Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
Nimesitikitika.
Isije kuwa mumeo alimkuta mdogo wako ktk mazingira tatanishi na mwanaume au ashamsikia anaongea na simu na mwanaume so jamaa anaona yeye analea halafu kuna fala anakula kama kaoa.

Pia, inawezekana jamaa tu hataki anataka kulea watoto wake kwa amani.

Au anafantasi flan hivi akiwa home ajiachie na kiboksa tu sa ahapo huyo dogo anambana.

Yote kwa yote fanya hivi uwe unafanya maombi kila siku usiku kuhusu hilo suala atabadilika. Au anaweza kusikiankuwa umelfanya ktkaombi so anaweza kubadilika au kuongea shida iko wapi
 
Nimesitikitika.
Isije kuwa mumeo alimkuta mdogo wako ktk mazingira tatanishi na mwanaume au ashamsikia anaongea na simu na mwanaume so jamaa anaona yeye analea halafu kuna fala anakula kama kaoa.

Pia, inawezekana jamaa tu hataki anataka kulea watoto wake kwa amani.

Au anafantasi flan hivi akiwa home ajiachie na kiboksa tu sa ahapo huyo dogo anambana.

Yote kwa yote fanya hivi uwe unafanya maombi kila siku usiku kuhusu hilo suala atabadilika. Au anaweza kusikiankuwa umelfanya ktkaombi so anaweza kubadilika au kuongea shida iko wapi
Asante kwa ushauri wa maombi. 🙏
 
Ila kuna mdau anasema kwa ushuhuda na umemtokea yeye akiwa kwa Shem

Shem mkali kujionyesha kumbe ni wivu na anamtamani ( mdogo mtu)

Angalia pande zote pia hamu ina Vishawishi vingi sana mchunguze mmeo au mwondoe mdogo wako hapo

Huo ni ushauri tu kwani kila kitu linawezekana chini ya Jua

Dunia hii haijaanza leo na machafu ni mengi ila yanatofautiana
Pole sana ila natumaini umepata picha kubwa hapa kwa wadau

Usikurupuke bali uwe mwangalifu pia
Dua zangu
Asante sana🤝🙌🙏
 
Kuhusu kuzaa wala sio kikwazo tuko vizuri. Namrudishaje nyumbani mtoto sasa nawaambiaje? Wakati mimi ndo nilishadadia aje akae huku karibu na chuo. Leo nasema arudi kwasababu gani.

Na kingine mdogo wangu anaweka mambo yake sawa atarudi tu nyumbani ila huo mda wa miezi kadhaa mbona ntakoma mimi. Maana mume kila siku anaibuka na jipya naumia
Inaonekana wewe ulitaka dogo aje kuishi hapo kwenu bila kujadili na mumeo na kujiridhisha kuwa ameridhia. Wanawake mnamajaribu sana muda mwingine na kutaka watu waonekane wanaroho mbaya.


Kuna rafiki yangu anapitia hii changamoto. Yaani mkewe anaweza ongea na mama yake jambo wakapanga sijui kuna ndugu anakuja mkoani kuja kufanya labda interview au kuja kwa swala lolote lile bila ya kumshirikisha mwanaume wake. Halafu anakuja mwambia mgeni yupo njiani anakuja na basi ameshakaribia kuwa kuna mtu anakuja.


Jamaa ameshamkanya mara kadhaa na kumuelekeza kuwa maisha hayaendi hivyo mwanamke haelewi.

Kuna siku kulikuwa na harusi ya upande wa mwanamke kuna wageni wakaja mjini mwanamke anakuja mshirikisha mwanaume wageni wapo sebuleni, sasa unamshirikisha nini hapo na maamuzi tayari keshafanya.

Jamaa akatazama ile tupsi akaona haina shida. Kimya kimya akabeba nguo zake chache akaenda zake kulala guest akawa anaamkia huko kwenda kwenye shughuli zake na kurudia huko. Mwanamke akashtuka jamaa harudi home.

Kumpigia simu jamaa akamwambia unajiskiaje mimi kufanya maamuzi bila kukwambia lolote?!

