Mufindi: Watu 18 wamefariki katika ajali ya Coaster na lori

Mufindi: Watu 18 wamefariki katika ajali ya Coaster na lori

Watu 18 wamefariki dunia papo hapo, katika ajali ya gari Wilayani Mufindi katika barabara Kuu ya Iringa-Mbeya.

View attachment 2255971
View attachment 2255981

Source: ITV

========


Watu 18 wamefariki dunia papo hapo baada ya basi dogo aina ya Costa kugongana uso kwa uso na lori la mizigo karibu na eneo la Changarawe, Mafinga mkiani Iringa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, ACP Allan Bukumbi amethibitisha kutokea vifo hivyo akisema kuwa taarifa ziaidi zitatolewa baadaye

"Ni kweli ajali imetokea na inasadikika watu zaidi 10 wamepoteza maisha papo hapo," amesema.

Wakizungumza kwa njia ya simu baadhi ya watu walio katika eneo la tukio wamesema mpaka saa tatu asubuhi, jitihada za kuokoa majeruhi na kutoa miili ya watu zinaendelea.

Eneo ambalo ajali hiyo imetokea, ndilo ambalo basi la Majinja liliangukiwa na lori mwaka 2015 na kuua zaidi ya watu 40

CHANZO: MWANANCHI

Watu 18 wamefariki katika ajali ya Coaster na lori Rais Hana habari na hajatuma Hata salami Za Rambi Rambi kwa wafiwa na majeruhi? Nchi ya ajabu sana hii​

 
Imetokea ajali mbaya iliyohusisha basi dogo aina ya Coaster na lori

Watu 18 wamekufa eneo la tukio

Source ITV habari
 
Hakuna hata shuhuda wa kusema nini kilitokea...?

Moja ya barabara bora kabisa hii, barabara pana, alama zote zinezibgatiwa... . Poleni sana wafiwa.
 
Imetokea ajali mbaya iliyohusisha basi dogo aina ya Coaster na lori

Watu 18 wamekufa eneo la tukio

Source ITV habari
Toa taarifa kamili wewe Mzee Mgaya. Nina maslahi na hilo eneo la Wilaya ya Mufindi kwa ujumla wake.

Coaster ilikuwa inatoka wapi, kwenda wapi! Chanzo cha ajali ni nini!!
 
hapo lazima kuna mmoja alikuwa wrong lane
Mwenye Coaster ndiye mwenye makosa alikuwa kushoto linakopanda lorry mwenye lorry yeye alikuwa ameshawajibika kwa kosa lake kwa kuhamia upande wa kulia ila coaster ghafla akarudi upande wake ndo yakatokea hayo.

Ukiangalia Costa ilivyoharibika vibaya inaonekana hiko kishindo siyo cha gari iliyotoka mbali pana distance ndogo sana ndo maana bado kwa kiasi makalio ya coaster yapo upande wa kushoto.
 
Toa taarifa kamili wewe Mzee Mgaya. Nina maslahi na hilo eneo la Wilaya ya Mufindi kwa ujumla wake.
Taarifa kilo itatolewa na RPC

Ila coaster Ilikuwa inatoka Dar ikagonga lori bovu lililokuwa limeegeshwa barabarani

Wakati wa uokozi lori lingine likatokea na kugomga majeruhi
 
Toa taarifa kamili wewe Mzee Mgaya. Nina maslahi na hilo eneo la Wilaya ya Mufindi kwa ujumla wake.

Coaster ilikuwa inatoka wapi, kwenda wapi! Chanzo cha ajali ni nini!!
Hiyo hapo
Screenshot_20220610-101242.jpg
Screenshot_20220610-101254.jpg
 
Mungu awape pumziko jema na kuwafariji wafiwa, majeruhi awape upinyaji wa haraka, binafsi kazi zangu zunahusisha sana safari, huwa nawaza na kujiachia kwa Mungu, kama binadamu hatuna uwezo nazo, matukio ni mengi sana huko barabarani, tusiache kusali wakuu kila inapobidi.
 
Poleni Sana Dah njia yangu hii napita Mara nyingi
 
Madereva wengi hawafuati sheria ,wanabahatisha. Ukisafiri na basi halafu ukakaa siti ya mbele madereva wanaovatake pasiporuhusiwa ila bahati tu mbele hakuna gari inayokuja. Na bado abiria tuna/wanacheka na dereva.
Ajali haina kinga ila ka huna roho ngumu kwny bus usikae mbele asee jamaaa wanaovateki kihasara sana hata mkifika salama kosa kosa za uso kwa uso na malori huwa kibao....

Mtu anaovateki semi 4 afu anarudi kwake dk ya mwsho kbs unasikia vuuu
 
Sad indeed.

Hii coaster siyo zile wanajiita Hakuna Kulala huwa wanasafiri usiku tu hao jamaa mwendo wao ni kama kimondo kuna siku nilimsikia nadhani mkuu wa mkoa wa Iringa akitoa tamko zisionekane barabarani na ajali hii inawezekana ikawa uchovu wa driver pamoja na hali ya ukungu ktk mikoa mingi kwa sasa,ukiiangalia hiyo picha ni kama Coaster ilikuwa wrong lane lorry likamkataa kwa kurudi kulia kisha Costa tena akataka arudi upande wake ndo akajaa.

Mungu azipokee roho za wahanga majeruhi awape afuweni na pole kwa wote waliowapoteza wapendwa wao.
Mkuu hivi umejipa hata muda wa kusoma habari kamili? Maana hiki ulichoandika na ambacho RPC amezungumza ni tofauti kabisa.
Hakuna driver anayeingia barabarani ili akapate ajali bali huwa ni miscalculation tu hutokea. Hivyo tusiweke speculation nyingi za kuwalaumu hata bila kuwasikiliza kujua kipi kilitokea.
 
Dah unakuta hapo abiria wa irnga mjin wameshuka zao salama..mbelen wenzao umauti unawakuta...yaan maisha bna yaani hata unachokitafuta muda mwingine hata hufaham...
 
Back
Top Bottom