Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

Yani ndugu yangu acha tu. Kuna tuvisa tudogo dogo hadi unaona aibu hata mtu wa nje akiskia. Anaweza tu akaamka akaanza kusema hivi kule ana mashuka mangapi kayachukue si ulimuazima siku moja tu. Nyie nachanganyikiwa naona kama hii roho inamuandama. Akili iliyonijia hapa ni kupiga maombi. Naona aibu kwakweli. Sio kawaida
[emoji23][emoji23][emoji23]...Aisee mwamba anaulizia hadi vi shuka anavotumia mdogo ako?Asee hii ni Abnormality yani dume zima kabisa na midevu linahangaikia na vitu vidogo vya kijinga namna hii?
 
Na kweli nimjuaji ,na ana maneno mengi hashauriki,walomshauri ampangie ndugu yake wametisha sana,hiyo ndo solution.. anaonekana anapenda misifa anataka mamaake amuone *HERO*kwamba anamsaidia majukumu huku kwny reality analeta mvurugano na mmewe anaependa privacy,ndoa bado changa "km alivyo sema mtoa post"mme anataka privacy a-enjoy na mkewe , awe huru na mji wake ,sema mkewe ndo much know wa viwango
Watu wa jamiiforum msiwe wepesi kuhukumu. Mbona nimesema kabisa sina uwezo wa kumpangia. Sasa mnaposema nataka kuwa hero kwa mzazi wangu, hivi mzazi hakai dar, amekuachia mtoto umlee kwasababu akiwa mwenyewe mzazi anaamini hana usimamizi. Na mimi sina uwezo wa kumpangia na mzazi atauliza unampangia si umrudishe nyumbani. Nnachotaka ni sababu ya kumtoa hapa nyumbani. Huo ndo ushauri nnaotaka na sio mnanihukumu. Yani nnachoelezea ni hiyo wananiambia mtoe dogo mpangie sina ela hiyo na kumtoa ni kumpeleka home, nahitaji tu maneno ya busara ya kumwambia. Sasa mnakaza kunihukumu hamna kingine. Wenye busara maneno wanaweza kunipa ndo nayasubiri.

So far asante kwa hukumu ila ungejua maisha au sapoti ambayo mama yangu anahitaji sio kipesa ila ile ya kuona ana msaada tu wa kumuangalizia watoto huku dar ndo ungeelewa . Ila siwalaumu mna haki ya kunihukumu kwasababu hamjui mengine
 
Simple tu, umeolewa na mtu asiyekupenda na mwenye roho ya kimasikini
Very simple ukweli mchungu mtu anaekupenda hawezi kuchukia ndugu zako hata kidogo dada hapo cha kufanya mpeleke mdogo wako hostel basi kuepusha kero zisizo na kichwa wala miguu...mimi pia naishi na mdogo wangu na mume wangu anamchukulia kama mdogo wake
 
"naomba nikute siti ya kukaa" ,,[emoji1787][emoji1787][emoji1787] huyo kaka yetu ana roho mbaya.
 
Very simple ukweli mchungu mtu anaekupenda hawezi kuchukia ndugu zako hata kidogo dada hapo cha kufanya mpeleke mdogo wako hostel basi kuepusha kero zisizo na kichwa wala miguu...mimi pia naishi na mdogo wangu na mume wangu anamchukulia kama mdogo wake
Nnavotamani hizi comment niwe natoa mimi🙌🏼 ila watu wanakazana kunihukumu. Nyie kufukuza ndugu ni jambo rahisi hivi?
 