Basi nimekupisha ukae na wageni mimi naona hatusikilizani na unafanya mambo bila kunishirikisha. Nitatafuta sehemu yangu nyingine ya kuishi nitakaa huko, wewe kama utataka kuonana na mimi utakuja na kunitembelea ila huko mimi siji tena. Nimekupisha ukae na kwa uhuru ukaribishe unayejiskia bila kuhangaika kunambia. Mwanamke akaomba msamaha na kutaka yaishe. Jamaa akakaa siku kadhaa mwanamke akalalamika balaa kwa familia ya jamaa.

Kukakaliwa kikao jamaa akafunguka yote. Tokea siku ile mwanamke akaacha hayo mambo.
 
Umeongea vyema sana kaka angu. Ntatafuta tena neno lenye busara nimwambie kwamba huyu ni mtoto. Amlee tu kama mwanae
Unaonekana unampenda sana mdogo wako. Ila kuwa na mipaka na hisia zako. Kuna wanaume wanapenda sana mama na baba zao kiasi kwamba akioa anataka waje waishi nyumba moja, sidhani kama utafurahia akifanya hivyo.
 
Ni mchoyo mmeo
Kwan mumeo anashinda nyumbani muda mwingi wanakutana wapi??mdogo wako anaenda chuo mmeo kwenye mihangaiko yake wanakutana wapi muda mwingi
 
Tupo ndugu zaidi ya wawili wapi sasa? Mimi na mdogo wangu mmoja anaeenda chuo anarudi jioni, ndo kurundikana? Soma vizuri maelezo. Mtoto ambae humlipii ada, humpi nauli, mara moja moja hata chakula ananunua yeye mdogo wangu akijibana chuo anatuletea vizawadi maskini.

Kwetu hatuna shida na nyumba dar ipo lakini nauli mtoto anaweza kutumia hata elfu 10 kutoka nyumbani kwenda chuo. So sio kwamba kwetu ni kijijini lakini nyumba ya hapa dar ilipo ni mbali na chuo. Nimeshaelezea sana.

Muhamishie hostel
 
Mpangishie mdogo wako chumba acha kuishi na mke mwenzio atakapokuchukulia mume hii umefungiliwa na Mungu mdogo wako anamsumbua mumeo ndio maana hataki akae hapo ndugu sio vizuri kuishi Kwa wanandoa
 
Unaonekana unampenda sana mdogo wako. Ila kuwa na mipaka na hisia zako. Kuna wanaume wanapenda sana mama na baba zao kiasi kwamba akioa anataka waje waishi nyumba moja, sidhani kama utafurahia akifanya hivyo.
Kwangu mimi sioni shida akileta mama yake. Mama namjua ni mtu mwenye upendo sana ikitokea hivyo sitaona shida. Basi naona tuko tofauti
 
Inaonekana wewe ulitaka dogo aje kuishi hapo kwenu bila kujadili na mumeo na kujiridhisha kuwa ameridhia. Wanawake mnamajaribu sana muda mwingine na kutaka watu waonekane wanaroho mbaya.


Kuna rafiki yangu anapitia hii changamoto. Yaani mkewe anaweza ongea na mama yake jambo wakapanga sijui kuna ndugu anakuja mkoani kuja kufanya labda interview au kuja kwa swala lolote lile bila ya kumshirikisha mwanaume wake. Halafu anakuja mwambia mgeni yupo njiani anakuja na basi ameshakaribia kuwa kuna mtu anakuja.


Jamaa ameshamkanya mara kadhaa na kumuelekeza kuwa maisha hayaendi hivyo mwanamke haelewi.

Kuna siku kulikuwa na harusi ya upande wa mwanamke kuna wageni wakaja mjini mwanamke anakuja mshirikisha mwanaume wageni wapo sebuleni, sasa unamshirikisha nini hapo na maamuzi tayari keshafanya.

Jamaa akatazama ile tupsi akaona haina shida. Kimya kimya akabeba nguo zake chache akaenda zake kulala guest akawa anaamkia huko kwenda kwenye shughuli zake na kurudia huko. Mwanamke akashtuka jamaa harudi home.

Kumpigia simu jamaa akamwambia unajiskiaje mimi kufanya maamuzi bila kukwambia lolote?!

