Hamna kesi hapo. Hata angekushika UGONI live si jinai. Akipiga simu pokea halafu hakikisha unamrekodi kisha kafungue kesi ya KUTISHIA KUUA KWA MANENO (JINAI) halafu mkutane mahakamani nakuhakikishia hiyo kesi inampeleka jela huku unaendelea kupiga bibie tena kitandani kwake.
Binafsi, niliwahi kufumaniwa CITY STYLE HOTEL, Sinza Mugabe (kwa ushahidi nenda kawaulize wahudumu wa mapokezi) na anayedaiwa ni mume wa mwanamke niliyekua nae faragha. Jamaa wamevamia na makamera room, tukiwa uchi. Wakachukua video na makelele kibao walipotoka parking wakavunja kioo cha gari langu na kutoa upepo tairi, baada ya hapo wakanitishia kurusha picha za utupu mitandaoni. Baadae jamaa akarusha video aliyoturekodi kupitia whatsapp yangu.
Sasa, akajiloga, akapiga simu (voice call) vitisho vya kuniua mimi hapo NAREKODI vyote. Haikuchukua muda jamaa anapelekewa wito mahakamani kesi inaunguruma mwaka wa pili huu na jamaa bado anasota. Anaomba msamaha kama mtoto Mdogo.