Mulugo: Mwaka Kesho Serikali itashindwa kuwapeleka watoto Sekondari

Mulugo: Mwaka Kesho Serikali itashindwa kuwapeleka watoto Sekondari

Yaa hii inawezekana iwe kama wanavyofanya kwenye hospitali teule,Bima ya afya nk serikali inashea na wamiliki binafsi.Pia itasidia kupunguza mzigo kwa serikali kwa sababu wamiliki binafsi wana miundombinu ya kutosha.

Ila tuu wajadiliane gharama za kulipia,mwisho wale ambao watakosa shule za serikali zilizopo na za binafsi ndio watajengewa madarasa mapya.

Hii nchi kasi ya uzazi ni kubwa sana sio mchezo,huko usukumani ndio balaa
 
Rais yeye hajui hilo. Yeye kichwani kwake anawaza tu kujenga shule za wasichana na Academy za michezo kila mkoa.
Wewe ni mropokaji tuu, hizo shule za wasichana watakaoingia ni tofauti na hawa anaowataja Mulugo?

Pili hizo academy ni za kuwajengea watu skills ili waje kujiajiri badala ya huo mzigo kuachiwa serikali au kila mtu kuwa machinga,anajaribu ku diversify soko la ajira na skills kwa vijana.
 
Hakuna anayekosa hoja nzuri kwenye kutetea ugali wake

Angetoa ushauri huu ukiwa na suluhu kwa kuzingatia gharama za shule yake huku akilinganisha na uwezo wa watanzania haswa wale wapiga kura wake pale jimboni. Angekuja na ushauri wa jinsi ya kuisaidia serikali kuendelea kutoa elimu kwa kugharamia kila kitu ili watoto wa kitanzania waelimike katika usawa

Yeye kama mtu aliyeamua kuwekeza kwenye elimu anaweza kuendelea kupokea wanafunzi wachache wenye uwezo wa gharama zake

Pia ni muda muafaka kwake kuangalia mahitaji ya taifa hili kwenye elimu kwa level nyingine kama Ufundi stadi, kilimo na ufugaji akawekeze huko
Gharama zinajadilika, kwani bima ya afya ikoje? Pia gharama ya kumsomesha mtoto bila ada inajulikana sasa hapo ndipo pa kujadiliana na hawa wamiliki binafsi.

Kwamba serikali iwe tayari kutoa wanafunzi kama rasilimali ambayo wao hawana na wao wakubali kushusha bei ili waache kulia lia kukosa wanafunzi
 
Naibu Waziri wa zamani wa Elimu na Mbunge wa Songwe, Philip Mulugo leo Bungeni amesema mwaka kesho serikali itashindwa kuwapeleka watoto Form one kwenye shule za serikali kwasababu mpango wa elimu bure ulianza miaka sita iliyopita hivyo watoto waliopo leo darasa la sita ni takribani 1.8 milioni ilhali madarasa na madawati ya shule za serikali uwezo wake ni kuchukua wanafunzi laki saba na nusu.

Amesema serikali itabidi ijenge shule jambo ambalo hadhani kama itawezekana, ameiomba serikali ije na mpango wa PPP kwani shule binafsi zina kila kitu lakini zinakosa wanafunzi na nchi ni ya wote hivyo ameomba wake pamoja.

Mulugo ame-declare interest kwamba yeye ni mdau wa elimu na mmiliki wa shule binafsi.


Nampongeza kwa kudeclare interest kama miongoni mwa wamiliki wa shule binafsi
 
Hakuna anayekosa hoja nzuri kwenye kutetea ugali wake

Angetoa ushauri huu ukiwa na suluhu kwa kuzingatia gharama za shule yake huku akilinganisha na uwezo wa watanzania haswa wale wapiga kura wake pale jimboni. Angekuja na ushauri wa jinsi ya kuisaidia serikali kuendelea kutoa elimu kwa kugharamia kila kitu ili watoto wa kitanzania waelimike katika usawa

Yeye kama mtu aliyeamua kuwekeza kwenye elimu anaweza kuendelea kupokea wanafunzi wachache wenye uwezo wa gharama zake

Pia ni muda muafaka kwake kuangalia mahitaji ya taifa hili kwenye elimu kwa level nyingine kama Ufundi stadi, kilimo na ufugaji akawekeze huko
Uwezekano wa serikali kuingia ubia au kutoa ruzuku ni solution nzuri, kwa maana watoto wasikose nafasi.
Kuliko kuanza from 0 kujenga madarasa, waalimu na miundombinu mingine, sekta binafsi tayari hivyo wanavyo. Inaweza tatua changamoto kwa muda kuliko kukaa hadi tatizo lipigiwe kelele.

Shida ya mindset za serikali za kijamaa ni kuona kama private sector ni mbaya kuchangia maendeleo ya jamii
 
Rais yeye hajui hilo. Yeye kichwani kwake anawaza tu kujenga shule za wasichana na Academy za michezo kila mkoa.
Hao wasichana,ni miongoni mwa hao 1.8,kwa hiyo zikijengwa hizo shule za wasichana,ambao huwenda wakawa 65%,ya wanafunzi wote wa msingi,hapo imeshapunguza idadi ya wanafunzi,ukitoa watakaokwenda ufundi kama ni 15%,ukitoa watakashindwa kuendelea na watakao soma shule binafsi,bado kuna watakaokosa masomo?
 
Gharama zinajadilika, kwani bima ya afya ikoje? Pia gharama ya kumsomesha mtoto bila ada inajulikana sasa hapo ndipo pa kujadiliana na hawa wamiliki binafsi.

Kwamba serikali iwe tayari kutoa wanafunzi kama rasilimali ambayo wao hawana na wao wakubali kushusha bei ili waache kulia lia kukosa wanafunzi

Jaribu kuangalia Opportunity Cost hapo☺☺☺☺
 
Amekuwa muwazi kwamba anamiliki shule inaitwa "Southern High land"

Pia issue ya capacity ya miundombinu ya kubeba form one in the comming years ni ndogo sana. Sijui kama itawezekana. Halafu tatitizo litakuwa endelevu hata kwenda A-level pia vyuo.
Souther Highland ni ya akina Joseph Mungai
 
Wewe ni mropokaji tuu, hizo shule za wasichana watakaoingia ni tofauti na hawa anaowataja Mulugo?

Pili hizo academy ni za kuwajengea watu skills ili waje kujiajiri badala ya huo mzigo kuachiwa serikali au kila mtu kuwa machinga,anajaribu ku diversify soko la ajira na skills kwa vijana.
Umemaliza mjadala,umeelezea vizuri sana.
 
Uwezekano wa serikali kuingia ubia au kutoa ruzuku ni solution nzuri, kwa maana watoto wasikose nafasi.
Kuliko kuanza from 0 kujenga madarasa, waalimu na miundombinu mingine, sekta binafsi tayari hivyo wanavyo. Inaweza tatua changamoto kwa muda kuliko kukaa hadi tatizo lipigiwe kelele.

Shida ya mindset za serikali za kijamaa ni kuona kama private sector ni mbaya kuchangia maendeleo ya jamii

Kabla ya kusema ni wazo zuri tujue kwenye elimu sasa hivi serikali inamgharamia mwanafunzi kiasi gani cha pesa?
 
Ni Mulugo huyu huyu aliyeunganisha Physics, Chemistry na Biology kuwa Somo moja?
 
Back
Top Bottom