Muhtasari wa kilimo cha baadhi ya mazao jamii ya kunde

Mkuu hizo ni stori za watu tu ukweli halisi haupo hivyo, hebu soma hapa labda mimi naona vibaya, pitia hii link uone halihalisi

CHANGAMOTO YA KUKOSA SOKO LA UHAKIKA KWA WAKULIMA CHANZO CHA UMASIKINI

WAKULIMA wa zao la dengu katika kijiji cha Amani kata ya Salawe halmashauri ya wilaya ya Shinyanga bado wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa soko la uhakika kwenye zao hilo ikiwemo miundombinu ya barabara kuwa mibovu hali ambayo inawafanya kushindwa kusafirisha mazao yao.

Wakiongea na mwandishi wa habari aliyetembelea wakulima wa kijiji hicho walisema kuwa zao hilo limekuwa mkombozi katika kunyanyua pato la familia lakini kubadilika kwa bei ikiwa wengine wanauza shilingi 45,000 mpaka 55,000 kwa gunia moja na kukosa soko la uhakika imekuwa ni tatizo, ikiwemo wadudu wahalibifu pamoja na panya.
 
Habari wadau,

Kampuni ya Kilimo Business and Associates www.facebook.com/KILIMOBIZNET kwa kushirikiana na Chama Cha wakulima wahitimu Tanzania (Tanzania Graduate Farmers Association-TGFA) www.facebook.com/TanzaniaGFA inapenda kuwataarifu wajasiriamali na wadau wengine wa kilimo kwamba tunaendelea kupokea order za mbegu za mikunde kama dengu, mbaazi, choroko, kunde n.k.


Mbegu hizi tunazinunua kwa makubaliano maalum kutoka kwa wanunuzi wa mazao hayo (baadae atakuja kununua kama watakubaliana bei na mzalishaji) pia vituo vya utafiti pamoja na agents wa mbegu hizo zenye ubora na viwango.

Tunashauri wale wakulima ambao wangependa kuwa na hakika ya biashara yao na hata kununua mbegu zenye ubora wakubali kutumia huduma zetu kwa kuuliza na hata kutoa order mapema kabla mzimu haujaanza.

BONYEZA HAPA Ili kuweza kuwekwa kwenye list ya wadau muhimu pamoja na kutoa order yako ya mbegu ama kutafutiwa soko la hakika tafadhali BONYEZA HAPA.
Kumbuka mbegu zote tunazosambaza zimefanyiwa tafiti na zimethibitishwa na TOSCI..... Pia mkumbuke mbegu ikishakaa zaidi ya miez 7 lazima irudishwe ikapimwe.

Kwa mawasiliano zaidi piga namba 0718664645 ama 0789856246 ama 0763954635 email kilimobiznet@gmail.com

 
TUnashukuru kwa wale ambao wanaendelea kutupigia simu na hata kutuandikia email... Usichukie ukikuta simu yako haipokelewi. Tutakupigia ama kukujibu sms utakayotuma
 

Mkuu waweza nipa ushari mzuri wa zao hili?tafadhali tuwasiliane kupitia medardaristides@yahoo.com
 
Mm niliwachek mkaniambia hamna mbegu za kunde kwa sasa..
Nashsuri mkajipange kwanza then mtakuja upya.
 

Mkuu tupe mrejesho wa muhogo ilikuwaje kwenye mavuno katika hekali ulizolima ulipata tani ngapi kwa kila hekali, na ulitumia mbegu gani, na sokoni bei ilikuwaje wakati wa kuuza mzigo wako??
 
Habari wataalam wa kilimo na ufugaji,
Naomba kwa mwenye ufahamu na zao la kunde,
1. Hekari moja inaweza kutoa gunia ngapi za kunde(mavuno)
2. Ni mbegu gani inayo zaa sana ya muda mfupi na inayo pendwa sokoni?
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwenu.
 
Samahani wakuu nilipotea kwa muda, kuhusu mihogo baadhi ilipata ugonjwa ikaaribika iliyobakia niliuza kwa sh, 150000/= tu, nikaona nibadilishe zao nimepanda miembe ya kisasa aina ya Ngowe heka moja mwaka jana, na mihogo pia ninayo heka 1 yakutoka mwezi wa 9 na mengine heka 2 itatoka mwakani kwenye mwezi wa 2-3. Kweli kilimo kinachanga moto wakuu kinahitaji uvumilivu sana
 
Naomba kwa anaye jua bei ya choroko na kunde kwa jumla inauzwaje anijuze tafadhali..
 
Naomba kwa anaye jua bei ya choroko na kunde kwa jumla inauzwaje anijuze tafadhali..
Bei 1600 mpaka 3000 kwA wanunuzi wa export
Lakini kwA sahvi msimu wa choroko ushapita ni mpaka messi wa tatuu mwakani...mkuu
 
Bei 1600 mpaka 3000 kwA wanunuzi wa export
Lakini kwA sahvi msimu wa choroko ushapita ni mpaka messi wa tatuu mwakani...mkuu
Nilitaka nilime mvua za vuli zikianza mwezi wa kumi kama heka 5 hivi, so sinto pata soko?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…