Basi nimekupisha ukae na wageni mimi naona hatusikilizani na unafanya mambo bila kunishirikisha. Nitatafuta sehemu yangu nyingine ya kuishi nitakaa huko, wewe kama utataka kuonana na mimi utakuja na kunitembelea ila huko mimi siji tena. Nimekupisha ukae na kwa uhuru ukaribishe unayejiskia bila kuhangaika kunambia. Mwanamke akaomba msamaha na kutaka yaishe. Jamaa akakaa siku kadhaa mwanamke akalalamika balaa kwa familia ya jamaa.

Kukakaliwa kikao jamaa akafunguka yote. Tokea siku ile mwanamke akaacha hayo mambo.
Sasa kwanini mke alete ndugu wa kijijini anaekuja kwenye interview bila mawasiliano na mume.

Hadi nalalamika ni kwamba miaka mitatu kabla ya kuoana mume wangu alilijua hili swala. Na wala haikua kuchukua ndugu zangu wote. Ni huyu mmoja tu awe karibu na shule.

Sasa kama mtu anakubali then anakuja kugeuka baadae basi hapo ni changamoto
 
Mi nimekuelewa unampenda mdogo wako na unaipenda sana ndoa yako vizuri sana, unashindwa kumrudisha dogo home kwamba unaanza kuwaambiaje mama sio.! Pia kwa hali hiyo labda ungetamani Kufata ushauri wa wadao hapo kumhamishia mdogo wako hostel ila bahati mbaya bado uchumi wako sio safi saf,i sasa unafanya nini? Umejinasibu mme wako ni mtu safi sana na anajali saana si ndio? Sasa fanya ngea nae kwa faragha KUU muombe huyo dogo amalizie siku zake za masomo hapo kwenu then apite hivi, Mme wako anataka muwe nyie tu mfurahie life yenu ya mwanzomwanzo ya ndoa msikilize, Uafrika unaousema wewe utakuja tu na ataelewa vizuri
 
Mungu ni mwema: nimepokea mgeni kutoka kijijini kwa mume wangu kaingia mchana huu kiukweli nimefurahi na mengi. Mume wangu atajifunza Kupitia hili kwamba ukishakua mkubwa kuna mambo hayaepukiki. Picha linaanza mapokezi niliyompa haamini. Na tutakua nae hapa kwa mwezi. Labda maneno yatapungua. Ushauri wenu wa kumtoa mdogo wangu nimeupokea Mungu anipe busara ya maneno ya kumuondoa ila hadi aondoke na huyu ndugu yake aondoke atatoka na funzo kubwa sana.

Asanteni
 
Kwa uzoefu:-
  • Unayempigania sasa hivi, baada ya kupata kazi au mji wake anaweza kuwa changamoto kwako, na asikumbuke namna unavyoweka ndoa yako rehani kwa sasa.​
  • Kwa sababu yuko chuo, akae hosteli au nyumbani kwa wazazi wake wewe uwe unamsapoti pale panapohitajika.​
  • Kuendelea kumtetea yeye, ni kuweka ndoa yako rehani kwa kitu ambacho huna uhakika uko mbeleni kama mtakuwa bega kwa bega.​
  • Uwe upande wa mumeo na usimpande kichwani, tokeni 'out' mkiwa wawili na akupe sababu kwa nini kuna hizo changamoto, na nini kifanyike​
  • Kwa wale waliopitia mafunzo; maisha ya ndoa ni mke na mme tu ndio wanaofanya maamuzi, sio ndugu wala wazazi.​
  • Punguza msongamano hapo nyumbani, ili uweze kumpa mapenzi vizuri, iwe; jikoni, bafuni, kolidoni n.k​
  • Mzalie watoto wa kutosha; na pambania watoto, na usipambanie ndugu kwa sababu na wao watakuwa na wake/waume zao na hawatamkumbuka mumeo, ingawa kwa sasa wanatumia hela zake.​
 
Yaani umekaza kichwa kama hamnazo.
Sasa mnataka niseme na mama mkwe Simpendi tena? Au ndo wanadamu hawana jema. Watu wameshauri nifukuze mdogo wangu. Hakuna hata mmoja aliekuja kuniambia wangu nilimfukuza na imekua hivi hivi. Yani hakuna jema
 
