi yenye mazingira mabaya kabisa ya uwekezaji kwenye sekta ya madini, ikifuatiwa na Venezuela.

Usichojua, hakuna nchi hata moja Dumiani iliyokuwa maskini iliyowahi kupata maendeleo na kuondokana na umaskini kwa kuongeza kodi.
 
Back
Top Bottom