Mufindi: Watu 18 wamefariki katika ajali ya Coaster na lori

Mara nyingi madereva wanamwagilia moyo na Pombe za take away,watatunaliza
 
Kumbe umewasoma? Yaani wanabahatisha tu hawana tahadhari.
Mimi ninaamini kwanini zikifuatwa ipasavyo ajali zitabaki chache ile mbaya. Ila watu wanaamini ajali hazizuiliki na kwamba kama ipo ipo tu(wanasubiri kudra za Mungu azuie)
 
ni lini hizi ajali zitakwisha maisha ya watu yanusurike???

Kuna tatizo kubwa Sana la ukaidi wa kutofuata sheria za barabarani
 
Hizi zilikuwepo tangu zamani zilikuwa hazitangazwi tu-Alisikika Nyumbu mmoja akiropoka!
Li-mtu Hilo ni li-NYUMBU kweli-kweli kiwango cha Serengeti. Jambo ni la kusikitisha mno halafu mtu (na labda hakuwepo ndani kwenye hiyo gari iliyopata ajali) anasema kwa kuropoka eti zilikuwepo tangu zamani ......si bora angekaa kimya tu?
Pole kwa wafiwa. Mungu awape wepesi majeruhi wapate unafuu mapema iwezekanavyo.
 
ni lini hizi ajali zitakwisha maisha ya watu yanusurike???

Kuna tatizo kubwa Sana la ukaidi wa kutofuata sheria za barabarani
UKAIDI na UZEMBE wa madereva na kukosekana/kuzorota utendaji kwa weledi wa maTraffic wanaosimamia Usalama barabarani. Polisi- (Vehicle) Leseni kwa Madreva zinapatikana kiulaini sana i.e. kimchongo bila kujali ni aina (gari ya Abiria au Binafsi) atakayoenda kuendesha.
 
Ajali haina kinga ila ka huna roho ngumu kwny bus usikae mbele asee jamaaa wanaovateki kihasara sana hata mkifika salama kosa kosa za uso kwa uso na malori huwa kibao....

Mtu anaovateki semi 4 afu anarudi kwake dk ya mwsho kbs unasikia vuuu
sema tu umaskini kikwazo ila dawa ya ajali za hivi ni 4 Lanes tu kwa highway zote ,tutawalaumu sana madera lakini hata ukipewa steering ya basi wewe utafanya tu vilevile.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
dah kicheche hicho...

RPC wa Morogoro, Iringa na Mbeya wanapaswa kwa pamoja kuwa na joint meeting kucrack vichwa namna gani wafanye kuondoa ajali maeneo yao with joint forces...

Road patrol nje za mara kwa mara, emmergence barrier' s, kuwe na speacial forces ya traffic police maeneo hayo kuhakikisha kwa pamoja wanapambana na tatizo......randomly Inspection ya magari kwenye barriers mkitumia mafundi competency, madereva wawe wanafanyiwa randomly interaction huko barabarani na kupimwa pombe na utimamu wakiwa safarini...

Polisi wa barabarani waache kuendekeza rushwa waanze kuwa na weredi wakupumbe maisha ya watu yako mikononi mwaona hii ni dhambi duniani na ahera..

Serikali iwe serious na kitengo cha utoaji leseni za udereva hasa kwa madereva wa magari ya mizigo na abiria, kuna maeneo tuwe makini nayo saana na rushwa isiwe na nafasi kabisa.... Utoaji wa hizi leseni uendane na competency ya mhusika..

Abiria tuache kupuuza na kujifunza kusimamia wenyewe safari zetu tukiwa kwenye mabasi kwa kuangalia aina ya makonda na madereva na tuhakikishe wakati wote wa safari wako serious.
 
hoja yenye tija sana hii itapendeza sana kama wahusika wakapata ushauri huu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa kuna uzembe wa wengi
1. Hili eneo, kwa mujibu wa mchangiaji mmoja pameshatokea ajali. Ina maana ni eneo hatarishi. Serikali ilichukuwa hatua gani?
2. Dereva wa lori lililoharibika aliweka ishara kama inavyotakiwa kuonyesha mbele kuna gari bovu barabarani?
2. Dereva wa coaster hakuwa makini na huenda alikuwa kwenye mwendo mkali ndiyo maana akaligonga lori bovu
3. Dereva huyo huyo wa coaster hata baada ya kusababisha ajali, pengine hakuweka alama kuonyesha mbele kuna ajali.
4. Dereva wa lori jingine naye hakuwa makini na huenda alikuwa kwenye mwendo mkali.,
 
sema tu umaskini kikwazo ila dawa ya ajali za hivi ni 4 Lanes tu kwa highway zote ,tutawalaumu sana madera lakini hata ukipewa steering ya basi wewe utafanya tu vilevile.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana aisee. Ndio Utaovateki nakubali, lakini unakuwa makini na mwangalifu sana na kwa kuzisoma alama za nyakati. Sio kuovateki tu kwa sababu kuna kuovateki.Kumbuka hata wewe dereva ni miongoni mwa abiria na unaweza kufa au kujeruhiwa vibaya sawa na abiria uliowabeba.
 
Mwenyezimungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi.
Amin.
 
Serikali ianze sasa kuwa makini na hizi biashara za usafirishaji, ni wakati wakuhakikisha hii biashara inafanywa na watu wenye muscles na kuweka restriction ya magari mapya ya abiria na mizigo..

na kama ni used basi Serikali iwe na kitengo chini ya jeshi la polisi na TBS kucertify all used commercial vehicles na wapewe certificates kuhakikisha kweli yamefanyiwa ukaguzi wa kina na kupewa kibari cha kuingia barabarani...

Madereva wa magari ya abiria na mizigo kuwe na speacial tests za kila miaka 2 kupima utimamu wao wa akili na competency..... Yeyote anayetumia kilevi kama bangi, Unga na pombe iwe marufuku kuwa dereva wa commercial vehicles..
Driving licence renewal ya commercial vehicles iwe 2yrs tofauti na 5yrs...

Jeshi la polisi liajili vijana competent kwenye road accident investigation, road patrols, na vehicles inspections....TUACHE JANJAJANJA this is SERIOUS WORLD...

Ajali ikigundulika ni uzembe wa dereva au Mwenye gari kampuni husika ipigwe faina kuuubwa na kufungiwa licence yake..

TUWE SERIOUS NA MAISHA YA WATU.....
 
Ndio ni kweli kuna uzembe wa wengi lakini mwanzilishi/mwasisi wa uzembe wote ni dereva wa coaster ambaye kagonga lori bovu lililokuwa limesimama. Je, Hakuliona au hakutambua kuna kitu kisicho cha kawaida barabarani akiwa bado mbali? Je, Hapakuwa na nafasi pembeni mwa lori bovu? Coaster Hana breki? Yapo mambo siku hizi kwa madreva hasa madreva pamoja na mkonda vijana wawapo barabarani : Mwendo mkali, Mziki mnene, Video, Mazungumzo ya hovyo e.g. timu za mpira na Stori mbalimbali utadhani wapo kijiweni na wanajisahau wapo kazini-tena kazi nyeti.
 
Hii habari iko hapa toka saa tatu asubuhi so ulichokisoma wewe ni update mwanzo haikuandikwa hivi.

But siyo kesi maana hata kamanda mwenyewe ametoa taarifa za hisia.
 
Umemaliza Mkuu. Comment Safi sana. Ubarikiwe.
Laiti wahusika wangelizingatia hayo.
 
Mkuu 'kicheche' ina maana gn?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…