Kwa uzoefu:-
  • Unayempigania sasa hivi, baada ya kupata kazi au mji wake anaweza kuwa changamoto kwako, na asikumbuke namna unavyoweka ndoa yako rehani kwa sasa.​
  • Kwa sababu yuko chuo, akae hosteli au nyumbani kwa wazazi wake wewe uwe unamsapoti pale panapohitajika.​
  • Kuendelea kumtetea yeye, ni kuweka ndoa yako rehani kwa kitu ambacho huna uhakika uko mbeleni kama mtakuwa bega kwa bega.​
  • Uwe upande wa mumeo na usimpande kichwani, tokeni 'out' mkiwa wawili na akupe sababu kwa nini kuna hizo changamoto, na nini kifanyike​
  • Kwa wale waliopitia mafunzo; maisha ya ndoa ni mke na mme tu ndio wanaofanya maamuzi, sio ndugu wala wazazi.​
  • Punguza msongamano hapo nyumbani, ili uweze kumpa mapenzi vizuri, iwe; jikoni, bafuni, kolidoni n.k​
  • Mzalie watoto wa kutosha; na pambania watoto, na usipambanie ndugu kwa sababu na wao watakuwa na wake/waume zao na hawatamkumbuka mumeo, ingawa kwa sasa wanatumia hela zake.​
Hiyo sababu ya kwanza umeongea point kubwa sana. Najua kabisa mdogo wangu akipata kwake hata ye anaweza asiwe na moyo nliokua nao maana wanadamu tunabadilika sana. Hili nimelielewa sana tu. I’m sure huyu mtoto akiondoka mume wangu atakua na amani
 
Mungu ni mwema: nimepokea mgeni kutoka kijijini kwa mume wangu kaingia mchana huu kiukweli nimefurahi na mengi. Mume wangu atajifunza Kupitia hili kwamba ukishakua mkubwa kuna mambo hayaepukiki. Picha linaanza mapokezi niliyompa haamini. Na tutakua nae hapa kwa mwezi. Labda maneno yatapungua. Ushauri wenu wa kumtoa mdogo wangu nimeupokea Mungu anipe busara ya maneno ya kumuondoa ila hadi aondoke na huyu ndugu yake aondoke atatoka na funzo kubwa sana.

Asanteni
Hakuna mwanaume anafundishwa na mwanamke king'ang'anizi kama wewe.Mimi nakuambia zingatia msingi mkuu wa ndoa ambao ni watu wa wili tu.Hao wengine wote wabaki kuwa ndugu wasalimiaji tu.Vinginevyo utavunja Ndoa kwa sababu ya hao ndugu.
 
Hiyo sababu ya kwanza umeongea point kubwa sana. Najua kabisa mdogo wangu akipata kwake hata ye anaweza asiwe na moyo nliokua nao maana wanadamu tunabadilika sana. Hili nimelielewa sana tu. I’m sure huyu mtoto akiondoka mume wangu atakua na amani
Pambania ndoa yako; kuna ule wimbo-' kila mtu, atauchukua mzigo wake mwenyewe'
 
Sasa mnataka niseme na mama mkwe Simpendi tena? Au ndo wanadamu hawana jema. Watu wameshauri nifukuze mdogo wangu. Hakuna hata mmoja aliekuja kuniambia wangu nilimfukuza na imekua hivi hivi. Yani hakuna jema
Ndugu,tafuta muda ujifunze kwa watu waliokuzunguka juu ya kuharibu ndoa.Ndoa nyingi zimechangiwa na upande mmoja kuruhusu nduku kuingilia maisha ya wanandoa.Hili mahitaji maneno mengi dadangu.Sisi wanaume tunaojua maana ya uhuru ndani ya Ndoa,ndiyo tunakupa ukweli.
 
Kwanza huyo Jamaa anapata wapi muda wa kuonana na watu wa nyumbani,mie huwa nikiondoka nyumbani SAA 12:30 kurudi ni SAA 3-6 usiku hadi watoto huwa wananimisi.
Ndugu akija nyumbani anaweza akamaliza wiki nzima ndio akaniona has a Jumapili.
Jamaa anashinda nyumbani, huwa ana hesabu nyanya na vitunguu 😂😂, ulinzi madhubuti.
 
Back
Top Bottom