Na kweli nimjuaji ,na ana maneno mengi hashauriki,walomshauri ampangie ndugu yake wametisha sana,hiyo ndo solution.. anaonekana anapenda misifa anataka mamaake amuone *HERO*kwamba anamsaidia majukumu huku kwny reality analeta mvurugano na mmewe anaependa privacy,ndoa bado changa "km alivyo sema mtoa post"mme anataka privacy a-enjoy na mkewe , awe huru na mji wake ,sema mkewe ndo much know wa viwango
Watu kama hawa katika familia wapo sana, wanapenda sifa na kuonekana wema bila kujali anaumiza upande wa mume.
Mimi binafsi napenda privacy sana.
Kwangu hawezi kukaa ndugu yangu wala upande wa pili.
Nitasaidia wakiwa mbali.
Kama kuja kwetu wasalimie na kukaa siku kadhaa wasepe.
Kukaa na ndg ni mzigo, watakufanya uishi maisha wayatakayo wao, watataka special treatment na mimi huo ujinga sinaga kabisa.
Nikiwa kwangu mimi ndiye mfalme sitakagi mbambamba za ndg.

Kwa misimamo yangu nitawaudhi kwani sitaki kuuishi uongo uongo
 
Kwa maelezo haya huyu mwanaume ni mbinafsi na hapendi watu wa upande wako, anapenda ndugu zake tu. Kwa kuwa umesema ana upendo kwako, jipange kuzungumza naye kwa Upendo kabisa. Tafuta sehemu nyingine tofauti na nyumbani, muulize nini shida. Wengine Wana mitazamo mibaya juu ya ndugu wa mke wake.
Ikishindikana tafuta utaratibu mwingine wa kumsaidia mdogo wako, usipoteze ndoa kwa sababu ya Hilo. Maana sio lazima kuishi na ndugu zako humo, wadogo Wana kwao.
 
Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
Tabia nikama ngozi haiwezi kubadilika ila pia inawezekana labda mumeo ni mbinafsi ndo maana hapendi ndugu zako hivyo ili asije akaleta madhara kwa ndugu zako jaribu kuwa makini nae ikiwezekana huyo mdogo wako mrudishe tu nyumbani ili kuepusha matatizo
 
Watu kama hawa katika familia wapo sana, wanapenda sifa na kuonekana wema bila kujali anaumiza upande wa mume.
Mimi binafsi napenda privacy sana.
Kwangu hawezi kukaa ndugu yangu wala upande wa pili.
Nitasaidia wakiwa mbali.
Kama kuja kwetu wasalimie na kukaa siku kadhaa wasepe.
Kukaa na ndg ni mzigo, watakufanya uishi maisha wayatakayo wao, watataka special treatment na mimi huo ujinga sinaga kabisa.
Nikiwa kwangu mimi ndiye mfalme sitakagi mbambamba za ndg.

Kwa misimamo yangu nitawaudhi kwani sitaki kuuishi uongo uongo
Hayajakukuta, au kwenu uko peke yako, subiri siku uumwe af mkeo awe mbali af ita ndugu uliowakataza kuja kwako uone kama utapata msaada. Sio kazi ya kuhukumu. Usijione kama huna shida ya watu. Ipo siku utawahitaji na hutowaona. Mungu atusaidie sote🤝
 
Hayajakukuta, au kwenu uko peke yako, subiri siku uumwe af mkeo awe mbali af ita ndugu uliowakataza kuja kwako uone kama utapata msaada. Sio kazi ya kuhukumu. Usijione kama huna shida ya watu. Ipo siku utawahitaji na hutowaona. Mungu atusaidie sote🤝
Sikiliza dada.
Jambo la msingi ni kudumisha upendo lkn sio kuishi pamoja.
Hivyo watakuja wanakaa siku kadhaa na kuondoka.
Lkn huwezi kuweka ndg standby kusubiria uumwe akusaidie.

Au mngekuwa yatima ni haki kumkaa na mdogo wako hadi ufike muda wa kujitegemea
 
Na kweli nimjuaji ,na ana maneno mengi hashauriki,walomshauri ampangie ndugu yake wametisha sana,hiyo ndo solution.. anaonekana anapenda misifa anataka mamaake amuone *HERO*kwamba anamsaidia majukumu huku kwny reality analeta mvurugano na mmewe anaependa privacy,ndoa bado changa "km alivyo sema mtoa post"mme anataka privacy a-enjoy na mkewe , awe huru na mji wake ,sema mkewe ndo much know wa viwango
Ni kweli huyo jamaa anaoneka hapeni kuishi na watu zaidi ya mke na watoto au mfanyakazi jamaa atakuwa ana tabia za kizungu kupenda uhuru bila buguza ndani ya nyumba, Huyo dada itabidi alete mfanyakazi wa ndani ili aone huyo mfanyakazi atachukuwa na mumewe.
 
Kwa maelezo haya huyu mwanaume ni mbinafsi na hapendi watu wa upande wako, anapenda ndugu zake tu. Kwa kuwa umesema ana upendo kwako, jipange kuzungumza naye kwa Upendo kabisa. Tafuta sehemu nyingine tofauti na nyumbani, muulize nini shida. Wengine Wana mitazamo mibaya juu ya ndugu wa mke wake.
Ikishindikana tafuta utaratibu mwingine wa kumsaidia mdogo wako, usipoteze ndoa kwa sababu ya Hilo. Maana sio lazima kuishi na ndugu zako humo, wadogo Wana kwao.
Mkuu huyu mwanaume ni mbinafsi yeye kama yeye siyo tu kwa upande wa ndugu wa mke ata kwa upande wa ndugu zake, ndiyo maana ndugu zake wanaenda kwake kwa kupita na kuondoka na siyo kwa kuishi inamaana ndugu zake wanamjua ndugu yao ni mtu wa kupenda kuishi maisha ya peke yake bila mapishano kwenye nyumba.
 
ondoa mdogo wako Mambo anayosema kwenu kuhusu MUMEO yahovyo Sana kibaya mdogo wako hajui anaowambia hayo maneno wanamrudishia MUMEO Kama yalivyo. hauishi morogoro wewe na baba ako kipindi ulimwambia aje bila kumtaarifu mumeo
 
Mumeo kakuoa wewe sio mdogo wako acha kumpa mwamba mzigo usiomhusu mrudishe Mdogo wako nyumbani kwao.
 
Asante kwa ushauri,

naweza kuwapa benefit of doubt katika kugegedana, mdogo wangu amefata nyayo zangu na ananijua vizuri tu na kiukweli uhuni hana.

Mume wangu kusema anatembea nae naweza kumtetea kwa sasa, mimi ni mtu mfatiliaji sana wa hisia so kama kuna mahusiano kati yao ntakuwa wa kwanza kujua ila kwasasa ntakua natenda dhambi kumuhukumu mume wangu siku akinipa
Hiyo sababu ntajua tu.

Sababu ambayo nahisi ni kwamba mume wangu hajawahi kuishi na familia kubwa yenye ndugu mchanganyiko kama mimi nilivyokua wazazi wetu maisha yao yoye wamekua wakiishi na ndugu zao so nilijifunza huko kuwa kila mtu ni mwanadamu mwenye uwezo wa kukosea.

Kilichonileta natamani mume wangu awe na amani na mdogo wangu naumia kuwa katika position ya kumfukuza mdogo wangu wakati mimi ndo nilishadadia aje hapa ili awe karibu na chuo. Leo namwambiaje nenda nyumbani? Ni mbali sana kutokea nyumbani kwenda chuoni kwao. So kwa hapa kwangu anarahisisha.

IMG_1895.jpg
 
Sasa yatima unakaa nae wakati mume hamtaki?
Si ndo yale yale.

Mume kama hataki ndugu ni hataki tu. Kikubwa tupo Afrika. Kama mtu umeamua kufukuza ndugu fukuza tu. Ila siku ukiwahitaji naongea kwa experience hutowaona.

Sikiliza dada.
Jambo la msingi ni kudumisha upendo lkn sio kuishi pamoja.
Hivyo watakuja wanakaa siku kadhaa na kuondoka.
Lkn huwezi kuweka ndg standby kusubiria uumwe akusaidie.

Au mngekuwa yatima ni haki kumkaa na mdogo wako hadi ufike muda wa kujitegemea
 
Back
Top Bottom